Pre GE2025 Stephen Wasira amrithi Kinana nafasi ya Makamu Mwenyekiti CCM Tanzania Bara

Pre GE2025 Stephen Wasira amrithi Kinana nafasi ya Makamu Mwenyekiti CCM Tanzania Bara

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mtulivu sana huyu mzee!anaweza pia!

Angepewa makonda ningefurahi sana nadhani angefanya ziara nchi nzima!
 
Mtu sahihi kabisa
Ni mzoefu wa siasa na strategist mzuri
Sio muumini wa fujo na vioja
 
Kuna kambi huko CCM ishanyukwa kuelekea Oct 2025
 
Mwenyekiti wa CCM amemtangaza Mhe. Pinda ambaye ni Waziri Mkuu mstaafu kuwa mrithi wa Kinana. Wajumbe na wanachama sambamba na wananchi wameonekana kutopokea positive pendekezo hili au wameshtuka kwa kilichotokea. Je, walimtegemea nani?

Tukumbuke cheo hiki hakuna kugombania bali linapelekwa jina moja ambalo litapata kura za ndio na hawana. Lakini pia historia inaonyesha kila pendekezo la Mwenyekiti huwa linapita kwa asilimia 90+ hivyo ni wazi Pinda ndiye makamu mwenyekiti ajaye wa CCM Bara.
Uwongo mtupu, subiri jina lenyewe
 
Ni wasira.

Chuma kutoka Bunda.

Mwanamikakati wa CCM
 
Chama Cha Mapinduzi kimempendekeza Ndugu Stephen Masatu Wassira kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara.

Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amewasilisha jina la mwanasiasa mkongwe nchini
Stephen Wassira kwa wajumbe wa mkutano mkuu maalum wa CCM wa Taifa unaofanyika Jijini Dodoma, kwa ajili ya kupigiwa kura kuwa Makamu Mwenyemiti wa CCM Bara.

Wasira aliyezaliwa Julai Mosi, 1945 wilayani Bunda Mkoa wa Mara, kwa zaidi ya nusu karne amejijengea heshima kutokana na mchango wake mkubwa katika siasa, uchumi na maendeleo ya jamii.

Wasira ni miongoni mwa wana CCM waliowahi kutangaza nia ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Ni mmoja wa viongozi wakongwe wenye ushawishi mkubwa ndani ya CCM, ambapo tangu mwaka 2007 amekuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM tangu mwaka 2011.

Rekodi yake ya uongozi na uchapakazi wake, imemuweka kuwa katika nafasi nzuri ya kuonekana kama nguzo muhimu ndani ya CCM.

FB_IMG_1737193512620.jpg
 
Mwenyekiti wa CCM amemtangaza Mhe. Pinda ambaye ni Waziri Mkuu mstaafu kuwa mrithi wa Kinana. Wajumbe na wanachama sambamba na wananchi wameonekana kutopokea positive pendekezo hili au wameshtuka kwa kilichotokea. Je, walimtegemea nani?

Tukumbuke cheo hiki hakuna kugombania bali linapelekwa jina moja ambalo litapata kura za ndio na hawana. Lakini pia historia inaonyesha kila pendekezo la Mwenyekiti huwa linapita kwa asilimia 90+ hivyo ni wazi Pinda ndiye makamu mwenyekiti ajaye wa CCM Bara.
Ukome. Makamu ni Mzee Wasira
 
Back
Top Bottom