Swali: Kama umeme unaleta hasara ukisafirishwa umbali mrefu, huo wa Ethiopia via Kenya haupotei?

Mnapewa mkopoo mkubwa mjenge bwawaa la kuzalisha umeme mnazalisha umeme mnaomba mkopo mwingine wa kusambaza umeme mahali ambapo zamani umeme ulikuwa unafika vizuri tu sasa sijajua umeme unaozalishwa sasa una utofauti gani na wa miaka hiyo. Ni UPUUZI NI UPUMBAVUUU.
 
Ni Mimi au ni Tanesco na Serikali? By the way huo umeme wa bwawa la Nyerere ni kweli sehemu yake utakuwa hasa Zambia na kazi inaendelea
Kwahiyo tulijenga ili tuwanufaishe kwanza Wazambia?

Hapa kwetu umeme ni ghali ukilinganisha na nchi kama Zambia, swali langu ni je, tutawauzia Zambia kwa bei nafuu ili waununue ama ni vipi?

Wamesema kusafirisha umeme kutoka kusini mwa Tanzania kwenda kaskazini mwa nchi ni ghali je, kuutoa umeme Rufiji kwenda Zambia ndiyo karibu?
 
Naona Tanzania imeamua kurudisha RICHMOND, ESCROW NA MEREMETA kijanja. Yani utamshauri nani kuwa umeme wa kutoka bwawa la Nyerere ni gharama kubwa kuzambaza kwenda Kanda ya kaskazini. Je Kigoma, Lindi, Ruvuma, Mtwara itakuwaje. Yani mnataka kusema chumvi iliyopo kabatini ni gharama sana kuichukua na kuitumia, eti kwenda kuomba ya jirani ndo inakuwa rahisi? Msitutanie tunawaangalia tu. Alafu mheshimiwa Samia mbona kama wewe ni mwepesi tu kudanganywa? Au hii mipango inawekwaga tu wewe unaletewa kutusomea wananchi?
 
Tumezoea kuagiza kila kitu nje ya nchi tukiamini ni bora kuliko vinavyozalishwa ndani. Nadhani umeme wa Ethiopia ni bora au mtamu zaidi kuliko wa JNHPP.
February Marope planned it all kila alichoplan Marope kinatekelezwa, deal done alipochomolewa hayo yote yalipigwa chini na juzi Mpishi kasema anamrudisha Marope naona yale ya Marope yote yanatekelezwa taratibu sana yaan
 
Hayo maswali hawayataki na hawatokujibu wao wanachotaka ni hela wakanunue umeme Ethiopia hayo ya Ethiopia wanapata hasara au faida kusafirisha umeme haiwahusu, hela washachukua kwenda kununua umeme Ethiopia tulia au wamefanya vibaya kukupa taarifa? Mpishi amekosea?
 
Maji ya ziwa Victoria yanayoenda kuzalisha umeme Ethiopia, leo hii tuna mito, bahari, mabwawa, ziwa tena tukanunue umeme kwa hawa ambao kila siku tunawaita wakimbizi haramu.

Hii imekaa vibaya.
 
Maji ya ziwa Victoria yanayoenda kuzalisha umeme Ethiopia, leo hii tuna mito, bahari, mabwawa, ziwa tena tukanunue umeme kwa hawa ambao kila siku tunawaita wakimbizi haramu.

Hii imekaa vibaya.
Hamtaki au Mnataka? Watu wameambiwa hivyo cha kushangaza nasikia makofi mara shangwe watu wanashangilia kununua umeme kutoka Ethiopia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…