Suala la DP WORLD na chuki za Watanganyia dhidi ya Wazanzibar

Ni wapuuzi sana Watu wa Bara,mie Sio Mzanzibari ila upuuzi Huwa sipendi..

Harafu wanavyowasema utadhani huo Muungano Wazanzibar ndio walilazimisha wakati ni Tanganyika
 
Zanzibar IPO miaka Zaid ya 500 nyuma wakati nyinyi mnavaa ngozi tuu
 
Kati ya vilaza niliosoma nao chuo walikuwa ni wazanzi.

Walikuwa slow learners sana class.

Mdembwedo sanaaaa

Mtihani ukifika ni kutetemeka mikono na jasho Hadi kwenye meno
 
Wazanzibari wako brain washed kiasi kwamba wanisikia mwarabu wanahaha hata ninaokaa nao huwambii kitu kuhusu mwarabu .hao hao wakienda kuosha vyoo uarabuni ni utumwa kwenda mbele .mleta mada ni moja ya brain washed dude
 

Mtu ukiwa na chuki na roho mbaya unadhani maisha yako yatakuaje mzee mwenzangu, sema wengi wetu imani hatuna! Wapo watanzania ambao wanachuki mbaya dhidi ya waarabu miaka na miaka na hiyo ipo kwenye damu kitambo washakaririshwa na kujazwa chuki , sasa hawa kweli utawaweka kundi gani kwa mfano! Muulize hapo alipo amepata faida ipi tangu aonyeshe chuki na roho mbaya zake! Chukulia mfano wa football, mwarabu akishinda mechi ni FIGISU, akibeba kombe ni FIGISU, mara ooh wanaharibu mpira wa afrika utadhani ni wageni kwenye hili bara, yani anaeongea anajiona ana haki ya kuishi kuliko mwenzie 😁 mwenye akili ataelewa
 
Ndani ya miaka 2 Samia kauza Bandari, hadi kufikia miaka 10 Ziwa Victoria, Serengeti national park na hata Ziwa Tanganyika vitakua vimeuzwa.

Samia ndani ya miaka 2 tayari kasaini ama anakaribia kusaini mikataba mikubwa sana ya nchi hii ambayo inaweza kuja kua na matokeo mabaya kwenye usalama wa nchi kwa miaka mingi ijayo, mkataba wa DP World na LNG.

Nchi hii haina historia nzuri ya uwekezaji chini ya CCM, uwekezaji ama wawekezaji wote walioletwa mwisho wa siku tumeishia kulipa mabilioni ya shilingi, mfano ni Symbion, Dowans, Songas nk.

Tukumbuke serikali ya ccm ilichukua mkopo kutoka EXIM Bank ya China kujenga bomba la gesi, tukaambiwa uchumi wa gesi, Tanzania itakua kama ulaya, tutauza umeme nje nk lakini hadi leo tunalipa tu deni la Exim, hakuna chochote, gesi sio yetu, deni liko pale pale, wahusika walishapiga chao cha juu wanakula kuku kwa mrija.

Leo Makamba anakuja na hadithi zile zile kwamba LNG ndio uchumi wenyewe, tutakua kama ulaya na mambo kede kede ila ukweli unajulikana, wanapigia kelele 10% yao halafu huko mbele non of their business.

Kama Samia anawategemea Makamba na Nape kama washauri wake wakuu, unategemea nini, hii nchi itauzwa tu kama alivyosema Ndugai, wakati mwingine saa mbovu husema ukweli.
 
Wazanzibari wako brain washed kiasi kwamba wanisikia mwarabu wanahaha hata ninaokaa nao huwambii kitu kuhusu mwarabu .hao hao wakienda kuosha vyoo uarabuni ni utumwa kwenda mbele .mleta mada ni moja ya brain washed dude

Acha chuki fanya kazi lisha familia yako, mwanaume mzima unalalamika hata aibu huoni! Halafu unataka wanaowapenda waarabu wafuate nyayo zako!! Hivi fainali ya juzi kati ya Al ahly na Wydad casablanca uliifurahia kweli?
 
Kwani nyinyi huko Zanzibar mna nini zaidi ya kuinyonya Tanganyaka?
Umeme hamlipii mnatumia bure,mishahara mnalipwa kutokana na fedha za Tanganyika.
Kwa kudeka Kama watoto wadogo hamjambo.
 
Zanzibar kuna uchumi gani wa watu kukimbilia watu ma mwinyi kama nyinyi kazi yenu kuvizia wazungu tu kuomba omba hela na kutaka kulelewa.
 
Mwalimu Nyerere na Karume hawakututendea kabisa haki wananchi wa Tanganyika na Zanzibar. Maana huu muungano haukutakiwa kabisa kuwepo.
Walifanya kosa kubwa moja la karne ambapo hata viongozi wa ccm wanaendelea kulifanya,kutoandaa mchakato wa kura ya maoni ya wananchi wa Tanganyika na Zanzibar kuamua iwapo wanataka Muungano au la maana nchi hizi ni za wananchi si za Nyerere au Karume au Kiongozi yoyote yule ,najua hawako tyr kwa hilo kwa sbb wanajua kitakachotokea,hakuna muungano wa hovyo kama huu duniani, believe me
 
Zanzibar wapo million 2
 
Nasikitika jukwaa hili kuvamiwa na watu wenye akili ndogo za kitoto. Si rahisi nchi hii kugawanyika mpaka wajukuu na vitukuu vyenu, mnaongelea mambo ya kitoto tu. Mungu ambariki rais wetu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania. Hakuna anayeijua nchi inaitwa Tanganyika wengi wenu humu zaidi ya kuwa mmezoea ubaguzi na chuki dhidi ya wananchi wenzenu. Baada ya kuipata hiyo Tanganyika msiyoifahamu mtaanza kudai kanda baadaye mikoa. Nyie ni mashetani tu ya kupuuzwa. Marekani ni muungano wa nchi 50 hawana huo upumbavu wenu kila raia wake anajisikia fahari kujiita mmarekani. Angalieni nyi mlivyokuwa km manyani wala siyo binadamu
 
Adui wala sio mtanganyika au mzanzibari. Adui yetu sote ni CCM chama cha wajaa laana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…