Taarifa kwa Umma: Humphrey Polepole Kufanya Mkutano na Waandishi wa Habari Leo Jumapili Kuanzia Saa 8 Mchana

Taarifa kwa Umma: Humphrey Polepole Kufanya Mkutano na Waandishi wa Habari Leo Jumapili Kuanzia Saa 8 Mchana

Ndugu Mtanzania Mzalendo tafadhali mkumbushe & Mtaarifu Mwenzako

Tuna Jambo Letu Leo

Iko faida ya kuuishi na kuusema ukweli, Na leo nitausema na kuudhihirisha ukweli. Kura zote kwa Mkweli Namba1, Dkt. Magufuli
View attachment 1582246
Maskini mmechanganyikiwa kiasi hiki? poleni...hizi Press conferenec hazitakiwi kufanywa na msemaji wa chama bali zinatakiwa kuwa za mgombea mwenyewe...kwani mgombea anashida gani mbona mnataharuki kiasi hiki!!polenii MATAGA
 
Kampeni zinaendelea, CCM chama changu mmejifungia sijua wapi. Kila siku Polepole anaitisha waandishi wa habari kuwaeleza yaleyale, kwanini tusimkemee na kumfundisha namna ya kutengeneza habari zinazouza? Jambo likirudiwa mara kwa mara kwa njia ileile hata Kama ni zuri linaboa.

Press kila siku hazina tija kwa wapiga kura wala wanachama, tunatamani tukimbie Kama wanavyokimbia wenzetu huku mtaani.

Kampeni za Lisu yupo peke yake bila usaidizi wa Mbowe wala figure kubwa ya chama na anatoboa, sisi tunakwama wapi?

Kwanini tumepoteza mvuto kwa wapiga kura? Kwanini tusitumie mbinu kuwajua wanaotuhujumu na kukaa nao meza moja ya maridhiano kuliko kuwatisha?

Uanachama Ni haki ya mtu, tuwarudie tuliowakata na kuwaomba radhi ili wakasimame majukwaani na sisi. Muda unaotumia kufanya press ungetengeneza maridhiano ndani ya chama na kukubali kwamba ninyi watu wachache amwezi kushinda uchaguzi Wala kuwavutia watu wawachague.

Mlishawatukana Watanzania, mliwaambia wabunge wetu wasiguswe hata wasipofanya chochote na wao wakabweteka kwa sababu tulisema wasiguswe. Tulidhani wanaoumia ni wapinzani kumbe mliwaumiza Watanzania, wabunge wetu walichaguliwa na wananchi na si wapinzani, ombeni radhi kwa kuwadharau wapiga kura.

Achana na press fanyeni Mambo yanayoonekana Kama wenzenu, wao wamesoma wapi Hadi wawe na upeo mkubwa kiasi hiki? Sisi tunakosaje wanamikakati Kama walivyo CHADEMA?
Unaenda dukani kuwanunulia watoto nguo halafu wanakataa kuvaa. Unawalazimisha wanalia na kukimbilia kwa jirani.

Sent from my Nokia 6.1 using JamiiForums mobile app
 
Baada ya Lissu kuwambia watu ufisadi wa kiwanja Chato na eka elf 25 karagwe na mzee baba kukosa hofa ya ku COUNTER ATTACK watu wengi wamepunguza imani na uaminifu kwa mzee baba. Lissu kinachombeba ukiachia hoja zake kali hana makandokando ya ufisadi. Waliokosa hoja dhidi yake wanatumia hoja dhaifu eti katumwa na mabeberu.
 
Baada ya Lissu kuwambia watu ufisadi wa kiwanja Chato na eka elf 25 karagwe na mzee baba kukosa hofa ya ku COUNTER ATTACK watu wengi wamepunguza imani na uaminifu kwa mzee baba. Lissu kinachombeba ukiachia hoja zake kali hana makandokando ya ufisadi. Waliokosa hoja dhidi yake wanatumia hoja dhaifu eti katumwa na mabeberu.
Ujasiri pia unamsaidia.
 
Huyu mkubwa si kaongea juzi tu hapa? Anahisi hakuweza kufikisha ujumbe vizuri anataka arudie?
Chakubanga ni mtu anayejiona anajua saana, na ana uwezo mkubwa sana wa kueleza na kufafanua jambo likaeleweka vizuri kwa watu kuliko mtu mwingine yeyote.
Kwenye sakata la tril.1.5 alijifanya anaelewa sana na kujaribu kulitolea ufafanua, watu wa aina ya Chakubamga ndivyo walivyo, they are suprisingly confident!!
 
CCM ina kampeni za kisayansi
Walioko na wanaogombea CCM ni wasaka tonge tu wala hawana uchungu na WANANCHI na ndio maana wametuletea Sheria za ajabu sana za MAFAO wakati wenyewe washachukua chao ni UBINAFSI WA HALI YA JUU SANA. WOTE MBWA TUU.
 
Back
Top Bottom