Uchaguzi 2020 Swali fikirishi: Je, kuna mtu timamu kiakili atamchagua John Magufuli licha ya ugumu wa maisha, uonevu kwa wafanyabiashara, wakulima na wafanyakazi?

Uchaguzi 2020 Swali fikirishi: Je, kuna mtu timamu kiakili atamchagua John Magufuli licha ya ugumu wa maisha, uonevu kwa wafanyabiashara, wakulima na wafanyakazi?

Sio kweli,utafuatilia watu zaidi ya milioni 10 kwa faida ipi sasa?,mda wenyewe upo?,
Kama hujui bora unyamaze kimya. Nimesema na ninasema tena kuna watu wanawafuatilia upigaji wa kura wao, sijasema wapiga kura wote. Kwani ulijuwa kama simu za viongozi zinasikilizwa?
 
Paschal unajipaka kinyesi kwa kutetea vitu vya ajabu.Yaani mtu na akili zako timamu umpe kura Magu ? Kwa sababu zipi hasa? Ndege 11? Bwawa ambalo lipo 20% kwenye ujenzi wake au reli ambayo ndo kwanza kipande Cha Moro dar kipo 50% ya ujenzi wake?
Shida ni pale propaganda zinapozidi uhalisia
 
Angalau unavyo vya kutaja vya Magu, vipi vya Lissu?
Lissu alikuwa anakusanya Kodi ipi ya kumuwezesha kujenga miundombinu? Ama kweli nawe ni great thinker wa jf huenda unaaminika Hadi mtaani kwenu!
 
Siwezi kumchagua sababu: anatufanya tuwe tegemezi, hakuna ajira, hakuna mikopo kwa watu wa hali ya chini,gharama za maisha n ngumu kiujumla
 
P!
Is it you au wamehaki account yako? Mbona umeamua kuichagua elimu na nafsi yako? Au Maisha yamekuwa tight Sana Hadi ujitoe ufahamu kwa kujidhalilisha hivi? Hebu Rudi kwenye uhalisia wako na uache kujirahisi hivi! Kwani ni lazima Sana upewe uteuzi ndio ule? Au unamtetea poti kwa kusaidiana na Bishop mfufua wafu?
 
Hata wew ukiwa raisi leo huwez kupendwa na kumfraisha kila mtu..hata Tl akichukua Nchi after 5 yrs wa TZ mtakua hamumtaki
 
Lissu alikuwa anakusanya Kodi ipi ya kumuwezesha kujenga miundombinu? Ama kweli nawe ni great thinker wa jf huenda unaaminika Hadi mtaani kwenu!
Maisha nyuma ya keyboard ni tofauti na maisha halisi mkuu!
 
Kwanza pole!, pili dalili za udikiteta ni jambo moja, na Udikteta halisi ni jambo jingine!.
Kwa Tanzania mahali tulipofikia, hadi kuwa shamba la bibi, tulihitaji mtu kama Magufuli, na matokeo tumeyaona, ndani ya miaka 5, tumeuaga umasikini na kuwa nchi ya uchumi wa kati!.

Tukumpa mitano mingine, tunakwenda kuwa nchi ya uchumi wa kati mkubwa, na tukibadili katiba aendelee tuu,Tanzania tunakwenda kuwa nchi ya uchumi mkubwa, nchi tajiri, a donor country.

Fuatilieni utawala wa Tiger Nations, bila udikiteta, zisinge toka!. Sio kila udikiteta ni udikiteta mbaya, au udikiteta katili, kuna udikiteta wa kizalendo unaitwa, benevolence dictatorship!, hivyo rais Magufuli ni dikiteta Mzalendo anayefanya udikiteta kwa nia njema kulikomboa taifa!.

Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata!. Atakayeleta Fyoko, Ataisoma Namba!

P

Hivi umewahi kusafiri nje ya nchi? maana naona kama unahitaji ufunguliwe fikra. Hivi yule Mayala aliyeuliza swali Magufuli ni wewe kweli?
 
Hata ujikombe vipi wewe you are done with this regime. Kuna watu wamemuita yesu (Kangi Lugola) na bado amewatosa. Mayalla tunajuwa uwezo wako wa kuchambua na uandishi, wewe siyo type ya kusifu na kuabudu ila unafanya hivyo ili wakuone. Fanya yako, be yourself, linda hadhi uako. Hii njaa ina mwisho
 
Hakuna labda kichaa tu na mnufaika wa utawala huu ,mtu timamu heri amchague hata Rungwe tu
 
Naona Shida Sio Dr. Magu.
Shida ni CCM na makada, au watendaji (wateuliwa) makada.

Naona Kama Kuna baadhi na inaweza ikawa wengi. Wanamdanganya kwa kutompa uhalisia.

Au wanaogopa kumwambia ukweli, au wanaogopa kumshauri.

Vyovyote vile sio kisingizio kwa Hao waliopewa dhamana kwenye nafasi mbalimbali, kukwepa majukumu yao ya kumsaidia Raisi kutenda kwa kuendana na Sheria. Maana Raisi anaweza asiwe mtaalam wa Sheria.

Mfano nimeuona kipindi hiki Cha uchaguzi, na kipindi kile Cha uchaguzi wa serikali za mitaa.

Inaonekana, Kama sio watendaji walifanya uonevu, Basi walikosa busara.


Hata Sasa hivi, sijaelewa imekaaje wagombea mbali mbali wa Upinzani wameenguliwa. Na Kuna vituko vingine vya wazi wazi, vilivyofanywa na wakurugenzi wa baadhi ya halmashauri.


Hiyo inafanya serikali ikose sifa, au inachafuliwa sifa ya kuwa serikali isiyo baguzi, na inayotenda haki kwa usawa.Hivyo inakosa haki ya kimaadili kupewa dhamana ya kusimamia Uchaguzi.

.
.
.hivyo jibu Ni NDIO wapo watu wengi walio timamu watakao mpigia Kura mgombea wa Uraisi wa CCM. Na wengi tu watawapigia wagombea wengine wa CCM.

Pia wapo watakaopiga kwa Maslahi binafsi, wapo watakao piga sababu ya mazoea na hawafuatilii Siasa, au mwendo na matendo ya Serikali . . . .

Wapo watakao chagua CCM, kwa sababu tofauti, tofauti. Na wapo wengi Sana, naamini zaidi ya unavyohisi ama kufikiria. . . .na Dr.Magu Ana nafasi ya Kushinda Uchaguzi kihalali kabisa, Kama ilivyo kwa mgombea/au wagombea wengine wa Uraisi.. .

Hata Mimi tangu kampeni zinaanza , pamoja na kuusikiliza Sera za Vyama ambavyo walisha tambulisha sera/ ilani zao Kama CHADEMA.

Pamoja na Mapungufu Mengi niloyaona kipindi Cha uongozi huu, bado niliona na nilikua na Nia ya kumchagua Dr. Magu. Sababu kila uongozi una Mapungufu yake.


Tatizo lilikuja nilipoanza kufuatilia Kampeni za CCM. Zilini sikitisha. Naamini kabisa, gharama wanazotumia hazikua na ulazima huo.Nguvu wanayotumia kupata hadhira , haipo sawa (haipo fair).

Swala Hilo limenitafakarisha Sana. Kwamba kwa nini wanatumia nguvu kubwa Sana kutafuta kuchaguliwa.

Je hizo rasilimali zinazotumika kufanya kampeni(gharama), sio za watanzania kweli!. ( Maana naona Kuna kila ishara kwamba fedha zinazotumika haziwezi kuwa ni za Chama tu. Japo CCM Ina mali nyingi{ haijalishi wamezipataje}, bado haiwezi ikawa na fedha kiasi cha kuweza kuzitumia kiasi hiki kwenye kampeni).

Kama ni fedha za wanachi(serikali), kwanini zitumike namna hii, kupita kiasi. Ukiangalia kwamba, hazina uwiano kabisa na gharama wanazo tumia wapinzani wao, hata hao wa Karibu ACT, na CHADEMA. Hawajafikia hata kwa mbali matumizi yao.

Zadi Kuna namna mtu akiongea ananikosesha Imani, kudhihakiana(bila matusi),kupingana kupo.
Ila Kuna swala Dr. Magu sikubaliani nae. Ninaweza nikamchagua yeye kwa nafasi yake ya Uraisi. Ila nisimkubali mbunge wa CCM. Nikaamua kumchagua mwakilishi kutoka Chama Kingine.

Sasa hapo Dr. kasema wazi wazi kwamba ukimchagulia mwakilishi wa chama tofauti na Chake, hata leta maendeleo kwenye eneo husika. Sasa sijui ni vitisho au anamaanisha.

Ila kwa kusema hivyo maana yake ni kwamba mimi( wanachi) wanampa Kura yeye kwa kumuamini. Halafu yeye anawaadhibu kwa kufanya Uchaguzi sahihi wa mwakilishi wao(wanaomtaka).


Ili kuepuka Adhabu hiyo inawapasa wafanye nini.

Inawapasa wasi mchague yeye. Huo ndio ujumbe anao wapa. Kwamba Kama hamumkubali mgombea wa CCM kwenye nafasi ya Ubunge. Hakikisheni pia na Mimi siwi Raisi wenu. Nikiwa Raisi , haijalishi hata kama mlinipigia Kura Mimi kwenye nafasi ya Uraisi . Imekula kwenu.


Pamoja na Mambo mengine Mengi.

Jinsi CCM na Dr.Magu anavyoendesha Kampeni, anafanya hata Yale mazuri yalipatikana kipindi Chake yasiwe na maana kwenye kumuongezea Point( credits ). Japo yeye alichochea kwenye kuyasimamia na kuhakikisha utekelezaji wake, inaonekana Sasa kwamba kumbe ni juhudi tu za watumishi na baadhi ya watendaji.

Ushauri wangu ni , kabla ya kuanza Kampeni Raisi aliye madarakani aachie ngazi , awe Raia Kama wengine.
Ili apate mapumziko aweze kweli kuongea hoja bila stress.

Au walau, apewe likizo ya Lazima. Angalau Week Mbili.

Majukumu yake wapo wengi tu wa kuyakaimu. Akiwemo Makamu wake.

.

Nadhani Sasa hivi Dr. Yupo mapumziko.
Naamini akirudi atakuja na namna Bora ya kutoa hoja kwenye Kampeni.


Vinginevyo, Kuna mawili endapo atakuwa Raisi kwenye Miaka mitano ijayo.

Aidha itakua mizuri yenye Maendeleo Makubwa zaidi ikiwemo na kukamilika kwa Miradi aliyoianzisha. Hivyo kuwa na ziada ya kuweza kuboresha Maslahi kwa wananchi, Watumishi, ikiwemo kuwapandisha madaraja na mishahara.

Na yeye akaretire zake kwa amani na furaha.

Ama mitano ikawa mibaya zaidi.

Kutopeleka "Maendeleo" kwa wenye wawakilishi wa upinzani.

Kukaza Zaidi maana Hana haja ya kubembeleza sababu Hana mpango wa kuja kuwaombea Tena ridhaa.

Kukaza Zaidi, pia ilikulazimisha Miradi yake inaisha kabla hajatoka madarakani.

Au ikawa Noma zaidi, kujiongezea Muda.

Hilo ndilo pekee ninaloliona la yeye kuhitaji wabunge wawe wa CCM tu. Kama anavyosema ili aweze kuwabana. Maana yake hata kwenye Hilo akiamua anaweza akawabana wakabadili katiba/ Sheria ikamruhusu akae zaidi ya kumi.

Nimejibu ama nimepitiliza
 
wewe ni kundi gani? mkulima, mwananchi usiye na kazi, mfanyabiashara, mfanyakazi ama upo upo tu wala hujielewi?
Haha mku nilikuwa shamba nakujibu sasa, mimi ni
1.Mkulima
2.Mfanyabiashara
3.Mwajiliwa
4.Mwajili wa wafanyakazi 15. Wenye elimu professional ni 2. 13 ni wasaidizi tu.
Unalingine?
 
.
FB_IMG_15998592496809455.jpg
 
Ko unamlilia nani?
Baba mpumbavu ndiye pekee anaweza asiwanunulie watoto wake chakula au kuwalipia wanae Ada eti kisa anajenga nyumba.Kuacha kuongeza mishahara ya wafanyakazi.

kuacha kuwapandisha madaraja, kuacha kuwapa increment yao ya kila mwaka kwa kisingizio cha kujenga SGR or mwl Nyerere Hydro power si tu ni upumbavu wa baba bali roho mbaya na uuwaji.

kiufupi Magu hakupaswa hata kuteuliwa na CCM kugombea maana hajui kazi za msingi za serikali ni zipi na hajui nani mmiliki wa serikali aliyokuwa anaiongoza.Hovyo kabisa huyu mtu.
 
Back
Top Bottom