Pre GE2025 Stephen Wasira amrithi Kinana nafasi ya Makamu Mwenyekiti CCM Tanzania Bara

Pre GE2025 Stephen Wasira amrithi Kinana nafasi ya Makamu Mwenyekiti CCM Tanzania Bara

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Aanza kutupa madongo kwa upinzani, asema watakamata dola tena, kila mahali wamefamya maendeleo. Ataka dunia ijue chama chao ni chama cha amani, ataendeleza 4R za MARIDHIANO
 
View attachment 3205078
===
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, kilichoketi leo tarehe 18 Januari 2025, Dodoma, kuelekea Mkutano Mkuu Maalum wa CCM utakaofanyika Leo tarehe 18 na 19 Januari, jijini Dodoma.
View attachment 3205079
#KaziIendelee
Wajumbe wa chadema fanyeni Mambo tuletee vyuma , Lissu na Heche, uchaguzi mkuu 2025 ,ngoma imeisha mapema sana.
 
Aisee... Sasa hili kopo lita mshauri nini rais jamani.?

Ili ujue mwelekeo wa hii nchi ona wanaoteuliwa kwenye vyombo vya maamuzi walivyo

Lisu awe mwenyekiti tu aanze kukinukisha kwakweli
 
Habari Wakuu,

Fuatilia moja kwa moja yanayojiri katika Mkutano Mkuu wa CCM Dodoma leo na kesho January 19-19, 2025.

Nani kumrithi Kinana?

Makundi mbalimbali ikiwemo vyama vya siasa ndani na nje ya nchi, wasanii, taasisi za dini, mabazi na wanamichezo ni kati ya wanaohudhuria mkutano huu wa CCM unaofanyika Dododom.
Rais Samia amefungua mkutano huo kwa kuanza na hotuba ya ufunguzi, ambapo mbali na kuongelea maendeleo ya chama kwa ufupi ametoa onyo kwa wanachama wanaeonda majimboni kwa lengo la kufanya kampeni waache kufanya hivyo mara moja.

Pia awaonya CCM kuwa na makundi wakati wa kuteua wagombea.

Rais Samia awahimiza CCM kuhimiza wananchi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura na wale ambao wanahitaji kuboresha taarifa zao kufanya hivyo.

====

Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar amesoma azimio la kikao cha NEC kilichofanyika 18/1/2025 Dodoma ilipokea na kujadili mapendekezo na kamati kuu ya ccm taifa kuhusu mrithi wa Kinana, baada ya kujadili mapendekezo hayo Halamshauri kuu ya CCM imemteua Steven Wassira kuwa ndiye mwanachama atakayesimama katika uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara ili kupigiwa kura.

CV ya Mzee Wassira, soma CV na Historia ya Mzee Stephen Wasira


Wassira achaguliwa kwa kura 1910 kuwa Makamu Mwenyekiti CCM Tanzania Bara

Kura zilizopigwa: 1921
Kura zilizoharibika: 4
Kura halali: 1917
Kura za hapana: 7
Kura za ndio: 1910 sawa na 99.42%


Kazi kweli kweli...
 
Aisee... Sasa hili kopo lita mshauri nini rais jamani.?

Ili ujue mwelekeo wa hii nchi ona wanaoteuliwa kwenye vyombo vya maamuzi walivyo

Lisu awe mwenyekiti tu aanze kukinukisha kwakweli
Hata wewe Nzi wa kijani Leo hii umeichoka Ccm ?

Kweli siasa ina vitimbi
 
Wajumbe wa chadema fanyeni Mambo tuletee vyuma , Lissu na Heche, uchaguzi mkuu 2025 ,ngoma imeisha mapema sana.
Actually, hivyo vyuma ndio vinatosha, wajumbe wafanye vema kuleta vyuma hivyo. CCM wamejipanga tayari kwa battle ya uchaguzi mkuu. CHADEMA walete vyuma vya uzani wa juu kwa battle hiyo ya uchaguzi
 
NDULA LA KIJESHI LIMEINGIA KAZI IPO ANAKIJUA CHAMA, ANAJUA KUJENGA HOJA NA KUZITETEA, ANAUMRI MKUBWA LAKINI DAMU BADO INACHEMKA, STELING WA MAGOLI YA MKONO, UTAMSHINDAJE?NI MWALIMU WA KINA NAPE,MZEE WA FORCE KINGI
 
Hizo kura wanapiga za nn wakati hamna ushindani?
Ushindani Siyo watu wawili kuwania nafasi moja. Ushindani Ni kutumia maneno mawili ili neno mojawapo liibuke kidedea. Neno "Yes" au "No"; "Ndiyo" au "Hapana". Hayo maneno yamesimama kwa niaba ya watu wawili. Hakika hii Ni "Demo-ghasia" 🤔🤔👐👐
 
Hata wewe Nzi wa kijani Leo hii umeichoka Ccm ?

Kweli siasa ina vitimbi
Mimi sijawahi kuwa nzi wa kijani...

Bali nilikuwa mfuasi wa misimamo ya JPM.
.
Na siku zote nilikuwa naponda uhuni wa chadema chini ya Mbowe, na leo hii ule uhuni tuliokuwa tunapinga umejidhihiriaha tena kutoka kwa watu wenyewe wa chadema.


Kwa sababu hiyo wewe ukaona mimi ni mfuasi wa ccm.
 
Actually, hivyo vyuma ndio vinatosha, wajumbe wafanye vema kuleta vyuma hivyo. CCM wamejipanga tayari kwa battle ya uchaguzi mkuu. CHADEMA walete vyuma vya uzani wa juu kwa battle hiyo ya uchaguzi
Upo sahii, mpaka sasa sioni group la watu makini wa kumvusha Mgombea wa ccm, siasa za majukwaani zinahitaji mvuto pia , na watu wa kujibu hoja zilizo mbele ya ccm wala siwaoni kabisa.

Uchaguzi wa mwaka huu ni mwepesi sana kwa wapinzani , wakimaliza chaguzi zao salama ,
 
Back
Top Bottom