Swali kwa Jaji Mkuu: Je, ni haki kwa kina Rostam Aziz kutozwa faini badala ya kifungo lakini kina Mbarikiwa kupewa kifungo badala ya faini?

Mmmh🙄🙄🤔

Yaani huyu Akram Aziz alikutwa na makosa ya kuwa na silaha hizi zote akizitumia kwa ujangili kinyume cha sheria na ikathibitika hivyo pasipo shaka yoyote lakini hakimu akaona kosa hilo kuwa ni "minor offense" na hivyo kutozwa faini ya pesa tu?

Kama ni hivyo, basi ninakubaliana na wewe kuwa mahakimu/majaji wetu na mahakama zetu kwa ujumla wake zimeshanunuliwa na mfumo wa uovu dhidi ya haki na hivyo wao ndio wana dictate kesi iweje na hukumu iwe ya namna gani..!

====================================================
KKUHUSU MCH. MBARIKIWA DICKSON MWAKIPESILE NA HUKUMU YAKE.

Kiukweli Mch Mbarikiwa Mwakipesile ni binadamu kama tulivyo mimi na wewe na kila mmoja anayesoma. Ana mapungufu na madhaifu yake ya kibinadamu.

Ni kweli pia kuwa katika mfumo wake wa maisha ni mtu mwenye ujasiri wa ajabu kidogo na huutumia ujasiri huo kumtuhumu na kumshambulia yeyote kwa maneno awe mtu wa kawaida, kiongozi wa serikali au kisiasa, wachungaji wenzake nk nk ili mradi tu amhisi kuwa anakosea au amemkosea yeye mwenyewe binafsi..

Lakini kutumia udhaifu wake usiovunja sheria yoyote isipokuwa tu eti tu kwa kuwa hapatani na baadhi ya viongozi wa kisiasa na serikali wenye nguvu na mamlaka za kiserikali kumkomoa kwa kesi za uongo na kisha kumfunga gerezani wakidhani wanaondoa kero na kikwazo cha kuendelea desturi zao za uovu na uonevu, ni kosa kubwa na baya sana..

Inashangaza mno kuoina mahakama ikiwa ime - compromise na waovu hawa na kuacha sheria na adili..

Mkono wa Bwana uwe juu ya wahalifu hawa wote..
 
Aisee!
 
Mkuu hii nchi imeshatamalaki kwa tabia OVU ZA YULE MWOVU.
CCM imeharibu sana hii nchi kiasi kwamba mahakimu na majaji hukumu zao ni za kisiasa kwa matakwa na wanasiasa wa CCM. majajji na mahakimu weledi hauzingatiwi tena! Ni aibu yao milele na kiyama chao kitakuwa kibaya sana mbele ya Mwenyezi Mungu,
 
KUna wehu mbaya kuliko ule wa kuwatoa kafara watu kwenye mkesha wa kukanyaga mafuta?
Think again!
Wote hao ni kitu kimoja. Panapowezekana kudhibiti uyoga wa madhehebu ya kishenzi, basi tuiunge mkono Serikali.
 
Kosa la Huihui2 halihalalishi kosa la Mtu Alie Nyikani . Zumaridi ahukumiwe kama Zumaridi na Mwakipesile kama Mwakipesile. Ukiachia mijitu mishenzi kama Mwakipesile, utakuwa unaandaa Taifa la kishenzi.


Simpendi Paul Kagame wa Rwanda lakini kwenye huu UHAYAWANI wa madhehebu UCHWARA amedhibiti. Kwa Rwanda lazima mchungaji aonyeshe shahada ya Chuo Kikuu kwenye Theology.
 
mbarikiwa aliyataka mwenyewe. kwani jaji mkuu ndiye aliyehukumu kesi yake? ninyi vijana wa mbarikiwa amewaharibu akili wote mpo kama yeye. ukristo haupo hivyo.
 

Sijui mtatoka gizani lini au nyinyi ni wasahaulifu kiasi gani?

Pichani huyo ni aliyewahi kuwa CJ Marehemu Augustino Ramadhani alipochukua fomu za urais kupitia CCM, hapo bado hamjiulizi tu kuwa mahakama zinapiga magoti kwa rais , Ndugai tu kakoroma kidogo kapewa mkwara katupa joho huko.

Katiba mpya ni muhimu otherwise mkatae mkubali mahakama na bunge ni mali ya CCM ndio maana unaona hata viongozi wa CCM wanaiamrisha serikali.

Katiba mpya ije na kipengele cha mgombea binafsi habari za vyama hizi sasa zimekua ni upumbavu mtupu.
 
Ni vizuri tukaijua Nchi hii na utawala wake! Kwamba wenye haki wanaopigania haki ni target ya watawala. Lakini waovu ni kivutio cha watawala.
By the way wakili peter Madeleka amepost kuwa kaitwa kizimkazi hajui anaitiwa nini.
Tufuatilieni jamani kwa sababu hizi ni nyakati mbaya kwa wapenda haki!!

Wenye mawasiliano na Madeleka please tutoeni hofu! Haya majambazi yameazimia kutumaliza!!
 
Hahah!!! Kwaiy anayo yafanya Zumaridi kwa kuuza Binadamu ni sawa na anayo yafanya Mwamposa ni sawa wenyew hawatakiwi kuhukumiwa kwa sabab ya Makosa yao ni differ na ya wengine aisee...
Binafsi mm sioni Kosa la hiyo mbarikiwa kama swala ni kibali kwann hawakumfungia kanisa kuliko kumkamata na kumfunga yeye. Na ali-operate hilo Kanisa Miaka 3 je hapo serikali ilikua haijaona.
Ndugusheria na Katiba zipo kwa. Ajili ya kutenda haki kwann umhukum huyu Alfu mwingine usimhukum basi hakuna umhimu basi wa Kuwa na sheria kama hiyo sheria ipo kwa ajili ya watu malum lakin wengine haihukum Bora isiwepo.

Zumaridi asingetakiwa awe uraiani akina Mwamposa wanasababisha vifo vya watu lakin sheria hazichukuliw, lakin kosa tu kibali
mkuu think Twice
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…