Surveyormunkondya sasa nipo jamiiforum kwa ajili ya elimu juu ya masuala ya ardhi

Surveyormunkondya sasa nipo jamiiforum kwa ajili ya elimu juu ya masuala ya ardhi

tafuta mtu wa mipango miji achukue coordinates za pale, then ataenda kwenye ramani za za mipango miji na kuangalia ardhi ya hapo matumizi yake ni yapi.... jana nimefanya hivyo, therefore nakupa uzoefu wangu
Ndio pia unaweza kumtumia mtu wa mipango miji japo kazi hii hufanywa na wapima ardhi au masurveyor
 
asante sana. Hivi planned areas, zina wamiliki wake. Sasa mnapokwenda kufanya planning katika eno la mtu bila kumhusisha, kesho akauza eneo ambalo mmepanga liwe wazi akampa akajenga nyumba ya kuishi, sheria inasemaje hapo kwa mmiliki wa hiyo ardhi? Kuna matatizo nayaona huku nilipo
Mara nyingi sehemu ambazo hupangwa au kuandaliwa mchoro (planned area) huwa ni sehem ambazo hazijaendelezwa au hazijajengwa kabisa ndo hupangwa ili watu wauziwe viwanja na kujenga katika viwanja vilivyo pangwa na mara nyingi maeneo haya huwa ni ya serikali alafu serikali inaanza kuuza viwanja kupitia manispaa lakni kwa maeneo ambayo yanamilikiwa na watu alafu ikitokea serikali imeandaa mchoro huwa hivi.
Kwanza inaweza kuwalipa wananchi ili eneo liwe la serikali au itawashirikisha wananchi juu ya zoezi husika la uandaaji wa mchoro...
Isipo fanyika hivo basi wewe mwenye eneo lako na serikali imeandaa mchoro bila wewe kuwa na taarifa Utamwita surveyor(mpima ardhi) atachukua vipimo vya mipaka yako alafu ataangalia limedondokea wapi katika mchoro wa mpango mji ili ujue eneo lako lina viwanja vingapi katika mchoro wa mpango mji ndo vitakuwa vyako kulingana na eneo lako alafu unavipima unatafutia hati miliki...

Lakini mara nyingi serikali lazima iwashirikishe wananchi wenye maeneo husika kabla haijaanda mchoro..
Ahsante karibu kwa swali jingine
 
Haki Miliki
Kuna aina za umiliki ardhi kama unavyotambuliwa na sheria za nchi uko wa aina mbili:-
(i) Haki miliki ya kiserikali (granted right of occupancy), na
(ii) Haki miliki ya kimila(customary right of occupancy).
Aina hizi za kumiliki ardhi sio ngeni kwani ndizo zilikuwa
zinatumika hata katika Sheria ya Ardhi ya zamani ambayo ilifutwa na kutungwa sheria za ardhi za mwaka 1999, isipokuwa
mabadiliko mawili makubwa yamejitokeza katika sheria hizi
mpya nayo ni:-
a. Katika sheria ya zamani hakimiliki ya kisheria ilihusisha kupewa hati inayotolewa na Kamishna wa Ardhi, wakati
hakimiliki ya kimila haikuhitaji hati. Hivi sasa utaratibu ushafanyika kuwezesha hata hakimiliki ya kimila kuwa na
hati inayotolewa na kijiji.
b. Katika sheria ya zamani, hakimiliki ya kimila ilidhaniwa tu (dhana ya umiliki) kuwa na hadhi sawa na hakimiliki ya
kisheria lakini kiutekelezaji hilo halikuwezekana kwani
hakimiliki ya kimila ilichukuliwa kama haki ya matumizi tu ya ardhi na haikubeba uzito kama ilivyo kwa hakimiliki ya
kiserikali. Kwa hiyo, ilipotokea mgogoro kati ya wamiliki wawili, mmoja akiwa na hatimiliki ya kiserikali na mwingine akiwa na hakimiliki ya kimila, basi hakimiliki ya kimila ilionekana kuwa haina nguvu na hivyo kutotambuliwa. Kwa hivi sasa haki miliki ya kimila ina hadhi sawa sawa na hakimiliki kiserikali. Hata hivyo itachukua muda mrefu
kwa watu kuzoea jambo hili.

Nani Anaweza Kumiliki Ardhi?
Mtu yeyote ambaye ni;
a. Mtanzania, mwanamme au mwanamke.
b. Kikundi cha watu ambao ni raia wa Tanzania walio katika
umoja wa kisheria au la, au ni wabia au washirika,wanaweza
kumiliki ardhi.
Ifahamike kwamba mtu ambaye sio raia wa Tanzania, au kikundi
cha watu au mtu ambaye ana shirika lenye hisa, ambao wengi
wa wanahisa wake sio Watanzania hawana haki ya moja kwa moja ya kumiliki ardhi nchini na kupewa hakimiliki ya ardhi isipokuwa tu kama watapewa ardhi hiyo kama wawekezaji wa mujibu wa Sheria ya Uwekezaji ya mwaka 1997.

Utaratibu wa Maombi ya Hati ya Hakimiliki ya Kiserikali

Itaendelea.....
By surveyorMunkondya(mpima ardhi)
Simu;0765532858
Whatsapp;0673540985
 
Naomba kujua tofauti ya Ile Hati ya Ya serikali ya mtaa na Ile ya Ardhi....
 
Naomba kujua tofauti ya Ile Hati ya Ya serikali ya mtaa na Ile ya Ardhi....
Serikali ya mtaa haitoi hati na haina mamlaka ya kuuza ardhi wala kuidhinisha mauziano ya ardhi,,hati miliki ya kisheria hutolewa na serikali kupitia halmashauri husika katika kiwanja kilichopimwa hivyo basi tuliowengi kwasababu ya kutoelewa na kuamini kwamba serikali ya mtaa ndo inamtambua mmiliki halali wa eneo ndo maana wengi tunauziana kupitia kwako na hutuandika barua za mauziano na sio hati na mara nyingi hufanywa kwenye ardhi ambayo haijapimwa..
Ahsante karibu kwa swali jingine
 
Serikali ya mtaa haitoi hati na haina mamlaka ya kuuza ardhi wala kuidhinisha mauziano ya ardhi,,hati miliki ya kisheria hutolewa na serikali kupitia halmashauri husika katika kiwanja kilichopimwa hivyo basi tuliowengi kwasababu ya kutoelewa na kuamini kwamba serikali ya mtaa ndo inamtambua mmiliki halali wa eneo ndo maana wengi tunauziana kupitia kwako na hutuandika barua za mauziano na sio hati na mara nyingi hufanywa kwenye ardhi ambayo haijapimwa..
Ahsante karibu kwa swali jingine
Ok,Ahsante...kuna hasara gani Ukimiliki Ardhi kwa kutumia hizi barua za mauziano za serikali ya mtaa.
,
 
Nifuate utaratibu gani ili nipate hati halali ya kumiliki aridhi mfano kiwanja kilichopimwa?.
 
Mkuu asante sana kwa kuja na hii topic muhimu sana. Naomba kuuliza swali. Hivi kama nikiuziwa kiwanja harafu nikaenda halmashauri kwa malengo ya kutaka kujua hicho kiwanja kina wamiliki wengine. Nikipewa invoice za kulipia hati tayari huo ni ushahidi tosha kwamba hicho kiwanja hakina mmiliki mwingine? Kwa kifupi hivi halmashauri inaweza kutoa invoice za kulipia hati kwa watu wawili??? Naomba elimu hapa!
 
Ok,Ahsante...kuna hasara gani Ukimiliki Ardhi kwa kutumia hizi barua za mauziano za serikali ya mtaa.
,
Hasara ni kubwa sana kwasababu hizo barua sio halali hivyo basi serikali haitambui umiliki wako mfano ikitokea mtu ana hati miliki kwenye hilo eneo na wew una barua ya mauziano serikali itamtambua huyo mtu mwenye hati miliki ndo mmiliki halali na sio wewe mwenye barua ya mauziano..
Lakini pili ni rahisi kwa mwenyekiti kuhararisha mauziano na mtu mwingine katika eneo moja na ndo maana migogoro mingi ya mauziano ya nyumba au kiwanja kwa zaidi ya mtu mmoja hufanywa katika serikali za mitaa...
 
Serikali ya mtaa haitoi hati na haina mamlaka ya kuuza ardhi wala kuidhinisha mauziano ya ardhi,,hati miliki ya kisheria hutolewa na serikali kupitia halmashauri husika katika kiwanja kilichopimwa hivyo basi tuliowengi kwasababu ya kutoelewa na kuamini kwamba serikali ya mtaa ndo inamtambua mmiliki halali wa eneo ndo maana wengi tunauziana kupitia kwako na hutuandika barua za mauziano na sio hati na mara nyingi hufanywa kwenye ardhi ambayo haijapimwa..
Ahsante karibu kwa swali jingine
HILI, umelifanyia utafiti vizuri? Kwa maana ni Kwamba wanasheria Wanatumia serikali za mitaa Kwa sababu ndiyo watu wanaojua maeneo, na Hii ni Kwa mauziano ya ardhi ambazo hazijapimwa, na hizo hati za kimila zinatolewa na sheria ya ardhi ya vijiji na kanuni zake,
 
Sheria ya usajili wa ardhi (land registration act) na kanuni zake, zinakuruhusu kwenda kufanya search kwenye masijala za ardhi, ili kugundua Kama hicho kiwanja kina milikiwa kweli na anayekiuza,
Mkuu asante sana kwa kuja na hii topic muhimu sana. Naomba kuuliza swali. Hivi kama nikiuziwa kiwanja harafu nikaenda halmashauri kwa malengo ya kutaka kujua hicho kiwanja kina wamiliki wengine. Nikipewa invoice za kulipia hati tayari huo ni ushahidi tosha kwamba hicho kiwanja hakina mmiliki mwingine? Kwa kifupi hivi halmashauri inaweza kutoa invoice za kulipia hati kwa watu wawili??? Naomba elimu hapa!
 
pia lukuvi alishasema kununua ardhi kwa wenyekiti ni sawa na kununua bomu muda wote linaweza kulipuka sababu moja wapo mihuri ya wenyekiti haina kibali cha kutumika kwenye mauziano ya ardhi hivyo ni sawa haujanunua kitu, hilo hilo eneo akitokea mwingine amenunua kwa mkataba wakili ujue bomu limeshalipuka
Hasara ni kubwa sana kwasababu hizo barua sio halali hivyo basi serikali haitambui umiliki wako mfano ikitokea mtu ana hati miliki kwenye hilo eneo na wew una barua ya mauziano serikali itamtambua huyo mtu mwenye hati miliki ndo mmiliki halali na sio wewe mwenye barua ya mauziano..
Lakini pili ni rahisi kwa mwenyekiti kuhararisha mauziano na mtu mwingine katika eneo moja na ndo maana migogoro mingi ya mauziano ya nyumba au kiwanja kwa zaidi ya mtu mmoja hufanywa katika serikali za mitaa...
 
HILI, umelifanyia utafiti vizuri? Kwa maana ni Kwamba wanasheria Wanatumia serikali za mitaa Kwa sababu ndiyo watu wanaojua maeneo, na Hii ni Kwa mauziano ya ardhi ambazo hazijapimwa, na hizo hati za kimila zinatolewa na sheria ya ardhi ya vijiji na kanuni zake,
Ndio mkuu serikali ya kijiji inatoa ardhi ya kijijini lakini serikari ya mtaa ambayo ndo ipo mjini haina mamlaka ya kuuza ardhi mkuu
 
Back
Top Bottom