Suala la Salim Kikeke kuhamia EFM na akili za watanzania

Suala la Salim Kikeke kuhamia EFM na akili za watanzania

Watu huwa tunaajiriwa kwa ajili ya mambo matatu.
Kujikimu kimaisha, kuongeza ujuzi au maarifa ya kitu Fulani na kutafuta connection. Tatizo la watanzania tulio wengi tunaajiriwa kwa ajili ya kujikimu kimaisha hivyo hudhani kila aliyeajiriwa lengo lake ni hilo. Tukumbuke Salim kikeke ameishi kwenye hii tasnia kwa muda mrefu ila amehudumia media za kimataifa hivyo kama atahitaji kuwekeza kwenye media za nyumbani huwenda asiendane na soko letu. Hivyo kulazimika kufanya kazi katika media za nyumbani ili kujifunza ni namna gani media zetu zinavyoendeshwa. Au kuna mambo anahitaji kuyafanya hivyo kufanya kazi EFM ikawa ni moja ya njia anayotumia kufanikishia.
N.b Haya ni mawazo yangu tu
Kama ni hivyo basi ni jambo la heri.
 
Nimeona jinsi watu wanavyomshambulia Kikeke kwenye akaunti zake za kijamii kwa uamuzi wake wa kujiunga na kituo cha matangazo cha E-fm.

Nimebaki kuajabia tabia ya watanzania. Maisha ni yake, uamuzi ni wake cha ajabu anatukanwa na kudhalilishwa na wachangiaji juu ya uamuzi wake huo.

Tanzania ni taifa la watu wa hovyo sijapata kuona.
Hapana watanzania siyo wa hovyo ila wameshangaa, Walitegemea kusikia amekuwa msemaji wa Serikali au msema wa Young Africa [emoji23][emoji23][emoji23], Ni sawa na Victor osimhen aondoke timu yake ya Napoli aje kuchezea Sigida big star.
 
Tz ina watu wenye mitazamo ya hovyo sana.
Hapana mkuu Tanzania tunampenda na tunapenda tuendelee kumuona kimataifa mfano alitakiwa aende CNN, Al-Jazeera, yani aendelee kucheza kwe ligi yake, Ndiyo maana Samata alivyoondoka Astoni villa watanzania tulikasirika tulitamani aendelee kuwepo Uingereza ili tuwe tunamuona kila wiki kwenye TV ndiyo maana alivyoondoka watanzania tukaanza kuihama timu kwa asila.
 
Umaarufu una gharama zake, na gharama zenyewe ni pamoja na hii kupangiwa uishi maisha gani na watu ambao hata huwajui....
Ni kweli umaarufu ni shida, Ray c alikuwa ana hojiwa akasema kuna kipindi alifuria mpaka akawa ana panda usafiri wa umma na kabla ya kupanda alikua ana jificha uso ili abiria wasimuone.
 
Hapana mkuu Tanzania tunampenda na tunapenda tuendelee kumuona kimataifa mfano alitakiwa aende CNN, Al-Jazeera, yani aendelee kucheza kwe ligi yake, Ndiyo maana Samata alivyoondoka Astoni villa watanzania tulikasirika tulitamani aendelee kuwepo Uingereza ili tuwe tunamuona kila wiki kwenye TV ndiyo maana alivyoondoka watanzania tukaanza kuihama timu kwa asila.
Sidhani kama ni sahihi
 
Amekaa sana BBC ni wakati wa kuwa na kitu chake mwenyewe sasa tusubiri ni suala la muda tu.Pia amekaa sana kwenye utangazaji habari Kuna haja ya kubadili upepo kidogo.
 
@Dr Rutegarwera
Naam namie nimeliona hili jambo nikaona nitie neno.

Bila shaka linaashiiria tabia za watanzania. Tupe picha tu mengine tulijijazia .

Lakini muhimu zaidi cha kujifunza ni kipi?



Jitihada za elimu hazijasaidia watanzania wengi ambao bado wapo kwenye giza tororo la ufahamu. Kwamaana hiyo uwezo wetu wa kuchakata mambo na msimamo wa maisha ni mepesi ajabu.

Mapungufu ya Radio zetu Tanzania ni makubwa kiasi kwamba ndugu yetu salim kutaka kujiunga baada ya kujijejngea brand kubwa kumewachanganya na kuwashangaza wadau wa habari

Bila shaka wanaosimamia maudhui TCRA wanafahamu hilo na ama wanapuuza au wnaaacha maudhui ya ohvyo yapite kwa kuwa hali hiyo inasaidia kulinda maslahi ya mabwana wakubwa-huwezi kuhoji utawala bora ikiwa kila kukicha redio na TV inajadili mahusiano na wanahabari ndio wanenguaji wakuu na machawa

Ripoti zetu nyingi bila shaka hazihaririwi ili kuhakiki. Michezo ndio kwenyewe ni simba na Yanga tuu

Ndugu yetu Salim ni brand kubwa kuliko karibia redio na TV zote ndani ya nchi -ni muda sasa wa vyombo vyetu hivi kujitafakari ama wabaki kama walivyo au wabadilike
 
Inaweza kuwa alikua analipwa pesa ndogo BBC na labda ndio sababu ya kuacha. Sio watangazaji wote wa BBC wanalipwa mishahara mikubwa, kuna mambo walio mle ndani ndio wanayajua.

Kuna hata mwingine alishakua head wa hiyo idhaa ya kiswahili lakini sasa anafanya Azam media. Hii inathibitisha kuwa hawalipwi mishahara mikubwa kama tunavyodhani
Gharama za Maisha Ulaya ziko juu we fikiria Mpk kumiliki tv unalipia Kodi(nilimsikia Zuhura Yunus akisema)wakati huku kwetu ukiwa mjana utalipa inderect tax zile za lazima zingine zitakupita!!
 
Back
Top Bottom