Suguye ni mchawi au ni Mtumishi wa Mungu?

Suguye ni mchawi au ni Mtumishi wa Mungu?

Ukiona hivyo ujue kuwa huko kunakoitwa makanisa ya kweli wameshindwa kupata ufumbuzi wa shida zao

Wanaona tu kanisa kongwe ni sehemu tu ya kufunzwa Bible Study na kufunzwa doctrine tu za dini husika lakini solution za real problems za watu hawana!!

Ndio.maana watu wanakimbilia huko kwingine. Kungekuwa na solution walipo wasingehangaika kwenda kwa mitume na Manabii

Kanisa lijitazame ndani zaidi kuliko kulaumu huko wanakoenda na kuwaita hawajui neno nk

Mtu haendi kanisani kwenda tu.kukaririshwa mistari ya Biblia na doctorines za kanisa pekee!! Watu wana issues. Yesu na mitume walikuwa na majibu kwa real problems za watu hawakuishia tu kuwafundisha bible study na doctorines za kanisa
1. Wapi Yesu alihubiri miujiza ya pesa tu bila ya kuhubiri uponyaji au wokovu?

Acheni kutetea huu upumbavu maana BIBLIA inanena wazi

MATHAYO 5:9.
"Heri wapatanishi;
Maana hao wataitwa wana wa Mungu."

Je we hapo unapatanisha au unapotosha?

2. BIBLIA inadadavua tena waenende kwa SHERIA/AMRI 10 ZA MUNGU na SHUHUDA/MAHUBIRI NA MATENDO waliyofanya Manabii na Yesu.

Je hao Manabii wa kizazi hiki cha karne ya 21 wanafanya hivyo?

ISAYA 8:19-20.

"Na wakati watakapokuambia, Tafuta habari kwa watu wenye pepo na kwa wachawi; waliao kama ndege na kunong’ona; je! Haiwapasi watu kutafuta habari kwa Mungu wao? Je! Waende kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?

Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili, bila shaka kwa hao hapana asubuhi."

3. Unaposema makanisa ya ukweli yameshindwa kupata ufumbuzi wa matatizo yao,

Una ushahidi gani?
Njia sahihi ni kuhalalisha hao Manabii wa uwongo?
Hawakutabiriwa na Mungu kuagiza Watu wajihadhari nao?

1 YOHANA 4:1-6.
MATHAYO 7:16-21.
MATHAYO 24.
2 WAKORINTHO 11:14-15.

4. ONYO:

UFUNUO 22:18-20.
 
Kuna mmoja ajiita nabii mihera jamaa anasura ya pombe atari,
Huyo Jamaa siku nyingi sana nilishamjua ni Nabii feki tu.

Ni wale wapumbavu wanaodanganya Watu kuwa kwa Mungu ni tambarare tu.

Inamaana hata wakishatatuliwa shida zao ndipo wataishi milele bila kupitia changamoto zozote kimaisha?

Mbinguni kwenyewe panahitaji Watu Majasiri, sasa utakuwa vipi Jasiri pasipokupitia vikwazo kisha uvishinde kiimani ilihali hata Manabii na Yesu walipitia hayo?

YOHANA 16:33.

Ayubu alipitia magumu mangapi na aliitetea imani vizuri tu japo hakuwahi kumkosea Mungu?

Pia matatizo/changamoto ni sehemu ya maisha.

YAKOBO 1: 1-8.
 
Ufumbuzi wa shida zao upo huko makisani na watu wengi wanapokea inahitaji kufata kanuni na taratibu tu za maandiko, sasa shida watu hawapendi kufata taratibu na kanuni wanapenda shortcut na mtelemkoooo kitongaa yan wapokee huku wanadanga wapokee huku wanafanya biashara haram wapokee huku wanazini wap na wap??

Kwaiyo unataka tuache kuhubiri injili yakuacha dhambi umpokee Yesu uponywe we unataka uponywe ili uendelee na dhambi, jingaa acha wakagaragazwe
Kabisa Ndugu, BIBLIA inanena wazi tena.

Maombi ya mwenye dhambi ni kelele tupu mbele zake Mungu.

Inamaana ukiwa Mcha Mungu haswaa basi pia imani yako iendane na matendo ya tabia yake Mungu = Upendo.

YOHANA 9:31.

"Twajua ya kuwa Mungu hawasikii wenye dhambi; bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake, humsikia huyo."
 
Sio uchanga wewe ndie hujui maandiko.Hujui umuhimu wa wengine kukuombea ukiwa na changamoto

Yak 5:13-15​

Mtu wa kwenu amepatikana na mabaya? Na aombe. Ana moyo wa kuchangamka? Na aimbe zaburi. Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana. Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.
kanisani hutoa msingi tu wa Mtu kupata maarifa ya kumjua Mungu anayeabudiwa katika Roho na Kweli

YOHANA 4:24.

Mtu akishapata mwanga anatakiwa asimame yeye kama yeye sababu kila Mtu ataubeba msalaba wake mwenyewe kuhakikisha anaupata ufalme wa Mungu.

YEREMIA 17:5-8.

Mungu husikia maombi ya yeyote isipokuwa awe ana imani thabiti, awe ametubu dhambi kwa dhati na amejikana nafsi akiishi katika utakatifu.

YOHANA 14:13-14.
 
Hilo lipo tangu kale mkuu, kuna wakati Kanisa lilipoa na baadaye Kristo akaleta uamsho.

Kuna wakati watu walirudi nyuma, walikata tamaa na kuangila lkn Mungu huachilia uamsho tena.

Vv
MITHALI 24:16.

"Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena;
Bali wasio haki hukwazwa na mabaya."
 
295828102_5221563811293209_8877219040337405313_n.jpg
Mchawi, Tapeli, Mganga wa kienyeji
 
Ukiona hivyo ujue kuwa huko kunakoitwa makanisa ya kweli wameshindwa kupata ufumbuzi wa shida zao

Wanaona tu kanisa kongwe ni sehemu tu ya kufunzwa Bible Study na kufunzwa doctrine tu za dini husika lakini solution za real problems za watu hawana!!

Ndio.maana watu wanakimbilia huko kwingine. Kungekuwa na solution walipo wasingehangaika kwenda kwa mitume na Manabii

Kanisa lijitazame ndani zaidi kuliko kulaumu huko wanakoenda na kuwaita hawajui neno nk

Mtu haendi kanisani kwenda tu.kukaririshwa mistari ya Biblia na doctorines za kanisa pekee!! Watu wana issues. Yesu na mitume walikuwa na majibu kwa real problems za watu hawakuishia tu kuwafundisha bible study na doctorines za kanisa
Mkuu YEHODAYA ni kweli unachosema, lakini hii isiwe sababu ya watu kuhalalisha vitu visivyo sawa kwa sababu tu wanataka kutatua matatizo yao.
Waingereza wanasema "the end doesn't justify the means." Hata kama njia fulani isiyo sahihi kibiblia inatumika na inaleta matokeo haimaanishi njia hiyo itakuwa sahihi mbele za Mungu as long as haikubaliani na Neno la Mungu. Hili ni funzo kwa watumishi wote wanaolitumia vibaya jina la Yesu Kristo kwa faida zao wenyewe, kuwa hata kama vitu wanavyofanya vilivyo nje ya Biblia vinaleta matokeo kwa watu, still mbele za Mungu ni kazi bure. Bwana Yesu atawahukumu tu kwa wakati wake Yeye.

Hivyo ushauri wako ni mzuri kuwa wale walio na mafundisho sahihi basi waongeze viwango vya kumtafuta Mungu na wasibweteke tu bali wasaidie watu wenye mahitaji.

Lakini pia Wakristo wasiwe tu watu wa kupokea kila kitu bila kukipima kwa maandiko kama kiko sahihi. Neno la Mungu linasema tuzijaribu roho. Hata kama mtumishi wa Mungu anatumika kea viwango gani, akifanya kitu kilicho nje na Neno la Mungu basi lazima tuhoji na tujithibitishe juu ya hilo.

“Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. ”
— 1 Yohana 4:1 (Biblia Takatifu)
 
Msiwaseme wapakwa mafuta wa Bwana.


Biblia inasema msiwaguse masihi wangu wala msiwadhuru nabii zangu Zaburi ya 105: 15
Ni kweli rafiki Donatila lakini pia Neno la Mungu hilo hilo linasema hapa:
“Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.

— 1 Yohana 4:1 (Biblia Takatifu)
 
“Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. ”
— 1 Yohana 4:1 (Biblia Takatifu)
Hata hao wanaokimbilia kwenye makanisa ya mitume na manabii huzijaribu roho za hao viongozi kwenye makanisa walipo kama zina ufumbuzi wa matatizo yao au la .Wakiona hamna wanakimbia.wanaona hiyo huduma haitokani na Mungu sababu haina ufumbuzi wa Changamoto

Hilo andiko la kuzijaribu roho kama zimetoka kwa Mungu ni upanga unaokata kuwili.kule wanakotoka na kule wanakoenda kote zinajaribiwa .Mtu hajiondokei tu hilo andiko ndilo anakuwa kulitumia kupima roho ya kiongozi hapo alipo

Hilo swala binafsi naona changamoto kubwa iko kwa viongozi na sio waumini wahamaji.Viongozi wajitathimini badala ya kutathimini waumini
 
Wiki chache hapo nyuma huko nchini Uganda, kuna mtumishi aliwaonyesha waumini jinsi ya kula tunda. Alimchukua mwanamama kamweka kimbuzi akawa anamswaga kwa nyuma yake.
N.B
Hakumvua chochote.
 
Haya mambo ya kiimani hayana Elim mkuu.
Lejea walio rililika kwenda kunywa kikombe .
Kabisa kabisa mkuu. Lakini tunapaswa kua na mfumo mzuri wenye kuruhusu watu kua na uwezo wa kuhoji.
Mf. Kuwe na debates, presentation, simple research tu kuanzia msingi.
Kuanzishwe mtaala wa kufundisha watoto walau misingi ya sheria na saikolojia.
Tupunguze kupata watendaji kwa kutumia maelezo badala yake tutumie ufanisi na utendaji. Kuna kitu tutakiongeza kwenye jamii.
 
Elimu Elimu Elimu

Tunalia na kuipambania Tanzania yenye Elimu bora.

Haya yote yanazuilika kabsaaa.
Ulaya wamesoma sana makanisani hawaendi kabisa wengi na makanisa mengi yanayzwa mingine kuwa misikiti na mengine kuwa maduka ya biashara au ma godown

Elimu zao zimewapeleka kwenye hadi ndoa za jinsia moja
 
Wapi Yesu alihubiri miujiza ya pesa tu bila ya kuhubiri uponyaji au wokovu?

Acheni kutetea huu upumbavu maana BIBLIA inanena wazi
Na pia hakuna mahali Yesu alihubiri bila kufungua watu wenye changamoto

Hakuishia tu kuwa na madarasa ya bible study kila siku ya ibada kama ilivyo.siku za leo kwa.watumishi wengi .Wanadhani kazi ya ibada ni kufundisha Biblia tu na kukusanya sadaka na watu kuondoka!!!!

Watu ujue wako wengine wamechoka na mizigo ya changamoto za maisha wanataka ufumbuzi. Kama kanisa halina ufumbuzi lisipige yowe likiwaona wanaenda kwa waganga wa kienyeji
 
Miaka ya tisini kurudi nyuma ilikuwa mtu akipandisha mashetani anatafutwa ustaadhi au sheikh anaongea nalo linataka nini na hata kulitoa, Pwani waliita maruhani au majini ~ WAISLAMU WAKAITWA WAFUGA MAJINI.

miaka ya 2000 mpaka sasa makanisani wachungaji na maaskofu wako busy kutoa mapepo hasa mabinti huku wakirukaruka kama ng'ombe anayechinjwa vile ~ haya yanayoitwa mapepo ndio yaleyale majini aka maruhani ~ SASA HAPA SIJUI WAKRISTO NAO WANAFUGA MAJINI.

Hivi mlioko ulaya kuna wachungaji huko wanawatoa mabinti wa kizungu mapepo na wao kurukaruka kama ng'ombe anayechinjwa.

Sisi tuliowahi kwenda kwa waganga wa kienyeji tunashindwa sana kutofautisha hizi huduma siku na zile za waganga wa kienyeji wapiga ramli. Ramri imekatazwa kwenye dini zote lakini mchungaji kanisani unamuona live akipiga ramli kama wafanyavyo wapiga tunguri.
 
Back
Top Bottom