Swali kuhusu tabia ya kususa, kugomea au kuzira: Je, si tabia za kike, si utoto?

Swali kuhusu tabia ya kususa, kugomea au kuzira: Je, si tabia za kike, si utoto?

Mwanamke wa kususa susa ni mtamu sana.... unakuta kamesusa na kasura kake kazuri... unakabembeleza mpaka raha... utasikia usirudie tena kwa kasauti ka aibu aibu...
Katikati ya utamu anabana pua ".....lakini we huwa unaniudhi, usirudie baby....". Huu uchaguzi wa kurudiwa,kwani ni lazima mzee wa 'sawasawa' awe mshindi? Wagombea wa nafasi zingine kwa nini nao wasuse? Wanatetea utamu wa mtu moja,ila jamaa alikuwa anakamua kama makamu I wa Rais,wakati wengine wanasota,huko anang'ang'ania hamtambui Shein kama Rais. Utalii wa ndani,hakuna haja kwenda serengeti.
 
Pasco. Hili ni jukwaa la siasa lakini sioni chambe ya siasa bali social matters ambayo ungeweka kwenye jukwaa la hoja mchanganyiko.
Mkuu , mada yangu imeanza na kususa general, ingeishia kwenye kususa generally ningeiweka kwenye Jukwaa la Hoja Mchanganyiko, lakini hii mada ya kususa, nikuwa more specific kwenye kususa kisiasa, hivyo hapa kwenye Jukwaa la Siasa ni mahali pake stahiki.

Tunazungumzia kususa kwenye context ya kisiasa nikiuliza the motive behind na the the expected outcome, na sio kususa uli mradi kususa!, this is pure politics.

Pasco
 
Pasco wa jf, sio mwanachama wa chama chochote, sio mkeeketwa, mfuasi, au mshabiki wa chama chochote au mtu yoyote, ila Lowassa nilimkubali sana tuu na bado namkubali, kama nilivyomkubali Zitto, Deo Filikunjombe etc.

Ila hata Magufuli, namkubali sana tuu, hebu nisome hapa niliwahi kumshauri nini Lowassa,
Ushauri: Lowassa Asikanyage Arumeru!, Atamponza Sioi ..
halafu angalia kilichotokea.

Na kuhusu Magufuli hata kabla hajateuliwa na CCM, nisome hapa nilisema nini!,
Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 ni John Pombe Magufuli.
alipoteuliwa tuu na CCM, nisome hapa nilimshauri nini Lowassa,
Ushauri wa Bure Kwa Lowassa: Kwa Vile ni Magufuli, Kubali Ma
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Hata kama ni kweli uliibiwa kura;

na baada ya ushindi niliwashauri nini UKAWA!.
Ushauri Wa Bure kwa ENL, Chadema na UKAWA ...

Pasco
Asante kwa viambatanisho,
 
Pasco kiukweli unatia huruma ! maana huku si kushuka wala kuporomoka , yaani sijui niseme umeserereka ? kwa ujumla hoja zako za sasa zinatia aibu , shida nini , njaa ?
Ukitimia akili za kushikiwa itakuchukuwa miaka angalau 20 kuelewa,ila ukiwa huru kifikra ni punde tu utaelewa,kususa uchaguzi si takwa la wanaCUF wa kawaida bali ni makubaliano ya Seif,EL,watu wachache ndani ya CUF na CCM.
 
Ukitimia akili za kushikiwa itakuchukuwa miaka angalau 20 kuelewa,ila ukiwa huru kifikra ni punde tu utaelewa,kususa uchaguzi si takwa la wanaCUF wa kawaida bali ni makubaliano ya Seif,EL,watu wachache ndani ya CUF na CCM.
Huna lolote , baraza kuu limeamua na mkutano mkuu umeridhia halafu unaleta uongo hapa ? shame !
 
Pasco, kususa (boycott) hapa inahusisha tu taasisi au nchi (sio hayo mambo ya kitoto na kike). Kususa ni silaha yenye nguvu kubwa inayotumika kuonyesha kutokuridhishwa na ukiukaji wa misingi ya kiimani, kifalsafa na hata kitamaduni uliofanywa na taasisi au nchi dhidi ya taasisi au nchi nyinyine. Mfano, 1976 Tanzania iliongoza nchi zingine za Kiafrika kususia michezo ya Olympic ya Montreal, Canada kutokana na kitendo cha kamati ya Olympic ya kimataifa (IOC) kukataa pendekezo la Tanzania la kutaka New Zealand iuzuiwe kushiriki michezo hiyo baada ya kuruhusu timu yake ya rugby kufanya ziara Afrika Kusini na kucheza na timu ya Makaburu. Gharama zipo! Wakati huo Tanzania ilikuwa na wanariadha mahiri waliokuwa kwenye kilele cha ubora wao ambao wangeipatia nchi angalau medali nne za dhahabu. Bayi alikuwa anashikilia ubingwa wa dunia mbio za 1500m na maili moja. Nyambui alikuwa bingwa wa Afrika 3000m. Kutoshiriki Afrika kulifanya michezo ikose msisimko na dunia kujifunza kuwa ushirikiano na Makaburu haulipi!
 
Pasco, kususa (boycott) hapa inahusisha tu taasisi au nchi (sio hayo mambo ya kitoto na kike). Kususa ni silaha yenye nguvu kubwa inayotumika kuonyesha kutokuridhishwa na ukiukaji wa misingi ya kiimani, kifalsafa na hata kitamaduni uliofanywa na taasisi au nchi dhidi ya taasisi au nchi nyinyine. Mfano, 1976 Tanzania iliongoza nchi zingine za Kiafrika kususia michezo ya Olympic ya Montreal, Canada kutokana na kitendo cha kamati ya Olympic ya kimataifa (IOC) kukataa pendekezo la Tanzania la kutaka New Zealand iuzuiwe kushiriki michezo hiyo baada ya kuruhusu timu yake ya rugby kufanya ziara Afrika Kusini na kucheza na timu ya Makaburu. Gharama zipo! Wakati huo Tanzania ilikuwa na wanariadha mahiri waliokuwa kwenye kilele cha ubora wao ambao wangeipatia nchi angalau medali nne za dhahabu. Bayi alikuwa anashikilia ubingwa wa dunia mbio za 1500m na maili moja. Nyambui alikuwa bingwa wa Afrika 3000m. Kutoshiriki Afrika kulifanya michezo ikose msisimko na dunia kujifunza kuwa ushirikiano na Makaburu haulipi!
Mkuu Nginana, kwanza asante kwa elimu hii kuhusu boycott, kwenye maelezo yangu awali nilisema boycott ya watoto ni to seek attention, na boycott ya wanawake ni kutaka kubembelezwa!. Tanzania tuliposusa, zile zilikuwa ni enzi za 'cold war', sasa tuko kwenye era nyingine na dunia nyingine!. Huu sasa ni wakati wa 'result oriented decisions', na sio wakati wa kususa tuu kutaka attention, then what?, kususa bila ku achieve anything tangible is a waste!. Jee unaweza kunisaidia Tanzania tuliposusa, tuliachieve nini?!.

Politics is a game, na rules of the game zinaeleweka, kama mechi imepangwa, usipopeleka timu uwanjani, aliyepeleka timu, anapewa ushindi wa mezani!. Nimeuliza huku kususa kisiasa, kususia uchaguzi halali, lengo lake ni nini?!, what do they want to achieve?!.

Paskali
 
Ha ha
Mkuu Nginana, kwanza asante kwa elimu hii kuhusu boycott, kwenye maelezo yangu awali nilisema boycott ya watoto ni to seek attention, na boycott ya wanawake ni kutaka kubembelezwa!. Tanzania tuliposusa, zile zilikuwa ni enzi za 'cold war', sasa tuko kwenye ea nyingine na dunia nyingine!. Huu sasa ni wakati wa 'result oriented decisions', na sio wakati wa kususa tuu kutaka attention, then what?, kususa bila ku achieve anything tangible is a waste!. Jee unaweza kunisaidia Tanzania tuliposusa, tuliachieve nini?!.

Politics is a game, na rules of the game zinaeleweka, kama mechi imepangwa, usipopeleka timu uwanjani, aliyepeleka timu, anapewa ushindi wa mezani!. Nimeuliza huku kususa kisiasa, kususia uchaguzi halali, lengo lake ni nini?!, what do they want to achieve?!.

Pasco
ha ha ha wengi wanatamani kutokee machafuko kisha waovu wajifiche kwenye migongo ya wananchi bila kujua serikali ina mkono mrefu na huko The Hague ni rahisi kupelekwa wao na kutengenezwa ushahidi utakao watia hatiani na ndipo ninaposema wasemaji,waamuzi,viongozi wakuu ukawa ni mawakala wa CCM...kifupi kwa sasa Cuf,Chadema nk ni matawi ya CCM.
 
Pasco,
Kususa ni mbinu kama mbinu nyingine yeyote ile katika kupigania haki. Inaweza kutumika kama negotiation tactic, and sometimes it works. Swali hapo ni kwamba je mbinu hii inamsaidia anayeitumia sasa? Hata hao wanawake uliowatumia kama mfano kwenye hii mada (with all due respect) wengine huwa wanafanikiwa kupata wanachokitaka kupitia kususa. Hasa wale wapiga "mizinga". Akiacha kupokea simu na wewe unamuhitaji kwa wakati huo, utatuma tu "salio" au hata na vingine vingi. Kwa suala la CUF na CCM mbinu hii inaweza kusaidia endapo itasababisha Tanzania kutengwa zaidi kimataifa. Hapo lazima kutakuwa na madhara kwa Tanzania kwa ujumla na kupelekea shinikizo kubwa la kuwepo uwazi na haki kwa chaguzi zijazo, kama siyo uchaguzi huu. It may help in the long run. Isitoshe, kuna haja gani ya kushiriki mechi ambayo mshindi tayari ameshapangwa (assuming madai ya CUF ni ya kweli)?. Hata kama suala ni "kufa kiume", huko kutakuwa ni kufa kiume kijinga.
Mkuu y cam, nafuatilia huku kususa kupya kulikotangazwa jana.

P.
 
Ha ha

ha ha ha wengi wanatamani kutokee machafuko kisha waovu wajifiche kwenye migongo ya wananchi bila kujua serikali ina mkono mrefu, ndipo ninaposema wasemaji,waamuzi,viongozi wakuu ukawa ni mawakala wa CCM...kifupi kwa sasa Cuf,Chadema nk ni matawi ya CCM.
Naifuatilia hoja hii.

Paskali
 
Me naona twende kibabe dawa ya moto ni moto kama mbwai mbwai kususa hakuna maana mfano upo zanzibar,kenya watu wamesusa wengine maisha yanaendelea
 
Huyu naye ameshafika bei lkn anajitahidi kuandika amufurahishe mkulu. Muda si mrefu mahusiano yake na ccm yatadhihirika. Kafulila alifiwa kule jimboni akafika bei, Mayala lilifafanuliwa maana yake kwa kisukuma nahisi naye amefika bei.
 
Wanabodi,

Hili mada ya swali kuhusu tabia ya kususa, huu mtindo wa kuzira au kususia jambo, sio tabia za kike hizi au sio tabia za kitoto?!.

The Motive Behind Kususa.
Jee ni nini the motive behind kususa, na baada ya kususa, jee hao wasusaji huwa wanakipata kile walichokusudia?!.

Nakumbuka nikiwa mtoto, kususa ni kuonyesha protest ili kupata attention, kisha ubembelezwe!. The motive behind kususa kwingi ni ama ku create attention au kutaka kukomoa.

Tabia hizi za kususa ni tabia za kitoto, zimekuwa zikiendelezwa sana na wanawake, kwa leongo la kukomoa, mfano mke, au mpenzi wako wa kike, akigundua kuwa amesaidiwa katika kumhudumia mtu wake, na yeye anaamua kususa kutoa zile huduma, kwa hoja kuwa nenda ukapate hizo huduma kule kule!.

Au mume ukirudi home umechelewa sana usiku mkubwa karibu na alfajiri, huku umelewa, mke anasusa kukufungulia, mlango eti rudi ukalele huko huko ulikotoka!.


Baadaye ukimbeleza mke, anakusamehe, unafunguliwa mlango, mke anarudi room na kukupiga biti usimguse!, ukiendelea kubembeleza, mambo yanakishwa na life goes back to normal, hivyo kwa sisi wanaume wa Kiafrika wenye tabia za Kiafrika, hii tabia ya kususiwa na kusamehewa, ni kitu cha kawaida sana, wengi wa wasusaji, huwa wanasusa kutokana na hasira, lakini hasira zikipoa, kususa huwa kunaisha.

Kufuatia Kususa Kufanywa na Wanawake Zaidi, Jee Kususa Kisiasa Ni Tabia Za Kike?.
Kufuatia kususa susa kufanywa zaidi na wanawake, jee huku kususa kisiasa sio tabia za kike?!. Tabia za kiume ni kukabili, kupambana, kufight to the end hadi risasi ya mwisho na tone la mwisho la damu!.

Kususa Kisiasa, Lengo Lake ni Nini?. Jee Kususa, Huku, Kumewahi Kuzaa Matunda?!.
Kuna msemo wa Kiwahili usemao, "ukisusa wenzio twala", jee kuwasusia ngendere shamba la mahindi, kutasaidia au watu walisusa tuu ili wabembelezwe?, na wasipobembelezwa, jee kususa huku kuna faida kwao?!.

Nawatakia Ijumaa Njema.

Paskali
Mkuu ninaamini kuwa ukiingia vitani kwenye mapambano yasio kuwa na faida, ni busara kujitoa kwenye mapambano hayo ili usipoteze muda wako na resources zako. Haswa ikiwa ni dhahiri kuwa kwa namna yoyote utakavyopambana hutapata ushindi. Ni mpumbavu tu ambaye ataingia kwenye vita ambayo ana uhakika kuwa hawezi kushinda. Kujitoa kwenye mapambano inakupa muda wa kujijenga upya, kwa maana ya kudai fair play katika nyanja zote za mchuano, pasipo na mshiriki yoyote kubebwa na msamamizi au chombo chochote cha dola. Kudai mazingira kamili ya usawa kwa washiriki wote wa mchuano kwenye uwanja wa mapambano. Kususa kwa maana niliyoielezea huwezi kuiita ni tabia ya kitoto au ya kike. Kususa kwa maana yako mkuu kuna lenga zaidi, kugomea jambo, kwa sababu umeudhiwa, japo jambo hilo huwa mara nyingi na faida kwako, na hayo hufanywa na watoto na labda wakina dada kama ulivyoeleza. Hivi mkuu unaweza kuingia darasani na kufanya mtihani ambao dhahiri unajua kwamba hutafaulu? Si utapoteza energy yako na muda wako bure. Ni vema kutafakari kwa undani sababu za mtu kujitoa au kususia jambo fulani, kuliko kukimbilia kumhukumu.
 
Kumsusia mwanamke(yaani mke wa ndio) ni adhabu kubwa kwake kuliko kumpiga, sisi wahenga mke akikuletea za kuleta unampa pesa yake ya matumizi lakini wewe hauli chakula chake ni adhabu kubwa sana kwa mwanamke, ikibidi hata kumsusa yeye mwenyewe kwa muda fulani, hizo ni adhabu za wake. Tatizo vijana kujifanya kujua kwingi kutoa vipigo ndio maana ndoa hazidumu siku hizi
 
Mkuu The Big Boss, naomba nikuhakikishie katika maisha yangu yote, sijawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa. Paskali, hanunuliki na yeyote kwa lolote kwa sababu hana price tag. Mimi ni priceless, sio CCM wa Chadema, wala Ukawa, wala Lowassa wala Magufuli, ana uwezo wa kuninunua, kwa sababu I'm not for sale, na sina any price tag!.

Naomba uniamini hili ni swali tuu, nimeuliza hawa wanaosusa, wamesusa ili wapate nini?!.

Ni swali tuu.

Paskali

Mkuu paskali wewe ni mmoja wa great thinker mkongwe tunakueshimu sana ,umenizidi kila kitu mimi nimesoma chuo cha kata vya kuunga unga,wewe mkuu nasikia umesoma chuo nambari one Tanzania UDSM i respect you,sasa embu sema ukweli na Mungu akuone usiwe biased kuna kauli kua wakurugenzi wameambiwa wasiwatangaze wapinzani wakishinda,tumeona uchaguzi wa madiwani police wanakamata mawakala wa upinzani ndani ya chumba cha kupigia kura,wakuregenzi na ccm wanatengeneza technically kasoro ili tu kuwakomoa mawakala wa upinzani,mkurugenzi wa uchaguz mfano ubungo siku mbili kajificha ili asisaini barua za mawakala wa cdm,na akijua kua bila saini yake hawaruhusiwi kusimamia kweli hayo ndo mazingira ya uchaguz huru?ok tukubali ndio labda fomu za wakala zina upungufu kwann Nec kama msimamizi asiwaite before kuwaambia warekebishe wajaze upya then wasubmitt kuliko hii kuviziana na kuwekeana mitego,mnapowakosoa cdm kususia waambieni na ccm na nec yake wawe fair basi hata police
 
Mleta mada eti naye anajiita great thinker duh!.....

Mkuu jadili hoja, na usimjadili mleta hoja. Hoja hapo si mleta hoja kama ni GT au sio GT. Ni wapi kwenye uzi wake mtoa hoja kajiita GT? Mkuu kama wewe unajiona ndio great thinker tupe maoni yako, unaonaonaje hili swala la watu kususia jambo. Acha dharau zako za kipuuzi mkuu.
 
Mkuu Pasco acha stereotype kuhusu wanawake , wanawake ni mama zetu na generalization sio poa
 
Hivi we paskali!we hujawahi kususa au kugoma
Ndomana kuna wengine huwa wanagoma kula ilimradi matakwa Yao yatimizwe!hata Mugabe aligoma kula?tena alikuwa mwanasiasa nguli,
So kususa ni kawaida.....

Ova
 
Back
Top Bottom