Suluhisho la vita ya Mashariki ya kati ni kwa Wapalestina kutulia au kuhama kabisa pale Gaza

Suluhisho la vita ya Mashariki ya kati ni kwa Wapalestina kutulia au kuhama kabisa pale Gaza

1. Kama ni suluhisho basi Waizraili nao waondoke maeneo hayo na sio Wapalestina pekee.
2. Unazungumzia chokochoko za Hamas na kuwasahau wanaowasaidia Waizrail ambao ni akina Marekani na washirika wake. Hili hujaliona?
3. Pamoja na kuhitaji msaada, Wapalestina wanapigania haki yao ya kuishi bila kujali watasaidiwa na nchi yoyote iwayo.
4. Ukisema eneo la Ghaza ni dogo hivyo Wapalestina wasilipiganie, huo udogo haubadiliki kuwa ni ukubwa kwa Israel kulipigania kwa nguvu zote. Udogo unapaswa kuonekana na pande zote na sio Wapalestina pekee. Hili nalo ulijue.
5. Ukisema Israel ndio wanamiliki Ghaza kwa namna yoyote, wengine wanasema Wapalestina ndio wanamilki Ghaza ndo sababu kubwa wanalipigania.
6. Ikiwa Israel ina dhamira na nguvu ya kuwakandamiza Wapalestina, kama unavodai, waendelee kufanya hivyo na Wapaestina wataendelea kuipigania ardhi hiyo hadi mwisho.
7. Hakuna wafia dini, kama unavyodai, wanaotaka vita iendelee ila kinachotakiwa ni kupatikana haki kwa kila upande.
8. Ni kweli tumechoka na vita na hatutaki vita. Maneno haya yanapaswa kuonekana kwa vitendo na moyo wa dhati kuanzia kusema, kuandika na katika nyanja zote. Uzi huu hauna sifa hizo. Kwa hivyo nadhani yanasemwa mdomoni, yanaadikwa makaratasini huku kukiwa hakuna imani ya kinachosemwa na kinachoandikwa. Au ndo ule msemo wetu Waswahili "mkuki kwa ngurue, kwa binadamu mchungu?"
Israel wana haki, na waarabu ni wanafiki saizi wanaopata tabu ni wagaza, Ayatollah yupo Iran kanyanyua miguu juu, palestina ishafutika hata kwenye ramani haipo.

Waamue hivo vipande viwili vya gaza na west bank waunganishe ndani ya Israel wote wawe raia wa Israel tu
 
Nilitaka kusema "mbovu", yaani 'opinion' mbovu, lakini namheshimu sana mleta mada. Siwezi kusema hivyo.

Ubovu wa mada yake unaanzia katika kuangalia upande mmoja tu wa waPalestina na kuwatwisha mzigo wote wa lawama. Na kama vile haitoshi, mkuu 'Zanzibar - ASP anasahau jambo moja, kwamba, nyumbani ni nyumbani, hata kama ni pangoni. Gaza inaweza kuwa hakuna kitu, lakini ni nyumbani, hawa watu hawajui mahali kwingine kokote zaidi ya hapo.
Sasa sijui kama hukumbuki kuwa eneo alilopewa Israel lina mipaka yake? Suluhu ni kuwa Israel naye akae mahali pake, ndani ya mipaka yake; ikifanyika hivyo, atakayechokoza mwingine lawama iwe juu ya huyo mchokozi.

Ubinaadam ni zaidi ya mahitaji ya kawaida ya kila siku. Unaweza kumhudumia binaadam huyo kwa kila kitu, lakini ukashindwa kutambua ubinaadam wake na heshima anayostahili, mtu huyo ni lazima atapambana na wewe.
Wapalestina hawawezi kuishi wakifanywa kama wametawaliwa na watu wengine. Kama ni kuishi kwa pamoja,, ni lazima kila mmoja wao amheshimu mwenzake kwa usawa; isiwe Israel ndiye awe mtawala wa kila kitu.

Mwisho mkuu Zanzibar-ASP, ukweli ni kwamba Israel hawezi kuishi pale kwa amani kwa kutegemea mabavu ya kivita kama unavyosema wewe. Hakuna silaha inayoweza kuleta amani pale. Leo hii utamwona Israel akiwachakaza waPalestina kwa mabomu, lakini haitoshi. Kesho na keshokutwa m-pPalestina hatahitaji mabomu kama aliyotumia wakati huu, kutakuwa na njia za maangamizi zaidi na nyepesi kutumika na watu wachache tu kwa kumuumiza sana Israel.
Sasa labda upendekeze Israel awamalize wa-Palestina wote duniani.
Asante sana kwa kunijibu kwa hekima na kujenga hoja muhimu.

Mimi nimesema ili amani iwepo pasipo kutaka kuchimba nani mwenye haki na nani mbaya. Choko choko yoyote ya kivita inayoanzishwa na wapelestina inapelekea kufa kwa waisrael wachache zaidi lakini inaishia kufa kwa wapalestina wengi wengi, Israel kuchukua eneo kubwa zaidi, miji mingi ya wapalestina kukaliwa kimabavu na mateso ya kimaisha kuzidishwa maradufu.

Sote tunajua kwa sasa Israel
1. Ametawala eneo kubwa.
2. Ana nguvu kubwa ya kijeshi.
3. Amedhamiria kuangamiza kila kimelea wa Hamas
4. Hana tena huruma wala simile dhidi ya mpalestina yoyote anasimama mbele yake kupambana naye.
5. Amepata sababu ya kutaka kulifuta kabisa taifa la Palestina kwa mtutu wa bunduki pale Gaza.

Sasa katika mazingira hayo, nini suluhisho la amani pale Gaza?
Kuendelea kulaani tu?
Wapalestina kuendelea kukaza shingo?

Dawa ni wapalestina wakae kwa utulivu pale Gaza (wakose uhuru lakini amani waipate) ama wahame kabisa Gaza (wakose makazi yao ya asili lakini maisha yao yaendelee popote).
 
Wewe usicheze na huo moto.
Hao watu waone hivyo hivyo wanavyo lia lia huko huko kwao.

Watakuja kuiharibu hii nchi kabisa.
Sababu ni moja tu itikadi kali za kidini.
Watakuja na Hamas, Hezbollah, na wanaofanana na hao.
Hao watu sio salama kwa kizazi chetu.
Waache wauane huko huko.
1980s wapalestina waliwahi fukuzwa Jordan kwa kuunda nchi ndani ya nchi na king Hussein ndio wakaenda Lebanon nako huko msala tu pia wakafukuzwa kwenda Tunisia waarabu wamewachoka aise
 
Ubishi, ukaidi na ujeuri wa wapalestina kutaka kupambana na Israel itapelekea maafa na mateso zaidi kwa watu wasiokuwa na hatia. Ama kwa kupenda au kutokupenda, suluhisho rahisi na lenye kuleta amani mashariki ya kati ni wapalestina kuwa watulivu ili waendelee kukaa pale kwa amani au kuhama kabisa maeneo yale ili kuepusha shari zaidi.

Hizi choko choko za vikundi vya Hamas nk. ni kujilisha upepo na kuongeza mateso, hazina msaada wowote endelevu kwa wapalestina. Wapalestina wakae wakijua, hakuna nchi ya kiarabu itajiingiza kichwa kichwa kuwapigania pale, sio Iran, Lebanon, Syria, Egypt, Jordan au Saudi Arabia ambayo ina muda, nguvu, rasimali au dhamira ya dhati ya kwenda moja kwa moja kuwapigania wapalestina, kila taifa linapambana na hali yake tu.

Hilo eneo la Gaza hapo mashariki ya kati ni dogo sana, kavu mnoo, halina rasilimali zozote muhimu za kiuchumi ukiachilia hizi blah blah za kiimani ambazo zinatumika na pande zote kinafiki tu na kimchongo ili kujitengenezea uhalali wa kumiliki hayo maeneo kwa sababu ya umuhimu wa kihistoria.

Sasa kwanini watu wakae kwa wagombana?
Kwani dunia haina sehemu zingine za kuishi?
Kuna raha gani kuishi katika hali hiyo?

Unaweza kusema au kuwaza kuwa kwanini waisraeli wao wasihamishwe pale? Jibu ni moja tu, Israel kwa sehemu kubwa ndio inapamiliki pale kwa sasa (iwe kwa haki au mabavu), Israel haina muda wa kuchokoza wapalestina ili iendelee kukaa pale bali ina dhamira, muda na nguvu za kutaka kuwakandamiza zaidi na kuwatuliza vilivyo ikiwa wapalestina watataka kuendelea kubakia pale.

Kama kuna wafia dini huku duniani wanaoona ni lazima kuendelea kupigana vita pale mashariki ya kati basi waende wao pale kwa vivuli vya dini yao kupigana na sio kutumia wapalestina kama chambo.

Note:
Taifa la Palestina lina mchanganyiko wa watu wenye imani tofauti tofauti wakiwemo waislamu (97%) na wakristo (3%), wakati taifa la Israel nalo lina waumini wa kiyahudi (81%), waislamu (14%), dini za asili (3%) na wakristo (2%). Lakini kote huko kwa hayo mataifa na hao waumini ukichunguza utagundua miongoni mwao kuna wapagani na wahuni kibao, hivyo tusilazimishe hii vita kuwa ni vita ya kidini wakati ni siasa na tamaa tu.

TUMECHOKA NA VITA
HATUTAKI VITA
Vita vikisitishwa misaada itaanza kuingia pande zote mbili !
Mabilioni ya dollar yatamiminwa huko kwa wakubwa wa pande zote mbili kwa ajili ya wananchi wao walioathirika na hiyo vita !!
Pesa nyingi kama kawaida zitaishia kwenye mifuko ya wajanja wakubwa wa pande zote mbili !!
Kufa kufaana lakini pamoja na yote hayo Two states solution ndio mpango mzima !!
Raia wema wa pande zote mbili hawaitaki hiyo vita maana inawaumiza sana! Tusijidanganye kwamba wanaoumia ni wapalestina pekee !
Chukulia mfano hapa Bongo wanapozuka Panyarodi tu shughuli inavyokua pevu mitaani !
Binadamu yeyote yule akiishi kwenye Nchi ambayo usalama wake ni mdogo huwa ni mateso sana na hakuna anayefurahia maisha ya kukimbia kimbia au ya kujificha kwenye mahandaki kila ving’ora vinapolia !!
 
Palestina haikaliwi kwa ubavu
images.jpeg

hata macho hayaoni.
katika nchi ambayo mipaka yake imezungumzwa wazi wazi kwenye vitabu vya dini na kihistoria ni ISRAEL
Acha uongo mipaka ya Israel kwenye Bible ipo huko Iraq kabisa mto Euphrates na Tigris Kama mnafuata Bible si mfuate ramani ya Bible why mnakua na unafiki.
Israel nchi ile ni ya JEWS
Acha uongo hao wayahudi walikuta watu wanaishi sio kwamba walikuta ardhi ipo wazi, na kingine ardhi alipewa Abraham ambaye ni baba wa mataifa mengi sio Israel pekee. Why mnajimilikisha?
Hao hao UN wanaunga mkono ushoga je ni sahihi kisa UN ndio kasema? Hao UN walisema Iraq ana silaha za nyuklia which haikuwa kweli je anaaminika vipi kuwa wakati wote yupo sahihi?
 
Vita vikisitishwa misaada itaanza kuingia pande zote mbili !
Mabilioni ya dollar yatamiminwa huko kwa wakubwa wa pande zote mbili kwa ajili ya wananchi wao walioathirika na hiyo vita !!
Pesa nyingi kama kawaida zitaishia kwenye mifuko ya wajanja wakubwa wa pande zote mbili !!
Kufa kufaana lakini pamoja na yote hayo Two states solution ndio mpango mzima !!
Raia wema wa pande zote mbili hawaitaki hiyo vita maana inawaumiza sana! Tusijidanganye kwamba wanaoumia ni wapalestina pekee !
Chukulia mfano hapa Bongo wanapozuka Panyarodi tu shughuli inavyokua pevu mitaani !
Binadamu yeyote yule akiishi kwenye Nchi ambayo usalama wake ni mdogo huwa ni mateso sana na hakuna anayefurahia maisha ya kukimbia kimbia au ya kujificha kwenye mahandaki kila ving’ora vinapolia !!
Sahihi kabisa
 
wapalestina waliwahi fukuzwa Jordan kwa kuunda nchi ndani ya nchi na king Hussein ndio wakaenda Lebanon nako huko msala tu pia wakafukuzwa kwenda Tunisia waarabu wamewachoka aise
Vipi wayahudi kuna nchi gani waliwahi kuishi bila kufukuzwa? Walichinjwa kuanzia Moscow mpaka Paris, na fungakazi ikawa Germany na Poland maana walikua hawafanyi kazi zaidi ya biashara ya kukopesha na kuchukua riba kubwa
 
Ubishi, ukaidi na ujeuri wa wapalestina kutaka kupambana na Israel itapelekea maafa na mateso zaidi kwa watu wasiokuwa na hatia. Ama kwa kupenda au kutokupenda, suluhisho rahisi na lenye kuleta amani mashariki ya kati ni wapalestina kuwa watulivu ili waendelee kukaa pale kwa amani au kuhama kabisa maeneo yale ili kuepusha shari zaidi.

Hizi choko choko za vikundi vya Hamas nk. ni kujilisha upepo na kuongeza mateso, hazina msaada wowote endelevu kwa wapalestina. Wapalestina wakae wakijua, hakuna nchi ya kiarabu itajiingiza kichwa kichwa kuwapigania pale, sio Iran, Lebanon, Syria, Egypt, Jordan au Saudi Arabia ambayo ina muda, nguvu, rasimali au dhamira ya dhati ya kwenda moja kwa moja kuwapigania wapalestina, kila taifa linapambana na hali yake tu.

Hilo eneo la Gaza hapo mashariki ya kati ni dogo sana, kavu mnoo, halina rasilimali zozote muhimu za kiuchumi ukiachilia hizi blah blah za kiimani ambazo zinatumika na pande zote kinafiki tu na kimchongo ili kujitengenezea uhalali wa kumiliki hayo maeneo kwa sababu ya umuhimu wa kihistoria.

Sasa kwanini watu wakae kwa wagombana?
Kwani dunia haina sehemu zingine za kuishi?
Kuna raha gani kuishi katika hali hiyo?

Unaweza kusema au kuwaza kuwa kwanini waisraeli wao wasihamishwe pale? Jibu ni moja tu, Israel kwa sehemu kubwa ndio inapamiliki pale kwa sasa (iwe kwa haki au mabavu), Israel haina muda wa kuchokoza wapalestina ili iendelee kukaa pale bali ina dhamira, muda na nguvu za kutaka kuwakandamiza zaidi na kuwatuliza vilivyo ikiwa wapalestina watataka kuendelea kubakia pale.

Kama kuna wafia dini huku duniani wanaoona ni lazima kuendelea kupigana vita pale mashariki ya kati basi waende wao pale kwa vivuli vya dini yao kupigana na sio kutumia wapalestina kama chambo.

Note:
Taifa la Palestina lina mchanganyiko wa watu wenye imani tofauti tofauti wakiwemo waislamu (97%) na wakristo (3%), wakati taifa la Israel nalo lina waumini wa kiyahudi (81%), waislamu (14%), dini za asili (3%) na wakristo (2%). Lakini kote huko kwa hayo mataifa na hao waumini ukichunguza utagundua miongoni mwao kuna wapagani na wahuni kibao, hivyo tusilazimishe hii vita kuwa ni vita ya kidini wakati ni siasa na tamaa tu.

TUMECHOKA NA VITA
HATUTAKI VITA
We kweli hamnazo.
Tukija kutawala Zanzibar na kuwakaba koo, wewe utaondoka tu kwa vile umezidiwa?
 
Acheni kuongea msivyovijua, mfano golan heights ni eneo la Syria ila Israel amelikalia kimabavu na yenyewe ilijadiliwa kwenye UN? Same to West Bank kuna maeneo yalinyofolewa Jordan hapo bado kipande cha Sinai kule Misri kilikaliwa kimabavu!!

Acheni justification, kama UN ndio kila kitu kwani mara ngapi UN resolutions zimefanyika kupinga uvamizi wa Israel huko Palestina na hamjaingia humu kusema Israel iheshimu maazimio ya UN?

Au pendekezo likilazimisha palestina linakua halali ila likiipinga Israel linakua batili? Hizi ndimi mbili kwa faida ya nani
Acha uzito wa kufikiri, Golan heights, Sinai na maeneo ya Jordan unajua chanzo cha Israel kukalia maeneo hayo?

Maeneo ya Jordan na Sinai yalirudishwa je unajua chanzo na sababu za kuyaachia maeneo hayo?

Toa mahaba yako hapo na ujinga mnaojazana huko madrasa ok, kama hujui unauliza kwa ustarabu braza then unaeleweshwa ok
 
Ubishi, ukaidi na ujeuri wa wapalestina kutaka kupambana na Israel itapelekea maafa na mateso zaidi kwa watu wasiokuwa na hatia. Ama kwa kupenda au kutokupenda, suluhisho rahisi na lenye kuleta amani mashariki ya kati ni wapalestina kuwa watulivu ili waendelee kukaa pale kwa amani au kuhama kabisa maeneo yale ili kuepusha shari zaidi.

Hizi choko choko za vikundi vya Hamas nk. ni kujilisha upepo na kuongeza mateso, hazina msaada wowote endelevu kwa wapalestina. Wapalestina wakae wakijua, hakuna nchi ya kiarabu itajiingiza kichwa kichwa kuwapigania pale, sio Iran, Lebanon, Syria, Egypt, Jordan au Saudi Arabia ambayo ina muda, nguvu, rasimali au dhamira ya dhati ya kwenda moja kwa moja kuwapigania wapalestina, kila taifa linapambana na hali yake tu.

Hilo eneo la Gaza hapo mashariki ya kati ni dogo sana, kavu mnoo, halina rasilimali zozote muhimu za kiuchumi ukiachilia hizi blah blah za kiimani ambazo zinatumika na pande zote kinafiki tu na kimchongo ili kujitengenezea uhalali wa kumiliki hayo maeneo kwa sababu ya umuhimu wa kihistoria.

Sasa kwanini watu wakae kwa wagombana?
Kwani dunia haina sehemu zingine za kuishi?
Kuna raha gani kuishi katika hali hiyo?

Unaweza kusema au kuwaza kuwa kwanini waisraeli wao wasihamishwe pale? Jibu ni moja tu, Israel kwa sehemu kubwa ndio inapamiliki pale kwa sasa (iwe kwa haki au mabavu), Israel haina muda wa kuchokoza wapalestina ili iendelee kukaa pale bali ina dhamira, muda na nguvu za kutaka kuwakandamiza zaidi na kuwatuliza vilivyo ikiwa wapalestina watataka kuendelea kubakia pale.

Kama kuna wafia dini huku duniani wanaoona ni lazima kuendelea kupigana vita pale mashariki ya kati basi waende wao pale kwa vivuli vya dini yao kupigana na sio kutumia wapalestina kama chambo.

Note:
Taifa la Palestina lina mchanganyiko wa watu wenye imani tofauti tofauti wakiwemo waislamu (97%) na wakristo (3%), wakati taifa la Israel nalo lina waumini wa kiyahudi (81%), waislamu (14%), dini za asili (3%) na wakristo (2%). Lakini kote huko kwa hayo mataifa na hao waumini ukichunguza utagundua miongoni mwao kuna wapagani na wahuni kibao, hivyo tusilazimishe hii vita kuwa ni vita ya kidini wakati ni siasa na tamaa tu.

TUMECHOKA NA VITA
HATUTAKI VITA

Sahihisho hakuna taifa la palestina,bali kuna wapalestina. Sawa sawa na kusema kuna taifa la zanzibar huta lipata duniani ila kuna wazanzibar ndani ya Taifa la tanzania.
 
Vipi wayahudi kuna nchi gani waliwahi kuishi bila kufukuzwa? Walichinjwa kuanzia Moscow mpaka Paris, na fungakazi ikawa Germany na Poland maana walikua hawafanyi kazi zaidi ya biashara ya kukopesha na kuchukua riba kubwa
Tatizo lako moja tu ndugu wewe ni mzito kufikiri, huko hakukuwa Uyahudini ok, kulikuwa ni ugenini, Uyahudini ndio pale Israel na sasa wamesimama kwao so wapalestina watulie
 
Nilitaka kusema "mbovu", yaani 'opinion' mbovu, lakini namheshimu sana mleta mada. Siwezi kusema hivyo.

Ubovu wa mada yake unaanzia katika kuangalia upande mmoja tu wa waPalestina na kuwatwisha mzigo wote wa lawama. Na kama vile haitoshi, mkuu 'Zanzibar - ASP anasahau jambo moja, kwamba, nyumbani ni nyumbani, hata kama ni pangoni. Gaza inaweza kuwa hakuna kitu, lakini ni nyumbani, hawa watu hawajui mahali kwingine kokote zaidi ya hapo.
Sasa sijui kama hukumbuki kuwa eneo alilopewa Israel lina mipaka yake? Suluhu ni kuwa Israel naye akae mahali pake, ndani ya mipaka yake; ikifanyika hivyo, atakayechokoza mwingine lawama iwe juu ya huyo mchokozi.

Ubinaadam ni zaidi ya mahitaji ya kawaida ya kila siku. Unaweza kumhudumia binaadam huyo kwa kila kitu, lakini ukashindwa kutambua ubinaadam wake na heshima anayostahili, mtu huyo ni lazima atapambana na wewe.
Wapalestina hawawezi kuishi wakifanywa kama wametawaliwa na watu wengine. Kama ni kuishi kwa pamoja,, ni lazima kila mmoja wao amheshimu mwenzake kwa usawa; isiwe Israel ndiye awe mtawala wa kila kitu.

Mwisho mkuu Zanzibar-ASP, ukweli ni kwamba Israel hawezi kuishi pale kwa amani kwa kutegemea mabavu ya kivita kama unavyosema wewe. Hakuna silaha inayoweza kuleta amani pale. Leo hii utamwona Israel akiwachakaza waPalestina kwa mabomu, lakini haitoshi. Kesho na keshokutwa m-pPalestina hatahitaji mabomu kama aliyotumia wakati huu, kutakuwa na njia za maangamizi zaidi na nyepesi kutumika na watu wachache tu kwa kumuumiza sana Israel.
Sasa labda upendekeze Israel awamalize wa-Palestina wote duniani.

Mkuu umesahau hao wapalestina ndio waliokataa ile mipaka iliyowekwa na UN mwaka 1947,wakiungana n waarabu kukataa kabisa uwepo wa wayahudi hapo middle east,
 
1. Kama ni suluhisho basi Waizraili nao waondoke maeneo hayo na sio Wapalestina pekee.
2. Unazungumzia chokochoko za Hamas na kuwasahau wanaowasaidia Waizrail ambao ni akina Marekani na washirika wake. Hili hujaliona?
3. Pamoja na kuhitaji msaada, Wapalestina wanapigania haki yao ya kuishi bila kujali watasaidiwa na nchi yoyote iwayo.
4. Ukisema eneo la Ghaza ni dogo hivyo Wapalestina wasilipiganie, huo udogo haubadiliki kuwa ni ukubwa kwa Israel kulipigania kwa nguvu zote. Udogo unapaswa kuonekana na pande zote na sio Wapalestina pekee. Hili nalo ulijue.
5. Ukisema Israel ndio wanamiliki Ghaza kwa namna yoyote, wengine wanasema Wapalestina ndio wanamilki Ghaza ndo sababu kubwa wanalipigania.
6. Ikiwa Israel ina dhamira na nguvu ya kuwakandamiza Wapalestina, kama unavodai, waendelee kufanya hivyo na Wapaestina wataendelea kuipigania ardhi hiyo hadi mwisho.
7. Hakuna wafia dini, kama unavyodai, wanaotaka vita iendelee ila kinachotakiwa ni kupatikana haki kwa kila upande.
8. Ni kweli tumechoka na vita na hatutaki vita. Maneno haya yanapaswa kuonekana kwa vitendo na moyo wa dhati kuanzia kusema, kuandika na katika nyanja zote. Uzi huu hauna sifa hizo. Kwa hivyo nadhani yanasemwa mdomoni, yanaadikwa makaratasini huku kukiwa hakuna imani ya kinachosemwa na kinachoandikwa. Au ndo ule msemo wetu Waswahili "mkuki kwa ngurue, kwa binadamu mchungu?"
Nimekusoma na kukuelewa.
Nataka kukuuliza haya maswali.
1. Hizi unadhani katika mazingira haya, wapalestina wanaweza kushinda hii vita?

2. Toka wapalestina waanze chokochoko za kupambana na Israel mpaka sasa, wapalestina wamefanikiwa kwa lipi katika kurudisha ardhi yao, kuishi kwa uhuru na kuepusha maafa kwa raia wa kipalestina?

3. Nini kitaendelea kwa wapalestina ikiwa vita hii itaendelea kwa muda mrefu zaidi?

4. Hivi unadhani ipo siku Israel kwa hiari yake tu au kushinikizwa kwa maneno ataamua kuandoka na kuyaacha hayo maeneo ya Gaza kwa wapalestina?

5. Hivi unaamini hilo eneo lina thamani kubwa kimaisha (kuishi kwa raha, furaha, amani, uhuru na mafanikio ya kiuchumi) kwa wapelestina kuliko sehemu zingine duniani?
 
Tufikirie pia nje ya boksi.

Kuna matatizo makubwa matatu.

1. Mataifa mawili Israeli na Palestina kurasimishwa na kutambuliwa kimataifa. Hapa tatizo ni kwamba Hamas wana msimamo (na imeandikwa kwenye vitabu vyao) kwamba hakuna taifa liitwalo Israeli ndani ya ardhi ya mpalestina ambayo ni Uingereza kwa hila zao waliwapa wale walowezi na wahamiaji wa kutoka Ulaya.

Tukumbuke kwamba wakati wa machafuko huko Ulaya nyakati za akina Adolf Hitler kuwasaka hawa wayahudi wa Ulaya (Wayahudi wa ulaya ni kutoka Poland, Lithuania, Romania na nchi zingine ndogondogo) wengi walikimbilia hapo palestina ilokuwa chini ya mwingereza ambae alianza kuwaruhusu kuwa na ardhi.

Palestina ilikua chini ya uangalizi wa Uingereza (Palestine Mandate under UK) baada ya vita kuu ya kwanza ya Dunia ambapo Uingereza iliwashinda waturuki wa Himaya ya Ottoman na kuchukua sehemu hiyo.

Hivyo hapo mleta mada wakosea sana unaposema mpalestina aondoke kwenye ardhi yake.

2. Paletina kuwa ni sehemu ya kistratejia kwa mataifa ya magharibi. Hii haisemwi sana lakini ndo inotakiwa kuwa sababu namba moja kwani haka kasehemu ka Gaza kana hifadhi kubwa ya gesi asilia ambayo ndo yamezewa mate na mataifa haya khasa Marekani na Uingereza. Palestina ikiachwa yenyewe ijitawale na ifanye maamuzi yake kama taifa kamili basi itakuwa rahisi kuwavuta nchi kama Iran, Syria na hatimae kuwakaribisha nchi kubwa za Russia na China katika ukanda wake wa bahari ya Mediterranean.

3. Mpango wa Marekani kuishambulia Iran ili kuhodhi ukanda mzima wa Ghuba. Marekani imekuwa kwa muda mrefu ikijianda kuishambulia Iran ambayo sasa hivi imejizatiti kwa kuwa na mitambo imara ya ulinzi (ADS) dhidi ya mashambulizi yoyote ya Marekani.

Msingi mkubwa wa vita ya kuu ya pili ya Dunia ulikuwa ni kwa Marekani kuhakikisha inatawala hifadhi ya nishati katika eneo lote la Mashariki ya kati na Magharibi mwa Asia. Iran ina hifadhi kubwa ya mafuta na gesi asilia na pia kijiografia ipo sehemu nzuri ya kimkakati ikiwa katikati ya Afghanistan, Pakistan, sehemu ya India, Asia ya kati na mfereji wa Hormuz.

Huu mfereji wa Hormuz ndo asilimia 25 ya nishati yapita hapa kwenda Ulaya na Marekani lakini ni Iran ndo kikwazo kwa mataifa ya magharibi na taifa mteja la Israeli ( Client State) kwani Iran khasa baada ya mapinduzi ya 1979 bado ni taifa huru na Iran yatishia usalama wa taifa la Israeli na mstakabali mzima wa kuhodhi sehemu hiyo ya ghuba. Pia Iran yatishia matumizi ya Dola ya Marekani pamoja na nguvu yake ya kijeshi.

Iran mpaka sasa imejiendeleza na kutengeneza mifumo imara ya kiusalama kiasi cha kuweza kuzizuia Marekani na Israeli kuifanyia mashambulizi ya moja kwa moja kama walofanya kwa Irak na Afghanistan. Iran ina makombora ya maafa marefu na yale ya masafa mafupi (ballistic and cruise missiles) ambayo mengine yaweza kutua Israeli na kusini mwa bara la Ulaya.

Jambo hili pia latiliwa mkazo na Iran kujiunga na nchi za Urusi, China na Korea Kaskazini katika kupambana na Marekani na mataifa ya magharibi. Hivyo hapo harakati zote ni kutafuta sababu ili Iran ijiingize kwenye huu mgogoro lakini yashindikana kwani Iran ipo chini ya mwongozo wa Urusi na China.

Hizi ni sababu chache tu ambazo zaweza kukupa mwanga kwamba Israeli yupo katika kufanya kazi alotumwa na Marekani ambayo kwa mbali ameweka meli zake mbili za kivita katika bahari ya Mediterranean.

Ndo nikasema katika mada kadhaa humu kwamba huu ni mpango maalum kwa kuhakikisha wale walowezi wa Israeli ambao ni kizazi cha wale walowezi waloteka na kuchukua ardhi baada ya vita kuu ya 1967 ( Six Days War) na ambao wengi wamo kwenye baraza la mawaziri wa Benjamini Netanyahu, sasa hivi wataka kuchukua ardhi zaidi upande wa kaskazini wa Ukanda wa Magharibi jambo ambalo limestukiwa na wapalestina.

Haya masuala yamo kwenye historia yameandikwa uzuri ni kutafuta muda mzuri na kusoma kisha kufanya uchambuzi wako na kufikia hitimisho.

Haya yote usingeyaandika kama
Hamas wasinge fanya ugaidi,sasa israel akirudisha mapigo manaanza kujifanya wachambuzi mara iran anamakombora mara sijui gaza ina gasi asilia,mlikua wapi kabla ya hamasi kufanya ugaidi kuleta huu uchambuzi wa kifala.

Kwa taarifa yako usa na washirika wakiamua kweli kumtandika iran hata hao urusi na china hawatamuunga mkono,mabepari huwa na lengo moja tu.
 
1980s wapalestina waliwahi fukuzwa Jordan kwa kuunda nchi ndani ya nchi na king Hussein ndio wakaenda Lebanon nako huko msala tu pia wakafukuzwa kwenda Tunisia waarabu wamewachoka aise
Huko ni kwa waarabu wenzao na wanafanya fujo hadi wanafukuzwa sembuse huku kwa weusi ambako sisi wenye nchi wanatuona Kama manyani.
Hao wabakie huko huko nadhani kuna laana fulani inawazunguka.

Ni watu wa vita kila kukicha, Kama sio ya Kisiasa basi ni ya Kidini.
Unawakaribisha siku mbili tatu wanaanza kumpigania Mungu wao.
 
Ndio nini hiki umeandika? Kwahiyo hata Putin aachiwe Ukraine kisa ndio umekalia baadhi ya maeno ya nchi ile?

Are you sure? Mbona kila mwaka inajitanua na kuweka walowezi kwenye ardhi ya Palestina?

Kwa hiyo hata kina Mandela wangekaa kimya huko Sauzi kisa makaburu walikua na nguvu?

Huwezi laumu watu wanaopigania sovereignty yao na wakati mvamizi anajulikana. Hii dunia imejaa unafiki sana, mbona unapinga Russia kuvamia Ukraine na wala hujawahi muita Zelensky ni mchokozi!! Ila palestina ambao nao wanakaliwa kimabavu unaona ndio wakorofi kupigania uhuru wao??

Kuna haja ya somo la Foreign relations kuwekwa mashuleni.
Unataka kulinganisha haya yanayoendelea ukanda wa Gaza na mengine duniani, tukienda hivyo tutatoka nje ya mstari.

Nimesema kadri ambavyo Palestina anacharuka na kuua waisrael ndivyo ambavyo Israel huongeza makali ya kuua, kuteka, kutesa, kujitanua na kutawala Palestina. Vice versa is true.

Sasa kama Palestina ameamua kupambana kivita na Israel, hakuna mtu kulaumu wala kumhurumia mpalestina pale anapouwawa na kuteswa, maana amechagua upande.

Suala la nani ana haki ya umiliki wa eneo na kukaa pale, toka mwanzo nimesema sio lengo la hii mada. Lengo la hii mada ni amani iwepo Gaza.
 
Haya yote usingeyaandika kama
Hamas wasinge fanya ugaidi,sasa israel akirudisha mapigo manaanza kujifanya wachambuzi mara iran anamakombora mara sijui gaza ina gasi asilia,mlikua wapi kabla ya hamasi kufanya ugaidi kuleta huu uchambuzi wa kifala.

Kwa taarifa yako usa na washirika wakiamua kweli kumtandika iran hata hao urusi na china hawatamuunga mkono,mabepari huwa na lengo moja tu.
🤣🤣
Kimya sahivi suwasikiii kabisaa
 
Acha ujinga Palestina haikaliwi kwa ubavu, katika nchi ambayo mipaka yake imezungumzwa wazi wazi kwenye vitabu vya dini na kihistoria ni ISRAEL na sio SOUTH AFRICA wala TANZANIA

Israel nchi ile ni ya JEWS hata UN wanajua sasa mpumbavu mmoja kutoka Taita Taveta hata elimu hauna unatwambia nini hapa
🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom