Swali kwa Ayubu Rioba: Siku hizi sera ya Taifa inaruhusu taasisi za kidini kunufaika na fedha za walipa kodi kupitia TBC?

Swali kwa Ayubu Rioba: Siku hizi sera ya Taifa inaruhusu taasisi za kidini kunufaika na fedha za walipa kodi kupitia TBC?

View attachment 1792731
Dk. Ayub Chacha Rioba, Mkrugenzi Mtendaji wa TBC

Leo nimeona matukio mawili yasiyo ya kawaida kwenye luninga ya Taifa TBC1, inayoongozwa chini ya Ukurugenzi wa Dk. Ayub Rioba.

1. Asubuhi kabla ya kipindi cha Bunge cha mswali na majibu TBC1 walirusha kipindi cha "Madrasa" kilichokuwa na ujumbe unaotembea kwa upande wa chini ukisomeka "Mashindano ya Kuhifadhi Kurani Tukufu kwa Waislamu Wanawake Yameandaliwa na Taasisi ya Kiislam ya African Relief Foundation."

2. Mchana, mara tu baada ya matangazo ya Maadhimisho ya miaka 40 ya kuanzishwa kwa SADC, ambako Ayub Rioba alikuwa mwongozaji, kilifuata kipindi ncha swala ya Kiislamu.

Nafahamu pia kwamba, TBC1 imekuwa na kawaida ifuatayo:

1. Kila alfajiri madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya asububi.

2. Kila usiku wa kati, kabla ya saa sita, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya kufunga siku.

3. Kila Jumapili pia, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma ibada za Jumapili.

Lakini, TBC ni mali inayoendeshwa kwa kodi ya umma chini ya usimamizi wa serikali isiyofungamana na dini yoyote, kama tunavyosoma kwenye katiba ya nchi.

Pia, dini nyingi tayari zinavyo vyombo vyake vya habari kwa ajili ya kuendesha shughuli zake za kidini, kwa lugha wanazozitaka wao, hata kama sio lugha ya Taifa.

Nakumbusha kuwa, kwa sehemu kubwa, sala nyingi za madhehebu ya KiIslamu zinatumia lugha ya Kiarabu, jambo ambalo linakiuka sera ya kujenga umoja wa kitaifa kwa kutumia lugha ya Taifa.

Hata litania nyingi za Kikristo zinasomwa kwa lugha ya Kilatini ambayo sio lugha ya Taifa.

Kama hivi ndivyo, kwa nini TBC inatumika namna hii?

Ni muhimu swali hili lijibiwe ili tujichunguze kama vyombo vya habari vya kitaifa vinakweza maslahi ya vikundi kama vile taasisi za dini au vinatweza maslahi ya pamoja kama vile umoja wa kitaifa.

Napendekeza kwamba ni kosa kutumia kodi ya raia asiye na dini kuhudumia taasisi za kidini.

Ni kama ambavyo ni kosa kutumia kodi ya mtu asiye na chama cha siasa kutoa ruzuku kwa chama cha siasa.

Kuna tatizo hapo.

Waumini wa madhehebu hayo ni walipa kodi pia wa namna moja au nyingine kwa hiyo sioni ubaya kituo cha taifa TBC kurusha shughuli za madhehebu mbali mbali labda kama kuna yanayobaguliwa!

Sent from my itel A32F using JamiiForums mobile app
 
Hujaaoma wala kuelewa hoja. Siongelei uislamu. Tuliza kichwa chako, vaa miwani kama macho yana tatizo
Dada mi ni mkristo lkn niseme ukweli kwamba kimtazamo wang naona kama hoja yako haijakaa kitaifa bali imekaa kidini. Na ndo maana hoja hii imekosa wachangiaji wengi, hii ni kwa sababu watu wengi humu wameshachoka na hoja zenye kuleta malumbano ya kidini baina yetu kama Taifa. Wengi humu tumeoleana na kuzaliana ktk imani tofauti. Unakuta baba muislam mama mkristo, au baba mkristo mama muisilam, watoto wanaozaliwa wanapokuwa wakubwa wanaamua wenyewe imani ya kufuata nk, hapo sijaongelea mtaani, mashuleni, maofisini na sehem mbali mbali za miji na nchi kwa ujumla. Umekiri mwenyewe kwamba unafahamu kitambo kuhusu vipindi vya dini vinavyorushwa kila siku asubuh na usiku wakati wa kulala, yan muda wa kufungua vipindi na muda wa kufunga vipindi, pia umekiri kuwa kuna vipindi vya kikristo huwa vinapitishwa kila jumapili kwa ajili yetu sisi wakristo lkn haukuwahi kuja kuhoji chochote kuhusu vipindi hivyo vya jumapili, lkn leo umeona na ndugu zetu na wao wameanza kupewa muda wa kuangalia au kufuatilia vipindi vyao TBC siku ya ijumaa umekuja haraka haraka kuzungumzia habari za kodi, ila wakati walipokuwa wanarusha vya kwetu kila ijumapili bila kupitisha hiki cha ijumaa swala la kodi haukulihoji. Tupendane jamani sisi wote ni taifa moja hao waliotuletea hizi imani kwa sasa wapo mbali baada ya kupuuza mawazo ya aina hii.
 
TV ya taifa inaendeshwa kwa mtindo wa push technology, sio kwa mtindo wa pull technology, ambako mtazamaji huchagua programu gani aangalie

Kwa hiyo, yafaa ionyesha programu za kitaifa pekee, kwa kutumia lugha ya Taifa pekee.

Taasisi za dini zina TV na REDIO zake.

Wajihudumie bila kuhujumu umoja wa kitaifa kupitia mgongo wa kodi ya umma wote
Mh! Kwahiyo hata miziki wasiweke na filamu wasiweke pamoja na vipindi vya makabila?

Ila mimi naonaga tatizo ni pale tunaposema tu mlipa kodi mlipa kodi ila nafikiri hatumjui huyo mlipa kodi hasa ni nani.
 
Wasio na dini/ wapagani nao walete vipindi vyao TBC1 vitarushwa bila chenga ili kodi yao itumike vizuri au unasemaje hapo??!!
 
Waumini wa madhehebu hayo ni walipa kodi pia wa namna moja au nyingine kwa hiyo sioni ubaya kituo cha taifa TBC kurusha shughuli za madhehebu mbali mbali labda kama kuna yanayobaguliwa!

Sent from my itel A32F using JamiiForums mobile app

Yapo madhehebu yanayobaguliwa.

Mara nyingi tunaambiwa kuna dini kuu mbili.

Sio kweli.

Kuna dini kuu tatu, Ukristo, Usislamu, na ATR wakati waumini wa ATR ni wengi kuliko waumini wa Ukristo na Usislamu wakijumulishwa.
 
Wasio na dini/ wapagani nao walete vipindi vyao TBC1 vitarushwa bila chenga ili kodi yao itumike vizuri au unasemaje hapo??!!
Haitasaidia kuondoa tatizo.

Ukweli uko hivi:

1. Dini zilizosajiliwa mambo ya ndani ni zaidi ya 500

2. Baadhi zinasali Jumapili (Katoliki, Luteri, Anglikana, etc), zingine Jumamosi (Sabato), kuna za Jumatano (Bahai), nk

3. Kwa hiyo, ratiba ya kuwatendea haki wote kupitia TBC sio halisia.

Kwa hiyo, mjadala huko hivi:

1. Katiba inatenganisha dini na kazi za serikali.

2. Kuna njia mbili za kutekeleza falsafa hii ya kikatiba: American-style or German style

3. German style haitekelezeki bila kubagua baadhi ya dini.

4. Kwa hiyo, Tanzania tufuate American style?

Karibu tena....
 
Mh! Kwahiyo hata miziki wasiweke na filamu wasiweke pamoja na vipindi vya makabila?

Ila mimi naonaga tatizo ni pale tunaposema tu mlipa kodi mlipa kodi ila nafikiri hatumjui huyo mlipa kodi hasa ni nani.
Mlipa kodi ni:

1. Mkristo (x)

2. Mwislamu (y)

3. mwana-ATR (z)

Zingatia:

4. ambapo z>(x+y)

5. Kwa hiyo, sio sawa kutumia kodi ya watu wa seti z kuwahudumia watu wa seti ya (x+y)
 
Tatizo Dini au Uislam

Tatizo hili hapa:

1. Serikali ya TZ haina dini japo watu wake wana dini, ambapo falsafa hii inaweza kutekelezwa kwa njia ya America-style policy or German-style policy

2. Dini za TZ ni Ukristo, Uislamu, u-ATR, ambapo waumini wa ATR ni wengi kuliko waumini wa Ukristo na Uislamu kwa pamoja

3. Kwa sababu ya utitiri wa dini zilizosajiliwa MOHA (500+) German-style policy haitekelezeki

4. Kwa hiyo, twende America-style, yaani, kufuta vipindi vya dini kwenye luninga ya Taifa.

Zingatia:

5. Tayari taasisi za dini zina vyombo vyake vya habari kwa ajili ya kuendesha mambo yao kwa jinsi wanavyoona inafaa.
 
Quote Nakumbusha kuwa, kwa sehemu kubwa, sala nyingi za madhehebu ya KiIslamu zinatumia lugha ya Kiarabu, jambo ambalo linakiuka sera ya kujenga umoja wa kitaifa kwa kutumia lugha ya Taifa.

Na hapo sijaongelea jinsi sare moja ya wanafunzi wote shuleni ilivyo nyenzo muhimu kwa ajili ya kutekeleza sera ya umoja wa kitaifa.

Kama hivi ndivyo, kwa nini TBC inatumika kidini namna hii?

Ni muhimu swali hili lijibiwe ili tujichunguze kama vyombo vya habari vya kitaifa vinakweza dini na kutweza utaifa. End Quote




Ukimsoma vizuri jamaa hana shida na wakristo kutumia TBC, yeye shida yake ni Waislam. Hii ni kwasababu Jpili na siku nyingine amesikia Wakristo wakiendesha Ibada hakushtuka, ila leo ameshituka baada ya kuona swala na ibada za Waislam, ikamtuma kukimbilia huku kufungua uzi.
Uzi wa kijinga. Waislam wamekuwa wakifundisha dini yao kabla ya TBC miaka ile ya RTD na hakuna aliyeona ni jambo lisilo la kawaida.

Enzi za marehemu Sheikh Hemed bin Juma bin Hemed miaka ya 1970-80.
 
Mama Amon covid -19 mnaelekea chama gani baad ya kutimuliwa CHADEMA? mana sifikiri kama CCM watakuhitajini zama za jiwe zimepita
 
View attachment 1792731
Dk. Ayub Chacha Rioba, Mkrugenzi Mtendaji wa TBC

Leo nimeona matukio mawili yasiyo ya kawaida kwenye luninga ya Taifa TBC1, inayoongozwa chini ya Ukurugenzi wa Dk. Ayub Rioba.

1. Asubuhi kabla ya kipindi cha Bunge cha mswali na majibu TBC1 walirusha kipindi cha "Madrasa" kilichokuwa na ujumbe unaotembea kwa upande wa chini ukisomeka "Mashindano ya Kuhifadhi Kurani Tukufu kwa Waislamu Wanawake Yameandaliwa na Taasisi ya Kiislam ya African Relief Foundation."

2. Mchana, mara tu baada ya matangazo ya Maadhimisho ya miaka 40 ya kuanzishwa kwa SADC, ambako Ayub Rioba alikuwa mwongozaji, kilifuata kipindi ncha swala ya Kiislamu.

Nafahamu pia kwamba, TBC1 imekuwa na kawaida ifuatayo:

1. Kila alfajiri madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya asububi.

2. Kila usiku wa kati, kabla ya saa sita, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya kufunga siku.

3. Kila Jumapili pia, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma ibada za Jumapili.

Lakini, TBC ni mali inayoendeshwa kwa kodi ya umma chini ya usimamizi wa serikali isiyofungamana na dini yoyote, kama tunavyosoma kwenye katiba ya nchi.

Pia, dini nyingi tayari zinavyo vyombo vyake vya habari kwa ajili ya kuendesha shughuli zake za kidini, kwa lugha wanazozitaka wao, hata kama sio lugha ya Taifa.

Nakumbusha kuwa, kwa sehemu kubwa, sala nyingi za madhehebu ya KiIslamu zinatumia lugha ya Kiarabu, jambo ambalo linakiuka sera ya kujenga umoja wa kitaifa kwa kutumia lugha ya Taifa.

Hata litania nyingi za Kikristo zinasomwa kwa lugha ya Kilatini ambayo sio lugha ya Taifa.

Kama hivi ndivyo, kwa nini TBC inatumika namna hii?

Ni muhimu swali hili lijibiwe ili tujichunguze kama vyombo vya habari vya kitaifa vinakweza maslahi ya vikundi kama vile taasisi za dini au vinatweza maslahi ya pamoja kama vile umoja wa kitaifa.

Napendekeza kwamba ni kosa kutumia kodi ya raia asiye na dini kuhudumia taasisi za kidini.

Ni kama ambavyo ni kosa kutumia kodi ya mtu asiye na chama cha siasa kutoa ruzuku kwa chama cha siasa.

Kuna tatizo hapo.
Wakati kabla Rais hajahutubia kwenye shughuli za kitaifa wanasimama viongozi wa dini na kuliombea taifa na miongoni kwao yupo yule anaswali kihindu..bongo wahindu ni wachache lakini yule yupo siku zote.

Taifa letu halina dini ila mimi na wewe tuna dini zetu.

Kama huwezi kuvumilia kusikiliza masuala ya dini nyingine basi badilisha channel ili wenye kuelewa waendelee na ibada inayowahusu.

Hawezi kufurahishwa kila mtu tena kila wakati.
 
Kuna wapuuzi huwa mnaumizwa vichwa na vitu vya kipuuzi mno, yaani mtu anashupaza shingo lake kwa midini ya kuletewa
 
Mlipa kodi ni:

1. Mkristo (x)

2. Mwislamu (y)

3. mwana-ATR (z)

Zingatia:

4. ambapo z>(x+y)

5. Kwa hiyo, sio sawa kutumia kodi ya watu wa seti z kuwahudumia watu wa seti ya (x+y)
Kwenye kukusanya kodi haijarishi wewe ni muislamu mkristo au hauna dini wote mnatoa kodi ila kwenye matumzi ya hizo kodi ndipo kwenye utata, ukiingiza hoja ya walipa kodi huwezi kumtoa mkrsto na muisamu maana nao wanalipa kodi.
 
Dada mi ni mkristo lkn niseme ukweli kwamba kimtazamo wang naona kama hoja yako haijakaa kitaifa bali imekaa kidini. Na ndo maana hoja hii imekosa wachangiaji wengi, hii ni kwa sababu watu wengi humu wameshachoka na hoja zenye kuleta malumbano ya kidini baina yetu kama Taifa. Wengi humu tumeoleana na kuzaliana ktk imani tofauti. Unakuta baba muislam mama mkristo, au baba mkristo mama muisilam, watoto wanaozaliwa wanapokuwa wakubwa wanaamua wenyewe imani ya kufuata nk, hapo sijaongelea mtaani, mashuleni, maofisini na sehem mbali mbali za miji na nchi kwa ujumla. Umekiri mwenyewe kwamba unafahamu kitambo kuhusu vipindi vya dini vinavyorushwa kila siku asubuh na usiku wakati wa kulala, yan muda wa kufungua vipindi na muda wa kufunga vipindi, pia umekiri kuwa kuna vipindi vya kikristo huwa vinapitishwa kila jumapili kwa ajili yetu sisi wakristo lkn haukuwahi kuja kuhoji chochote kuhusu vipindi hivyo vya jumapili, lkn leo umeona na ndugu zetu na wao wameanza kupewa muda wa kuangalia au kufuatilia vipindi vyao TBC siku ya ijumaa umekuja haraka haraka kuzungumzia habari za kodi, ila wakati walipokuwa wanarusha vya kwetu kila ijumapili bila kupitisha hiki cha ijumaa swala la kodi haukulihoji. Tupendane jamani sisi wote ni taifa moja hao waliotuletea hizi imani kwa sasa wapo mbali baada ya kupuuza mawazo ya aina hii.

Hoja yako: Dada mi ni Mkristo lkn niseme ukweli kwamba kimtazamo wangu naona kama hoja yako haijakaa kitaifa bali imekaa kidini. Na ndo maana hoja hii imekosa wachangiaji wengi, hii ni kwa sababu watu wengi humu wameshachoka na hoja zenye kuleta malumbano ya kidini baina yetu kama Taifa.

Jibu: Haya sio malumbano ya kidini. Ni malumbano juu ya sera ya Taifa kuhusu namna bora ya kutenganisha dini na dola. Kuna sera za aina mbili duniani. Sera ya KImarekani na Sera ya KIjerumani. Wamarekani hawana hii habari ya kila dini kupewa airtime kwenye luninga ya Taifa. KIla dini ina luninga yake. Wajerumani wanweza kuruhusu baadhi ya dini kwenye luninga ya Taifa kama wanavyofanya wanapotumia TRA yao kukusanya sadaka kwa niaba ya makanisa. Lakini utitiri wa makanisa yaliyosajiliwa na serikali huwalazimisha kujikuta wanabagua baadhi ya madhehebu.

Hoja yako: Wengi humu tumeoleana na kuzaliana ktk imani tofauti. Unakuta baba muislam mama mkristo, au baba mkristo mama muisilam, watoto wanaozaliwa wanapokuwa wakubwa wanaamua wenyewe imani ya kufuata nk, hapo sijaongelea mtaani, mashuleni, maofisini na sehem mbali mbali za miji na nchi kwa ujumla.

JIbu: Kuoleana na mambo kama hayo sio hoja iliyo mezani. Mkristo akioana na Mwislamu wanaishi ktk nyumba yao wawili. Hilo sio suala la umma mpana wa kitaifa. Hoja yetu hapa ni jinsi gani bora ya kutofautisha maisha ya umma wa kitaifa na maisha binafsi. Maisha ya umma mpana wa kitaifa uko shuleni, ktk ofisi za serikali, ktk vyombo vya habari vya kitaifa, ktk vyombo vya usafiri wa umma, masoko, nk.

Hoja yako: Umekiri mwenyewe kwamba unafahamu kitambo kuhusu vipindi vya dini vinavyorushwa kila siku asubuh na usiku wakati wa kulala, yaani muda wa kufungua siku na muda wa kufunga siku, pia umekiri kuwa kuna vipindi vya kikristo huwa vinapitishwa kila jumapili kwa ajili yetu sisi wakristo lkn haukuwahi kuja kuhoji chochote kuhusu vipindi hivyo vya jumapili, lkn leo umeona na ndugu zetu na wao wameanza kupewa muda wa kuangalia au kufuatilia vipindi vyao TBC siku ya Ijumaa umekuja haraka haraka kuzungumzia habari za kodi, ila wakati walipokuwa wanarusha vya kwetu kila ijumapili bila kupitisha hiki cha ijumaa swala la kodi haukulihoji.

Jibu: Kila jambo lina sababu za karibu na sababu za mbali. Kabla ya leo Rioba alikuwa anaongoza kongamano Morogoro wakiwepo viongozi wa TEF. Pale alieleza vema dhima ya vyombo vya habari na nafasi ya lugha ya Taifa katika kujenga umoja wa kitaifa. Siku moja baadaye nikaona chombo anachokiongoza kinapingana na kauli zake za siku moja kabla. Nikafanya udadavuzi na kuibuka na hoja hii. Ni hoja ambayo haiwalengi Waislamu pekee wala Wakristo pekee. Ni hoja pana zaidi. Inawahusu Wakristo, Waislamu, Wabuda, Wahindu, Wabahai, na Wa-ATR. Pia KIlatini ni lugha ya Taifa ya Italia wakati Kiarabu ni lugha ya Taifa ya Saudia. Lugha ya Taifa ya Tanzania ni Kiswahili. TBC wanawajibika kukuza lugha ya Taifa la Tanzania na sio vinginevyo. Tujadili hoja niliyoweka mezani.

Hoja yako: Tupendane jamani sisi wote ni taifa moja hao waliotuletea hizi imani kwa sasa wapo mbali baada ya kupuuza mawazo ya aina hii.

Jibu: Njia bora zaidi ya kupendana ni kukubaliana kuhusu njia bora ya kisera katika kutekeleza matakwa ya kikatiba yanayosaema kuwa serikali ya Tanzania haina dini hata kama watu wake wana dini. TBC ni chombo cha umma kinachosimamiwa na serikali hiyo. Mjadala uendelee.
 
Ryoba alimsapoti Mwendazake kwenye uovu wake, toka siku hiyo namuona kama shetani tu.
 
Kuna wapuuzi huwa mnaumizwa vichwa na vitu vya kipuuzi mno, yaani mtu anashupaza shingo lake kwa midini ya kuletewa
Cha muhimu kwenye dini ni ile imani yako vile unavyoamini,iwe umeikuta umeletewa au umeiunda mwenyewe mwisho wa siku ni uamuzi wako kuamini au kutoamini. Dini/imani sio kama kabila kwamba utakuwa utatambulika wewe ni kabila fulani kwa sababu baba ako ni kabila hilo, kwahiyo hoja ya dini za kuletewa au sio za kuletewa haina mashiko kama tungeangalia tungeanza kukataa vya kuletewa kuanzia tiba, vifa vya mawasiliano hadi usafiri ila tuliona vina faida na ndio maana tunatumia. Kwahiyo tukatae kitu kwa hoja za msingi na sio et vya kuletewa.
 
Back
Top Bottom