jiwe angavu
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 20,419
- 39,217
Sina tatizo na Historia aliyoandika Mohamed, tungependa wengi wawasilishe ili tupate upana wa kuelewa.Kimsingi ilitakiwa iwe hivyo, lakini kwa bahati mbaya historia nyingi zimeandikwa kimaslahi. Nitakupa mifano michache tu.
Hivi unaamini kuwa katika historia tulikuwa tunasoma kuwa ZIWA VIKTORIA, TANGANYIKA nk yaligunduliwa na wazungu...... Licha ya kukuta watu katika maeneo hayo wakiishi na kuvua samaki. Hali kadhalika mlima Kilimanjaro...na ....na...na.
Unajua kuwa katika vitabu vya historia vya Afrika Kusini wakati wa utawala wa wazungu kabla ya Mandela kuingia madarakani: Viliandika kuwa Watu wote Afrika ya kusini ni wahamiaji.......(sasa imefutwa)- Hii iliwekwa kwa lengo maalum, kuwa Afrika kusini hakuna wazawa (native). Hali kadhalika huko Australia.....
Ndugu yangu, Historia ndio mahali pekee kwa watawala husika kuelekeza matakwa yao na kuyarudia mara milioni mpaka mkaamini hivyo. Sijasema ya ziwa Nyasa au Ziwa Malawi. Niishie hapo.wa
Hapana Wachangiaji hawana tatizo, shida imeanza Mohamed kuwaondoa katika mada na kujadili yasiyokuwepo. Mfano, bandiko 56, nimejaribu kumrudisha katika mada lakini kwa makusudi au kutojua akaingiza mambo yasiyohusiana na mada. Nyerere na Mtikila wanaingiaji kwa Video aliyotuma Ansber Ngurumo? Pili, kwanini hamjibu mleta Video anamshambulia kama Taasisi. Je, naye kwa maoni yake ni ya Taasisi? Ni ipi hiyo.Unaweza kuwa sahihi, lakini kwa bahati mbaya wachangiaji ndio wamevutika huko. Pengine ungemshauri abadili kichwa cha habari. Kwa sababu kwa ajenda 1,2 na 3 ni pana sana na ni vigumu kwa wachangiaji kuelewa wajikite kwa Chadema/uislam/ukatoliki au Uarabu na DP N.K.
Nilimshauri afute bandiko kwa kuchelea kwamba hoja ni nyepesi na hata kama ni nzito hazina mashiko na hataweza kuzitetea au kuzijadili. Nilimshauri, lakini pia nikakiri kwamba ana uhuru wa kutoa maoni.Binafsi sikuona busara kumshauri afute bandiko. Haya ni maoni yangu.
Ndivyo ilivyoandika biblia ?Jaribu kuwaza nje ya box. Muungano uliasisiwa na watu kwa hiari yao. Na jambo likishakubaliwa na wengi kiimani ni mpango wa Mungu. Je, wewe ulitaka Askofu Pengo achochee watu kanisani wapinge muungano? Kuutaka muungano au kutoutaka ni jambo la kisiasa na si jambo linaloshughulikiwa na Kanisa.
Hayo ni mawazo ya watoto wa nzi , hulaumikiSasa naamini hata wapumbavu mnazeeka ..... Sio kila Mzee ana hekima ...wewe ni mpumbavu ....kila Andiko lako ni udiniudini udini ....
Wewe tunakuelewa ulitaka lisifiwe kanisa tuStill bado jf mnampa credit huyu kichaa,lengo lake kubwa ni kutafuta mpasuko wa kidini nchini,yupo katika siku zake za mwisho hana cha kupoteza kazi yake ni kuona nchi hii inaingie katika mgogoro wa kivita baina ya waislam na wakristo.
Serikali iwe makini naye sana ikiwezekana hatua za msingi zichukuliwe dhidi ya huyu mfia dini gaidi.
Ndiyo fikara Za watoto wa mainziSasa naamini hata wapumbavu mnazeeka ..... Sio kila Mzee ana hekima ...wewe ni mpumbavu ....kila Andiko lako ni udiniudini udini ....
Nguruvi3,Sina tatizo na Historia aliyoandika Mohamed, tungependa wengi wawasilishe ili tupate upana wa kuelewa.
Nina tatizo anapodai 'yakwake ni ya kweli haihitaji kuhojiwa. Nina tatizo anapofanya makosa yale yale ya Wandishi wa awali ya kuwa biased'' na hata kupotosha kwa makusudi au bahati mbaya.
Hapana Wachangiaji hawana tatizo, shida imeanza Mohamed kuwaondoa katika mada na kujadili yasiyokuwepo. Mfano, bandiko 56, nimejaribu kumrudisha katika mada lakini kwa makusudi au kutojua akaingiza mambo yasiyohusiana na mada. Nyerere na Mtikila wanaingiaji kwa Video aliyotuma Ansber Ngurumo? Pili, kwanini hamjibu mleta Video anamshambulia kama Taasisi. Je, naye kwa maoni yake ni ya Taasisi? Ni ipi hiyo.
Rudi usome kwa utulivu utagundua Mohamed amechangia kuwapoteza Wasomaji na Wachangiaji kwa kuwaondoa katika Mada aliyoleta.
Hili si jambo geni kwa baadhi yetu, Mo anaposhindwa kukabiliana na hoja hiyo ni staili yake, mapicha n.k.
Mwenyewe anaita mkando kando ya mjadala bila kujua ni kuwapoteza Wasomaji
Zawadi Ngoda , nimemuuliza Mohamed kwa wema , kwamba, amefanya kazi Bandari ingalikuwa jambo jema angeonyesha wanaopinga Mkataba wa DP wanakosea wapi au Uzuri wa Mkataba upo wapi. Mohamed hakufanya bali kutupa lawama zisizo na msingi kwasababu hoja inajengwa juu ya 'facts'. Hana!
Pili, amedai Chadema walishirikiana na TEC kupinga Mkataba. Nilimuuliza Vipi ACT Wazalendo na CUF ya Prof Lipumba? Mbona nao walipinga, je waliungana na TEC? Hakujibu akaamua kumfuata Mtikila Kaburini.
Tatu, akasema Waislam waligundua hila hawakuungana nao ! Nimemuuliza, si waliungana na CCM! ni kwa mahaba gani na ya lini Waislam hawa hawa wenye malalamiko mengine hayajajibiwa na serikali ya CCM, leo waungane na Watesi wao wa miaka 60! Kulikoni. Mohamed hakujibu akaamua kumfuata Nyerere Kaburini.
Mo akaingiza Uarabu na DP. nikamuuliza kwani Uarabu ni Tusi? Mbona tuna Wazungu!
Kwa hayo machache nilijaribu kumrudisha katika madaasimamie anachoamini , haikufanikiwa kwasababu ku-focus si utamaduni wa majadiliano wa Mohamed, ata 'dance' kila mahali na kila 'tune'
Nilimshauri afute bandiko kwa kuchelea kwamba hoja ni nyepesi na hata kama ni nzito hazina mashiko na hataweza kuzitetea au kuzijadili. Nilimshauri, lakini pia nikakiri kwamba ana uhuru wa kutoa maoni.
Ushauri si shurti ni hisani tu, kuukubali au kuukataa si tatizo
Uzuri MO hata ukimkejeli, yeye anakurudisha ktk hoja. Huu ndio uungwana. Ni shule kubwa sana hii, sote tujifunze toka kwake.Sasa naamini hata wapumbavu mnazeeka ..... Sio kila Mzee ana hekima ...wewe ni mpumbavu ....kila Andiko lako ni udiniudini udini ....
Zawadi..Uzuri MO hata ukimkejeli, yeye anakurudisha ktk hoja. Huu ndio uungwana. Ni shule kubwa sana hii, sote tujifunze toka kwake.
Shauri wa bure kwako Mtoto wa Inzi: kutukana kunakupunguzia hekima yako, ni busarna kutumia lugha mbadala hata kama hukubaliani kabisa na hoja mwenzako.
Naam, mie ni mfuasi wa ilmu yako ya history ya TanganyikaTresor...
In Shaa Allah,
Elimu bila khiyana.
Tresor...Naam, mie ni mfuasi wa ilmu yako ya history ya Tanganyika
Mzee wangu nikukumbushe ila sijui kama utanikumbuka niliwahi kufika kwako pale magomeni tukafanya maongezi nilipata 'ilmu' kubwa sana.. nakumbuka moja ya story ulitupatia ni ya Mzee wangu Kitwana Kondo kuwa alienda Nje kusomea "strategic " hahahaha hivyo mie ni kijana wako kabisa niko hapa kujifunza ilmu ya history ya Tanganyika na huwa naitumia ktk maongezi yangu na kukutolea mifano .Tresor...
Ndugu yangu sote hapa tunajifunza.
Mimi ilm hii si kwa kuwa labda nimesoma sana la hasha.
Nimeijua historia hii kwa kuwa ni historia ya wazee wangu.
Wao ndiyo walioasisi harakati hizi za kupigania uhuru wa Tanganyika wakianza na African Association na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika, TAA na TANU.
Wao ndiyo waliompokea Mwalimu Nyerere Dar es Salaam wakawa na yeye hadi uhuru umepatikana.
Sababu ni hii tu.
Mimi nina mengi pia ya kujifunza kwa wengine kwani huko kwao walikuwapo wazee wao na huenda na wao waliwaona katika harakati mfano wa hizi.
Tresor...Mzee wangu nikukumbushe ila sijui kama utanikumbuka niliwahi kufika kwako pale magomeni tukafanya maongezi nilipata 'ilmu' kubwa sana.. nakumbuka moja ya story ulitupatia ni ya Mzee wangu Kitwana Kondo kuwa alienda Nje kusomea "strategic " hahahaha hivyo mie ni kijana wako kabisa niko hapa kujifunza ilmu ya history ya Tanganyika na huwa naitumia ktk maongezi yangu na kukutolea mifano .
Jaribu kuwaza nje ya box. Muungano uliasisiwa na watu kwa hiari yao. Na jambo likishakubaliwa na wengi kiimani ni mpango wa Mungu. Je, wewe ulitaka Askofu Pengo achochee watu kanisani wapinge muungano? Kuutaka muungano au kutoutaka ni jambo la kisiasa na si jambo linaloshughulikiwa na Kanisa.
Mohamed, sijasema umelazimisha. Nilichosema ni kauli yako ya '' Historia ya Kweli'' uliyoandika. Kumbu kumbu zipoNguruvi3,
Sijapata kulazimisha kuwa historia ya uhuru wa Tanganyika niliyoandika mimi kila mtu aikubali.
Uwezo huu mimi nitautoa wapi?
Nimeandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes na nimeeleza vipi African Association ilivyoundwa na nimeweka majina ya waasisi wake.
Nikaeleza historia nzima.
Sina haja ya kurudia yale ambayo hakuna aliyekuwa akiyajua hadi nilipoyaeleza.
Wasomaji wamepokea kitabu hiki vizuri kupita mategemeo yangu.
Mfano ndiyo huu hapa JF tunakijadili kitabu hiki toka 2008 na nikapewa tuzo mara mbili ya Mwandishi Bora wa Historia.
Halikadhalika Waislam wamenipa tuzo mara mbili pia.
Wanahistoria bobezi wa African History wakafanya pitio mara tatu na kuchapwa katika Cambridge Journalists of African History.
Nikatiwa katika miradi minne ya kuandika historia, mradi wa Harvard na Oxford University Press New York, Mradi wa Oxford University Press Nairobi, mradi wa kuandika historia ya Julius Nyerere na mradi wa historia mpya ya Tanganyika ulioletwa na Rais Magufuli.
Miradi yote hiyo utanisoma ila wa Magufuli huu haukuchapwa.
Sijawalazimisha hawa wote kuniingiza katika miradi yao.
Huu ndiyo ukweli.
La haukupendezi hakuna tatizo.
Aisee... Nilikuona kupitia tv kumbe wewe ni ntu mzima vizuri tu tatizo una utoto mwingi uliojificha kwenye chuki za kiimani. Wewe mzee ni mdini waziwazi. Shida sana
Anachojaribu kukifanya huyu msemaji ni kutaka wasiokuwa Wakatoliki waamini kuwa Kanisa Katoliki bado lina nguvu ile ile iliyokuwanayo kabla ya sakata la "Waarabu" na Bandari ya Dar-es-Salaam.
Kanisa Katoliki katika sakata hili halikupata kile ambacho wamezoea kupata kuanzia wakati wa ukoloni hadi kufikia hili la bandari kupewa "Waarabu," katika Tanganyika huru.
TEC imefedheheka na hili limewaumiza na kwa mara ya kwanza wameshindwa kupata walichotaka kama ilivyokuwa mazoea.
Hawa walikuwa wakikataa kitu basi hakipiti.
Hawakuitaka EAMWS.
Hawakuitaka OIC.
Hawakuitaka Mahakama ya Kadhi.
Hili la bandari hawakulitaka kama ilivyo kawaida.
Wameshindwa safari hii kwa mara ya kwanza.
"Waarabu" wamekabidhiwa bandari.
Imekuwaje kwa TEC kushindwa?
Imeshindwa kwa sababu kuu moja ingawa zipo nyingi.
Hapa nitaeleza hii sababu moja kuu.
Waislam katika sakata la bandari walijikusanya pamoja na kujiweka mbali sana na wale ambao kila wamuonapo "Mwarabu" wao wanauona Uislam ambao lazima upigwe vita kwa hali yoyote ile.
Lakini kulikuwa na kitu kilichoongeza ladha katika kachumbari iliyokuwa ikitengenezwa na TEC.
Waliokuwa wanapinga Waarabu kuendesha bandari walikuwa wa imani moja na pamoja na CHADEMA.
Mifano iko mingi lakini hapana haja kueleza yote hapa.
Waislam kimya kimya wakaiunganisha CHADEMA katika orodha yao.
Chama hiki kikawekwa kundi moja na TEC na hii haikuwa kazi kubwa ya kumtoa mtu jasho la kwapa.
Ndani ya serikali na CCM kuna watu waliona mapema kabisa asubuhi kuwa nchi imeshagawanyika mapande mawili katika misingi ya imani.
Walio ndani ya serikali na CCM iliwadhihirikia kuwa Waislam wamejitenga wako mbali na wanaowapiga vita "Waarabu" na kwa mara ya kwanza kwa namna ya ajabu kabisa Waislam wakawa wanasubiri muda uwadie wapambane na TEC na mwenza wake CHADEMA.
Zikavuja taarifa kuwa Waislam nje ya BAKWATA wanajiandaa kwenda mahakamani kuhoji mengi yanayowasibu ndani ya serikali.
Waliokuwa serikalini na CCM walitambua watuhumiwa watakuwa nani.
Wenye akili zilizotimia ndani ya serikali na CCM haraka wakajiuliza tumefikaje hapa?
Hawa Waswahili si ndiyo waliopigania uhuru wa Tanganyika hadi ukapatikana?
Wenye akili timamu wakatambua vipi wamefika hapo.
Waingereza wana msemo, "You do it once too often."
Wakatoliki wamejidekeza kupita kiasi kwa kuhodhi kila kitu kuanzia serikali yenyewe, bunge, vyama vya siasa na kila kitu bila ya kukutana na kizingiti chochote.
Waislam wako nje na katika hili la "Waarabu," na bandari wamejiweka pembeni makusudi ili Ukristo ndani ya Tanzania ujivue nguo wenyewe hadharani.
Wametishika na wakarudi nyuma.
Hatari iliyokuwa inawakabili waliitambua.
Serikali ikatimiza maamuzi yake.
Taifa likabakia limetulia.
Kanisa likabakia limefedheheka.
Ile nguvu waliyodhani bado TEC inayo kumbe haipo tena.
TEC bila shaka imejiuliza baada ya haya nini kitafuatia?
Sababu ya kushindwa kwao wanaijua fika.
Sasa msemaji anasema Vatican siyo iliyomwalika Rais wa Tanzania bali serikali imeombwa ialikwe Vatican.
Nani mwenye kawaida ya kuongopa?
Kinachotafutwa hapa ni kujaribu kujifuta tope baada ya kuanguka.
Inataka ieleweke kuwa Rais wa Tanzania ana hofu na amejisalimisha Vatican.
Msemaji ananadi kuwa Kanisa Katoliki lina nguvu si watu wa kupuuzwa.
Ukweli ni kuwa hakika Kanisa limehodhi serikali kwa uwiano wa 80% kwa 20%.
Hali hii leo si mtaji tena kwao kwa sababu zilizo wazi kwani mengi yasiyopendeza yanaelezwa dhidi ya Kanisa na hatari yake ishajitokeza.
TEC imedhoofika bila yenyewe kutambua.
Hii ndiyo sababu ya TEC na CHADEMA kujikuta wako peke yao katika sakata la bandari na vita yao dhidi ya "Waarabu."
Iwe iwavyo hali ya siasa imebadilika.
Hizi propaganda kuwa Rais wa Tanzania ana hofu hazitasaidia kitu.
Zinaweza zikaamsha makubwa ambayo hawayategemei.
Zinaweza hizi propaganda pengine zikazua makubwa kuliko ule ukimya walioonesha Waislam wakati wa sakata la bandari.
Wasisahau ukimya mwingi una kishindo.
Ni muda kdg , Nilikuja kama mgeni wa kawaida katika kujifunza , na nilijifunza mengi sana toka kwakoTresor...
Hapana sikumbuki.
Ulikuja kunirekodi au tulizungumza tu kama mgeni wa kawada?
Nguruvi3,Mohamed, sijasema umelazimisha. Nilichosema ni kauli yako ya '' Historia ya Kweli'' uliyoandika. Kumbu kumbu zipo
Sikubaliani na hilo kwamba wewe una 'monopoly' ya ukweli hasa nikiangalia matundu katika historia yako.
Hayo mengine uliyoandika hayanishwishi lakini tunashukuru tumeelewa unakubalika wapi.
Turudi kwenye mada
1. Kwani uarabu ni tusi?
2. Hawa wanaopinga Mkataba wa DP wanakosea wapi? Ukiwa mstaafu wa Bandari ni wapi uzuri wa mkataba wa DP
3. ACT Wazalendo na CUF walipinga mkataba , je nao ni 'washirika wa TEC' kama ulivyosema kuhusu Chadema?
4. Lini CCM imekuwa na uzuri na Waislam, na je hoja zimejibiwa na Serikali ya CCM? Madhila ya miaka 60 yameisha?
5. Huyo mleta mada umemhusisha na TEC kwa maoni yake, wewe unahusishwa na Waislam. Hili ni sawa?
Raia...Aisee... Nilikuona kupitia tv kumbe wewe ni ntu mzima vizuri tu tatizo una utoto mwingi uliojificha kwenye chuki za kiimani. Wewe mzee ni mdini waziwazi. Shida sana
🚮🚮🚮
Yaani unataka CHADEMA waruhusu tu bandari apewe Muarabu kirahisi hivyo ata kama mikataba ni ya ovyo,kisa Kuna maslahi ya Mwarabu ambaye ndie mwenye uislam wake ili kuwavutia Waislamu waipende Chadema??.......Hicho kitakuwa sio Chama cha siasa,bali ni taasisi ya diniKinj...
Tatizo la bandari kupewa Waarabu TEC na CHADEMA walisimama upande mmoja.
Sasa si mimi ndiye niliowaunganisha.
Hili la udini angalia wewe mwenyewe na fanya utafiti utajua.