Swali Rahisi: Nyerere aliwashughulikiaje Waganda "Illegals" wakati wa "chokochoko" Za Idi Amin?

Swali Rahisi: Nyerere aliwashughulikiaje Waganda "Illegals" wakati wa "chokochoko" Za Idi Amin?

Mkuu pengine wewe ulikuwa bado kinda mwaka 1972 hadi 1978 ilipoanza vita rasmi na Idi Amin.
Nyerere alifanya kosa la kimsingi kutochukua hatua ya ku- contain the fith column.
Hata hivyo by mwaka 1978/79 somo lilikuwa limeshaeleweka baada ya Amin kuingia Kagera kama nyumbani kwake.
Mwalimu aliwakusanya kina Oyite Ojok na hata kina Museveni, waganda, wakapigane kwa ajili y ao wenyewe na kwa ajili ya Tanzania.

JK kafanya kweli, ni lazima adui ajulikane toka mwanzo kwa vile ameshajitanabahisha toka mapema, pa kupiga paeleweke mapema.
Kama mtu anafikiri kutukanwa na kutishiwa maisha kwa mkuu wa nchi na bado mtu ukachekelea kama huna akili nxuri, basi hata a
yekutukana atajua kuwa wewe ni zuzu.

Kikwete ameliingiza taifa kwenye machafuko na chuki ya kibaguzi kwa majirani bila sababu za msingi.
Heshima ya Tanzania imezikwa na Kikwete.
 
Swali hili linahitaji jibu; jibu lake linaweza kuwa rahisi au gumu. Lakini ni jibu linalotegemea ujuzi wa historia. Ni jibu linalojaribu kuangalia kama uamuzi wa serikali ya Tanzania kutekeleza sheria kwa upendeleo (selective justice) ni uamuzi sahihi au ni miongoni mwa maamuzi mabovu kabisa yaliyowahi kuchukuliwa na watawala wetu. Na pia ni swali ambalo linauliza kama kutoa adhabu ya jumla (collective punishment) kwa kosa la Kagame ni jambo sahihi. Lakini pia ni lazima tujiulize baada ya muda uliotolewa kwa wahamiaji wageni kuondoka nchini wale waliobakia wakianza kutendewa vibaya na wenyeji serikali itawachukulia hatua hawa wenyeji au itawaachia kwa sababu wale ni wageni wahamiaji? Quran na Biblia vinafundisha (na vinakubaliana kwa kiasi kikubwa) jinsi ya kuwatendea wageni wahamiaji katika nchi; na haihusishi kuwafukuza kwa nguvu! Katika Biblia kuna uhamiaji wa aina nyingi ambao wote una mafunzo kwa waamini; kuna uhamiaji wa Ibrahim (Abram) toka Uru wa Wakaldo Kulikua hakuna. Na kama walikuepo hawakutenda maovu na walitii amri za nchi na kuishi kwa amani.
 
Swali hili linahitaji jibu; jibu lake linaweza kuwa rahisi au gumu. Lakini ni jibu linalotegemea ujuzi wa historia. Ni jibu linalojaribu kuangalia kama uamuzi wa serikali ya Tanzania kutekeleza sheria kwa upendeleo (selective justice) ni uamuzi sahihi au ni miongoni mwa maamuzi mabovu kabisa yaliyowahi kuchukuliwa na watawala wetu. Na pia ni swali ambalo linauliza kama kutoa adhabu ya jumla (collective punishment) kwa kosa la Kagame ni jambo sahihi. Lakini pia ni lazima tujiulize baada ya muda uliotolewa kwa wahamiaji wageni kuondoka nchini wale waliobakia wakianza kutendewa vibaya na wenyeji serikali itawachukulia hatua hawa wenyeji au itawaachia kwa sababu wale ni wageni wahamiaji?

Quran na Biblia vinafundisha (na vinakubaliana kwa kiasi kikubwa) jinsi ya kuwatendea wageni wahamiaji katika nchi; na haihusishi kuwafukuza kwa nguvu! Katika Biblia kuna uhamiaji wa aina nyingi ambao wote una mafunzo kwa waamini; kuna uhamiaji wa Ibrahim (Abram) toka Uru wa Wakaldoyo kwenda nchi ya ahadi; kuna uhamiaji wa Yusuph kwenda Misra (baada ya kuuzwa na nduguze) na uhamiaji wa kundi kubwa la Waisraeli Misri; kuna uhamiaji (katika Agano Jipya) wa Yesu Masihi kwenda Misri pia baada ya kutafutwa na Herodi auawe akiwa kichanga.

Katika Uislamu bila ya shaka somo kubwa kabisa la uhamaji (hijra) ni ule wa Mtume Mohammed kutoka Mecca kwenda Madina. Ni uhamiaji mkubwa na muhimu sana katika Uislamu kiasi kwamba mwaka wa kwanza katika Kalenda ya Uislamu unaanzia katika tukio hilo (Al Hijra) la mwaka 622 (AD). Ujio wa Mohammed Medina ulitenganisha matendo aliyotendewa na njama alizotendewa na watu wa Mecca hadi kumlazimisha yeye na waamini wa mwanzo kuondoka hapo kwenda Medina katika hali ya kificho na hatari tupu!

Dini zetu kubwa hizi mbili (hata ya Kiyahudi) zinatufundisha kuwatendea wageni vizuri; haijalishi kama walihamia kihalali au la. Tuweke utaratibu mzuri wa kuwashughulikia na kuwahalalisha au hata kuwarudisha makwao katika heshima inayotokana na utu wao. Tukumbuke kuwa Katiba yetu inasema (Ibara 12 hadi 13) kuwa:



Utaona kuwa Ibara hizo hazisemi "kila Mtanzania" au "Kila raia wa Tanzania" na wala hazisemi "Kila aishiye TAnzania"! Zinasema kuwa "Kila mtu" anazaliwa akiwa huru na ni wote ni sawa! Yaani, Mhaya wa Kagera na Mkurya wa Tarime wote ni sawa! Kwamba inasema "Kila mtu anastahili heshima na haki ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake"; yaani Mndengereko na Mzaramo wana haki sawa kabisa ya kuthaminiwa utu wao kama ilivyo kwa Mnyarwanda na Mhabeshi! Yaani, hata kama wamevunja sheria ya uhamiaji - na inawezekana wengi wamefanya hivyo - hilo peke yake haliwafanyi wawe binadamu nusu au siyo watu kama wengine na hivyo hawalindwi na Katiba yetu! Katiba yetu inamlinda kila mtu aliyeko Tanzania!

Ndio maana hili swali linaendelea kusimama, Nyerere alishughulikiaje wahamiaji haramu kutoka Uganda wakati wa chokochoko? Kuna mtu anakumbuka au tuwasaidie hawa wa kizazi kipya somo la historia kidogo maana inaonekana watu wasiojua historia wanaenda kurudia makosa yake!

Tunaweza vipi kukubali serikali ichukue hatua za sheria kwa mfumo wa kibaguzi na udhalilishaji wa utu wa binadamu na bado tunajiita Watanzania?

Mungu atusaidia tusifurahie vitendo kama hivi kwa jina la 'uzalendo'!


MMM
jibu ni kwamba hakukua na wahamiaji haramu kipindi hicho,kama walikuwepo hawakufika hata kumi so hawangeweza kuwa tishio.wapinzani wa idd amini wengi walikuwa wamekimbilia Tanzania akiwamo obote,hao hawakuwa tishio kwa usalama.

Wanyaru wa sasa wanatishia amani huko mikoa ya pembezoni.
 
Ningemlaumu Rais Kikwete angewashupalia wahamiaji haramu wa Rwanda kwa kuwa tu ametukanwa kwani ningemwona hana uvumilivu.Tatizo ni pale wahamiaji haramu wanapofanya matukio ya kihalifu na kutumia nguvu dhidi ya wazawa kufaidi rasilimali haswa ardhi.Kama dalili ya mvua ni mawingu nadhani ni hatua sahihi japokuwa yaweza kuwa kwa njia isiyo na taswira nzuri.
Mpaka sasa iko tofauti ya tafsiri ktk tamko la JK; tafsiri moja kubwa na maarufu ni kuwafukuza "Wanyarandwa" na sio "Wageni waishio nchini isivyo halali".

Kuna uwezekano wa hisia (hasira nk) ktk hilo tangazo, au kilicho nyuma ya pazia ndicho kinachotekelzwa. Ila kwa namna nilivyosoma lile tamko la Rais Kikwete lilikuwa "too general" kuliko "application" ninayoiona. Na hapa ndipo napojikita kwa maswali ili nipate majibu.

Ningependa kuona tafsiri na utendaji mpana wa sheria kila siku/mahali (na sio kusubiri tamko la Rais); lile tamko lilipaswa tu kuwapa watendaji some moral support etc
 
Tatizo la Mwanakijiji ni kutokuijua Tanzania vizuri.

Yaani macho yake yameishia kuona kwamba wahamiaji haramu ni swala linalohusu chokochoko za kagame. Hujui kabisa kuwa Tanzania kuna sehemu huwezi kusafiri bila escort ya polisi kwa sababu ya wahamiaji haramu.

Hivi hao waganda unaowazungumzia walikuwa wanazuia watanzania kufanya movements zao nchini kwao?

Kumchukia kwako Kikwete kunakufanya kila analosema au kulifanya utafute jinsi ya kulipinga!

By the way, unapomlinganisha Nyerere na Kikwete unataka kujustify nini???

Chuki itakupeleka kubaya Mwanakijiji.


  1. Mimi nadhani hujamwelewa MMM, mleta hoja. Alichokileta Mwanakijiji ni HOJA FIKIRISHI na kwa kweli kwa watu wanaofikiri vizuri, akiaamua kujielekeza kujibu hoja,basi ataijibu kwa HOJA!!
  2. Hapo katika BOLD GREEN, unachobishia ni nini Mkuu??...Si amri ya JK imetoka baada ya hawa wakuu wawili wa mataifa huru kuanza kurushiana maneno??...Na hivi ni kweli kabisa kuwa kila palipo na uhalifu ni kwa sababu ya wahamiaji haramu?...Watanzania sisi wenyewe miongoni mwetu hakuna wahalifu??
  3. Sidhani kama MMM anataka kujustify lolote lenye chuki kama ulivyomaliza hoja yako kwa kuwalinganisha JMK na JKN zaidi tu ya kwamba Nyerere aliwahi kuwa kiongozi wa taifa hili (Rais) kwa takribani miaka 25 na huyu Kikwete ndiye Rais wetu wa sasa. Aidha wakati wa Nyerere kulitokea mfarakano uliosababisha vita kati yetu na majirani zetu Uganda. Na sasa kwa namna huyu Rais wetu JK anavyoshughulikia mgogoro wake na mwenzie wa Rwanda PK kuna kila dalili kuwa anaweza kusababisha matatizo makubwa zaidi tofauti na kinyume kabisa na namna ambavyo yeye mwenyewe binafsi na washauri wake pale Magogoni wanavyofikiri!!....Kwa hiyo ni haki na ni lazima wajadiliwe kwa sasa na walinganishwe kwa namna wanavyotenda kama viongozi wetu

Mwisho hakuna anayekubaliana na tatizo la watu wa mataifa mengine kuingia nchini kwetu pasipo kufuata sheria hata kama tunawaita WAHAMIAJI HARAMU. Ishu ni moja, kwamba, tunatumia njia gani kushughulika na mtu/watu wa namna hii mara tunampowatambua wamo nchini mwetu isivyo halali hata kama pia watakuwa wametumia udhaifu wa mifumo yetu ya utendaji?? Je ni hivi inavyofanya serikali yetu? Na je, watanzania wenzetu walioko katika mataifa mengine kwa njia hizihizi nao watendewe hivihivi au??......Hebu Rejea tena kwenye Katiba yetu inasemaje juu UTU na UBINADAMU na angalia pia maisha ya watu wa mipakani jinsi yalivyo.....hapa naamanisha muingiliano kwa sbb nchi hazina mipaka ya ukuta na idara zetu za uhamiaji haziwezi kuweka ofisi ktk kila njia ya mpakani. Hapa Rais na serikali imechemka si ktk nia yake tu bali pia ktk mfumo wa utekelezaji wenyewe wa agizo la Rais!!

Let us think deeply kwa kuweka itikadi zetu za vyama pembeni na kila mtu atoe mchango wake bila kumuonea mtu. Binafsi nampongeza MMM ameleta hoja hii kwa wakati mwafaka na serikali wakifikiri vizuri inaweza kuwasaidia kutenda vizuri zaidi katika kushughulikia tatizo la "wahamiaji haramu" na bado ikawa na heshima yake ileile nzuri mbele ya uso wa kimataifa!!
 
Ni vyema wachangiaji wakalinganisha mifumo mbalimbali ilivyokabiliana na swala la wahamiaji haramu....ili kutanua uwigo wa kujadili hoja hii.
Case studies:
David Cameron vs wahamiaji haramu
USA/Obama na sera za uhamiaji haramu
South Afrika na sekeseke la vipigo dhidi ya wahamiaji kutoka zimbabwe n.k

Tusimshambulie mleta hoja bali tujadili hoja.
 
naamini mwanakijiji anaishi marekani kama mhamiaji haramu na hana any legal documents zakumfanya aishi huko!! kwa maana kama anaelewa athari za wahamiaji haramu asingeongea huu utumbo aliouandika, ulaya nzima kwa sasa kampeni za kisiasa hutawaliwa na ishu ya kuhandle wahamiaji haramu, uingereza, ufaransa,italy,spain,sweden nakadhalika kote huku wahamiaji haramu wanawekwa maeneo maalum wanachunguzwa sababu za uhamiaji wao na kama hawakidhi vigezo wanakuwa deported back to their countries!!

tuseme haya mwanakijiji hayafahamu? au kujitia hamnazo tu ili apate sababu ya kupinga serikali? hana tofauti na Dr Slaa kwamba yeye kila kitu cha serikali basi ni kupinga tuuu, hizi ni akili za kawaida au akili za kukariri? wana tofauti gani basi hawa na wabunge wa CCM ambao hupinga kila mchango wa mbunge wa upinzani?

unafiki ni janga kubwa tulilonalo Tanzania, na kama hakuna uzalendo wa dhati basi hatuna chetu tena
 
Hivi kwa nini mtu ukipinga huu mgogoro unaitwa Mnyarwanda? Jana mie Mnyamwezi nimeitwa MTUSI na mjinga fulani.

Wewe leo unamwita Mwanakijiji Mnyarwanda wakati wengi tunafahamu Baba yake alikuwa nani na Mama yake ni Msukuma.

Kama huna la kuandika si ukae kimya kuliko kuropoka? Mzee Mwanakijiji anafahamika kabisa kuwa Mtanzania na sehemu anayotoka, ungelionekana walau una akili kidogoo ukamwita Mmalawi au Mzambia. Sasa utamwita hata Mbowe kuwa Mnyarwanda. Mchaga na Mtusi wapi na wapi?
Mwanakijiji na unyarwanda wako pamoja na pasi ya Tanzania unayo2mia haukufanyi kudhihaki maamuzi ya nchi ye2
 
ukishasema wahamiaji haramu hauna haja ya kuuliza kama mi halali kuwachukulia hatua au la. Jk angekuwa amewafukuza waamiaji halali hapo tungehoji.
 
Ndugu Kobelo,

Ni kweli malalamiko ya wenyeji yalianza siku nyingi. Lakini kwa nini hatua hizo ziwe sasa? Kwani hiyo siku nyingi Rais na serikali yake walikuwa wapi? Kwani wakati wahamiaji hao wanahamia kienyeji, iwe ni kwa kutoroka makambi ya wakimbizi au kuvuka mpaka kienyeji serikali ilikuwa wapi?

Lina kuja hili la haki za hawa wahamiaji kikatiba. Katiba yetu imetamka wazi binadamu wote, watu wote kuzaliwa HURU na KUWA NA HAKI SAWA MBELE YA SHERIA. Ni kweli Wanapaswa kurejeshwa kwao kama wamekuwa humu kinyume na sheria zetu. Lakini siyo kwa kufukuzwa kienyeji. What is the meaning of diplomacy then? Ni mara ngapi hata wafungwa wanaporejeshwa makwao kunafanyika mawasiliano baina ya nchi husika, utaratibu wa kuwakabidhi na kuwapokea unafanyika kwa murua kabisa? Ni kweli kwamba Wafungwa wana hadhi kuliko hawa wageni?

Halafu kifuate hiki kipengele cha nasaba kati ya nchi jirani na wananchi waishio mipakani. Kwa waliowahi kuishi mipakani watakuwa mashahidi kuwa ni vigumu kuzingatia mpaka wa nchi. Ukienda maeneo hayo ni kawaida kuona mtoto anatoka asubuhi kwenda shule "Kenya" kwa sababu ni karibu na nyumbani kuliko ya "Tanzania" hata kama ni kwa kilomita 1. Kule ni kawaida mtu kukwambia naenda kwa mjomba ikawa anaenda "Kenya" au kukuta mtu anaaga naenda kisimani na ikawa anaenda kuchota maji Burundi. Mwisho wa siku, pamoja na malalamiko yote, siyo halali sana kuwafukuza tu kienyeji kwa sababu wengine ni Wajomba zao na Wahaya flani au ni mama mdogo wa rafiki yako wa pale mpakani na huenda mama mzazi wa Mtanzania flani! Na Kama wamekuwa "Wahamiaji Haramu" ghafla, nataka kukubaliana, kwa mantiki hiyo ya nasaba na kulinda utu, na mwana JF mmoja aliyewatambua hawa wageni kwa mtazamo wa "Wajomba zetu Haramu", "mama zetu haramu" au "Mkeo haramu" (Which is Mbaya)...Na kama wote ni wahalifu basi nasikitika kwani kuna wake za wenzetu siyo "Wananchi kabisa" na wengine wetu ni mapolisi wakuu (Law upholders)! What do you think. In the end hawa ni binadamu wa kawaida! Kuvunjika kwa sheria za uhamiaji hakuwatoi ubinadamu wao!. Jamani hata muhalifu pia ana haki zake.

Vyovyote inavyokuwa kitendo kile kilifanyika kwa jazba za kiongozi na kwa hasira ya matusi ya Rais wa jirani na si kwa kujali sana vilio vya wananchi. Na sitaki kuamini kuwa kwa vilio vya muda huo mrefu ndiyo Rais anavisikia juzi!

Mwisho nahitimisha kwa kusema ni vema tukawa mfano kwa wenzetu kwa vile tunavyotaka watufanyie sisi. Kama wote tungefanya hivyo sidhani kama kungekuwa na mahusiano mazuri na yeyote duniani. Imagine the world where ukipata wageni waliovunja sheria unawakusanya tu unakwenda nao mpakani kwao unawabwaga hapo na kuondoka! Kwamba na China ikusanye wale wauza unga "wetu" wote iwasafirishe mpaka bandarini iwaache kienyeji. Au Afrika ya Kusini ijibebee kina "Masogange wetu" wote ije iwamwage mpakani na kuondoka kimyakimya! Jamani kutakuwa kumebaki thamani ya ubinadamu duniani?......Ile ilikuwa hasira na haikuwa sawa. Siyo kitendo cha mfano wala hakifai kuigwa na si cha kupongezwa kwa namna yoyote hasa kufanywa na kiongozi tena mwenye washauri kibao.

Binafsi naona Mwanakijiji is right. And I do apologize, sincerely, if my understanding is contradictory to yours.

Unasema mwenyewe "Ni kweli malalamiko ya wenyeji yalianza siku nyingi."

Bila shaka tumepata sababu nzuri ya kuanza kuyashughulikia wakati huu. Ilikuwa ni lazima ifike muda fulani hatua zichukuliwe. Kama wanavyosema - sooner or later.

Wala haijasemwa wasije Tanzania. Wafuate taratibu zilizowekwa. Rwanda wapo Wa Tanzania wengi mpaka kwenye vyuo vayo wanategemewa. Hao wote wamefuata taratibu za kwenda huko.

Inaniuma sana kuwahangaisha jamaa zetu wamasai na wasukuma na mifugo. Wamefukuzwa Kilombero. Badala ya Wanyarwanda kuchunga mifugo yao Bongo, bora ndugu zetu waende huko. Mwisho wa siku mifugo hiyo inanifaisha uchumi wa Tanzania. Wanyarwanda hapa kwetu wanalisha tu, hatimaye wanaenda nayo kwao.
 
Unasema mwenyewe "Ni kweli malalamiko ya wenyeji yalianza siku nyingi."

Bila shaka tumepata sababu nzuri ya kuanza kuyashughulikia wakati huu. Ilikuwa ni lazima ifike muda fulani hatua zichukuliwe. Kama wanavyosema - sooner or later.

Wala haijasemwa wasije Tanzania. Wafuate taratibu zilizowekwa. Rwanda wapo Wa Tanzania wengi mpaka kwenye vyuo vayo wanategemewa. Hao wote wamefuata taratibu za kwenda huko.

Inaniuma sana kuwahangaisha jamaa zetu wamasai na wasukuma na mifugo. Wamefukuzwa Kilombero. Badala ya Wanyarwanda kuchunga mifugo yao Bongo, bora ndugu zetu waende huko. Mwisho wa siku mifugo hiyo inanifaisha uchumi wa Tanzania. Wanyarwanda hapa kwetu wanalisha tu, hatimaye wanaenda nayo kwao.


If it takes a decade for a government to find what to do then to hell with it. Na kwa nini siyo wahamiaji wote waliojazana nchini? Why ni Kagera tu? Hao wanaobaki wana uhalali gani? Na bado huajibu swali: Walipkuwa wanaingia Serikali ilikuwa wapi?

Hakuna alipendekeza waendelee kukaa siyo Mwanakijiji wala mimi sijasema hivyo. Nilichosema ni utaratibu unaotumika unawanyanyasa utu wao na ni uvunjaji wa haki ya kuthaminiwa utu wao na usawa kisheria.

Jaribu kurudia kusoma posti ya Mwanakijiji , rudia na yangu...then karibu tena.
 
Dar es salaam hakuna wahamiaji haramu ambao ni wahalifu pia ? arusha je? Au Mwanza hakuna wahamiaji haramu ? Kwanini agizo hili linahusu Kagera tu? Isn't that selective justice?
 
Mwanakijiji angeongeza kuwa ethnic cleansing anayoifanya Kikwete ni crime against humanity. Pia ku-destroy uchumi wa watu na kuwabakiza wakiwa masikini. Mhamiaji ana mifugi yake, ndo kila kitu, hana elimu, hajui bishara, hajui kulima, then unakuja unampa wiki mbili eti arudishe mifugo alikoitoa. Hajui kuwa hawa wafugaji hawajatoka kokote, ila wana asili tu ya Rwanda na Uganda, ila ni wa hapahapa. Unawafanya wauze ngome 1 kwa shs 20,00, ubinadamu huo? Hivi Kikwete si mwislamu?
 
Ndugu Kobelo,

Ni kweli malalamiko ya wenyeji yalianza siku nyingi. Lakini kwa nini hatua hizo ziwe sasa? Kwani hiyo siku nyingi Rais na serikali yake walikuwa wapi? Kwani wakati wahamiaji hao wanahamia kienyeji, iwe ni kwa kutoroka makambi ya wakimbizi au kuvuka mpaka kienyeji serikali ilikuwa wapi?

Lina kuja hili la haki za hawa wahamiaji kikatiba. Katiba yetu imetamka wazi binadamu wote, watu wote kuzaliwa HURU na KUWA NA HAKI SAWA MBELE YA SHERIA. Ni kweli Wanapaswa kurejeshwa kwao kama wamekuwa humu kinyume na sheria zetu. Lakini siyo kwa kufukuzwa kienyeji. What is the meaning of diplomacy then? Ni mara ngapi hata wafungwa wanaporejeshwa makwao kunafanyika mawasiliano baina ya nchi husika, utaratibu wa kuwakabidhi na kuwapokea unafanyika kwa murua kabisa? Ni kweli kwamba Wafungwa wana hadhi kuliko hawa wageni?

Halafu kifuate hiki kipengele cha nasaba kati ya nchi jirani na wananchi waishio mipakani. Kwa waliowahi kuishi mipakani watakuwa mashahidi kuwa ni vigumu kuzingatia mpaka wa nchi. Ukienda maeneo hayo ni kawaida kuona mtoto anatoka asubuhi kwenda shule "Kenya" kwa sababu ni karibu na nyumbani kuliko ya "Tanzania" hata kama ni kwa kilomita 1. Kule ni kawaida mtu kukwambia naenda kwa mjomba ikawa anaenda "Kenya" au kukuta mtu anaaga naenda kisimani na ikawa anaenda kuchota maji Burundi. Mwisho wa siku, pamoja na malalamiko yote, siyo halali sana kuwafukuza tu kienyeji kwa sababu wengine ni Wajomba zao na Wahaya flani au ni mama mdogo wa rafiki yako wa pale mpakani na huenda mama mzazi wa Mtanzania flani! Na Kama wamekuwa "Wahamiaji Haramu" ghafla, nataka kukubaliana, kwa mantiki hiyo ya nasaba na kulinda utu, na mwana JF mmoja aliyewatambua hawa wageni kwa mtazamo wa "Wajomba zetu Haramu", "mama zetu haramu" au "Mkeo haramu" (Which is Mbaya)...Na kama wote ni wahalifu basi nasikitika kwani kuna wake za wenzetu siyo "Wananchi kabisa" na wengine wetu ni mapolisi wakuu (Law upholders)! What do you think. In the end hawa ni binadamu wa kawaida! Kuvunjika kwa sheria za uhamiaji hakuwatoi ubinadamu wao!. Jamani hata muhalifu pia ana haki zake.

Vyovyote inavyokuwa kitendo kile kilifanyika kwa jazba za kiongozi na kwa hasira ya matusi ya Rais wa jirani na si kwa kujali sana vilio vya wananchi. Na sitaki kuamini kuwa kwa vilio vya muda huo mrefu ndiyo Rais anavisikia juzi!

Mwisho nahitimisha kwa kusema ni vema tukawa mfano kwa wenzetu kwa vile tunavyotaka watufanyie sisi. Kama wote tungefanya hivyo sidhani kama kungekuwa na mahusiano mazuri na yeyote duniani. Imagine the world where ukipata wageni waliovunja sheria unawakusanya tu unakwenda nao mpakani kwao unawabwaga hapo na kuondoka! Kwamba na China ikusanye wale wauza unga "wetu" wote iwasafirishe mpaka bandarini iwaache kienyeji. Au Afrika ya Kusini ijibebee kina "Masogange wetu" wote ije iwamwage mpakani na kuondoka kimyakimya! Jamani kutakuwa kumebaki thamani ya ubinadamu duniani?......Ile ilikuwa hasira na haikuwa sawa. Siyo kitendo cha mfano wala hakifai kuigwa na si cha kupongezwa kwa namna yoyote hasa kufanywa na kiongozi tena mwenye washauri kibao.

Binafsi naona Mwanakijiji is right. And I do apologize, sincerely, if my understanding is contradictory to yours.
Apology not accepted.

Sheria za uhamiaji zipo wazi, askari uhamiaji wameshindwa kulinda mpaka ipasavyo.

Kuhusu relationships mipakani, hebu acha kutupotosha, hata geitra nako??, mpaka mwanajeshi wa JWTZ auliwe ziwa tanganyika? .. usitake kutuongopea, you know this is a very peculiar case of border crossing and need to be handled as soon as possible.


Hakuna sheria inayosemaa eti tuongee na nchi wanakotoka kwanza. Wamepewa ultimatum, which is a very diplomatic way of deportation.

Usitumie mfano wa Masongange, that is stupid!! Tanzanians have automatic visas in SA, and when you break the law, you have the right to a due process/fair trial.

They should be arrested after the deadline. Tats just the law!!

But they should not be treated violently.
 
Maamuzi ya hekima na busara pekee hutoa majibu sahihi kwa matatizo mabalimbali.

Maamuzi ya kidikiteta, lazima na visasi hasa huishia katika utata, majanga na hata vita visivo na sababu wala lazima

Sikuwahi kusikia nyerere kawafukuza waganda kagera hata siku moja, nakama ilifanyika mwenyetaarifa sahihi aziweke hapa.

Hata pale Nyerere alipofanikiwa kuwatiamikononi wanajeshi na dege lao kutoka Libya, Nyerere aliwarejesha kwao kwa utaratibu maalum (kumbuka mateka wa kivita na waliletwa kwa lengo moja tu wale waarabu kutumaliza)

Nasikitika sana sana kwetu watanzania kushupalia kitendo hiki kiovu, kibaya na kinacholihalibia sifa nzuri taifa letu.

Hili ni tatizo:-

-kikwete anapoelekeza nguvu zake kwa kundi maalumu la watu maalu pekee.

-Kikwete anapochukuwa hatua bila maandalizi wala ushikishwaji bora wa wahusika

-Kikwete bila kuzingatia kwamba huko kwa majirani zetu, pia wapo watanzania wengi wanaioshi bila vibali kama hawa.

Nadhani Kiongozi wanchi yampasa kuruhusu hekima zaid kuchukuwa nafasi yake zaidi ya chochote.
adolay,

..naomba kutofautiana kidogo na wewe.

..Kagera kuna tatizo la ujambazi. Raisi ametoa wiki 2 kwa MAJAMBAZI kusalimisha silaha zao.

..Kagera kuna tatizo la walioingiza mifugo ktk maeneo yasiyostahili kama hifadhi za taifa. Hao pia wamepewa wiki 2 watoe mifugo yao.

..Kagera kuna tatizo la wahamiaji toka nchi jirani. Raisi kawapa wiki 2 waweke mambo yao sawa, au warudi nchi walikotoka.

..hivi Raisi anayebembeleza mpaka majambazi anapaswa kuitwa dikteta kweli? kuwapa muda watu waliovunja sheria waziwazi ni udikteta?

..Raisi amechukua maamuzi hayo baada ya kusikia malalamiko toka kwa wananchi wa Kagera. Nakushauri usome au usikilize hotuba ya Raisi.

..In 2010, Kikwete akiwa ndiyo Raisi wetu, Tanzania iliwapa uraia wakimbizi 160,000 toka Burundi. Sasa madai kwamba Kikwete ni mkatili na dikteta yanatoka wapi?

..Mwisho, natofautiana na Raisi Kikwete ktk masuala chungu nzima, lakini katika hili nakubaliana na hatua alizochukua.

cc Sikonge, Ogah
 
Last edited by a moderator:
Dar es salaam hakuna wahamiaji haramu ambao ni wahalifu pia ? arusha je? Au Mwanza hakuna wahamiaji haramu ? Kwanini agizo hili linahusu Kagera tu? Isn't that selective justice?
baada ya siku 14 kuna msako utaanza,bila shaka utahusisha maeneo ya Upanga kwa wahindi na kinondoni kwa wakongo!
 
Dar es salaam hakuna wahamiaji haramu ambao ni wahalifu pia ? arusha je? Au Mwanza hakuna wahamiaji haramu ? Kwanini agizo hili linahusu Kagera tu? Isn't that selective justice?

We nawe akili zako kama kichwa cha panzi.

Swali lako hili ni sawa na mtu aulize kwanini mradi wa maji uko Karatu kwani Dodoma hakuna shida ya maji.

Au mtu aulize kwanini barabara inajengwa Songea kwani Singida hakuna shida ya barabara.

Umeshawahi kusikia Dar es Salaam kuna mtu kashindwa kufanya shughuli zake kwa sababu ya wahamiaji haramu? Hujui Tanzania ilivyo, kazi yako kusambaza chuki tu...

Chuki inakupeleka kubaya sana...
 
Back
Top Bottom