Taarifa ya ajali ya Tanga vifo 17 naiona Aljazeera, TV za bongo zinaonesha miziki tu

Taarifa ya ajali ya Tanga vifo 17 naiona Aljazeera, TV za bongo zinaonesha miziki tu

Gari ya msiba ndio ili overtake

Wakiokufa 14 ni Ukoo mmoja wa Mrema

Watoto wa Marehemu wamekufa, Watoto wa Kaka yake, Mashemeji zake na wengine

Waliibiwa pesa zote na vitu vyao

Wanaomba msaada wakazike Uchagani


Mmoja wa wahusika wa Msiba akiongea na waandishi wa Habari
Unaweza kuta marehemu aliwaambia kabisa "nikifa msiende kunizika huko...." lakini hawakumwelewa.
 
Nimenukuu

Chanzo cha Ajali ni Mwendo Kasi na Uzembe wa Dereva wa Gari Na :T.673 CUC M/Fuso Kulipita gari la mbele Bila Ya kuchukua Tahadhari na kugongana Uso kwa uso Gari Na :T.863 DXN T/Coaster
Inaumaaa
 
Radio,TV bongo ni mwendo wa kukata mauno tu ,matangazo kamali ,umbea
Kuanzia asubuhi mpk kesho yake

Ova
Mtawalaumu bure hawa watu wa media. Hizi ni media zimetengenezwa kama chanzo cha kipato na hazijitoshelezi kifedha.
Wewe angalia Habari, mpira, maigizo, muziki, sijui vipindi gani vyote vinaoneshwa kwenye channel mmoja. Hata upande wa radio bado sana tulitakiwa tuwe
Television zinaonyesha michezo tu.
Television zinaonesha habari tu
Television za vipindi vya dini tu
Television za movie
Television kwa ajili ya documentary tu hata radio tu.
Mfano hai angalia
Aljazeera, Sony Ten 1, Discovery, wild animal.
Ukiangalia Safari channel huwa unakuta wameweka muziki au habari?
 
Ifike tu muda madereva wakisababisha ajali,mbali na kunyanganywa leseni,na magari yao yachukuliwe na hata kutaifishwa kabisa, maana huku barabarani kuna muda unaona kitu ambacho dereva anafanya,unaona kabisa kakusudia na siyo bahati mbaya, dereva wa gari kubwa anaona magari madogo yote ni takataka mbele yake,anaweza kufanya chochote, dereva wa gari dogo,ana muona bodaboda ni kama kumbikumbi,anaendesha anavyotaka, bodaboda na yeye ni kama vile fahamu huwa zinamtoka saa akiendesha, kuna haja ya hatua kali kabisa kuchukuliwa,faini za hali ya juu ziwepo,uzembe utapungua.
Kuna siku nikiwa na pikipiki yangu barabaran dereva wa Fuso ananiambia "Wewe Paki kibao chako Cha kukunia Nazi pembeni" daah nilijisikia vibaya sana
 
Kamejengeka ka mazoea ka msafara wa mazishi kuondoka usiku. Na kila msiba unaiga.
 
Gari ya msiba ndio ili overtake

Wakiokufa 14 ni Ukoo mmoja wa Mrema

Watoto wa Marehemu wamekufa, Watoto wa Kaka yake, Mashemeji zake na wengine

Waliibiwa pesa zote na vitu vyao

Wanaomba msaada wakazike Uchagani


Mmoja wa wahusika wa Msiba akiongea na waandishi wa Habari
Inauma
 
Nimeikuta ALJAZEERA wanaionyesha muda wote kwenye kimstari kinachopita chini, scrolling ticker. Yani wameipa umuhimu.

nikaenda kutafuta details kwenye TV za bongo, zote zinaonyesha vipindi vya miziki...

Ndio aina ya media ambayo inaruhusiwa. Serikali kwa makusudi inalea taifa la watu wasio na taarifa wala mijadala muhimu, kwa hiyo hatuwezi kutafuta majawabu ya matatizo yetu, deaf dumb and blind. Kwa ajili hiyo tunaendelea kufa.
Za bongo zimehamia kwenye kuhamasisha kamari (betting)
 
Kutofunga mikanda ndio sababu kuu ya hawa watu kufa, maana gari haikupinduka, waliobanwa ni waliokuwa siti za mbele na zinazofatia, wengine wote ......
 
Za bongo zimehamia kwenye kuhamasisha kamari (betting)
Mtawalaumu hawa watu wa media. Kumbuka taarifa ya habari, michezo, muziki, vipindi vya dini n.k vinaoneshwa kwenye channel moja. Mlolongo ni mrefu sana. Tulitakiwa tuwe na channel za habari, muziki, michezo n.k hapo ndiyo utaweza kuwalaumu.
Hiyo habari unaiona kipindi cha habari au breaking news.
 
Kuna siku nikiwa na pikipiki yangu barabaran dereva wa Fuso ananiambia "Wewe Paki kibao chako Cha kukunia Nazi pembeni" daah nilijisikia vibaya sana
Hahahah nmecheka kwa sauti ,utadhani iyo dereve anamiliki ata hiyo pikipiki sasa ,na ndio wa kwanza kutolewa kafara na maboss zao shenzi type

Sent from my Infinix X655 using JamiiForums mobile app
 
Mimi nimesikitika tu maiti iliyokuwa inaenda kuzikwa imekufa Mara mbili... kwa maana ya kifo Cha Mwanzo na kifo Cha ajali.
 
Mtawalaumu bure hawa watu wa media. Hizi ni media zimetengenezwa kama chanzo cha kipato na hazijitoshelezi kifedha.
Wewe angalia Habari, mpira, maigizo, muziki, sijui vipindi gani vyote vinaoneshwa kwenye channel mmoja. Hata upande wa radio bado sana tulitakiwa tuwe
Television zinaonyesha michezo tu.
Television zinaonesha habari tu
Television za vipindi vya dini tu
Television za movie
Television kwa ajili ya documentary tu hata radio tu.
Mfano hai angalia
Aljazeera, Sony Ten 1, Discovery, wild animal.
Ukiangalia Safari channel huwa unakuta wameweka muziki au habari?
Kenya wapo vizur wana channel nyingi ambazo zina jitegemea tofauti na hapa nyumbani TBC zipo mbili tu

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom