Swali kwa Jaji Mkuu: Je, ni haki kwa kina Rostam Aziz kutozwa faini badala ya kifungo lakini kina Mbarikiwa kupewa kifungo badala ya faini?

Eti mbarikiwa? Mbarikiwa wa nini? Huyo mtu ni mwehu na anatengeneza "cult" ya wehu. Naipongeza Serikali kwa hatua madhubuti waliochukua. Naye Kibwetere alianza hivihivi akawateka watu kwa kusingizia dini kisha akawachoma moto.

KUna wehu mbaya kuliko ule wa kuwatoa kafara watu kwenye mkesha wa kukanyaga mafuta?
Think again!
 

Wakati padri Mzungu anahukumiwa kifungo cha siku 1 baada ya kukutwa na meno ya tembo sijui kama ulikuwa ushazaliwa.

Tafuta pesa. Ndugu
 
Hii kesi ya Mdogo wake azizi ya Mwaka 2019 enzi za JPM nadhani kuna namna waliimaliza nje ya mahakama.

Hapana. Mashtaka yalibadilishwa, kesi ikaenda mpaka mwisho, Akram akatiwa hatiani. Magufuli iliisimamia mwenyewe. Nchimbi akawa anaivuruga. Lakini mwisho wa siku hukumu ikatoka. Cheki hapa: Akram Aziz akiri makosa yanayomkabili, alipa faini na kesi kuisha!

Na Mwandishi Wetu

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemuhukumu mdogo wa mfanyabiashara maarufu, Rostam Aziz, Akram Aziz kulipa faini ya Sh milioni 259.5 au kifungo cha miaka 20 jela baada ya kukiri mashitaka 73 ya kukutwa na nyara za Serikali ikiwemo nyama ya nyati na silaha.

Hata hivyo, Akram amefanikiwa kulipa faini na kuepuka kifungo hicho cha miaka 20 jela.

Pia mahakama imetaifisha nyara hizo na kuwa mali ya Serikali na kuamuru silaha zote ziwe chini ya polisi hadi hapo mshitakiwa atakapokamilisha taratibu za kisheria za kumiliki silaha hizo.

Kwa mara ya kwanza, Akram alifikishwa mahakamani hapo Oktoba 31, mwaka huu akikabiliwa na mashitaka 75 katika kesi namba 82/2018 ikiwemo kukutwa na nyara za Serikali, silaha, risasi na utakatishaji fedha wa dola za Marekani 9,018 lakini kwa mujibu wa sheria alifutiwa mashitaka hayo na kusomewa upya mashitaka 73 ukitoa ya utakatishaji fedha na meno ya tembo.

Akitoa hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri alisema kuwa katika mashitaka ya kukutwa na nyama ya nyati, mshitakiwa atatakiwa kulipa faini ya Sh 43,529,000 na katika makosa 72, yaliyobaki kila moja atatakiwa kulipa Sh milioni tatu.

Katika mashitaka hayo 72, jumla ya faini aliyotakiwa kulipa Akram ni Sh milioni 216.

Alisema mshitakiwa akishindwa kulipa faini hiyo atatakiwa kutumikia kifungo cha miaka 20 jela.

Kabla ya kutolewa kwa adhabu hiyo, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Paul Kadushi akisaidiana na Wakili wa Serikali, Wankyo Simon aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kutokana na uzito wa makosa hayo, kwa mshitakiwa ili iwe fundisho kwa wengine wanaofanya vitendo hivyo.

Pia waliiomba mahakama itaifishwe nyara zote iwe mali ya serikali.

Kwa upande wa mshitakiwa alidai kuwa anasumbuliwa na shinikizo la juu la damu na kwamba ni mkosaji wa kosa la kwanza, ana watoto 10 wanaomtegemea pamoja na mama yake mzazi ambaye ni mzee.

Inadaiwa Oktoba 30, mwaka huu maeneo ya Oysterbay wilayani Kinondoni, mkoani humo Akram alikutwa na nyara za serikali ambazo ni nyama ya nyati yenye uzito wa kilogramu 65, yenye thamani ya dola za Marekani 1,900 sawa na Sh 4,352,900 mali ya serikali bila kuwa na kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapoli nchini.

Katika mashitaka ya tatu hadi la 72, kwamba siku hiyo na eneo hilo hilo, mshitakiwa huyo alikutwa na silaha aina ya Pistol bila ya kibali cha mrajisi wa silaha.

Inadaiwa katika mashitaka ya 73 kuwa, Oktoba 30, mwaka huu maeneo ya Oysterbay mshitakiwa alikutwa na risasi 4,092 na katika mashitaka mengine ilidaiwa mshitakiwa alikutwa na risasi 2,404 bila kuwa na kibali.
 
Mkuu nimeshuhudia makanisa mengi yanayo enda kinyume na sheria lakin Mpaka Leo yapo wakina Mwamposa wanaendesha makongomano yanayo ua watu mbona hawafungwi au kulipishwa faini au hilo siyo kosa, mwingine Zumaridi anayejiita Mungu wamenda kwake wamekuta watoto wadogo amewafungia ndani anawafanya kama mazombi, na katka Uchunguzi ikabainika anafanya Biashara ya Kuuza Binadamu mbona hakuhukumia Wala sikuona Adhabu yeyote but after short time wakamwachia,,, Sasa huyo jamaa kosa lake ni lipi kudai haki yake kuuliwa mtoto wake au? Kingine alikua akilalamikia serikari kumnyima vibali kwa makusudi Huku akiwa ametimiza Kila kitu. Anyway kushindana na haki ya Mungu ni kosa kubwa sana. Na hili ndo lilimwangamiza Magufuri kukaidi na kupuuz kauli za Maskofu!!!! Na AWAMU inafany the same mistake.
 
Inadaiwa katika mashitaka ya 73 kuwa, Oktoba 30, mwaka huu maeneo ya Oysterbay mshitakiwa alikutwa na risasi 4,092 na katika mashitaka mengine ilidaiwa mshitakiwa alikutwa na risasi 2,404 bila kuwa na kibali.
Mbona risasi nyingi sana?
 
Zumarid ni Pro ccm.

You are safe when you are pro ccm. Do whatever no one touch you.
 
MASIKINI NCHI HII HAPATI HAKI
TAJIRI NCHI NDIO WENYE HAKI
TAJIRI ANAWEZA KUKUCHINJA PALE POSTA KWENYE MNARA WA ASKARI NA ASISHTAKIWE
 
Watu weupe walikuja wachache tu afrika ila waliweza kukamata maalfu ya watumwa, je nani aliwasaidia? Afrika tukijiona ni BINADAMU KAMILI, hilo nalo ni tatizo. Hakimu huyu angekuwepo enzi za watumwa unadhani angekuwa upande wa mtu mweusi? Ila huenda ni mkakati wa kumfitinisha na Wakristo! Na mtu mweusi yupo katika mpito wa kufikia binadamu kamili.
 
Hatimaye wajelajela wamepelekewa mtumishi wa mungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…