Sugu: TRA siyo CHADEMA, acheni janja janja lipeni kodi

Niga or negro kwa lugha rahis ni maneno yanayotumika kumrejelea mtu mweus labda uwe huna uelewa na maneno hayo yalitumika sana marekani miaka ya nyuma na nadhan mpaka sasa bado yanatumika though not to that extent.

Hapa sio marekani ni Tanzania, which is not a big deal. Tulipe Kodi maana huwa tunadhani hii nchi Ni ya CHADEMA.
 
Uadui binafsi wake na msanii usijumuishe kukandamiza wananchi Kwa mamilioni wanaolia Kila siku na manyanyaso ya TRA kuhusu Kodi za kubambikizwa.
SUGU alichoandika ni Sarcasm/Kejeli

Soma Vizuri tweet ya JonGwe... amesema "Kila siku mnnasikia tunapigia kelele hizo Sheria mbovu na mmekaa kimya",, Lengo lake amemaanisha Watu wawe wanaunga Mkono kukemea hayo matatizo na sio wanakaa kimya halafu wanakuja kulalamika...

Hakuna sehemu amekandamiza yeyote.
 
Kama
Huyo mondi kipindi Cha watu wasio julikana alitunga wimbo kuwa ananyamaza kimya kuhusu kutekwa na kupotezwa na watu. Watu walimshauri kuhusu hiyo kauli yake kwamaba hayamuhusu.

Ndio maana Leo watu wanamponda anapolia kuhusu TRA maana wakati wenzake wanatekwa na watu wasijulikana alijifanya hayamhusu. Hiyo tunaita karma.

Kama Mondi ana pesa ndefu alipe Kodi mbona analia Kama vile anafilisika?.
 

Tofautisha kukwepa Kodi na kuvunjiwa hoteli kwa hila za kisiasa. Kipindi kile kuwa CHADEMA was a crime huoni bilcanas ilivovunjwa faster?. Halafu Sugu alikuwa anajibu tuhuma za Diamond kuwa afisa wa TRA ni mwanchadema anataka kumgombanisha na Rais. Happy ndipo shida ilipoanzia.
 
Kwamba SUGU anatuma UJUMBE Kwa wanambeya wa Jimbo aliwahi kulitumikia kama mbunge,

Anawambia walipe KODI waache kulialia.

Namuomba AYAMEZE maneno yake kama ataweza, asipoweza basi ATUBU.

Manyanyaso ya TRA kuomba RUSHWA Kwa wananchi ni makubwa.

Ungemuelewa sugu usingesema hivyo. Sugu kasema wazi wamepiga kelele kuhusu sheria za Kodi lakini watu wapo kimya, Leo yamewakuta wanaanza kulia. Ndio maana kawaambia walipe halafu waende kudai katiba mpya itakayoweka mfumo mzuri wa kulipa Kodi.
 
Huyo kilaza wala hata nae hana ufahamu.

Wakusanya kodi wanayo hayo mamlaka Dunia nzima si Tanzania pekee.

Hakuna sheria mbovu hapo.
 
Mwambie Ccm wamfanye Exemption from paying of taxes kulalamika kuwa yeye Ni (mkimbizi ) ni upumbavu .

Kila siku anajisifu yeye ni muimba matusi namba moja Africa so why analalamika ???

Watz sisi hatuwezi kumtetea shetani .
 
Nilipata kwenye ujumbe wa sugu ni kwamba TRA ina sheria mbaya sana za kodi,iko haja ya kufanyiwa review
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…