THK DJAYZZ
JF-Expert Member
- Sep 14, 2011
- 2,166
- 175
Stress za uchaguzi mbaya sanaSuala hili lipigwe vita vikali sana kwa sababu ni sherehe tu ndio inayo namna ya kupika ili waliokuja kwenye hiyo shughuli wapate kula.
Haiwezekani umefiwa na kipenzi chako alafu hapo hapo unawapikia wanaokuja kumzika wale washibe waende zao.
Huyu ni selfish individual tu..Stress za uchaguzi mbaya sana
Yaani utakuta mmeuguza ndugu yenu zaidi ya miezi 3 hospitali. Tena mmeuza kila kitu ili kuweza kugharamia gharama za matibabu na mwisho wa siku Mungu ana twaa kiumbe chake...Halafu kuna mijitu inashinda msibani kuanzia asubuhi hadi usiku yupo tu na anakula chakula bila kuchangia hata senti eti anamfariji mfiwa, wengine wanalalamika msibani unakuta nyumba imejaa watu wanalala sebuleni, vyumbani hadi nje.
Ni utaratibu wa kipuuzi sana, wanatakiwa wabaki watu wachache wa karibu wasiozidi kumi.
Siumeona hapo mablack ndio wamemkimbilia kwa kumfariji. Sio kwamba wamemkimbilia mikono mitupu wakisubiri msosi tu!Mkuu chakula msibani ni mila ya kiafrika na ipo karne nyingi.
Kimsingi wafiwa wao hawapiki wao wenyewe kwa ajili ya msiba bali jamii inayo mzunguka mfiwa.
Nia ya mila hii ni kuwapunguzia wafiwa ukiwa na kuufanya msiba uwe wa jamii nzima.
Ukiitazama juujuu utafikiri msiba na kulisha waombolezaji ni jukumu la mfiwa, la hasha.
Tatizo linakuja pale mfiwa akiwa hana uhusiano mzuri na jamii inayomzunguka au hahudhurii misiba ya jamii yake.
Hapo mfiwa anaipata fresh.
Mila ya kuwapa waombolezaji chakula kabla ya mazishi ina ujumbe mzito zaidi. Kulisha watu ni kuwatakia heri ili maendeleo kimaisha yasikome, ni kama aliyefariki anawatakia heri wale waliobaki.
Huko Ulaya kuna jamaa yangu akiwa jirani na mzungu mmoja, apartment mlango huu unafuatana na mlango wake.
Kuna siku akapita jioni akitoka mishe zake akaona mlango wa jirani mzungu uko wazi na macho hayana pazia, kwenye kiti akamwona mke wa jirani yake kawasha mshumaa anaitazama picha ya mumewe huku machozi yakimtiririka.
Taratibu jamaa akaingia na kumuuliza mke wa jirani yake kulikoni?
Yule mama akamjibu kuwa mumewe amefariki mchana ule na hajui afanye nini maana amechanganyikiwa.
Huyu jamaa yangu akashituka, na akasikitika sana.
Lakini haraka akawaita waTanzania marafiki waliokuwa karibu.
Wakanunua vyakula na vinywaji na wakampa kampani yule mama hadi mazishi yalipofanyika.
Wazungu walioshiriki walikuwa wachache sana lakini waafrika walikuwa wengi.
Yule mama mfiwa kwa kweli alichangamka. Na baadaye alikiri kuwa waafrika wana moyo wa pekee duniani maana alikiri vile vile kuwa siku ile aliyomkuta akilia peke yake alikuwa akihisi kuchanganyikiwa na kutaka kujiua!
Alishukuru sana kwa kusaidia kubeba mzigo wa stress na kusema kuwepo kwao kulikuwa faraja kubwa.
Huu ni mfano ambao unaoonyesha jinsi sisi waafrika tumejaaliwa na Muumba namnaya kukabili misiba inayoleta matatizo makubwa kifikra kwa wafiwa.
Hizi ni taratibu za kabila la wajaluo. Mfiwa unawaandalia chakula wageni na kuwakaribishaSuala hili lipigwe vita vikali sana kwa sababu ni sherehe tu ndio inayo namna ya kupika ili waliokuja kwenye hiyo shughuli wapate kula.
Haiwezekani umefiwa na kipenzi chako alafu hapo hapo unawapikia wanaokuja kumzika wale washibe waende zao.
Wale wanaokuja kukupa pole na kuzika ndo wakupe chakula cha wewe kula kwa sababu umepatwa na msiba,umeshughulishwa na kuondoka kipenzi chako alafu inakuwaje uwaze kuwapikia wanaokuja kkuzika,hiyo sio sherehe.
Mtu anatoka nyumba ya pili tu hapo alafu anataka kuja kula kwako uliyefiwa haoni haya kabisa.
Nilishatangaza nyumbani kuwa nikifiwa na mtu aliyeko ndani ya mamlaka yangu chakula ni kwa ajili ya familia tu kama kawaida na wale wageni wa mbali ambao hata bila msiba wangepikiwa na sio vinginevyo.
Ndugu wengi wakimaliza maziko wanabaki na madeni yasiyo ya lazima kwa sababu ya kutimiza utaratibu waliokuta katika jamii licha ya kuwa unawaumiza utaratibu huo lakini wamo tu.
Mfiwa kupika chakula ni sawa na mwenye sherehe kupika chakula
,kama kweli wameguswa na msiba wako wao ndo wakuletee chakula wewe msibiwa.
Mungu aliyetuumba waafrika alitupa karama maalum ambayo wengine hawana.Siumeona hapo mablack ndio wamemkimbilia kwa kumfariji. Sio kwamba wamemkimbilia mikono mitupu wakisubiri msosi tu!
Uzi wangu unasema suala la wafiwa kuandaa chakula..
Wafiwa ni wale ndugu wa karibu wa marehemu.
Kwa hiyo nilichokusudia ni kuwa hawa wafiwa kuandaa chakula kwa ajili ya wanaokuja kuzika ndio ipigwe vita.
Hiyo ni tofauti na hawa wazikaji wakajichanga wakanunua chakula wakapika pale kwa marehemu kwa gharama zaoo hili halina tatizo na ndio jambo linaloendana na ustaarabu na huruma sana.
Wewe ndo ulichogusia,ama suala la wafiwa kuandaa gharama zote za chakula si suala ovu mno.
Vipi kuhusu ndugu wanaokuja kukuhani halafu wanaomba nauli ya kurudi kwao na hela ya kurudisha deni la nauli ya kujiaSuala hili lipigwe vita vikali sana kwa sababu ni sherehe tu ndio inayo namna ya kupika ili waliokuja kwenye hiyo shughuli wapate kula.
Haiwezekani umefiwa na kipenzi chako alafu hapo hapo unawapikia wanaokuja kumzika wale washibe waende zao.
Wale wanaokuja kukupa pole na kuzika ndo wakupe chakula cha wewe kula kwa sababu umepatwa na msiba,umeshughulishwa na kuondoka kipenzi chako alafu inakuwaje uwaze kuwapikia wanaokuja kkuzika,hiyo sio sherehe.
Mtu anatoka nyumba ya pili tu hapo alafu anataka kuja kula kwako uliyefiwa haoni haya kabisa.
Nilishatangaza nyumbani kuwa nikifiwa na mtu aliyeko ndani ya mamlaka yangu chakula ni kwa ajili ya familia tu kama kawaida na wale wageni wa mbali ambao hata bila msiba wangepikiwa na sio vinginevyo.
Ndugu wengi wakimaliza maziko wanabaki na madeni yasiyo ya lazima kwa sababu ya kutimiza utaratibu waliokuta katika jamii licha ya kuwa unawaumiza utaratibu huo lakini wamo tu.
Mfiwa kupika chakula ni sawa na mwenye sherehe kupika chakula
,kama kweli wameguswa na msiba wako wao ndo wakuletee chakula wewe msibiwa.
Sikopi aisee, wachangishane wajipikie chakulaYaani utakuta mmeuguza ndugu yenu zaidi ya miezi 3 hospitali. Tena mmeuza kila kitu ili kuweza kugharamia gharama za matibabu na mwisho wa siku Mungu ana twaa kiumbe chake...
Leo hii uanzee kukopa ili uwalishe watu wanaokuja kuzika.
Mungu akusaidie yasikufike kwa Umri huo. Huwezi kuwa na familia uwaze kuhusu vyakula kuliko mpendwa wako ulopoteza.Suala hili lipigwe vita vikali sana kwa sababu ni sherehe tu ndio inayo namna ya kupika ili waliokuja kwenye hiyo shughuli wapate kula.
Haiwezekani umefiwa na kipenzi chako alafu hapo hapo unawapikia wanaokuja kumzika wale washibe waende zao.
Wale wanaokuja kukupa pole na kuzika ndo wakupe chakula cha wewe kula kwa sababu umepatwa na msiba,umeshughulishwa na kuondoka kipenzi chako alafu inakuwaje uwaze kuwapikia wanaokuja kkuzika,hiyo sio sherehe.
Mtu anatoka nyumba ya pili tu hapo alafu anataka kuja kula kwako uliyefiwa haoni haya kabisa.
Nilishatangaza nyumbani kuwa nikifiwa na mtu aliyeko ndani ya mamlaka yangu chakula ni kwa ajili ya familia tu kama kawaida na wale wageni wa mbali ambao hata bila msiba wangepikiwa na sio vinginevyo.
Ndugu wengi wakimaliza maziko wanabaki na madeni yasiyo ya lazima kwa sababu ya kutimiza utaratibu waliokuta katika jamii licha ya kuwa unawaumiza utaratibu huo lakini wamo tu.
Mfiwa kupika chakula ni sawa na mwenye sherehe kupika chakula
,kama kweli wameguswa na msiba wako wao ndo wakuletee chakula wewe msibiwa.
siku hizi kuna hadi vyama vya kuzikana huyu jamaa sijui anakwama wapiNi kweli kabisa msiba na Arobain kunakuwa na madeni mengi.
Nimewahi kuona kwenye shughuli kama hizo wahusika wananunua maji ya katoni mengi sana, wanakodi viti, tent, maturubai. Usipo changa kwenye hiyo shughuli kama mwana Family au ukoo Ni ugovi mkubwa.
Shughuli inaishi Kuna madeni makubwa
Uaitafute justification mkuu.Mungu akusaidie yasikufike kwa Umri huo. Huwezi kuwa na familia uwaze kuhusu vyakula kuliko mpendwa wako ulopoteza.
Hujajua utu ni nini jifunze upendo na ukemee roho ya Uchoyo.
Hao ni watu wakuelimishwa kuwa kama hawakuwa na uwezo wa kuja haikuwa na ulazima wa wao kuja kwa sababu kuja kwao haina maana kuwa marehemu atafufuka.Vipi kuhusu ndugu wanaokuja kukuhani halafu wanaomba nauli ya kurudi kwao na hela ya kurudisha deni la nauli ya kujia