Surveyormunkondya sasa nipo jamiiforum kwa ajili ya elimu juu ya masuala ya ardhi

Surveyormunkondya sasa nipo jamiiforum kwa ajili ya elimu juu ya masuala ya ardhi

Boss nimeassume anamaanisha GPS receiver na sio GPRS(general packet radio service) kwa sababu GPRS ni kuhusu mambo mtandao wa simu 2G au 3G na havihusiani na ardhi..
Hivyo nimemjibu nikiamini anamaanisha GPR receiver kwa sababu ndo kifaa hutuka kwenye mambo ya upimaji wa ardhi...
Ahsante

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndivyo hivyo nilikosea jina, pia shukrani kwa jibu lako. Madhumuni hasa ya kugawa viwanja angalau nifanye kitaalamu kidogo maana huku kwetu watu wanapima viwanja kwa kuhesabu hatua tu! na nikisema niache mpaka nipate pesa ya kupimia kitaalam basi hata hilo eneo lenyewe nitalikosa maana jamaa zangu washaanza kulimega

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nataka kujua kama naweza kupimiwa ardhi ambayo nimepoteza ile karatasi ya mauziano nilipoinunua....ilikua muda kidogo na pameshajengwa tayari

Pls..naomba kueleweshwa hata kama swali liko nje ya mada
 
Ndivyo hivyo nilikosea jina, pia shukrani kwa jibu lako. Madhumuni hasa ya kugawa viwanja angalau nifanye kitaalamu kidogo maana huku kwetu watu wanapima viwanja kwa kuhesabu hatua tu! na nikisema niache mpaka nipate pesa ya kupimia kitaalam basi hata hilo eneo lenyewe nitalikosa maana jamaa zangu washaanza kulimega

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio mkuu unaweza kufanya hivyo na kishakujengea mipaka yako
 
Nataka kujua kama naweza kupimiwa ardhi ambayo nimepoteza ile karatasi ya mauziano nilipoinunua....ilikua muda kidogo na pameshajengwa tayari

Pls..naomba kueleweshwa hata kama swali liko nje ya mada
Kama majirani na serikali ya mtaa inakutambua wewe ni mmiliki halali wa hilo eneo hakuna shida yoyote unaweza kupima tu pasipo shaka yoyote
 
kwa hilii serikali inahitaji pongezi maana ukitazama mji kama dsm ni ni ishara tosha ya kushindwa kupanga huu mji ambao kijiographia ulipaswa uwe mji mmoja mzuri sanaaa yaan kama ungepangwa ....ukitazama mji kama nairobi umepangwa vizuri atleast hope dodoma kwa hili litazibitiwa
Kweli kabisa mkuu..serikali inazidi kuangalia namna nzuri ya kuboresha hili.
 
Bado si rafiki!
Kuna maeneo kiwanja kinauzwa kuanzia 150,000.
Being inapaswa kuendana na gharama za kiwanja eneo husika, ikiwa kama lengo ni kuhasisha watu wengi wapime.
Ikumbukwe, watu wengi (hasa vijijini) wana maeneo ambayo yakipimwa yanatoa viwanja vingi.
Kwa mfano, eneo likitoa viwanja 4, mmiliki atapaswa kulipia 600,000/-. Siamini kama wengi 'watajipendekeza'.
Ni kweli mkuu nadhani wadau wa ardhi tukiendelea kutoa mapendekezo kwa serikali kama tulivyo fanya kwenye hili tutapata jawabu na suluhu nzuri.
 
Hili nalo ni shida ,ukisikia laki na nusu ukienda kutafuta Kibali bei siyo hiyo na usumbufu wa kutosha juu wana sababu hao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hii bei ni kwenye maeneo ya yaliojengwa kiholela ndiko zoezi la urasimishaji linafanyika lakini maeneo yalipangwa vizuri bado bei za upimaji vipo juu japo tunaendelea kulisemea hili
 
Leo waziri wa ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi Mh.lukuvi alikuwa na kikao cha pamoja na makampuni ya upimaji. Kwa pamoja wamekubaliana kuwa gharama za urasimishaji zitakuwa si zaidi ya laki na nusu(150000) kutoka laki mbili na nusu(250000) hapo awali....
View attachment 1074324

Sent using Jamii Forums mobile app
Uchaguzi wa serikali za mitaa - 2019 na uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani- 2020.
 
Wala tatizo haliko kwa wapimaji .labda kwa wasio jua iko hiv, mpimaji kazi yake ni kusurvey eneo.kazi ya kurasimisha ili upate hati iko kwa serikali kuanzia kwa ofisi za ardhi katka halmashauri.hao watatakiwa kupitisha michoro na process zingine .hapa ndiyo shiida huanza .hapa kimsingi ndiyo kwenye gharama zaidi.watakupiga hela na watakuzungusha vile vile.hapo mimi nawaonaga hao
Poleni sanaa mkuu lakini kidogo saizi mambo yanaenda vizuri japo bado changamoto zipo..
 
Maafisa ardhi kwenye manispaa na halmashauri nyingi bado ni miungu watu ambao jicho la serilari bado halijawamulika vizuri.

Idara ya ardhi ni moja ya idara zenye vijana wapigadili wasio na uzalendo wala huruma kwa watanzania.

Wananchi wengi bado wanalizwa na hawa watumishi wa serikari ambao asilimia kubwa uzalendo wao uko chini ya alama 0.

Niwatu ambao wanataka uwapatie fedha hata mahala ambapo wanateleza majukumu yao ya kawaida.
 
Bado si rafiki!
Kuna maeneo kiwanja kinauzwa kuanzia 150,000.
Being inapaswa kuendana na gharama za kiwanja eneo husika, ikiwa kama lengo ni kuhasisha watu wengi wapime.
Ikumbukwe, watu wengi (hasa vijijini) wana maeneo ambayo yakipimwa yanatoa viwanja vingi.
Kwa mfano, eneo likitoa viwanja 4, mmiliki atapaswa kulipia 600,000/-. Siamini kama wengi 'watajipendekeza'.
Kijijini hawapimi viwanja, bali wanapima "Mashamba" na gharama ya kupima shamba kijijini ni sh. 1,000 kwa kila Ekari.
 
Leo nitawaeleza namna ardhi inavyopatikana tanzania
Kuna njia mkuu 5 za halali za namna watu wanavyo pata ardhi tanzania ambazo ni;
i)kutwa
ii)urithi
iii)kugawiwa na serikali
iv)kununua
V)upangishaji au kukodi

Upatikanaji wa Ardhi Tanzania
Upatikanaji wa ardhi Tanzania huwezeshwa kwa kupitia njia
kadhaa ambazo ni halali na zinazokubalika kisheria katika jamii.
Kwa ujumla mtu au taasisi anaweza kumiliki ardhi kwa ama kugawiwa, kurithishwa, kupewa, kutwaa au kununua. Sheria za Tanzania zinataja njia kadhaa ambazo mtu anaweza kupata
Ardhi nchini;
a. Kutwaa
Njia hii hutumika pale ambapo mtu huingia katika eneo
kama vile pori na kusafisha kisha kuliweka katika matumizi.
Njia hii ni kongwe sana hapa nchini. Pori linalosafishwa
linaweza kuwa ardhi ya kijiji, hifadhi au ya jumla. Ni ngumu
kutumia njia hii nyakati hizi, lakini bado inatumika katika
maeneo mengi ya Tanzania. Pale ambapo utatakiwa kufuata
taratibu kama vile kusajili utatakiwa kutii amri hiyo. Kama
utatakiwa kuhama eneo hilo basi mamlaka husika itatakiwa kulipa fidia ya maendelezo uliyoyafanya katika ardhi hiyo.
Hali kadhalika, mtu anaweza kutwaa ardhi kwa kuachwa
akae kwenye ardhi au nyumba ya mtu fulani kwa kipindi
kirefu kisichopungua miaka kumi na mbili (12) kama vile
yuko kwenye ardhi yake na kuweza kufanya kila atakavyo
bila kukumbushwa, kukemewa, kulipishwa kodi au bila
ya bughudha ya aina yeyote ya umiliki huhesabiwa kuwa
anamiliki ardhi ile kihalali. Hata hivyo, njia hii ya utwaaji
haiwezi kutumika dhidi ya ardhi inayomilikiwa na taasisi
ya serikali.

b.Urithi
Wewe kama mwanamke unaweza kupata ardhi kwa njia ya urithi. Mwanamke anaweza kurithi ardhi kutoka kwa mume
au wazazi wake kama kutakuwepo na wosia na mwanamke ametajwa katika wasio basi atakuwa na haki ya kurithi.
Kama hakutakuwa na wosia basi katika mgawanyo wa
mirathi mwanamke anayo haki ya kurithi ardhi pia. Jinsia
au tamaduni na mila haviwezi kuwa kigezo cha kumnyima
mwanamke haki hiyo ya kurithi ardhi. Mgao wowote
utakaomnyima haki hiyo kwa misingi ya jinsia au mila ni
batili na unaweza kuwafikisha wahusika mahakamani. Si tu mwanamke hata mwanaume pia.

Baada ya njia ya "urithi" kama njia moja wapo ya kupata ardhi tanzania kama nilivyo waeleza katika makala iliyopita sasa njia nyingine ni hizi hapa;

c. Kugawiwa na Serikali
Mtu anaweza kupata ardhi kwa kugawiwa na Serikali. Anaweza kuomba ardhi katika ardhi ya jumla au ya kijiji. Kamishina akiridhika kwamba umetimiza masharti atakugawia ardhi hiyo. Katika ardhi ya kijiji, serikali ya kijiji ndiyo yenye mamlaka ya kugawa ardhi. Mtu
akipeleka maombi ya ardhi serikali ya kijiji itayajadili na
kuyapeleka Mkutano Mkuu wa Kijiji kuyapitisha. Kama
maombi ni chini ya hekta 21 basi Halmashauri ya Kijiji
itamgawia ardhi hiyo.
d. Kununua
Hii pia ni njia mojawapo ambayo mtu unaweza
kuitumia kupata ardhi.Wakati mmiliki anapotaka kuuza
ardhi yake iwe ya kijiji, hifadhi au jumla, sheria inatoa ruhusa
ya kununua kama unaweza. Ugumu kwa wanawake walio
wengi kupata ardhi kwa njia hii ni uwezo wao mdogo wa
kiuchumi kuweza kumudu bei ya soko.lakini ni njia ambayo wengi hupata ardhi tanzania.
e. Upangishaji au kukodi
Upangishaji ni njia mojawapo ya kupata ardhi. Tofauti na njia nyingine za upatikanaji wa ardhi, upangishaji unakupatia haki pungufu na yule anayekupangisha.
Wanawake pia wanaweza kupata ardhi kwa kupangisha pia.

Hivyo basi watu wengi tanzania wana ardhi ya kutwa,ardhi ya kurithi,ardhi ya kugawiwa na serikali,ardhi ya kununua pamoja na ardhi ya kupangishiwa au kukodi.

*somo lijalo...
HAKI MILIKI

itaendelea......
By
Surveyor Munkondya (mpima ardhi)
Simu;0673540985
Whatsapp;0765532858
 
*Leo nitawaeleza namna ardhi inavyopatikana tanzania*
Kuna njia mkuu 5 za halali za namna watu wanavyo pata ardhi tanzania ambazo ni;
i)kutwa
ii)urithi
iii)kugawiwa na serikali
iv)kununua
V)upangishaji au kukodi

Upatikanaji wa Ardhi Tanzania
Upatikanaji wa ardhi Tanzania huwezeshwa kwa kupitia njia
kadhaa ambazo ni halali na zinazokubalika kisheria katika jamii.
Kwa ujumla mtu au taasisi anaweza kumiliki ardhi kwa ama kugawiwa, kurithishwa, kupewa, kutwaa au kununua. Sheria za Tanzania zinataja njia kadhaa ambazo mtu anaweza kupata
Ardhi nchini;
a. Kutwaa
Njia hii hutumika pale ambapo mtu huingia katika eneo
kama vile pori na kusafisha kisha kuliweka katika matumizi.
Njia hii ni kongwe sana hapa nchini. Pori linalosafishwa
linaweza kuwa ardhi ya kijiji, hifadhi au ya jumla. Ni ngumu
kutumia njia hii nyakati hizi, lakini bado inatumika katika
maeneo mengi ya Tanzania. Pale ambapo utatakiwa kufuata
taratibu kama vile kusajili utatakiwa kutii amri hiyo. Kama
utatakiwa kuhama eneo hilo basi mamlaka husika itatakiwa kulipa fidia ya maendelezo uliyoyafanya katika ardhi hiyo.
Hali kadhalika, mtu anaweza kutwaa ardhi kwa kuachwa
akae kwenye ardhi au nyumba ya mtu fulani kwa kipindi
kirefu kisichopungua miaka kumi na mbili (12) kama vile
yuko kwenye ardhi yake na kuweza kufanya kila atakavyo
bila kukumbushwa, kukemewa, kulipishwa kodi au bila
ya bughudha ya aina yeyote ya umiliki huhesabiwa kuwa
anamiliki ardhi ile kihalali. Hata hivyo, njia hii ya utwaaji
haiwezi kutumika dhidi ya ardhi inayomilikiwa na taasisi
ya serikali.

b.Urithi
Wewe kama mwanamke unaweza kupata ardhi kwa njia ya urithi. Mwanamke anaweza kurithi ardhi kutoka kwa mume
au wazazi wake kama kutakuwepo na wosia na mwanamke ametajwa katika wasio basi atakuwa na haki ya kurithi.
Kama hakutakuwa na wosia basi katika mgawanyo wa
mirathi mwanamke anayo haki ya kurithi ardhi pia. Jinsia
au tamaduni na mila haviwezi kuwa kigezo cha kumnyima
mwanamke haki hiyo ya kurithi ardhi. Mgao wowote
utakaomnyima haki hiyo kwa misingi ya jinsia au mila ni
batili na unaweza kuwafikisha wahusika mahakamani. Si tu mwanamke hata mwanaume pia.

Baada ya njia ya "urithi" kama njia moja wapo ya kupata ardhi tanzania kama nilivyo waeleza katika makala iliyopita sasa njia nyingine ni hizi hapa;

c. Kugawiwa na Serikali
Mtu anaweza kupata ardhi kwa kugawiwa na Serikali. Anaweza kuomba ardhi katika ardhi ya jumla au ya kijiji. Kamishina akiridhika kwamba umetimiza masharti atakugawia ardhi hiyo. Katika ardhi ya kijiji, serikali ya kijiji ndiyo yenye mamlaka ya kugawa ardhi. Mtu
akipeleka maombi ya ardhi serikali ya kijiji itayajadili na
kuyapeleka Mkutano Mkuu wa Kijiji kuyapitisha. Kama
maombi ni chini ya hekta 21 basi Halmashauri ya Kijiji
itamgawia ardhi hiyo.
d. Kununua
Hii pia ni njia mojawapo ambayo mtu unaweza
kuitumia kupata ardhi.Wakati mmiliki anapotaka kuuza
ardhi yake iwe ya kijiji, hifadhi au jumla, sheria inatoa ruhusa
ya kununua kama unaweza. Ugumu kwa wanawake walio
wengi kupata ardhi kwa njia hii ni uwezo wao mdogo wa
kiuchumi kuweza kumudu bei ya soko.lakini ni njia ambayo wengi hupata ardhi tanzania.
e. Upangishaji au kukodi
Upangishaji ni njia mojawapo ya kupata ardhi. Tofauti na njia nyingine za upatikanaji wa ardhi, upangishaji unakupatia haki pungufu na yule anayekupangisha.
Wanawake pia wanaweza kupata ardhi kwa kupangisha pia.


Hivyo basi watu wengi tanzania wana ardhi ya kutwa,ardhi ya kurithi,ardhi ya kugawiwa na serikali,ardhi ya kununua pamoja na ardhi ya kupangishiwa au kukodi.

*somo lijalo...
HAKI MILIKI

*itaendelea......*
By
Surveyor Munkondya (mpima ardhi)
Simu;0673540985
Whatsapp;0765532858
SAMAHANI, WEWE NI MWANASHERIA?
 
Aha ni taratibu zipi naweza kuhakikishiwa kuwa ardhi nilionunua uko sehemu sahihi kwenye ramani ya mipango miji mkuu?
 
Aha ni taratibu zipi naweza kuhakikishiwa kuwa ardhi nilionunua uko sehemu sahihi kwenye ramani ya mipango miji mkuu?
tafuta mtu wa mipango miji achukue coordinates za pale, then ataenda kwenye ramani za za mipango miji na kuangalia ardhi ya hapo matumizi yake ni yapi.... jana nimefanya hivyo, therefore nakupa uzoefu wangu
 
Aha ni taratibu zipi naweza kuhakikishiwa kuwa ardhi nilionunua uko sehemu sahihi kwenye ramani ya mipango miji mkuu?
Rahisi sana mtafute surveyor au mpima ardhi atakuja site au kweny eneo lako atachukua vipimo vya mipaka katika eneo lako alafu atapeleka wizarani au halmashauri kuangalia kama eneo lina mchoro na kama lina mchoro eneo lako lipo sehem gani katika mchoro ...
Ahsante kwa swali mkuu karibu tena
 
Hapana mkuu mimi geomatician au landsurveyor au mpima ardhi na kama mpima ardhi lazima uzijue sheria za ardhi,,hivyo basi nazijua sheria za ardhi mkuu
asante sana. Hivi planned areas, zina wamiliki wake. Sasa mnapokwenda kufanya planning katika eno la mtu bila kumhusisha, kesho akauza eneo ambalo mmepanga liwe wazi akampa akajenga nyumba ya kuishi, sheria inasemaje hapo kwa mmiliki wa hiyo ardhi? Kuna matatizo nayaona huku nilipo
 
Back
Top Bottom