Swali ambalo Hayati Mwalimu Nyerere aliulizwa na wazungu akajibu kisanii matokeo yake tunayaona sasa

Swali ambalo Hayati Mwalimu Nyerere aliulizwa na wazungu akajibu kisanii matokeo yake tunayaona sasa

Ulitaka ajibu vipi? Kwamba bado hatujakua tayari kujitawala? Wee ndio wale wamelewa kasumba ya wazungu. Kwani wenyewe unaamini walikua wanatutawala ili tupate uwezo wa kujitawala? Hakika watu ka wewe wanatia huruma kwa ujinga.
Anafikiri ni haki yake kutawaliwa na wazungu. Akili za kitumwa! Haelewi kwamba wazungu ndio waliharibu jamii zetu tungekuwa mbali sana bila kutawaliwa na hawa mashetani!
 
Ulitaka ajibu vipi? Kwamba bado hatujakua tayari kujitawala? Wee ndio wale wamelewa kasumba ya wazungu. Kwani wenyewe unaamini walikua wanatutawala ili tupate uwezo wa kujitawala? Hakika watu ka wewe wanatia huruma kwa ujinga.
Ujinga ni kuwa na kiherehere kilicho jaa ujinga wa kufikiri kila kitu kinahitaji majaribio
 
Wazungu hawa walimuuliza swali hili Nyerere lakini yeye akatoa majibu ya kisanii.

Matokeo ya hili swali tunayaona sasa baada ya miaka 60 kupitia katika mataifa yetu.

Hawa wazungu walikuwa sahihi sana kuulizia za hili swali bila shaka kuna kitu walikiona ambacho yeye Nyerere na wenzake kwa wakati huo hawakukiona.

Mfano mwengine uliohai ni Africa kusini mpira wanarudishiwa makabulu taratibu kwa aibu kubwa.


Nikushukuru, mkuu 'Mto Songwe' kwa kumbukumbu hiyo ya miaka mingi iliyopita.

Ila sioni jibu la "usanii" kama ulivyo liona wewe. Badala yake naona jibu linalojitosheleza kabisa toka kwa kiongozi mweusi anayejitambua kabisa, tena nyakati hizo za giza nene kwa wengi.

Sijui sababu zako za kulipa "usanii" jibu hilo, maanake hukujieleza vya kutosha (hilo pekee ni tatizo kwa upande wako), na badala yake ukatoa vi-mifano tu vya uongo na kweli hapa na pale; kama hiyo Afrika ya Kusini, mfano ambao nadhani huelewi maana yake.

Katika hilo jibu unaloliita la "kisanii", wewe kwa matarajio yako ulifikiri tokea mwaka namba moja katika hiyo sitini uliyoitaja, maendeleo yangekuwa yanatiririka tu kama mvua au siyo? Ungetegemea kila mwaka, katika miaka hiyo sitini uchumi uwe unapaa juu juu zaidi kila mwaka, bila ya vikwazo vyovyote!
Na ulitegemea hao hao tulionyang'anya uhuru wetu toka kwao wawe wapo wapo tu wakitushangilia jinsi tunavyoonyesha umahiri wetu kujiletea maendeleo!

Sifurahii kulisema hili, lakini leo hii unaiona Tanzania hii hii kama Mwalimu alivyo iona mwaka 1961, kweli?

Hebu ngoja: tueleze wewe, mkuu 'Mto Songwe', kati ya hao wakubwa tulionyang'anya uhuru wetu kwao, ni nani aliye weza leta mabadiliko makubwa katika nchi zao ndani ya hiyo miaka 60, unamjuwa?

Sasa naomba usinielewe vibaya. Hapa sitetei kwa namna yoyote ile maovu na uozo mwingi tunao ushuhudia katika nchi zetu hizi (za aki Afrika, sitaki kujihusisha na kwingine); lakini hili tunapolitambua lisiwe ndiyo iwe sababu ya kujidhalilisha utu wetu.
Ndio, tunao viongozi wa hovyo kabisa. Hili halimfurahishi yeyote; lakini wapo pia viongozi wanao pambania nchi zao na wananchi wao, hawa wapo; kama ilivyo kwa hao hao wakubwa unaowashadadia sana.

Hata katika nchi zetu hizi za kipuuzi, taratibu, tunakwenda hivyo hivyo mbele, hatutabaki daima wote kuwa kama Haiti.

Sasa tueleze wewe, ulitaka jibu la namna gani Mwalimu Nyerere alitowe katika mjadala huo ambalo lingeonekana kuwa sahihi kwa upande wako?
 
Pengine hata Nyerere hakuwa ameelika vya kutosha kuwa raisi,
Àliijenga nchi kisiasa Zaidi Kuliko kuwajengea wananchi wake ujuzi sahihi wa Maarifa ya kiuchumi kwenye uvuvi, ufugaji, utalii, Biashara.

Alifanya kila kitu kisimamiwe na serikali ambaye Ndio raisi, kupitia Chama chake.

Hakutaka wananchi kumiliki uchumi, hata kumiliki gar Benz unaonekana kitu cha ajabu, sasa kulikuwa na maana Gani ya kupata Uhuru, wakati wananchi hawana na hawatakiwi kumiliki uchumi wa nchi Yao,

Yani ilifikia kipindi aliyesoma na àsie soma kuwa ni kitu kimoja
Sikosei hata mara moja nikikuita wewe MJINGA.
 
Nyerere alijibu Kama ilivyotakiwa kuwajibu. Hilo jibu lilikuwa Smarter!
 
Hapa kajibu ki uvccm...
'do you have essential skills and equipment to govern yourselves?'
Hili swali mpk leo jibu ni no
Kaanza kuleta habari za jacket.

Hili ni swali wagombea wanapaswa kuulizwa.

Hata huyo mwana mama mzungu katika maelezo yake ya awali hajasema Afrika isipatiwe uhuru lakini kauliza swali ambalo Nyerere alipaswa kutuliza kichwa.
 
Nyerere alikua sahihi kwa jibu alilotoa , hata kama alituingiza kwenye mfumo wa ujamaa ! Ila watu wote waliopita kijiti walichoachiwa ndo wametufelisha mpaka hapa ! Hebu angalia kama CCM now yaan haina mvuto hata kidogo , raia tunapangiwa hata wakishindwa uchaguzi wanalazimisha !
Ni wezi , ni wazandiki na wanajipendekeza
Sioni sababu yoyote ya wewe na wengine kujutia mara kwa mara "...hata kama alituingiza kwenye mfumo wa ujamaa..." Hii ni kasumba tu iliyo ingizwa vichwani mwa watu, enzi hizo za "Vita Baridi."
China huyo hapo, kama mfano hai, ambaye hajutii chochote yeye kupitia na kuwa katika u-Komunisti.
Nionyeshe nchi yoyote ile Afrika, ambao wao hawakuwa na huo "ujamaa", lakini leo wame neemeka sana kwa mfumo mbadala ulio wawezesha.
Nionyeshe nchi yoyote ile duniani, ambayo, siyo leo tu, bali tokea enzi na enzi hawakuweza kuwa na "ujamaa" ndani yao.

Ni wakati sasa hivi kujisafisha vichwa vyenu muelewe kwamba hakuna mfumo wa uchumi unaojitegemea wenyewe, bila kuchanganyika na mwingine kuleta mabadiliko chanya katika nchi zao.
 
Wazungu hawa walimuuliza swali hili Nyerere lakini yeye akatoa majibu ya kisanii.

Matokeo ya hili swali tunayaona sasa baada ya miaka 60 kupitia katika mataifa yetu.

Hawa wazungu walikuwa sahihi sana kuulizia za hili swali bila shaka kuna kitu walikiona ambacho yeye Nyerere na wenzake kwa wakati huo hawakukiona.

Mfano mwengine uliohai ni Africa kusini mpira wanarudishiwa makabulu taratibu kwa aibu kubwa.

Nyerere aliwajibu jibu la kifalsafa sana, jibu la immanent critique, jibu la kuhoji swali lenyewe kama limekaa sawa ama la.

Waafrika wanastahili kujiongoza wenyewe, wakijiongoza vizuri au vibaya hilo ni tatizo lao.

Baada ya vita vikuu vya pili vya dunia wazungu walikuwa washachoka kuendesha makploni anyway.

Hatujapata uhuru kwa sababu Nyerere alidai uhuru.

Tulipata uhuru kwa sababu Waingereza waliona kuendesha makoloni ni gharama na wanaweza ku control dunia bila ya gharama za kuendesha makoloni.
 
Kaanza kuleta habari za jacket.

Hili ni swali wagombea wanapaswa kuulizwa.

Hata huyo mwana mama mzungu katika maelezo yake ya awali hajasema Afrika isipatiwe uhuru lakini kauliza swali ambalo Nyerere alipaswa kutuliza kichwa.
Mzungu hakuwa na haki ya kupanga Afrika ipate uhuru lini, kwa sababu uhuru wa Afrika haukuwa wa mzungu kuutoa.

Hayo matatizo mengine ya Afrika ni ya Waafrika.

Usichoelewa nini?

Zimbabwe imesubiri mpaka 1980 kupata uhuru, na mpaka sasa kuna matatizo.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Mzungu hakuwa na haki ya kupanga Afrika ipate uhuru lini, kwa sababu uhuru wa Afrika haukuwa wa mzungu kuutoa.

Hayo matatizo mengine ya Afrika ni ya Waafrika.

Usichoelewa nini?

Zimbabwe imesubiri mpaka 1980 kupata uhuru, na mpaka sasa kuna matatizo.
Umesikiliza hicho kipande chote cha interview ?
 
Wazungu hawa walimuuliza swali hili Nyerere lakini yeye akatoa majibu ya kisanii.

Matokeo ya hili swali tunayaona sasa baada ya miaka 60 kupitia katika mataifa yetu.

Hawa wazungu walikuwa sahihi sana kuulizia za hili swali bila shaka kuna kitu walikiona ambacho yeye Nyerere na wenzake kwa wakati huo hawakukiona.

Mfano mwengine uliohai ni Africa kusini mpira wanarudishiwa makabulu taratibu kwa aibu kubwa.

.. kama Kuna ukweli hivi!
 
Wazungu hawa walimuuliza swali hili Nyerere lakini yeye akatoa majibu ya kisanii.

Matokeo ya hili swali tunayaona sasa baada ya miaka 60 kupitia katika mataifa yetu.

Hawa wazungu walikuwa sahihi sana kuulizia za hili swali bila shaka kuna kitu walikiona ambacho yeye Nyerere na wenzake kwa wakati huo hawakukiona.

Mfano mwengine uliohai ni Africa kusini mpira wanarudishiwa makabulu taratibu kwa aibu kubwa.

Akina Nyerere, Mobutu, Mugabe,Jomo kenyata, Mseveni walipigani nchi zao sio kwa sababu wana uchungu kwa Raia na mataifa yao bali Uchu wa Madaraka tu.

Majority waliishia kuwa madikiteta na miungu watu tu na hawakutaka kabisa kuachia madaraka
 
Akina Nyerere, Mobutu, Mugabe,Jomo kenyata, Mseveni walipigani nchi zao sio kwa sababu wana uchungu kwa Raia na mataifa yao bali Uchu wa Madaraka tu.

Majority waliishia kuwa madikiteta na miungu watu tu na hawakutaka kabisa kuachia madaraka
MtoeNyerere,Mugabe n Kenyata hapo...z!
 
Back
Top Bottom