Swali Fyatu la Mwezi: Wakimpa Sifa Zake, Watapunguza za Kwao?

Shida ni low intelligence na underperformance ndiyo maana wanaiba na kupora kazi na jasho la wengine, unajiuliza Tanzania ni nchi inayoendelea kuna mambo mengi wanaweza kufanya sasa hivi na kujivunia lkn hawafanyi chochote daraja la Salenda walisema ni wao, hata la Busisi wanasema ni wao wamejenga, Stiegler ilikuwepo miaka yote hakuna aliyethubutu kujenga kaja mwamba kajenga leo hii wanajisifia wanasema ni wao wamejenga, shida ni hiyo hapo juu hawaoni kingine wanachoweza kufanya wanaishia kupora kazi za wengine, Mgufuli alikuwa anaibua mambo ambayo watu hata walikuwa hawaelewi, aliwezaje? Jibu ni intelligence, hiyo ndiyo tofauti, …
 
Mpango mzima wa kuhamisha makao makuu ya serikali kwenda Dodoma, pamoja na kujenga Ikulu mpya, ni White Elephant Project.

Yani tumetatua tatizo ambalo halipo, wakati matatizo yaliyopo mengi tu bado hatujayatatua.

Sasa hapo kuna kipi cha kusifia?
 
Wazo na mpango wa kuhamishia makao makuu Dodoma lilikuwa moja ya makosa makubwa ya Mwl. Nyerere. Hayati Magufuli akaongeza ukubwa wa kosa kwa kutumia rasilimali za nchi (na madeni juu) kukimbilia Dodoma.

Time will tell....and prove that they were both deadly wrong. Tuombe uzima 10-15yrs from now turudi hapa kujadili faida na hasara za Dodoma kwa nchi, uchumi na hata siasa za Tanzania from actual/experiential view stand.

Tunajaribu sana kutumia hisia na propganda kupingana na ukweli rahisi lakini Dodoma - ikulu, makao makuu nk ile ni sunk cost!
 
Sijui watu wanasifia nini ujinga huu.

Kibaya zaidi watu wanaongeza gharama kwa safari zisizoisha za Dar - Dodoma, mpaka wamemfanya Jenerali Ulimwengu aseme mji mkuu wa Tanzania ni barabara ya kati ya Dar na Dodoma!
 
Sijui watu wanasifia nini ujinga huu.

Kibaya zaidi watu wanaongeza gharama kwa safari zisizoisha za Dar - Dodoma, mpaka wamemfanya Jenerali Ulimwengu aseme mju mkuu wa Tanzania ni barabara ya kati ya Dar na Dodoma!
Pamoja sana Kiranga.

Wanashabikia mambo yanayoliumiza taifa, maisha yao, watoto wao na yasiyo na tija kabisa! Ni wazimu mtupu!

Let's hope, one day maybe, time will teach them something
 
Huyu mzee ndio maana anaishi umri wa kutosha. Ni mkweli wa dhati!
 
Mpango mzima wa kuhamisha makao makuu ya serikali kwenda Dodoma, pamoja na kujenga Ikulu mpya, ni White Elephant Project.

Yani tumetatua tatizo ambalo halipo, wakati matatizo yaliyopo mengi tu bado hatujayatatua.

Sasa hapo kuna kipi cha kusifia?
Mjadala sio faida na hasara za kuhamia Dodoma, bali watu kujivisha sifa wasizostahili kabisa. Bora wangesema ni white elephant za Magufuli tuelewe kuwa wanamalizia miradi kwavile hawana jinsi.
 
Mjadala sio faida na hasara za kuhamia Dodoma, bali watu kujivisha sifa wasizostahili kabisa. Bora wangesema ni white elephant za Magufuli tuelewe kuwa wanamalizia miradi kwavile hawana jinsi.
Huyo Magufuli na warithi wake wote wanaendeleza ujinga ule ule tu.

Sioni wapi unaanza kusifia.

Tatizo tunaendekeza siasa za team hii au ile.

Yani hata kama suala zima ni ujinga mtupu, tutashindana nani apate sifa.

Sifa za nini? Za kukamilisha ujinga?
 
Tuko nyuma sana na mambo mengine ni ya kawaidi sana kwa viongo kuamua.
 
Huo uchumi upo wapi jpm kawaachia karobu 5b usd leo mmezikopa kila mahalai ni ufisadi halafu mnakuja kusema eti pesa zimeongezeka
 
Wapwani si unawajua tena na korosho zao, wanahisi wakimtaja mwamba huyu hawana chao tena japo wanajisahauliaha na kujivika miwani ya mbao wakidhani kumuua JPM kutawafanya watanzania wamtoe mihoyoni mwao ....never ever!
 
Siasa za Africa sehemu nyingi zina tatizo kubwa sana la ku revolve around personalities kuliko ku revolve around policies.

Halafu Waafrika wengi hawawezi fikra dhahania, wanataka vitu vya kuona.

Ndiyo maana watu hawawezi kuongelea fiscal responsibility, lakini ni warahisi sana kuongelea nani kajenga nini.

Ndiyo uwezo wa watu wengi ulipoishia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…