Suala la VPN walengwa ni wapinzani, watumia VPN kuepuka gharama za mabando na kucheki mambo binafsi ondoeni hofu

Hiyo VPN ungetupa jina kwani TCRA wangekumania mbona umeachia hewani.
 
lakini pia kuna watu ndani ya hii nchi wanafikiri watalalamika milele! Kisa tu kutoridhika kwao, na uchu wa kunung'unika kuliko pitiliza.

Wanasahau kuna siku wao na watoto wao, malalamiko yao, Marafiki zao, shemeji zao, michepuko yao, wakulu zao, wenza wao, nk wata rest in peace.

Na nchi itaendelea kubakia daima na milele.....
 
Binafsi naona Trubo sio kwa ajili ya kusave bundle lako
 
Hakuna vpn itakayokusaidia kutumia internet bure vpn ipo kwaajili ya kuzifungua zile site zinazokuwa zimefungwa na serikali
Hii ya sites zilizofungwa inafahamika mkuu, lakini inaonekana kuna wadau wana utaalam wa hili la bundle pia
 
Ule mtandao wa Tanzania yetu VPN yake bado inapiga kazi?
Nilitafuta laini zao mpk nikachoka, nikaamua niachane nao tu.
Kama unazungumzia mtandao wa rangi ya alizeti laini zao niliendaga ofisi za kijito-meat zilikuwepo ingawa mtaani ni adimu. Nilishawahi endaga ofisi za UDSM wakasema Magomeni ambako nilikosa pia, nikaamua niende huko.
 
Bwana yule alitangulia ila waliobakia hai bado wanajitia upofu,kipindi cha utawala wake zilipitishwa sana sheria nyingi za hovyo ikiwemo hii ya kuwaminya watumiaji wa VPN.
 
Kuna vpn kama Ha tunnel na V2ray huwa zinatumika kutumia internet bure, kuna mwanafunzi nilikuwa namuona anajisomea sana kwa video tutorials nikaja gundua anatumia bure, hana uwezo wa kulipia bando kusomea mtandaoni.
Hawa sasa ndio TRA wanawatafuta, wanapunguza ukusanyaji wa mapato
 
KWAMBA KATAZO HILI NI KUMJULISHA MAMA WATU WANAFANYA KAZI, NA AWAKUMBUKE KWENYE UTEUZI?
AU NDIO KUJIHAMI NA UCHAGUZI UJAO BAADA YA WATU KUCHOSHWA, NA KAZI IENDELEE?

HIVI TTCL BADO IPO?
 
Kutumia vpn kunaongizaje hasara kampuni za simu wakati data zao zinakuwa hazijatumika?
Kumbe ndio maana serikali ilikataa Musk kuweka internet mbadala kuondoa ukiritimba wa hii mitandao.
 
Kutumia vpn kunaongizaje hasara kampuni za simu wakati data zao zinakuwa hazijatumika?
Kumbe ndio maana serikali ilikataa Musk kuweka internet mbadala kuondoa ukiritimba wa hii mitandao.
Mkuu una ufahamu wowote kuhusu VPN. Tunnel ?

Ni application ambazo unaweza kutumia payload au SSH kupata huduma ya Internet bute bila kutoa Thumni sasa mkuu unapochepusha Matumizi ambayo ungepaswa ununue unafikiri wale wanaongeza kipi?

watakuwa wanatumia fedha nyingu kuendesha kampuni while kuna watu wanatumia minala yao bila kulipia huku wakipata Private gain..

Ila kwenye Hizi Tunnel wahanga wakubwa ni TTCL na Airtel, Tigo sio sana cuz wanatoa Slow speed..
Ila TTCL unaweza kutumia Mpaka 1TB kwa mwezi..

Ila bora wapigww kitu kizito maana na wenyewe wamezidi kutapeli Aisee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…