Suala la Mugalu imenifanya nigundue jinsi gani wachambuzi wengi wa soka Bongo ni bendera fata upepo

Suala la Mugalu imenifanya nigundue jinsi gani wachambuzi wengi wa soka Bongo ni bendera fata upepo

Wewe na kocha wa simba nani anajua mpira?

Kama kocha wa simba anaona mugalu ndie best striker kuanza.. wewe nani umuone hafai..

Mpira wa ushindani mkali kama caf champions league usitegemee striker anaejua kufunga tu huku vingine hajui.. bali awe ana vya ziada vingii.. kama ball control, ball possession, na kusaidia kukaba na kuokoa kipindi ukiwa unashambuliwa... ni striker gani wa pale simba anamzidi mugalu kwa hizo factor zote...
Umenikumbusha kipindi cha Alex Ferguson wakati akimtumia Shaba Ranks Danny Welbeck.
Welbeck alikuwa anakosa magoli sana yaani kama Mugalu hivi. Lakini alikuwa anatimiza majukumu yote kama ulivyoelezea hapo juu. Nakumbuka Fergie aliulizwa kuwa kwasasa ni mchezaji gani ambae anacheza kama unavyoaagiza bila kusita alisema Danny Welbeck.
 
Siku ya mechi ya mwisho kati ya Simba na AS Vita, Mugalu alikosa magoli hadi Kocha nilimwona akimkasirikia.

Ilivyo kosa goli la mwisho akambadilisha na kumwingiza Bwalya huku nafasi ya Mkude akamwingiza Nyoni.

Kabla ya hapo tulikuwa tunawaongoza goli 2 kwa 1 na huku tukiwa tunashambuliwa kila wakati wakitaka kurudisha goli.

Baada ya kumtoa huyo Mugalu wenu Simba ilishinda goli mbili za haraka haraka. Goli la tatu likifungwa na sub ya Mugalu, Bwalya. La nne Chama.

Hapa inaonekana wazi jinsi Mugalu alivyotugharimu na kutukaba siku hiyo maana angeendelea kubaki uwanjani huenda angeendelea kukosa nafasi muhimu za kufunga hivyo Vita kuweza kusawazisha na pengine kushinda.

Kocha sio kwamba anamtumia Mugalu kwa kuwa ni mzuri ila hana namna. Kegere kaisha makali, Boko ni majeruhi.

Wakati wa Kocha kishingo alikuwa anamtumia John Boko ambaye ni mzuri kupita Mugalu na Kagere. Huyo Mugalu alikuwa anakalia benchi tu na Simba ilikuwa inapata matokeo mazuri.
Ni kwamba sasa hivi Simba tumekosa mfungaji mahiri.
Hapa hatuzungumzii footwork wala kuhold mipira, wala fomesheni ya mpira.
Hapa tunazungumzia mshambuliaji mfungaji wa Magori.
Kwa ma mild field wa Simba akina Chama, Luiz, Kagata, Bwalya, Morrison nk, pale Simba namba tisa angesimama hata Papaa Morringa angefunga magoli ya kumwaga.

Leo hii mfungaji bora wa ligi yetu anatokea Azam FC, Prince Dube.
Huyo ndiye mfungaji.
Hii inaonesha wazi kuwa pamoja na ubora wake Simba bado haina mshambuliaji mahiri wa kufunga magoli.
Kocha Gomez kumtumia mtu haina maana ndiye anayefaa, ni kwamba kakosa mtu anayestahiri katika hiyo namba.

Mugalu uwezo wa kufunga magoli hana.
Hayo mambo ya kuhold mipira na kugawa kwa wengine ni mada nyingine. Sijawahi kusikia mshambuliaji anapewa tuzo ya kuhold mipira na kugawa kwa wengine.
Mwambieni Mugalu wenu sisi tunataka afunge magoli maana ndio mshambuliaji tegemeo kwa sasa.
Siamini kwamba alisajiriwa ili ahold mipira.
Awe siriaz uwanjani na sio kutafuna Big G kila wakati.

Mkuu una msimamo thabiti ila argument zako sio za kiutu uzima.

1. Umesema kwenye mfumo wako utamtumia Kagere over Mugalu, wakati huo huo unasema Gomez anamtumia Mugalu kwa sababu Kagere amejiishia (kaisha). Maana yake wewe ungemtumia mshambuliaji aliyejiishia.

2. Unaposema Simba haina mshambuliaji mahiri kwa sasa. Unaweza kuwa sawa au si sawa. Lakini hii sio hoja mezani, hoja iliyopo ni kati ya washambuliaji WALIOPO ni nani ana tija zaidi.

3. Dube na Azam yake wameshacheza mechi 25 za ligi. Simba na akina Bocco, Kagere na Mugalu wana mechi 20 tu za ligi.
Litakua ni jambo la ajabu sana kushangaa watu wenye mechi tano mkononi kuzidiwa magoli mawili au moja na mtu aliyewatangulia mechi tano (dakika 450).
Tena hawa wenye mechi tano mkononi Wako kwenye ''timu yenye safu kali zaidi ya ushambuliaji'' katika ligi husika.

4. Kwa maneno mengine ni kwamba wewe unahoji credibility ya Gomes, mtu ambaye yuko mazoezini na wachezaji. Yeye na benchi la ufundi wanapokuja na kikosi kitakachokwenda kutekeleza mpangokazi uwanjani, Mugalu anaoangwa ''on merit'' sio kwa rushwa, uzuri wa sura, kujuana n.k.

NB: Naheshimu sana maoni yako, sifurahishwi na mshambuliaji (yeyote) kukosa magoli. Ila ninachoweza kukuhakikoshia ni kwamba Gomez atakukera sana msimu huu (Kama unakereka na chaguo lake kwenye eneo la mshambuliaji). Na ndio maana nikasema wewe na ''kocha mwenzio'' Gomez, mnatofautiana kwenye misingi (principles). Wewe uko sahihi, yeye yuko sahihi.
 
hasira za nini bwasheee??
tuliza mihemko

mimi kwa maoni yangu kwa mfumo wa Da Rosa chaguo la kwanza ni Mugalu alafu Bocco ndo huyo Kagere wako ambaye ni mtu wa kuvizia vizia uwanjani na kukimbia kimbia hovyo.

Kunywa chai
Sio Ditram Nshimbi? Maana nimegundua hii maada inachangiwa pia na utopolo walioamua kujifanya mashabiki wa Simba.Shabiki wa Simba anaeitakia mafanikio,hawezi kutaka timu yake iridhike na mchezaji wa aina ya Mugalu.

Yani kwamba Mugalu anazuia mabeki kupanda kushambulia? Umesahau kazi ya Djuma kule Congo, ilivyosababisha Miqiusone arudi nyuma kumsaidia Zimbwe,huyo Mugalu alikuwa wapi?? Mshambukiaji akiwa sharp magoli lazima yapatikane kulingana na nafasi zinazotengenezwa . Nakumbuka ile Yanga ya Zahera iliyokuwa na viungo wabovu, ila kazi ya Makambo ilionekana, na ndie aliachangia wao kumaliza katika nafasi ya pili.

Hebu fikiria yule Makambo wa kipindi kile,ndo angekuwa kwenye timu inayotengeneza nafasi nyingi kama simba.

NB;Kiufupi Mugalu ni striker butu,acheni kumpamba ovyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TUMJADILI MUGALU KWENYE
Mechi ya Simba vs Al mereik 3:0

Iyo mechi Simba walishambulia Sana, na kuutawala kabisa mchezo.

1. Simba walipiga JUMLA ya mashuti 11.

Cha ajabu, MUGALU alipiga shuti moja tu on target na ndo lilikua goli.

2. mugalu hakupiga key pass yeyote ile pamoja na kua Simba walkua kwny rythm nzur ya mchezo.

3. Tofauti na goli alilofunga, MUGALU alkua na pass accuracy mbovu kabisa ya passi 13 TU, sawa na 68%

4. Mugalu bado suala la kumiliki MPIRA lilimsumbua Sana, akiwa na possession lost Mara 10.
Ambapo kwa nafas anayocheza iyo Ni BIG SHAME.

5. Kuwaumbua mabeki,
Mugalu ameshindwa kabisa kugombea mipira na mabeki wa Tim pinzani.

- kwenye ground duels (mipira ya chini) 8, amewin 2 TU sawa na 25%

-kwenye aerila duels (mipira ya juu) 4, amewin 1 TU sawa na 25%

6.KEY PASSES,
pamoja na Simba kudominate Sana ule mchezo,
bado mugalu ameshindwa ata kutoa key pass yeyote sawa na 0%

NAWEZA KUHITIMISHA KUA IYO MECHI, Mbali na kufunga Lile goli, performance bado ilkua chini.

mugalu alibebwa na performance ya wenzie

NMEAMBATANISHA TAKWIMU HAPA CHINI[emoji116]View attachment 1746723View attachment 1746724View attachment 1746725

Wewe jamaa kabla ya kuangalia pass acculacy angalia zone ambayo mchezaji anacheza, kuna asilimia 3% hadi 5% ya kupoteza pasi ukiwa upande wako (zone yako). Pia mpaka 40% ukiwa kati kati ya uwanja. Mpaka 70%ya kupiteza mpila ukiwa kwenye zone ya adui, simply ni rahisi kufanikisha pass, drible, hata kupokonya mpila ukiwa kwenye zone yako hadi katikati ya uwanja. Yaani ni uchizi kutaka statistic za mugalu na thadeo. Ndio maana timu inaproduce offtaget nyingi kuliko on target. Inafikia hadi 13(2) haushangai? Nenda na fact basi kidogo. Yaani mugalu anacheza kwenye zone ya mpinzani unategemea awe na acculate pass ya 80-90% kama thadeo?
 
Sina hasira yoyote.
Nilielewa mshambuliji jukumu lake ni kufunga magoli.
Hayo mambo mengine sikuwa nayaelewa.
Asante kwa kunifahamisha.
Hata tukimpima kwa takwimu za kufunga huyo Mugalu, sidhani takwimu zake ni mbaya sana. Leading scorer kwenye mashindano ya CAF ana magoli matatu, yeye anayo magoli mawili (pungufu ya goli moja). Sidhani kama hizi ni ''takwimu mbaya sana'' kama ambavyo unataka umma uamini.
 
Wewe jamaa kabla ya kuangalia pass acculacy angalia zone ambayo mchezaji anacheza, kuna asilimia 3% hadi 5% ya kupoteza pasi ukiwa upande wako (zone yako). Pia mpaka 40% ukiwa kati kati ya uwanja. Mpaka 70%ya kupiteza mpila ukiwa kwenye zone ya adui, simply ni rahisi kufanikisha pass, drible, hata kupokonya mpila ukiwa kwenye zone yako hadi katikati ya uwanja. Yaani ni uchizi kutaka statistic za mugalu na thadeo. Ndio maana timu inaproduce offtaget nyingi kuliko on target. Inafikia hadi 13(2) haushangai? Nenda na fact basi kidogo. Yaani mugalu anacheza kwenye zone ya mpinzani unategemea awe na acculate pass ya 80-90% kama thadeo?
Mpira sio mpila. Unatatizo la R
 
Mkuu una msimamo thabiti ila argument zako sio za kiutu uzima.

1. Umesema kwenye mfumo wako utamtumia Kagere over Mugalu, wakati huo huo unasema Gomez anamtumia Mugalu kwa sababu Kagere amejiishia (kaisha). Maana yake wewe ungemtumia mshambuliaji aliyejiishia.

2. Unaposema Simba haina mshambuliaji mahiri kwa sasa. Unaweza kuwa sawa au si sawa. Lakini hii sio hoja mezani, hoja iliyopo ni kati ya washambuliaji WALIOPO ni nani ana tija zaidi.

3. Dube na Azam yake wameshacheza mechi 25 za ligi. Simba na akina Bocco, Kagere na Mugalu wana mechi 20 tu za ligi.
Litakua ni jambo la ajabu sana kushangaa watu wenye mechi tano mkononi kuzidiwa magoli mawili au moja na mtu aliyewatangulia mechi tano (dakika 450).
Tena hawa wenye mechi tano mkononi Wako kwenye ''timu yenye safu kali zaidi ya ushambuliaji'' katika ligi husika.

4. Kwa maneno mengine ni kwamba wewe unahoji credibility ya Gomes, mtu ambaye yuko mazoezini na wachezaji. Yeye na benchi la ufundi wanapokuja na kikosi kitakachokwenda kutekeleza mpangokazi uwanjani, Mugalu anaoangwa ''on merit'' sio kwa rushwa, uzuri wa sura, kujuana n.k.

NB: Naheshimu sana maoni yako, sifurahishwi na mshambuliaji (yeyote) kukosa magoli. Ila ninachoweza kukuhakikoshia ni kwamba Gomez atakukera sana msimu huu (Kama unakereka na chaguo lake kwenye eneo la mshambuliaji). Na ndio maana nikasema wewe na ''kocha mwenzio'' Gomez, mnatofautiana kwenye misingi (principles). Wewe uko sahihi, yeye yuko sahihi.
Gomez anafanya hivyo kwakuwa hana jinsi.
Nakuhakikishia, Mugalu ukiisha mkataba wake kama uchezaji wake utabaki huohuo wa kukaba badala ya kufunga magoli, basi utumishi wake Simba utaishia hapo.
Namaanisha jinsi Mugalu anavyocheza sasa hawezi kuongezewa mkataba hapa Simba.

Simba kwa sasa haihitaji sababu, au Mkabaji wapo wakabaji na Fraga anakuja kusaidia, Sumba inamhitaji mshambuliaji mahiri wa kufunga magoli.

Katika Mechi za Clab Bingwa nafasi moja ni muhimu sana.
Simba inahitaji mtumiaji sahihi wa nafasi hiyo moja, ambaye hayupo.

Kama Mugalu Mkabaji mzuri sawa tu kwakuwa Simba inahitaji mtu kama yeye pia.

Ila bado Simba kuna pengo la mfungaji mahiri, ndiye ninayemzungumzia hapa na sio Mugalu.
 
Mkuu una msimamo thabiti ila argument zako sio za kiutu uzima.

1. Umesema kwenye mfumo wako utamtumia Kagere over Mugalu, wakati huo huo unasema Gomez anamtumia Mugalu kwa sababu Kagere amejiishia (kaisha). Maana yake wewe ungemtumia mshambuliaji aliyejiishia.

2. Unaposema Simba haina mshambuliaji mahiri kwa sasa. Unaweza kuwa sawa au si sawa. Lakini hii sio hoja mezani, hoja iliyopo ni kati ya washambuliaji WALIOPO ni nani ana tija zaidi.

3. Dube na Azam yake wameshacheza mechi 25 za ligi. Simba na akina Bocco, Kagere na Mugalu wana mechi 20 tu za ligi.
Litakua ni jambo la ajabu sana kushangaa watu wenye mechi tano mkononi kuzidiwa magoli mawili au moja na mtu aliyewatangulia mechi tano (dakika 450).
Tena hawa wenye mechi tano mkononi Wako kwenye ''timu yenye safu kali zaidi ya ushambuliaji'' katika ligi husika.

4. Kwa maneno mengine ni kwamba wewe unahoji credibility ya Gomes, mtu ambaye yuko mazoezini na wachezaji. Yeye na benchi la ufundi wanapokuja na kikosi kitakachokwenda kutekeleza mpangokazi uwanjani, Mugalu anaoangwa ''on merit'' sio kwa rushwa, uzuri wa sura, kujuana n.k.

NB: Naheshimu sana maoni yako, sifurahishwi na mshambuliaji (yeyote) kukosa magoli. Ila ninachoweza kukuhakikoshia ni kwamba Gomez atakukera sana msimu huu (Kama unakereka na chaguo lake kwenye eneo la mshambuliaji). Na ndio maana nikasema wewe na ''kocha mwenzio'' Gomez, mnatofautiana kwenye misingi (principles). Wewe uko sahihi, yeye yuko sahihi.
Gomez anafanya hivyo kwakuwa hana jinsi.
Nakuhakikishia, Mugalu ukiisha mkataba wake kama uchezaji wake utabaki huohuo wa kukaba badala ya kufunga magoli, basi utumishi wake Simba utaishia hapo.
Namaanisha jinsi Mugalu anavyocheza sasa hawezi kuongezewa mkataba hapa Simba.

Simba kwa sasa haihitaji sababu, au Mkabaji wapo wakabaji na Fraga anakuja kusaidia, Sumba inamhitaji mshambuliaji mahiri wa kufunga magoli.

Katika Mechi za Clab Bingwa nafasi moja ni muhimu sana.
Simba inahitaji mtumiaji sahihi wa nafasi hiyo moja, ambaye hayupo.

Kama Mugalu Mkabaji mzuri sawa tu kwakuwa Simba inahitaji mtu kama yeye pia.

Ila bado Simba kuna pengo la mfungaji mahiri, ndiye ninayemzungumzia hapa na sio Mugalu.
 
Hata tukimpima kwa takwimu za kufunga huyo Mugalu, sidhani takwimu zake ni mbaya sana. Leading scorer kwenye mashindano ya CAF ana magoli matatu, yeye anayo magoli mawili (pungufu ya goli moja). Sidhani kama hizi ni ''takwimu mbaya sana'' kama ambavyo unataka umma uamini.
Yaani huyo mwenye 3 angepata nafasi za Mugalu angekuwa na goli 8 sasa hivi.
 
View attachment 1749016
Umeongea vyema mkuu, sisi bado tuna mpila wa kukalili, hawa hawa kuna kipindi walikuwa wanamtukana sven kutokuchesesha double strikers, na tulibishana sana humu kuhusu modern football. Same mugalu aliyekuwa ana statistic nzuri first leg ya vital na merreick hawakutaka kuongea, wametafuta mechi ambayo statistic zimekataa ndio wanafanya kama case study yao. Good enough kagere alianza last match against Ahly, na mipila haikuwa inakaa mbele, baada ya kuingia mugalu mabeki wa ahly walirudi na timu nzima ikawa inacheza defensive game. Lakini kwa kuwa mugalu hakushinda hawawezi kuliongelea hilo.
Mkuu walio wengi mpira wanaangalia au kuuongelea Kwa mihemko Tu na sio uhalisia au inavotakiwa kuwa. Utajikuta unachoma calories za kutosha kujaribu kumuelewesha mtu kumbe mwenzako anabishana, maana kuna tofauti ya kueleweshana na kubishana, so watu wa kubishana sio watu wa kuchoma calories zako ata kama ni Kwa nia njema, Achana nae atakuja kuelewa mbele ya safari
 
Sio Ditram Nshimbi? Maana nimegundua hii maada inachangiwa pia na utopolo walioamua kujifanya mashabiki wa Simba.Shabiki wa Simba anaeitakia mafanikio,hawezi kutaka timu yake iridhike na mchezaji wa aina ya Mugalu.

Yani kwamba Mugalu anazuia mabeki kupanda kushambulia? Umesahau kazi ya Djuma kule Congo, ilivyosababisha Miqiusone arudi nyuma kumsaidia Zimbwe,huyo Mugalu alikuwa wapi?? Mshambukiaji akiwa sharp magoli lazima yapatikane kulingana na nafasi zinazotengenezwa . Nakumbuka ile Yanga ya Zahera iliyokuwa na viungo wabovu, ila kazi ya Makambo ilionekana, na ndie aliachangia wao kumaliza katika nafasi ya pili.

Hebu fikiria yule Makambo wa kipindi kile,ndo angekuwa kwenye timu inayotengeneza nafasi nyingi kama simba.

NB;Kiufupi Mugalu ni striker butu,acheni kumpamba ovyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante sana Mkuu.
Hapa tunazungumzia mshambuliaji mahiri, nafasi ambayo bado Simba haijapata mtu sahihi.
Mi nashindwa kuwaelewa kwamba wanampa sifa gani Mugalu.

Sifa ya mfungaji mahiri au ya Mkabaji mahiri.
Kama anapewa nafasi ya Mkabaji basi wakubali kwamba sio mshambuliaji.

Mi nazungumzia mshambiliaji stadi. Na sio Mkabaji.
Katika fani ya ushambuliaji huyu Mugalu ni Butu.
Hakuna cha kupepesa macho.
 
Siku akipoteza nafasi zaidi ya Tano kama zile alizopoteza wakati tunacheza na Merikh na As vita pale Taifa, kwenye Mechi muhimu ambazo tunahitaji ushindi Kisha tukafungwa na kutolewa ndo mtakuja kukubaliana na sisi humu.


Tena kwa hii hatua ya mtoano inayohitaji wingi wa magoli zaidi ya point 3 (robo na nusu fainali),eti ndo tumeenda ugenini tunapata nasafi za wazi zaidi ya Tano tunaziacha, kisa tuna "mshambukiaji mkabaji" tutakuja kupoteana humu. Ukweli usemwe Simba Sc kwasasa inahitaji mshambukiaji mahiri pale mbele, maana Si Mugalu wala Kagere wanaotosha wote ni viazi tu kwa Sasa ingawa nampa heshima yake Kagere kwa huduma yake tukufu pale Msimbazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Gomez anafanya hivyo kwakuwa hana jinsi.
Nakuhakikishia, Mugalu ukiisha mkataba wake kama uchezaji wake utabaki huohuo wa kukaba badala ya kufunga magoli, basi utumishi wake Simba utaishia hapo.
Namaanisha jinsi Mugalu anavyocheza sasa hawezi kuongezewa mkataba hapa Simba.

Simba kwa sasa haihitaji sababu, au Mkabaji wapo wakabaji na Fraga anakuja kusaidia, Sumba inamhitaji mshambuliaji mahiri wa kufunga magoli.

Katika Mechi za Clab Bingwa nafasi moja ni muhimu sana.
Simba inahitaji mtumiaji sahihi wa nafasi hiyo moja, ambaye hayupo.

Kama Mugalu Mkabaji mzuri sawa tu kwakuwa Simba inahitaji mtu kama yeye pia.

Ila bado Simba kuna pengo la mfungaji mahiri, ndiye ninayemzungumzia hapa na sio Mugalu.
Mkuu nilidhani tunazungumzia CURRENT SITUATION, kwamba kwa washambuliaji waliopo sasa hivi ni kwanini Mugalu anaanza over hao wengine. Hoja zangu zilijikita hapa.

Ila kama mjadala ulihusu mambo ya baada ya msimu kuisha nani abaki nani atafutiwe mbadala, hapo naungama na wewe kwamba tunatakiwa kutafita better option kwenye eneo la ushambuliaji kuliko hawa tulionao.

NB: Nina uhakika hiki sicho tulichokua tunakijadili hapa.
 
Hii lugha ya Mugalu kuwazuia mabeki wa timu pinzani wasipande sijui imetokea wapi!!
Mechi ya As Vita Vs Simba kule Congo Mugalu alikuepo na wing backs wa As Vita walikua wakipanda kushambulia akiwepo na yule beki wao kile kiandunje Shabani.
hii ni capatin wa vital akimwongelea mugalu kuhusu mechi yao ya kwanza.
 
Mkuu walio wengi mpira wanaangalia au kuuongelea Kwa mihemko Tu na sio uhalisia au inavotakiwa kuwa. Utajikuta unachoma calories za kutosha kujaribu kumuelewesha mtu kumbe mwenzako anabishana, maana kuna tofauti ya kueleweshana na kubishana, so watu wa kubishana sio watu wa kuchoma calories zako ata kama ni Kwa nia njema, Achana nae atakuja kuelewa mbele ya safari

Hii inaitwa from a layman's eye.
Wana kamsemo kao kwamba ''mpira wote tunauona''
Ipo tofauti ya kuona na kutambua.
Kuna watu wanafanya kazi ili mambo yaonekane vile yanavyoonekana.
Wadau wanaamini Mugalu anapendelewa na zile nafasi zinazopatikana ni kwa sababu yeye ana bahati kuliko Kagere na ndio maana kwenye hoja zao wanasema ''Kama zile nafasi ambazo anapata Mugalu, angepata Kagere basi tungeshinda magoli....''

Wanasahau kwamba kuna utaratibu wa kuzitengeneza hizo nafasi. Jamani katika mpira wa miguu, scoring chances are created, sasa hawa ndugu wanadhani kwamba MNAZAWADIWA.
 
Mkuu nilidhani tunazungumzia CURRENT SITUATION, kwamba kwa washambuliaji waliopo sasa hivi ni kwanini Mugalu anaanza over hao wengine. Hoja zangu zilijikita hapa.

Ila kama mjadala ulihusu mambo ya baada ya msimu kuisha nani abaki nani atafutiwe mbadala, hapo naungama na wewe kwamba tunatakiwa kutafita better option kwenye eneo la ushambuliaji kuliko hawa tulionao.

NB: Nina uhakika hiki sicho tulichokua tunakijadili hapa.
Hapa nime kopi na ku pest, hoja ya mtoa mada hii. Unaweza kuipitia hasa aya ya kwanza na ya tatu ya mtoa mada.

"Mimi ni shabiki wa mpira na mpira ninaujua kwa kuutazama na kuucheza uwanjani. Haiitaji elimu kubwa kugundua kuwa Chris Mugalu hafai na hastahili kuanza kikosi cha kwanza kulingana na kiwango chake hasa uwezo wake wa kufunga. Bahati nzuri kwake ni kuwa udhaifu wake unafichwa na ubora wa timu.

Na kwa bahati mbaya zaidi wachambuzi wengi wa soka hapa bongo wamekuwa na 'upofu' katika uchambuzi. Analysis zao nyingi zina base kwenye matokeo. Mfano, hata kama timu ikicheza ovyo kwa dk zote 89, ila ikapata goli na kushinda dakika ya 90..Basi tegemea analyis positive kutoka kwa wachambuzi wetu.. Vice versa is true.

Vivyo hivyo kwenye swala la Mugalu, wachambuzi wetu hawajui chochote kuhusu soka. Hata uchambuzi wao juu ya viwango vya wachezaji umemezwa na matokeo ya timu. Wengi utawasikia kuwa Mugalu ni striker mwenye uwezo wa kuhold mpira na kufungua nafasi kwa wengine. Hawazungumzii kabisa ubutu wake golini.

Na mbaya zaidi wachambuzi karibu wote wana copy na kupaste opinions zao zinafanana. Katika kipindi hiki, huwezi kuta wachambuzi wanajadili weaknesses za Mugalu, badala yake wanaelezea umuhimu wake na faida yake kule mbele.Najiuliza, Hivi kama hafungi, ana umuhimu gani sasa wa kuanza?, na je kama timu isingekuwa inapata matokeo na bado Mugalu angekuwa anapoteza zile nafasi, bado wasingemuelezea udhaifu wake?...Jibu ni rahisi tu, wana chambua kulingana na matokeo.

Mfano wa pili, ni Jonas Mkude. Kwa mtu anaejua mpira na aliyeangalia ile game, ilikuwa sio rahisi kuamini kama Mkude angerudi uwanjani second half..Alikuwa flopy sana siku ile.

Cha ajabu timu imepata matokeo kwenye comments unasikia uchambuzi kuwa Mkude alifanya majukumu yake vizuri na aliiunganisha vizuri sana safu ya ulinzi na ushambuliaji..Hivi ni mkude huyu huyu aliyekuwa na pass accuracy mbovu kuliko wachezaji wote wa simba siku hiyo? Ina maana wachambuzi hamuoni udhaifu wa wachezaji kisa tu timu imepata matokeo?

Basi kama ni hivyo, hakuna kazi rahisi kama kucwa mchambuzi wa soka bongo."
 
Sio Ditram Nshimbi? Maana nimegundua hii maada inachangiwa pia na utopolo walioamua kujifanya mashabiki wa Simba.Shabiki wa Simba anaeitakia mafanikio,hawezi kutaka timu yake iridhike na mchezaji wa aina ya Mugalu.

Yani kwamba Mugalu anazuia mabeki kupanda kushambulia? Umesahau kazi ya Djuma kule Congo, ilivyosababisha Miqiusone arudi nyuma kumsaidia Zimbwe,huyo Mugalu alikuwa wapi?? Mshambukiaji akiwa sharp magoli lazima yapatikane kulingana na nafasi zinazotengenezwa . Nakumbuka ile Yanga ya Zahera iliyokuwa na viungo wabovu, ila kazi ya Makambo ilionekana, na ndie aliachangia wao kumaliza katika nafasi ya pili.

Hebu fikiria yule Makambo wa kipindi kile,ndo angekuwa kwenye timu inayotengeneza nafasi nyingi kama simba.

NB;Kiufupi Mugalu ni striker butu,acheni kumpamba ovyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
sawa
 
Back
Top Bottom