Swali Rahisi: Nyerere aliwashughulikiaje Waganda "Illegals" wakati wa "chokochoko" Za Idi Amin?

Swali Rahisi: Nyerere aliwashughulikiaje Waganda "Illegals" wakati wa "chokochoko" Za Idi Amin?

Swali hili linahitaji jibu; jibu lake linaweza kuwa rahisi au gumu. Lakini ni jibu linalotegemea ujuzi wa historia. Ni jibu linalojaribu kuangalia kama uamuzi wa serikali ya Tanzania kutekeleza sheria kwa upendeleo (selective justice) ni uamuzi sahihi au ni miongoni mwa maamuzi mabovu kabisa yaliyowahi kuchukuliwa na watawala wetu. Na pia ni swali ambalo linauliza kama kutoa adhabu ya jumla (collective punishment) kwa kosa la Kagame ni jambo sahihi. Lakini pia ni lazima tujiulize baada ya muda uliotolewa kwa wahamiaji wageni kuondoka nchini wale waliobakia wakianza kutendewa vibaya na wenyeji serikali itawachukulia hatua hawa wenyeji au itawaachia kwa sababu wale ni wageni wahamiaji?

Quran na Biblia vinafundisha (na vinakubaliana kwa kiasi kikubwa) jinsi ya kuwatendea wageni wahamiaji katika nchi; na haihusishi kuwafukuza kwa nguvu! Katika Biblia kuna uhamiaji wa aina nyingi ambao wote una mafunzo kwa waamini; kuna uhamiaji wa Ibrahim (Abram) toka Uru wa Wakaldoyo kwenda nchi ya ahadi; kuna uhamiaji wa Yusuph kwenda Misra (baada ya kuuzwa na nduguze) na uhamiaji wa kundi kubwa la Waisraeli Misri; kuna uhamiaji (katika Agano Jipya) wa Yesu Masihi kwenda Misri pia baada ya kutafutwa na Herodi auawe akiwa kichanga.

Katika Uislamu bila ya shaka somo kubwa kabisa la uhamaji (hijra) ni ule wa Mtume Mohammed kutoka Mecca kwenda Madina. Ni uhamiaji mkubwa na muhimu sana katika Uislamu kiasi kwamba mwaka wa kwanza katika Kalenda ya Uislamu unaanzia katika tukio hilo (Al Hijra) la mwaka 622 (AD). Ujio wa Mohammed Medina ulitenganisha matendo aliyotendewa na njama alizotendewa na watu wa Mecca hadi kumlazimisha yeye na waamini wa mwanzo kuondoka hapo kwenda Medina katika hali ya kificho na hatari tupu!

Dini zetu kubwa hizi mbili (hata ya Kiyahudi) zinatufundisha kuwatendea wageni vizuri; haijalishi kama walihamia kihalali au la. Tuweke utaratibu mzuri wa kuwashughulikia na kuwahalalisha au hata kuwarudisha makwao katika heshima inayotokana na utu wao. Tukumbuke kuwa Katiba yetu inasema (Ibara 12 hadi 13) kuwa:



Utaona kuwa Ibara hizo hazisemi "kila Mtanzania" au "Kila raia wa Tanzania" na wala hazisemi "Kila aishiye TAnzania"! Zinasema kuwa "Kila mtu" anazaliwa akiwa huru na ni wote ni sawa! Yaani, Mhaya wa Kagera na Mkurya wa Tarime wote ni sawa! Kwamba inasema "Kila mtu anastahili heshima na haki ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake"; yaani Mndengereko na Mzaramo wana haki sawa kabisa ya kuthaminiwa utu wao kama ilivyo kwa Mnyarwanda na Mhabeshi! Yaani, hata kama wamevunja sheria ya uhamiaji - na inawezekana wengi wamefanya hivyo - hilo peke yake haliwafanyi wawe binadamu nusu au siyo watu kama wengine na hivyo hawalindwi na Katiba yetu! Katiba yetu inamlinda kila mtu aliyeko Tanzania!

Ndio maana hili swali linaendelea kusimama, Nyerere alishughulikiaje wahamiaji haramu kutoka Uganda wakati wa chokochoko? Kuna mtu anakumbuka au tuwasaidie hawa wa kizazi kipya somo la historia kidogo maana inaonekana watu wasiojua historia wanaenda kurudia makosa yake!

Tunaweza vipi kukubali serikali ichukue hatua za sheria kwa mfumo wa kibaguzi na udhalilishaji wa utu wa binadamu na bado tunajiita Watanzania?

Mungu atusaidia tusifurahie vitendo kama hivi kwa jina la 'uzalendo'!


MMM

Kuna mtu anataka kutubugiza HOJA! Hoja ile ile inarudiwa kwa vichwa mbalimbali na mashambulizi kutoka kona mpya kila leo! Lakini msimamo wetu unabaki wazi:
"JAPO DR.KIKWETE ANA MAPUNGUFU YAKE, HAMKARIBII NYERERE HATA KIDOGO KWA BUSARA NA KUJENGA HOJA, LAKINI KWA MSIMAMO WAKE DHIDI YA WAHAMIAJI HARAMU 'HATARI', TUTAMUUNGA MKONO MPAKA DAKIKA YA MWISHO! NA TUNAANZA NA WALE WA MAZIWA MAKUU, AMBAO PAMOJA NA HUJUMA ZAO DHIDI YA UCHUMI WETU (KWA MASAFA MAFUPI NA MAREFU), WENGINE NI RAIA WA NCHI ZINAZOLETA 'KILIMILIMI' KANA KWAMBA TANZANIA NI KOLONI LAO!
KWA KIFUPI: HAWA WATU WARUDI KWAO MAPEMA, WAENDE KWENYE NCHI YAO YA 'MAZIWA NA ASALI, IF BLOOD AND PUSS QUALIFY!', WATUACHE NA BONGO YETU YENYE 'BAJETI TEGEMEZI KWA 40%?' (Rafiki yao mmoja kaanza kunya kwa domo lake!)
 
Apology not accepted.

Sheria za uhamiaji zipo wazi, askari uhamiaji wameshindwa kulinda mpaka ipasavyo.

Kuhusu relationships mipakani, hebu acha kutupotosha, hata geitra nako??, mpaka mwanajeshi wa JWTZ auliwe ziwa tanganyika? .. usitake kutuongopea, you know this is a very peculiar case of border crossing and need to be handled as soon as possible.


Hakuna sheria inayosemaa eti tuongee na nchi wanakotoka kwanza. Wamepewa ultimatum, which is a very diplomatic way of deportation.

Usitumie mfano wa Masongange, that is stupid!! Tanzanians have automatic visas in SA, and when you break the law, you have the right to a due process/fair trial.

They should be arrested after the deadline. Tats just the law!!

But they should not be treated violently.


Sasa kama unajua Uhamiaji na wenzao hawakufanya kazi zao unalalamikia kipi? Kwanini walipokuwa wanaingia hawakuelekezwa hayo matakwa ya sheria? So kama wakati wanaingia ilikuwa sawa leo kipi kimejiri?

Halafu Kobello, na hawa wa hapa Dar na Arusha ambao hata siyo Wanyarwanda wanatakiwa waendelee kukaa siyo? Au ni kwa vile wao Marais wao hawajagombana na Rais wetu?

Matakwa ya sheria? hakuna inayosema waongee na nchi jirani! But unajua lolote juu ya kitu kinachoitwa diplomacy na faida zake japo kidogo? Umewahi kufikiria ni kwa nini nchi zinakuwa na mikataba ya kubadilishana wahalifu? Kwa nini hatuwafukuzi tu? Kwa nini tunawakabidhi mipakani au kwenye ofisi za ubalozi? Labda naku overdose kwani wewe umesoma mpaka wapi? Nahisi kama hunielewi hata nilikuwa nasema kipi na kipi sijasema.

Mahusiano ya mipakani? you have no Idea na ni vipi watu wanaishi huko. Nakushauri tafuta watu wa mipakani. Wao watakwambia wanaishije. By the way nilipokuwa mtoto hata mimi nilikuwa na mawazo kama yako. Lakini kusafiri na kuishi maeneo mengi kunafundisha mengi.

Na kuhusu mifano ya kina Masogange nimeuliza unadhani SA ingeamua kuwabeba na kuwabwaga mpakani kimya kimya ingeleta muonekano upi diplomatically? Sikusema hawaruhusiwi kushitakiwa SA au Walitumia VISA na Passport gani!

Nadhani hata hujaelewa nilikuwa nasema kipi na ni kipi sijasema in the whole post. Nakushauri rudia kusoma, elewa nilichosema, halafu lete hoja upya. Hiyo ya sasa umekoroga mambo too much!
 
ZeMarcopolo,

..nadhani Mzee Mwanakijiji analinganisha apples and oranges hapa.

..kujibu swali la Mwanakijiji ni kwamba Mwalimu aliwapa SILAHA na MAFUNZO YA KIJESHI wakimbizi toka Uganda.

..sasa sijui kama mtoa mada anataka tuchukue hatua kama hizo baada ya Kagame kuanza kufurumusha matusi na kutishia kumdhuru Raisi wetu.

cc Kobello, Nguruvi3, Ogah, Jasusi,
 
Last edited by a moderator:
Kwa hili mbona Kikwete kaweka clear sana ni "WAHAMIAJI WOTE HARAMU WARUDI WALIPOTOKA"
Sasa kama kuna gazeti ama mtu anataka kubadili na kusema ni WARWANDA Pekee hatuwezi kumzuia..Hivi wale watu ambao boti zao huzamishwa wanapozamia Australia mbona hamsemi kuhusu Haki za Binadamu?
Yani mtu aingie ndani kwako kinyemela,Kistarabu kabisa una mpa muda wa kuondoka na Bado alalamike atake kuingia na chumbani? Tena wamshukuru Kikwete kwa uungwana aliouonyesha wa kuwavumulia muda wote huo waliokuwa wakikaa kinyemela...Ningekuwa Mimi hizo ng'ombe ningezitaifisha ili liwe funzo wasirudi tena...
Hatuwezi kuvumilia kuporwa na kuvuliwa nguo tunaposafiri ndani ya nchi yetu....Huruma ikizidi huponza....
Pia hata kama wamewekeza na kumiliki maelfu ya mifugo hilo haliondoi kosa Lao la kuishi nchini kinyume cha taratibu....walitakiwa wajue toka mwanzo kuwa wapo kinyume cha taratibu nchini.
HATUA ZISIPOCHUKULIWA TUNALALAMIKA ZIKICHUKULIWA TUNALALAMIKA..
 
adolay,

..naomba kutofautiana kidogo na wewe.

..Kagera kuna tatizo la ujambazi. Raisi ametoa wiki 2 kwa MAJAMBAZI kusalimisha silaha zao.

..Kagera kuna tatizo la walioingiza mifugo ktk maeneo yasiyostahili kama hifadhi za taifa. Hao pia wamepewa wiki 2 watoe mifugo yao.

..Kagera kuna tatizo la wahamiaji toka nchi jirani. Raisi kawapa wiki 2 waweke mambo yao sawa, au warudi nchi walikotoka.

..hivi Raisi anayebembeleza mpaka majambazi anapaswa kuitwa dikteta kweli? kuwapa muda watu waliovunja sheria waziwazi ni udikteta?

..Raisi amechukua maamuzi hayo baada ya kusikia malalamiko toka kwa wananchi wa Kagera. Nakushauri usome au usikilize hotuba ya Raisi.

..In 2010, Kikwete akiwa ndiyo Raisi wetu, Tanzania iliwapa uraia wakimbizi 160,000 toka Burundi. Sasa madai kwamba Kikwete ni mkatili na dikteta yanatoka wapi?

..Mwisho, natofautiana na Raisi Kikwete ktk masuala chungu nzima, lakini katika hili nakubaliana na hatua alizochukua.

cc Sikonge, Ogah
Enyi watanzania mliojaa unafiki miyoni mwenu na kujiita watu wa amani mbona matendo na maneno yenu yanawasuta.

1.Rais kikwete aliwahi kusema anawajua wauza unga kwa majina lakini hakuwataja wala kuwachukulia hatua.matokeo yake tumeona vijana kama kina Langa,Ngwea na Ray C wakiangamia kwa sembe

2.Rais kikwete aliwajua mafisadi walionyakua vitita vya mabilioni ya shilingi lakini aliwasamehe na kuwaomba warejeshe.
3.Serikali ya rais kikwete imeshuhudia matukio ya kikatili kama kuteswa kwa Dr Ulimboka,Kibanda.kupigwa mabomu kwenye mikutano ya kidini na mauaji kadhaa bila kuchukua hatua stahiki za udhibiti.
4.Serikali hiyo hiyo ya JK imeshindwa kutimiza ahadi ilizoahidi kwa wananchi na badala yake kuyafanya maisha kuwa magumu zaidi.

Leo hii ukiniambia kuondoa wahamiaji haramu walioko kagera ndio priority hasa baada ya msigano kati yake na kagame nitakuona u-mnafiki wa kutupwa.

Jambo hili halitasukuma maendeleo ya kiuchumi ukilinganisha na mambo niliyoyataja hapo juu,sanasana litazorotesha uchumi na uhusiano wetu wa kidiplomasia.

TUSIWE WANAFIKI!!!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu naomba ufafanuzi, hivi wahamiaji haramu Tanzania ni wanyarwanda tu?
Mbona sijasikia wakenya kule Namanga wakikemewa?, Kule mtwara wahamiaji toka msumbiji je?, Wazambia waliojazana tunduma mbona hawaambiwi kurudi makwao?
Na, kwa nini wakati huu tu baada ya kukosana na Kagame?
Give a dog a bad name and then kill it. In the first place serikali zinakuwa wapi hadi panakuwa na wahamiaji haramu? Naweza kuelewa ukizungumzia wakimbizi. Why would one enter a foreign country illegally awe ni Mtanzania au Mnyarwanda? This is wrong. Kwanini watendaji wa serikali maeneo ya mpakani wanakubali rushwa na kuruhusu watu kuingia bila utaratibu. Bila kujali Nyerere aliwashughulikiaje these must go. Kama wanataka kurudi waje kwa utaratibu unaoeleweka. Huu ujinga ndiyo unafanya nchi inabaki uchi kwani wamejipenyeza hadi kwenye majeshi. Wasakwe hata kama tumechelewa warudishwe kwao. Nyerere hakuwa Mungu. Yeye naye kama binadamu alifanya makosa.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Sasa kama unajua Uhamiaji na wenzao hawakufanya kazi zao unalalamikia kipi? Kwanini walipokuwa wanaingia hawakuelekezwa hayo matakwa ya sheria? So kama wakati wanaingia ilikuwa sawa leo kipi kimejiri?

Halafu Kobello, na hawa wa hapa Dar na Arusha ambao hata siyo Wanyarwanda wanatakiwa waendelee kukaa siyo? Au ni kwa vile wao Marais wao hawajagombana na Rais wetu?

Matakwa ya sheria? hakuna inayosema waongee na nchi jirani! But unajua lolote juu ya kitu kinachoitwa diplomacy na faida zake japo kidogo? Labda naku overdose kwani wewe umesoma mpaka wapi? Nahisi kama hunielewi hata nilikuwa nasema kipi na kipi sijasema.

Mahusiano ya mipakani? you have no Idea na ni vipi watu wanaishi huko. Nakushauri tafuta watu wa mipakani. Wao watakwambia wanaishije. By the way nilipokuwa mtoto hata mimi nilikuwa na mawazo kama yako. Lakini kusafiri na kuishi maeneo mengi kunafundisha mengi.

Na kuhusu mifano ya kina Masogange nimeuliza unadhani SA ingeamua kuwabeba na kuwabwaga mpakani kimya kimya ingeleta muonekano upi diplomatically? Sikusema hawaruhusiwi kushitakiwa SA au Walitumia VISA na Passport gani!

Nadhani hata hujaelewa nilikuwa nasema kipi na ni kipi sijasema in the whole post. Nakushauri rudia kusoma, elewa nilichosema, halafu lete hoja upya. Hiyo ya sasa umekoroga mambo too much!
Nimeuelewa upotoshaji wako sana!

On top of that, nimeelewa kutoelewa kwako. Hivi wew umeniona nikilalamika katika uzi huu?? Nimelalamika wapi?

Jamani, kwa akili yako unafikiri asilimia ngapi ya border crossings btn neighbors ipo recorded? Mbona kuna magulio mengi tu mipakani na watu wanafanya biashara kama kawaida?

Ila ukileta ming'ombe yako na kuanza kumiliki ardhi kinguvu, hapo utakuwa unachochea kuchinjwa. Yaani uingie kwa watu na kuanza kufuga ming'ombe yako mpaka kwenye mapori yaliyohifadhiwa?? m... thats too much pushing!!!

Unaweza ukasema watutsi wamekuwa targeted, thats okay kwa sababu, life style ya wafugaji inahitaji, na ina degrade ardhi, na unfortunately kwenye hili, watusi ni wafugaji na style yao ya ufugaji ni ya kizamani na inabidi ibadilishwe. Otherwise their survival will be affected.

Usitetee uharamia!!!

NB:Wewe sidhani kama unaweza kunioverdose kwenye infos zozote, nilisoma na kumaliza "Ant-duhring" by Friedrich Engels nikiwa form two. Na hapa nilipo karibu namalizia page kumi za mwisho za "Consciescism" by Kwame Nkrumah. Hiyo ni hobby tu.
Credentials zangu, siyo kivile ila ni above normal na sizungumzii population ya Tanzania .... so please don't go there.
 
Kikwete ameliingiza taifa kwenye machafuko na chuki ya kibaguzi kwa majirani bila sababu za msingi.
Heshima ya Tanzania imezikwa na Kikwete.
You have a troubled mind probably originating from a troubled past!

Mtu anakutukana kotaifa, halafu bado unamchekea chekea.
Heshima yako unayoiongelea must be from standards of your own troubled up bringing.
 
Kuna mtu anataka kutubugiza HOJA! Hoja ile ile inarudiwa kwa vichwa mbalimbali na mashambulizi kutoka kona mpya kila leo! Lakini msimamo wetu unabaki wazi:
"JAPO DR.KIKWETE ANA MAPUNGUFU YAKE, HAMKARIBII NYERERE HATA KIDOGO KWA BUSARA NA KUJENGA HOJA, LAKINI KWA MSIMAMO WAKE DHIDI YA WAHAMIAJI HARAMU 'HATARI', TUTAMUUNGA MKONO MPAKA DAKIKA YA MWISHO! NA TUNAANZA NA WALE WA MAZIWA MAKUU, AMBAO PAMOJA NA HUJUMA ZAO DHIDI YA UCHUMI WETU (KWA MASAFA MAFUPI NA MAREFU), WENGINE NI RAIA WA NCHI ZINAZOLETA 'KILIMILIMI' KANA KWAMBA TANZANIA NI KOLONI LAO!
KWA KIFUPI: HAWA WATU WARUDI KWAO MAPEMA, WAENDE KWENYE NCHI YAO YA 'MAZIWA NA ASALI!', WATUACHE NA BONGO YETU YENYE 'BAJETI TEGEMEZI KWA 40%?' (Rafiki yao mmoja kaanza kunya kwa dumo lake!)

Kumuunga mkono tu hata pale anapochemka hakumsaidii yeye kubadilika,haiwasaidii kitu washauri wake ambao walikaa kimya mpaka anajitumbukiza humo, haiwasaidii wanaosaidia uvunjaji wa sheria zetu za uhamiaji (wakiwemo askari uhamiaji), wala haiwasaidii Wananchi wa Nchi zote mbili ambapo kesho na keshokutwa watakutana na matokeo ya uhusiano mbovu baina ya nchi hizi! Na kumkosoa hakumaanishi hawa wahamiaji waendelee kukaa bila uhalali. Tunachosema ni kuwa kusiwe na upendeleo wa hukumu na kusiwe na hukumu za jumlajulma. Haki za wote zizingatiwe kikatiba. Wakati unasema "wahamiaji haramu" kumbuka unaweza kuwa unamwambia Mtanzania mwezio ana "mama haramu" au "mkewe haramu" au "mjomba haramu" Au hujui kama watu wa mipakani wameoleana, wana ndugu wengine nchi jirani, au huenda hata huduma za kijamii kama hospitali na shule wanapata nchi nyingine? Fuatilia hilo na utajua kuwa it is really a complex matter.Huu ni mgawanyiko utakaoanza kututafuna wenyewe. Trust me on that. Kushughulikia mambo ya mipaka kunataka busara ya hali ya juu sana!

Lakini ni vema ufahamu na kukumbuka kuwa "HATA BAADA YA KAGAME NA KIKWETE KUPITA, TANZANIA NA RWANDA ZITAENDELEA KUWEPO" So ni vizuri kila kitu kikachukuliwa kwa busara zake kwa faida ya Tanzania na Rwanda ya leo na kesho!
 
We nawe akili zako kama kichwa cha panzi.

Swali lako hili ni sawa na mtu aulize kwanini mradi wa maji uko Karatu kwani Dodoma hakuna shida ya maji.

Au mtu aulize kwanini barabara inajengwa Songea kwani Singida hakuna shida ya barabara.

Umeshawahi kusikia Dar es Salaam kuna mtu kashindwa kufanya shughuli zake kwa sababu ya wahamiaji haramu? Hujui Tanzania ilivyo, kazi yako kusambaza chuki tu...

Chuki inakupeleka kubaya sana...
wewe ni kichekesho halafu ni msahaulifu sana!hujawahi kusikia wamachinga wa Dar wakilalamikia 'wamachinga' kutoka china?Hawa nao wako kwenye mkondo wa siku 14?au tumewasahau kwa kuwa jingping ni best wa JK?
Au unataka mpaka waue mbongo ndio uone hawahitajiki nchini.

NASHUKURU UMERUDI ILI UENDELEE KUPATA DOSE!
 
Enyi watanzania mliojaa unafiki miyoni mwenu na kujiita watu wa amani mbona matendo na maneno yenu yanawasuta.

1.Rais kikwete aliwahi kusema anawajua wauza unga kwa majina lakini hakuwataja wala kuwachukulia hatua.matokeo yake tumeona vijana kama kina Langa,Ngwea na Ray C wakiangamia kwa sembe

2.Rais kikwete aliwajua mafisadi walionyakua vitita vya mabilioni ya shilingi lakini aliwasamehe na kuwaomba warejeshe.
3.Serikali ya rais kikwete imeshuhudia matukio ya kikatili kama kuteswa kwa Dr Ulimboka,Kibanda.kupigwa mabomu kwenye mikutano ya kidini na mauaji kadhaa bila kuchukua hatua stahiki za udhibiti.
4.Serikali hiyo hiyo ya JK imeshindwa kutimiza ahadi ilizoahidi kwa wananchi na badala yake kuyafanya maisha kuwa magumu zaidi.

Leo hii ukiniambia kuondoa wahamiaji haramu walioko kagera ndio priority hasa baada ya msigano kati yake na kagame nitakuona u-mnafiki wa kutupwa.

Jambo hili halitasukuma maendeleo ya kiuchumi ukilinganisha na mambo niliyoyataja hapo juu,sanasana litazorotesha uchumi na uhusiano wetu wa kidiplomasia.

TUSIWE WANAFIKI!!!
meningitis,

..kwanza, ktk mijadala yoyote ile usiwe mkali sana kama hapo unaposema "..watanzania mliojaa unafiki mioyoni mwenu..."

..tukirudi kwenye hoja yako, hata mimi sikubaliani na jinsi JK alivyoshughulika na kashfa luluki ktk nchi hii kwa mfano, EPA, madawa ya kulevya, mauaji ya Mwangosi, mabomu ya Arusha, etc etc

..lakini kwa haya maamuzi aliyochukua kurudisha RULE OF LAW ktk mkoa wa Kagera namuunga mkono. Zaidi namsisitiza Raisi na serikali yake wa-enforce the law ktk maeneo hayo mengine uliyoyataja, mfano EPA, madawa ya kulevya etc etc.

..RULE OF LAW ni moja ya vichocheo muhimu kabisa ktk ukuzaji uchumi na kuendeleza mahusiano mema ya kidiplomasia.
 
Last edited by a moderator:
wewe ni kichekesho halafu ni msahaulifu sana!hujawahi kusikia wamachinga wa Dar wakilalamikia 'wamachinga' kutoka china?Hawa nao wako kwenye mkondo wa siku 14?au tumewasahau kwa kuwa jingping ni best wa JK?
Au unataka mpaka waue mbongo ndio uone hawahitajiki nchini.

NASHUKURU UMERUDI ILI UENDELEE KUPATA DOSE!

Hivi hukuona siku lazaro Nyarandu alipotembelea Kariakoo na kutoa amri ya wahamiaji haramu wa kichina waondoke?

Au unafikiri serikali ni Kikwete tu?
 
Ahaa, hivi kumbe Wanyarwanda ni adui zetu? Now I get it.

Mkuu you are letting down your intellectual might.
Jirani yako anamshambulia jirani yenu-common- kwa jeshi lake analoliita M23
Jirani yako anaonyesha hostile maneuvres kwa ku- infiltrate nchi yako
Jirani ysko anakutukania mkuu ea nchi yako na kuahidi "kukufanyizia"

Halafu wewe unaamua kumchekea chekea kama zuzu
Better find a better class of neighbours!!
 
meningitis,

..kwanza, ktk mijadala yoyote ile usiwe mkali sana kama hapo unaposema "..watanzania mliojaa unafiki mioyoni mwenu..."

..tukirudi kwenye hoja yako, hata mimi sikubaliani na jinsi JK alivyoshughulika na kashfa luluki ktk nchi hii kwa mfano, EPA, madawa ya kulevya, mauaji ya Mwangosi, mabomu ya Arusha, etc etc

..lakini kwa haya maamuzi aliyochukua kurudisha RULE OF LAW ktk mkoa wa Kagera namuunga mkono. Zaidi namsisitiza Raisi na serikali yake wa-enforce the law ktk maeneo hayo mengine uliyoyataja, mfano EPA, madawa ya kulevya etc etc.

..RULE OF LAW ni moja ya vichocheo muhimu kabisa ktk ukuzaji uchumi na kuendeleza mahusiano mema ya kidiplomasia.
pole kwa kuhisi nimekuwa mkali.
Naona unakubaliana na MMM kwamba tusiwe na 'selective justice' yaani hiyo rule of law isiwe kwa kagera tu bali kwa maeneo yote na nyanja zote na pia iwe sustainable na halafu isije wakati tunapotukanwa au kukosana na watu flani!
 
Last edited by a moderator:
ZeMarcopolo,

..nadhani Mzee Mwanakijiji analinganisha apples and oranges hapa.

..kujibu swali la Mwanakijiji ni kwamba Mwalimu aliwapa SILAHA na MAFUNZO YA KIJESHI wakimbizi toka Uganda.

..sasa sijui kama mtoa mada anataka tuchukue hatua kama hizo baada ya Kagame kuanza kufurumusha matusi na kutishia kumdhuru Raisi wetu.

cc Kobello, Nguruvi3, Ogah, Jasusi,

Mkuu JokaKuu,

Wadau wanaomtetea Kagame na matusi aliyotoa kuna kitu wanashindwa kuelewa.

Iwapo jamii yetu itachanganyika na wahamiaji haramu wenye silaha kutoka kwenye nchi ambazo zina chuki na sisi, wahamiaji hawa wanaweza kutumiwa kama njiti ya kibiriti kwenye mafuta ya taa.

Vilevile hawa mashabiki wa Kagame wanashindwa kuelewa kuwa unapokuwa na wahamiajo haramu, adui yako anaweza kuleta wanajeshi wake nchini kwako washambulie huku wakijifanya kuwa wao ni wahamiaji haramu. Hili analifanya Kagame huko Congo kwa kupeleka wanajeshi wake na kuwavisha uniform za waasi.

Wahamiaji haramu maeneo za Kagera, Geita na Kigoma wana silaha kali sana kiasi kwamba wanakuwa tishio hata kwa askari wetu. Je, hizi silaha hawapewi na mtu mwenye chuki na sisi?

Tatizo ni kwamba kuna watu hawajali maisha ya watanzani wanaosumbuliwa na wahamiaji haramu, tamaa zao za kisiasa wanazipa nafasi kubwa kuliko ustawi wa maisha ya watanzania wenzao. Mfano wa watu wa namna hiyo ni Mwanakijiji...
 
Hivi hukuona siku lazaro Nyarandu alipotembelea Kariakoo na kutoa amri ya wahamiaji haramu wa kichina waondoke?

Au unafikiri serikali ni Kikwete tu?
hizo mbwembwe za nyalandu ziliishia wapi?alitoa siku ngapi vile?wachina walioondoka ni wangapi?
Kama serikali sio kikwete kwa nini hili la kagera hakuachiwa waziri husika....hapo ndipo unapozodi kudhihirisha kuwa jambo hili ni la kukurupuka na kisasi.
 
Swali hili linahitaji jibu; jibu lake linaweza kuwa rahisi au gumu. Lakini ni jibu linalotegemea ujuzi wa historia. Ni jibu linalojaribu kuangalia kama uamuzi wa serikali ya Tanzania kutekeleza sheria kwa upendeleo (selective justice) ni uamuzi sahihi au ni miongoni mwa maamuzi mabovu kabisa yaliyowahi kuchukuliwa na watawala wetu.


Ndio maana hili swali linaendelea kusimama, Nyerere alishughulikiaje wahamiaji haramu kutoka Uganda wakati wa chokochoko? Kuna mtu anakumbuka au tuwasaidie hawa wa kizazi kipya somo la historia kidogo maana inaonekana watu wasiojua historia wanaenda kurudia makosa yake!

Tunaweza vipi kukubali serikali ichukue hatua za sheria kwa mfumo wa kibaguzi na udhalilishaji wa utu wa binadamu na bado tunajiita Watanzania?

Mungu atusaidia tusifurahie vitendo kama hivi kwa jina la 'uzalendo'!


MMM

Mkuu kwa heshima kubwa uliyonayo humu JF na nje ya hapa, basi kuna haja ukaweka hiyo historia ya Mwalimu Nyerere kuhusu wakati wa matatizo na Uganda kabla hujahitimisha lawama zako kwa Serikali chini ya JK.Zaidi ya hapo hisia ya utendaji mbovu wa Serikali na mambo mengine unaweza kuwa sababu za huu mtazamo uliokuwa nao.

(selective justice)
Ebu tuangalie hapa tu ! Kwa hiyo kuanza kufanyia kazi sheria huko Kagera na Kigoma kunatosha kuitwa selective?


 
Nimeuelewa upotoshaji wako sana!

On top of that, nimeelewa kutoelewa kwako. Hivi wew umeniona nikilalamika katika uzi huu?? Nimelalamika wapi?

Jamani, kwa akili yako unafikiri asilimia ngapi ya border crossings btn neighbors ipo recorded? Mbona kuna magulio mengi tu mipakani na watu wanafanya biashara kama kawaida?

Ila ukileta ming'ombe yako na kuanza kumiliki ardhi kinguvu, hapo utakuwa unachochea kuchinjwa. Yaani uingie kwa watu na kuanza kufuga ming'ombe yako mpaka kwenye mapori yaliyohifadhiwa?? m... thats too much pushing!!!

Unaweza ukasema watutsi wamekuwa targeted, thats okay kwa sababu, life style ya wafugaji inahitaji, na ina degrade ardhi, na unfortunately kwenye hili, watusi ni wafugaji na style yao ya ufugaji ni ya kizamani na inabidi ibadilishwe. Otherwise their survival will be affected.

Usitetee uharamia!!!

NB:Wewe sidhani kama unaweza kunioverdose kwenye infos zozote, nilisoma na kumaliza "Ant-duhring" by Friedrich Engels nikiwa form two. Na hapa nilipo karibu namalizia page kumi za mwisho za "Consciescism" by Kwame Nkrumah. Hiyo ni hobby tu.
Credentials zangu, siyo kivile ila ni above normal na sizungumzii population ya Tanzania .... so please don't go there.

Way too out again. Hakuna anayesema waendelee kukaa Tanzania. Tunasema busara na diplomacy ni better than bifu!
 
hizo mbwembwe za nyalandu ziliishia wapi?alitoa siku ngapi vile?wachina walioondoka ni wangapi?
Kama serikali sio kikwete kwa nini hili la kagera hakuachiwa waziri husika....hapo ndipo unapozodi kudhihirisha kuwa jambo hili ni la kukurupuka na kisasi.

Kwnai mbwembwe za Kikwete zimeishia wapi mpaka unazifananisha na za Nyarandu?
 
Kumuunga mkono tu hata pale anapochemka hamsaidii yeye kubadilika, haiwasaidii wanaosaidia uvunjaji wa sheria zetu za uhamiaji, wala haiwasaidii Wananchi wa Nchi zote mbili ambapo kesho na keshokutwa watakutana na matokeo ya uhusiano mbovu baina ya nchi hizi! Na kumkosoa hakumaanishi hawa wahamiaji waendelee kukaa bila uhalali. Tunachosema ni kuwa kusiwe na upendeleo wa hukumu na kusiwe na hukumu za jumlajulma. Haki za wote zizingatiwe kikatiba.

Lakini ni vema ufahamu na kukumbuka kuwa "HATA BAADA YA KAGAME NA KIKWETE KUPITA, TANZANIA NA RWANDA ZITAENDELEA KUWEPO" So ni vizuri kila kitu kikachukuliwa kwa busara zake kwa faida ya Tanzania na Rwanda!

Unajua kutongoza! I GIVE YOU THAT! Hoja zako zinakwenda sambamba na jicho lako zuri (You must be very beautifull!), yaani unawezamlegeza chui mwenye njaa! Lakini hoja hapa sio Kikwete na Kagame, tatizo letu ni la muda mrefu la wahamiaji haramu ambao pamoja na kuharibu mazingira yetu na kutuletea biashara ya zana za kivita haramu na kujihusisha na vitendo vya ujambazi bado wengine wanaongozwa na vichaa wanaofikiri jumuia ya Africa mashariki inawapa nchi yetu kama koloni lao na Rais wetu kama mkuu wa mkoa!
NDUGU, MAAMUZI YA KIKWETE NI SAHIHI HATA DUNIA NZIMA IKIPINGA!
ANYATHING SHORT OF THAT IS "UTTER NONSENSE! AND IF IT IS AN IDEOLOGICAL PROBLEM THEN WE BETTER LEAVE IT WITH THOSE WHO HAVE IT, AND...,MAYBE, DEAL WITH IT LATER!"
 
Back
Top Bottom