Suala la wafiwa kuandaa chakula kwa ajili ya wanaokuja kuzika ni utaratibu wa kupigwa vita

Suala la wafiwa kuandaa chakula kwa ajili ya wanaokuja kuzika ni utaratibu wa kupigwa vita

Suala hili lipigwe vita vikali sana kwa sababu ni sherehe tu ndio inayo namna ya kupika ili waliokuja kwenye hiyo shughuli wapate kula.

Haiwezekani umefiwa na kipenzi chako alafu hapo hapo unawapikia wanaokuja kumzika wale washibe waende zao.
Stress za uchaguzi mbaya sana
 
Mkuu uko sehemu gani ya nchi!? Ambako wafiwa wanapika!?

Si vibaya nikifahamu la kabila lako.

Duh.. Hatari kweli.
 
Halafu kuna mijitu inashinda msibani kuanzia asubuhi hadi usiku yupo tu na anakula chakula bila kuchangia hata senti eti anamfariji mfiwa, wengine wanalalamika msibani unakuta nyumba imejaa watu wanalala sebuleni, vyumbani hadi nje.
Ni utaratibu wa kipuuzi sana, wanatakiwa wabaki watu wachache wa karibu wasiozidi kumi.
Yaani utakuta mmeuguza ndugu yenu zaidi ya miezi 3 hospitali. Tena mmeuza kila kitu ili kuweza kugharamia gharama za matibabu na mwisho wa siku Mungu ana twaa kiumbe chake...
Leo hii uanzee kukopa ili uwalishe watu wanaokuja kuzika.
 
Mkuu chakula msibani ni mila ya kiafrika na ipo karne nyingi.
Kimsingi wafiwa wao hawapiki wao wenyewe kwa ajili ya msiba bali jamii inayo mzunguka mfiwa.
Nia ya mila hii ni kuwapunguzia wafiwa ukiwa na kuufanya msiba uwe wa jamii nzima.

Ukiitazama juujuu utafikiri msiba na kulisha waombolezaji ni jukumu la mfiwa, la hasha.
Tatizo linakuja pale mfiwa akiwa hana uhusiano mzuri na jamii inayomzunguka au hahudhurii misiba ya jamii yake.
Hapo mfiwa anaipata fresh.

Mila ya kuwapa waombolezaji chakula kabla ya mazishi ina ujumbe mzito zaidi. Kulisha watu ni kuwatakia heri ili maendeleo kimaisha yasikome, ni kama aliyefariki anawatakia heri wale waliobaki.

Huko Ulaya kuna jamaa yangu akiwa jirani na mzungu mmoja, apartment mlango huu unafuatana na mlango wake.

Kuna siku akapita jioni akitoka mishe zake akaona mlango wa jirani mzungu uko wazi na macho hayana pazia, kwenye kiti akamwona mke wa jirani yake kawasha mshumaa anaitazama picha ya mumewe huku machozi yakimtiririka.
Taratibu jamaa akaingia na kumuuliza mke wa jirani yake kulikoni?

Yule mama akamjibu kuwa mumewe amefariki mchana ule na hajui afanye nini maana amechanganyikiwa.
Huyu jamaa yangu akashituka, na akasikitika sana.
Lakini haraka akawaita waTanzania marafiki waliokuwa karibu.
Wakanunua vyakula na vinywaji na wakampa kampani yule mama hadi mazishi yalipofanyika.
Wazungu walioshiriki walikuwa wachache sana lakini waafrika walikuwa wengi.

Yule mama mfiwa kwa kweli alichangamka. Na baadaye alikiri kuwa waafrika wana moyo wa pekee duniani maana alikiri vile vile kuwa siku ile aliyomkuta akilia peke yake alikuwa akihisi kuchanganyikiwa na kutaka kujiua!
Alishukuru sana kwa kusaidia kubeba mzigo wa stress na kusema kuwepo kwao kulikuwa faraja kubwa.

Huu ni mfano ambao unaoonyesha jinsi sisi waafrika tumejaaliwa na Muumba namnaya kukabili misiba inayoleta matatizo makubwa kifikra kwa wafiwa.
Siumeona hapo mablack ndio wamemkimbilia kwa kumfariji. Sio kwamba wamemkimbilia mikono mitupu wakisubiri msosi tu!
 
Suala hili lipigwe vita vikali sana kwa sababu ni sherehe tu ndio inayo namna ya kupika ili waliokuja kwenye hiyo shughuli wapate kula.

Haiwezekani umefiwa na kipenzi chako alafu hapo hapo unawapikia wanaokuja kumzika wale washibe waende zao.

Wale wanaokuja kukupa pole na kuzika ndo wakupe chakula cha wewe kula kwa sababu umepatwa na msiba,umeshughulishwa na kuondoka kipenzi chako alafu inakuwaje uwaze kuwapikia wanaokuja kkuzika,hiyo sio sherehe.

Mtu anatoka nyumba ya pili tu hapo alafu anataka kuja kula kwako uliyefiwa haoni haya kabisa.

Nilishatangaza nyumbani kuwa nikifiwa na mtu aliyeko ndani ya mamlaka yangu chakula ni kwa ajili ya familia tu kama kawaida na wale wageni wa mbali ambao hata bila msiba wangepikiwa na sio vinginevyo.

Ndugu wengi wakimaliza maziko wanabaki na madeni yasiyo ya lazima kwa sababu ya kutimiza utaratibu waliokuta katika jamii licha ya kuwa unawaumiza utaratibu huo lakini wamo tu.

Mfiwa kupika chakula ni sawa na mwenye sherehe kupika chakula

,kama kweli wameguswa na msiba wako wao ndo wakuletee chakula wewe msibiwa.
Hizi ni taratibu za kabila la wajaluo. Mfiwa unawaandalia chakula wageni na kuwakaribisha
 
Mkuu misiba ya kwetu waafrika inajiendesha yenyewe.
We ni kutangaza tu kwamba umefiwa.
Tatizo pale wewe usipohudhuria misiba ya wengine katika jamii.
Uzi wangu unasema suala la wafiwa kuandaa chakula..

Wafiwa ni wale ndugu wa karibu wa marehemu.


Kwa hiyo nilichokusudia ni kuwa hawa wafiwa kuandaa chakula kwa ajili ya wanaokuja kuzika ndio ipigwe vita.

Hiyo ni tofauti na hawa wazikaji wakajichanga wakanunua chakula wakapika pale kwa marehemu kwa gharama zaoo hili halina tatizo na ndio jambo linaloendana na ustaarabu na huruma sana.

Wewe ndo ulichogusia,ama suala la wafiwa kuandaa gharama zote za chakula si suala ovu mno.
 
Suala hili lipigwe vita vikali sana kwa sababu ni sherehe tu ndio inayo namna ya kupika ili waliokuja kwenye hiyo shughuli wapate kula.

Haiwezekani umefiwa na kipenzi chako alafu hapo hapo unawapikia wanaokuja kumzika wale washibe waende zao.

Wale wanaokuja kukupa pole na kuzika ndo wakupe chakula cha wewe kula kwa sababu umepatwa na msiba,umeshughulishwa na kuondoka kipenzi chako alafu inakuwaje uwaze kuwapikia wanaokuja kkuzika,hiyo sio sherehe.

Mtu anatoka nyumba ya pili tu hapo alafu anataka kuja kula kwako uliyefiwa haoni haya kabisa.

Nilishatangaza nyumbani kuwa nikifiwa na mtu aliyeko ndani ya mamlaka yangu chakula ni kwa ajili ya familia tu kama kawaida na wale wageni wa mbali ambao hata bila msiba wangepikiwa na sio vinginevyo.

Ndugu wengi wakimaliza maziko wanabaki na madeni yasiyo ya lazima kwa sababu ya kutimiza utaratibu waliokuta katika jamii licha ya kuwa unawaumiza utaratibu huo lakini wamo tu.

Mfiwa kupika chakula ni sawa na mwenye sherehe kupika chakula

,kama kweli wameguswa na msiba wako wao ndo wakuletee chakula wewe msibiwa.
Vipi kuhusu ndugu wanaokuja kukuhani halafu wanaomba nauli ya kurudi kwao na hela ya kurudisha deni la nauli ya kujia
 
Nilivyokua mdogo kuna ndugu yangu alifiwa na mtoto, Baada ya kuzika tu kesho yake akaitisha kikao kuwaambia wale ndugu kuwa
"Sasa msiba umeisha tawanyikeni hamna haja ya kuendelea kuwepo hapa"

Utoto wangu ulinifanya nimtafsiri alikua na roho mbaya ila Sasa nimekua na nimeelewa jamaa alikua sawa
 
Misiba mingi watu huwa wanachangia ama pesa au chakula kwa kiasi kikubwa, na ndio hutumika kulisha waliokuja msibani. Hujawahi kusikia mfiwa anakoshwa kwa mahanjumati na nguo. Na panapo msiba uwepo wa watu nao unasaidia kumpa mfiwa faraja sasa unataka watu waje wazike tu then waondoke basi hata wasiwape compay wafiwa. Ila pia kama familia ina uwezo sio mbaya kulisha watu wakiokuja msibani mana inakuwa ni sadaka pia ya marehemu
 
Yaani utakuta mmeuguza ndugu yenu zaidi ya miezi 3 hospitali. Tena mmeuza kila kitu ili kuweza kugharamia gharama za matibabu na mwisho wa siku Mungu ana twaa kiumbe chake...
Leo hii uanzee kukopa ili uwalishe watu wanaokuja kuzika.
Sikopi aisee, wachangishane wajipikie chakula
 
Suala hili lipigwe vita vikali sana kwa sababu ni sherehe tu ndio inayo namna ya kupika ili waliokuja kwenye hiyo shughuli wapate kula.

Haiwezekani umefiwa na kipenzi chako alafu hapo hapo unawapikia wanaokuja kumzika wale washibe waende zao.

Wale wanaokuja kukupa pole na kuzika ndo wakupe chakula cha wewe kula kwa sababu umepatwa na msiba,umeshughulishwa na kuondoka kipenzi chako alafu inakuwaje uwaze kuwapikia wanaokuja kkuzika,hiyo sio sherehe.

Mtu anatoka nyumba ya pili tu hapo alafu anataka kuja kula kwako uliyefiwa haoni haya kabisa.

Nilishatangaza nyumbani kuwa nikifiwa na mtu aliyeko ndani ya mamlaka yangu chakula ni kwa ajili ya familia tu kama kawaida na wale wageni wa mbali ambao hata bila msiba wangepikiwa na sio vinginevyo.

Ndugu wengi wakimaliza maziko wanabaki na madeni yasiyo ya lazima kwa sababu ya kutimiza utaratibu waliokuta katika jamii licha ya kuwa unawaumiza utaratibu huo lakini wamo tu.

Mfiwa kupika chakula ni sawa na mwenye sherehe kupika chakula

,kama kweli wameguswa na msiba wako wao ndo wakuletee chakula wewe msibiwa.
Mungu akusaidie yasikufike kwa Umri huo. Huwezi kuwa na familia uwaze kuhusu vyakula kuliko mpendwa wako ulopoteza.

Hujajua utu ni nini jifunze upendo na ukemee roho ya Uchoyo.
 
Kijjiiini kwetu huo utaratibu haupo. Mnazika mnapewa matangazo ya utaratibu wa kunawa maji Ni lini na kutandua matanga Ni lini..then mnasepa. Kula Ni lazima pale mtu/watu wanapokuja kuhani msiba(baada ya mazishi) na Mara nying wamama wanakujaga na vyakula kwenye mafurushi yao (raw food Kama unga, maharage etc) kwa ajili ya kulisha watu msibani na wababa Mara nyingi huacha rambi rambi kwnye sahani husika pale msibani.
 
Ni kweli kabisa msiba na Arobain kunakuwa na madeni mengi.

Nimewahi kuona kwenye shughuli kama hizo wahusika wananunua maji ya katoni mengi sana, wanakodi viti, tent, maturubai. Usipo changa kwenye hiyo shughuli kama mwana Family au ukoo Ni ugovi mkubwa.

Shughuli inaishi Kuna madeni makubwa
 
Ni kweli kabisa msiba na Arobain kunakuwa na madeni mengi.

Nimewahi kuona kwenye shughuli kama hizo wahusika wananunua maji ya katoni mengi sana, wanakodi viti, tent, maturubai. Usipo changa kwenye hiyo shughuli kama mwana Family au ukoo Ni ugovi mkubwa.

Shughuli inaishi Kuna madeni makubwa
siku hizi kuna hadi vyama vya kuzikana huyu jamaa sijui anakwama wapi
 
Mungu akusaidie yasikufike kwa Umri huo. Huwezi kuwa na familia uwaze kuhusu vyakula kuliko mpendwa wako ulopoteza.

Hujajua utu ni nini jifunze upendo na ukemee roho ya Uchoyo.
Uaitafute justification mkuu.

Hili jambo hata watu wazima waliotuzidi umri mimi na wewe,tena wana familia nabwenye kutambua utu linawatesa hasa wale ambao katika jamii zao mtu akifiwa ndo huyo huyo anaachiwa majukumu yote ya kuandaa chakula na hharama mbali mbali.

Alafu mkuu inakuwaje mtu kafiwa asipopika chakula uanze kumlaumu mchoyo ?

Ina maana huoni kama kafikwa na jambo zito kiasi kwamba umpe udhuru kuwa ilikuwa haki asipike ?

Huoni kama huo ni ulafi kutaka msibani wafiwa wapike ili ule wewe ?
 
Vipi kuhusu ndugu wanaokuja kukuhani halafu wanaomba nauli ya kurudi kwao na hela ya kurudisha deni la nauli ya kujia
Hao ni watu wakuelimishwa kuwa kama hawakuwa na uwezo wa kuja haikuwa na ulazima wa wao kuja kwa sababu kuja kwao haina maana kuwa marehemu atafufuka.

Sasa kwa wao kuja na madeni wanaongeza msiba wa pili huo.

Kiubinadamu wafiwa wasibughudhiwe hata kidogo.
 
Back
Top Bottom