Suluhisho la kulipa fidia ya mabilion nje ya nchi ni kubadili jina la nchi

Suluhisho la kulipa fidia ya mabilion nje ya nchi ni kubadili jina la nchi

Ila nchi za kiafrika kudaiwa tunajitakia tu wenyewe, laiti kama AU ingekuwa serious hakuna nchi ingedaiwa.

Me ningekuwa ndy mwenyekiti wa AU ningetoa tamko kwamba kama Nchi za ulaya ziliitawala Bara la Africa na wakafanya human and resources exploitation pamoja na torturing kwa watu. Bila kuwalipa fidia Raia wa nchi dhidi ya ukatili huu, basi hizo fedha za mikopo zikawe fidia ya kile kilichoitwa ukoloni na unyonyaji.

Hakuna nchi ya ulaya ambayo haijajengwa na rasilimali kutoka afrika.
Hakuna fidia yeyote tuliyoipata na UN haiwezi kuibua hoja katili kama hizi.

Kukandamizwa tunajitakia ila njia za kujikwamua ni nyingi wakuu.
 
Bado tunaendelea kupigwa kwenye kesi za fidia na makampuni ya kigeni.. Tunalipa mabilioni ya shilingi na mabilion ya dola kwa makosa ya watu wachache tuu.. Mostly kutoka chama chawala
Hakuna hata kesi moja tuliwahi kushinda..
Mikataba tuliyosaini kimagumashi inatutesa sasa.. Waliosaini kwa niaba yetu wapo na wanaendelea kula bata..hawana wasiwasi kabisa.. Na ni hao hao kati yao kwenye hizo fidia nao wana cha kwako😳🤬🤬🤬
Washeria wetu wa serikali
Ni vihiyo
Hawana uzalendo
Wananunulika
Ni mbumbumbu wa sheria za kimataifa na uwekezaji
Ni waoga
Mwisho wa siku tunaoumia ni sisi wananchi wa kawaida

Sasa imetosha.. Tumevumilia imefika mwisho.. Taifa linalodaiwa ni Taifa na nchi ya Tanzania
Hili lina lina nuksi
Hili jina lina sifa mbaya
Hili jina lina migogoro Mungu
Hili jina lina madeni mengi sana
Kuna shida gani tukiachana nalo sasa?
Turudi kwenye Tanganyika yetu..
Ni jina zuri
Linapendeza
Halina kashfa
Halina madeni
Halina nuksi
Halimilikiwi na chama chawala
Tubadili jina kutoka Tanzania kwenda Tanganyika.. Na madeni yote yatakoma.. Maana anayedaiwa ni Tanzania sio Tanganyika
Marehemu hadaiwi bali husamehewa madeni..
View attachment 3140428
kuna methali isemay mzigo wa mpumbavu haishia begani unajua maana yake? Ndo nchi yetu ilivo kwa sasa.
 
Inaoneka wewe ni mwanasheria mzuri mno tena msomi na unaelewa sana mambo, kulingana na Maelezo yako mazuri.

Sasa kwanini nyie wanasheria kupitia kile chama chenu cha wanasheria Tanganyika msingekuwa mnaisaidia serikali katika kusimamia maswala ya vifungu vya kimkataba, kutafsiri vifungu vya mkataba, sheria zake, conflict of interests, na kila kitu then mjue if mkataba ni sutable au ni wakutukandamiza, kwaajili ya maslahi mapana ya nchi.

Kwanini msitusaidie jamani hata sisi tusiokuwa na elimu ya sheria tufurahie uwepo wenu nchini nyie kama mashujaa wetu wa masuala ya sheria!.
Mkuu mimi sio mwanasheria ila ninasoma sana vitabu mbalimbali vikiwemo vya sheria. Kuhusu chama cha TLS kusaidia serikali nadhani wewe mwenyewe ni shahidi kumekua na ujinga mwingi sana unafanyika wakati wa vetting ya yupi anafaa kuwekwa kwenye maamuzi na yupi hafai. Ukileta hoja za kuisaidia nchi unaonekana mpinzani na wapinzani hawana nafasi katika hii nchi.
 
Mkuu mimi sio mwanasheria ila ninasoma sana vitabu mbalimbali vikiwemo vya sheria. Kuhusu chama cha TLS kusaidia serikali nadhani wewe mwenyewe ni shahidi kumekua na ujinga mwingi sana unafanyika wakati wa vetting ya yupi anafaa kuwekwa kwenye maamuzi na yupi hafai. Ukileta hoja za kuisaidia nchi unaonekana mpinzani na wapinzani hawana nafasi katika hii nchi.
dah asee inasikitisha mno, huu mfumo wa utawala umeoza.

It’s better tusisitize viongozi waingie kwa mikataba katika ofisi zao akishindwa kutimiza mahitaji ya mkataba afutwe na alipe kila gharama aliyopewa la si hivyo atumikie kifungo maana uchaguzi tu hauwezi kuondoa huu uozo jamani.

Me inaniuma sana taifa halina taswira tena ni kama mgodi wa marehemu kila mtu anajichotea tu atavyo.

Tuwaajiri hawa watu kwa mikataba em fikirieni hii hoja yangu please jamani.
 
dah asee inasikitisha mno, huu mfumo wa utawala umeoza.

It’s better tusisitize viongozi waingie kwa mikataba katika ofisi zao akishindwa kutimiza mahitaji ya mkataba afutwe na alipe kila gharama aliyopewa la si hivyo atumikie kifungo maana uchaguzi tu hauwezi kuondoa huu uozo jamani.

Me inaniuma sana taifa halina taswira tena ni kama mgodi wa marehemu kila mtu anajichotea tu atavyo.

Tuwaajiri hawa watu kwa mikataba em fikirieni hii hoja yangu please jamani.
Hoja yako ni nzuri pia nimeona uzi wa mwenzetu mmoja kuhusu serikali kutoa ajira za mikataba kwa miaka 10. Ni jambo zuri nadhani wenye mamlaka watapita na kuchukua yaliyobora kwa ustawi wa taifa letu
 
Hoja yako ni nzuri pia nimeona uzi wa mwenzetu mmoja kuhusu serikali kutoa ajira za mikataba kwa miaka 10. Ni jambo zuri nadhani wenye mamlaka watapita na kuchukua yaliyobora kwa ustawi wa taifa letu
Kaka kwenye ule uzi nimeongea mno nimebishana na watu mno, hawajui tu vile najiskia niona taswira mbovu hivi ya taifa letu, natamani kuona mabadiliko na maendeleo sana kaka na inawezekana tukiamua kwani lazma kumuumiza mwananchi ili kuishi vizuri viongozi!?

Kwani mishahara si wanapata lakini kwanini watufanyie ukatili hivi!?
 
Waziri wa Fedha wa sasa Mwigulu Nchemba, aliwahi kusema HATUTAGONGEWA MILANGO YETU KULIPA HILI DENI wasi wasi wetu ni nini?

Hatupaswi kujadili deni la TAIFA, analipa Yeye na Rais.Samia.
 
Waziri wa Fedha wa sasa Mwigulu Nchemba, aliwahi kusema HATUTAGONGEWA MILANGO YETU KULIPA HILI DENI wasi wasi wetu ni nini?

Hatupaswi kujadili deni la TAIFA, analipa Yeye na Rais.Samia.
Tuliingizwa cha wahuni trust me.. Maana cha wahuni kichambio gunzi
 
Kaka kwenye ule uzi nimeongea mno nimebishana na watu mno, hawajui tu vile najiskia niona taswira mbovu hivi ya taifa letu, natamani kuona mabadiliko na maendeleo sana kaka na inawezekana tukiamua kwani lazma kumuumiza mwananchi ili kuishi vizuri viongozi!?

Kwani mishahara si wanapata lakini kwanini watufanyie ukatili hivi!?
Ni nani yuko tayari kubanduka kwenye mkondo wa ulaji?
 
hata tukibadili jina DANJANIA kuwa DANGANYIKA tabu iko pale pale.lazima tutalipa tu DENI LA TAIFA.
 
mi napendekeza iitwe nchi ya Kilimanjaro,
tuachane na majina Tanganyika au Tanzania
herufi za mwanzo za haya majina ni vitu vinavyologwa sana na kupigwa sana au kuibiwa sana
 
Sizani kama mikataba iliovunjwa ilikua inakasoro ya kisheria kwa pande zote.
Tatizo ni pale wanasiasa wanapo ingilia na kutumia ubabe kuivunja au kubadili.
 
Kama huna ujasiri wa kuwa kama Ibrahim Traore ni heri uufyate tu.

Kondoo uutowe wapi ujasiri wa Mujahid?
 
Bado tunaendelea kupigwa kwenye kesi za fidia na makampuni ya kigeni.. Tunalipa mabilioni ya shilingi na mabilion ya dola kwa makosa ya watu wachache tuu.. Mostly kutoka chama chawala
Hakuna hata kesi moja tuliwahi kushinda..
Mikataba tuliyosaini kimagumashi inatutesa sasa.. Waliosaini kwa niaba yetu wapo na wanaendelea kula bata..hawana wasiwasi kabisa.. Na ni hao hao kati yao kwenye hizo fidia nao wana cha kwako😳🤬🤬🤬
Washeria wetu wa serikali
Ni vihiyo
Hawana uzalendo
Wananunulika
Ni mbumbumbu wa sheria za kimataifa na uwekezaji
Ni waoga
Mwisho wa siku tunaoumia ni sisi wananchi wa kawaida

Sasa imetosha.. Tumevumilia imefika mwisho.. Taifa linalodaiwa ni Taifa na nchi ya Tanzania
Hili lina lina nuksi
Hili jina lina sifa mbaya
Hili jina lina migogoro Mungu
Hili jina lina madeni mengi sana
Kuna shida gani tukiachana nalo sasa?
Turudi kwenye Tanganyika yetu..
Ni jina zuri
Linapendeza
Halina kashfa
Halina madeni
Halina nuksi
Halimilikiwi na chama chawala
Tubadili jina kutoka Tanzania kwenda Tanganyika.. Na madeni yote yatakoma.. Maana anayedaiwa ni Tanzania sio Tanganyika
Marehemu hadaiwi bali husamehewa madeni..
View attachment 3140428


Tatizo ni viongozi wa chama chetu tawala wana sign mikataba mibaya kwa kuhogwa halafu ukija uongozi mpya wanavunja mikataba ili wahogwe wenyewe na sio waliopita mwekezaji akataa kuhonga mara mbili. Baada ya hapo wanafuta mkataba bila kufuata sheria kwa “manufaa ya umma” sasa ni manufaa gani kama tunalipa mabilioni! Hii ndiyo ramani nzima

Kwahiyo mikataba yenyewe unakuta ilikuwa mibaya lakini wameshahongwa sana. Chenge ndiye alikuwa mwanasheria msomi na mla rushwa mkubwa sana
 
Back
Top Bottom