Supu Special Thread: Jifunze jinsi ya kupika aina mbalimbali za supu ya nyama na mboga mboga

Supu Special Thread: Jifunze jinsi ya kupika aina mbalimbali za supu ya nyama na mboga mboga

Michael Amon

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2008
Posts
8,768
Reaction score
3,622
Jinsi ya kupika supu ya ulimi wa ng'ombe/nyama ya ng'ombe/mkia wa ng'ombe/makongoro/nyama ya mbuzi/samaki/kuku/utumbo


b410dd16ddbe32ca91f58fc087e59c15c886bdea.jpeg


Mahitaji

  • Ulimi wa ng'ombe/nyama ya ng'ombe/mkia wa ng'ombe/makongoro/nyama ya mbuzi/samaki
  • Soy sauce
  • Ndimu au limao
  • Kitunguu saumu
  • kitunguu maji
  • Tangawizi
  • Chumvi
  • Pilipili
  • Karoti

Jinsi ya kupika

  1. Bandika sufuria jikoni, weka nyama ya ulimi wa ng'ombe/nyama ya ng'ombe/mkia wa ng'ombe/makongoro/nyama ya mbuzi/samaki, kamulia ndimu, weka vitunguu saumu na karoti.
  2. Kata karoti na kitunguu maji vipande vidogo kisha viweke kwenye sufuria yako.
  3. Weka maji ya kutosha kisha funika sufuria na mfuniko.
  4. Ikikaribia kuiva weka soy sauce, hii inasaidia kuongeza ladha kwenye supu.
  5. Onja kama nyama imeiva, kama tayari weka pilipili. Vilevile unaweza kuongeza pililipi ukishaipua supu toka jikoni.

NB: Unaweza kuipika pamoja nyanya ili kuongeza ladha zaidi kama ukipenda.


Jinsi ya kupika supu ya pweza


supu+ya+pweza.jpg



Mahitaji

  • 1 Samaki pweza mkate na msafishe vizuri
  • 50 gram kitunguu swaumu
  • 100 gram kitunguu maji chop chop
  • 100 gram kariti kata vipande vidogo
  • 1 pilipili ya kijani fresh
  • 1 kijiko kidogo cha chai unga wa korienda au girigilani
  • Chumvi
  • 5 gram pilipili manga
  • 100 ml mafuta ya kupikia
  • 50 ml juisi ya Limao
  • 150 gram nyanya ya kopo
  • 1.5 lita ya Maji

Jinsi ya kupika

  1. Weka mafuta katika sufuria kisha kaanga kitunguu maji na kitunguu swaumu.
  2. Baada ya hapo weka pweza kaanga kwa dakika 10 kisha weka viungo vyote vilivyobakia kaanga kidogo.
  3. Weka maji chemsha katika moto wa wastani kwa dakika 15 na baada ya hapo itakua imeiva na tayari kwa kuliwa.

Jinsi ya kupika supu ya maboga


Chef+Issa+Boga+supu+%283%29.jpg



Mahitaji

  • 240 gram maboga yaliyomenywa yakachemshwa pamoja na kitunguu maji kimoja na kusagwa katika blenda
  • 60 gram Karanga ya kusaga (peanut butter) laini kabisa
  • 1 kijiko kikubwa cha chakula siagi
  • 1 Kiazi kitamu
  • Chumvi
  • 5 gram pili pili manga

Jinsi ya kupika

  1. Safisha na katakata viazi vitamu kisha vichemshe na vikishachemka toa viazi vyako ktk sufuria kisha viweke kwenye blender na uvisage pia.
  2. Chukua siagi na uiweke ktk kiakaango chako kilichokwisha pata moto na ukaange ule mchanganyiko uliosagwa wa maboga, mchanganyiko wa viazi vitamu pamoja na peanut butter.
  3. Kisha ongezea maji kufanya mchanganyiko wako uwe laini na uweke chumvi na pili pili manga kupata ladha safi.
  4. Koroga mpaka iwe laini na imechanganyika vizuri hakikisha unachemsha kwa dakika 10 tu inakua tayari kwa kuliwa.
 
Ulimi wa ng'ombe!!! Unasafishwaje kwanza...tupe ujuzi mkuu ili hata ukiwa haukutengezwa vizuri tujue
 
Ulimi wa ng'ombe!!! Unasafishwaje kwanza...tupe ujuzi mkuu ili hata ukiwa haukutengezwa vizuri tujue

Binafsi sijui namna ya kuusafisha huo ulimi wa ng'ombe maana mimi huwa nanunua ambao umekwisha safishwa. Kama kuna wadau ambao wanajua namna ya kusafisha ulimi wa mbuzi wanakaribishwa kutoa ujuzi wao.
 
Jinsi ya kupika supu ya pweza

supu+ya+pweza.jpg


Mahitaji

  • 1 Samaki pweza mkate na msafishe vizuri
  • 50 gram kitunguu swaumu
  • 100 gram kitunguu maji chop chop
  • 100 gram kariti kata vipande vidogo
  • 1 pilipili ya kijani fresh
  • 1 kijiko kidogo cha chai unga wa korienda au girigilani
  • Chumvi
  • 5 gram pilipili manga
  • 100 ml mafuta ya kupikia
  • 50 ml juisi ya Limao
  • 150 gram nyanya ya kopo
  • 1.5 lita ya Maji

Jinsi ya kupika

  1. Weka mafuta katika sufuria kisha kaanga kitunguu maji na kitunguu swaumu.
  2. Baada ya hapo weka pweza kaanga kwa dakika 10 kisha weka viungo vyote vilivyobakia kaanga kidogo.
  3. Weka maji chemsha katika moto wa wastani kwa dakika 15 na baada ya hapo itakua imeiva na tayari kwa kuliwa.
 
kusafisha ulimi wa ng'ombe unakua kama vile unachoma nyama yaan unauweka ulimi juu ya wire, alafu baada ya muda kidogo ukishapata moto unachukua kisu na kufanya kama vile unapaa samaki ili kulivua lile gamba la juu, baada ya hapo ulimi utakua tayari kwa mapishi mengine
 
Jinsi ya kupika supu ya pweza

supu+ya+pweza.jpg


Mahitaji

  • 1 Samaki pweza mkate na msafishe vizuri
  • 50 gram kitunguu swaumu
  • 100 gram kitunguu maji chop chop
  • 100 gram kariti kata vipande vidogo
  • 1 pilipili ya kijani fresh
  • 1 kijiko kidogo cha chai unga wa korienda au girigilani
  • Chumvi
  • 5 gram pilipili manga
  • 100 ml mafuta ya kupikia
  • 50 ml juisi ya Limao
  • 150 gram nyanya ya kopo
  • 1.5 lita ya Maji

Jinsi ya kupika

  1. Weka mafuta katika sufuria kisha kaanga kitunguu maji na kitunguu swaumu.
  2. Baada ya hapo weka pweza kaanga kwa dakika 10 kisha weka viungo vyote vilivyobakia kaanga kidogo.
  3. Weka maji chemsha katika moto wa wastani kwa dakika 15 na baada ya hapo itakua imeiva na tayari kwa kuliwa.

Hii kitu mimi huwa ndo inanishinda kabisa, awe amekaangwa, amechemshwa, amechomwa, kaungwa n.k mimi huwa ananishinda.
Nimejaribu mara nyingi ila wapiii!!!!
 
Hii kitu mimi huwa ndo inanishinda kabisa, awe amekaangwa, amechemshwa, amechomwa, kaungwa n.k mimi huwa ananishinda.
Nimejaribu mara nyingi ila wapiii!!!!

Pole sana mkuu. Hata mimi hii kitu huwa inanishinda ila nimeweka recipe yake kwa faida ya wadau wanaopendelea pweza.
 
Jinsi ya kupika supu ya maboga

Chef+Issa+Boga+supu+%283%29.jpg


Mahitaji

  • 240 gram maboga yaliyomenywa yakachemshwa pamoja na kitunguu maji kimoja na kusagwa katika blenda
  • 60 gram Karanga ya kusaga (peanut butter) laini kabisa
  • 1 kijiko kikubwa cha chakula siagi
  • 1 Kiazi kitamu
  • Chumvi
  • 5 gram pili pili manga

Jinsi ya kupika

  1. Safisha na katakata viazi vitamu kisha vichemshe na vikishachemka toa viazi vyako ktk sufuria kisha viweke kwenye blender na uvisage pia.
  2. Chukua siagi na uiweke ktk kiakaango chako kilichokwisha pata moto na ukaange ule mchanganyiko uliosagwa wa maboga, mchanganyiko wa viazi vitamu pamoja na peanut butter.
  3. Kisha ongezea maji kufanya mchanganyiko wako uwe laini na uweke chumvi na pili pili manga kupata ladha safi.
  4. Koroga mpaka iwe laini na imechanganyika vizuri hakikisha unachemsha kwa dakika 10 tu inakua tayari kwa kuliwa.
 
Jinsi ya kupika supu ya karoti

Chef+Issa+carrot-soup+%25283%2529.jpg


Mahitaji

  • 2 kubwa carroti (ioshe vizuri kisha ikwangue kwangue. Usiimenye maganda)
  • 1 kiazi kikubwa, (osha vizuri na katakata vipande vipande ikiwa na maganda yake
  • 1 jani la celery, (kata kata na majani yake)
  • 120 ml maziwa
  • 1 kitunguu kikubwa, katakta vipande
  • 5 gram kitunguu swaumu cha kusagwa
  • 3 gram saffron (zafarani)
  • Chumvi
  • 5 gram pili pili manga

Jinsi ya kupika

  1. Chemsha carrots na viazi ulaya kwa dakika 4.
  2. Chukua maziwa ya uvugu vugu yaliyopo kwenye bakuli kisha weka saffron (zafarani).
  3. Weka kijiko kimoja cha mafuta katika sufuria yako yapate moto kisha weka kitunguu maji, kitunguu swaumu, chop celery na chumvi kisha kaanga mpaka iive kwa dakika 2.
  4. Chukua mchanganyiko wote na uumimine katika blender pamoja na carrots na viazi ulivyokwisha chemsha kisha saga.
  5. Baada ya kusaga vizuri kabisa rudisha katika sufuria na acha ichemke tena kwa dakika 2.
  6. Mimina maziwa yale uliyochanganya na saffron kisha punguza moto ichemke kwa dakika 3.
  7. Baada ya hapo supu yako itakuwa imeiva na tayari kwa kuliwa.

NB: Hakikisha unakoroga vizuri maziwa na mchanganyiko wako wa supu vichangayike vizuri kabisa wakati supu yako ikiwa bado jikoni.
 
Back
Top Bottom