Taarifa ya ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne katika shule za kanisa katoliki Tanzania

Taarifa ya ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne katika shule za kanisa katoliki Tanzania

Tumsifu Yesu Kristo. Taarifa hii inatolewa na Idara ya Elimu ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kuhusu matokeo ya mtihani wa kidato cha nne wa mwaka 2024 kwa shule za Kanisa Katoliki.

Lengo la kutolewa kwa taarifa hii ni kutoa tathmini ya ufaulu wa shule hizo ili kubaini maendeleo ya kitaaluma, maeneo yanayohitaji maboresho, na mwelekeo wa jumla wa elimu katika taasisi hizo.

Kwa mujibu wa takwimu, jumla ya watahiniwa wote nchini Tanzania walikuwa 516,695. Kati yao, wanafunzi wa shule za Kanisa Katoliki walikuwa 19,182, sawa na asilimia 3.6 ya watahiniwa wote.

Kwa upande wa ufaulu, wanafunzi waliopata daraja la kwanza hadi la tatu walifikia 18,745, sawa na asilimia 97.72 ya watahiniwa wa shule za Kanisa. Wanafunzi waliopata daraja la nne walikuwa 128 (asilimia 2.23), huku waliopata daraja la sifuri wakiwa watu 9 tu, sawa na asilimia 0.04.

Ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2023, ufaulu wa shule za Kanisa umeendelea kuimarika. Mwaka huu, kiwango cha ufaulu kimeongezeka kwa asilimia 1.66, tofauti na ongezeko la asilimia 0.15 mwaka uliotangulia.

TAKWIMU ZA UFAULU KWA KILA DARAJA

Daraja la Kwanza
: Wanafunzi 12,308 (64.16%)

Daraja la Pili: Wanafunzi 4,991 (26.01%)

Daraja la Tatu: Wanafunzi 1,146 (7.53%)

Daraja la Nne: Wanafunzi 128 (2.23%)

Daraja la Sifuri: Wanafunzi 9 (0.04%)

TAKWIMU ZA UFAULU KWA SHULE
Katika shule za Kanisa, jumla ya shule 65 zilipata ufaulu wa A, shule 160 ufaulu wa B, shule 47 ufaulu wa C, huku shule 2 zikipata ufaulu wa D. Hakuna shule hata moja iliyopata ufaulu wa E.

SHULE KUMI ZILIZOONGOZA KWA UFAULU

1. St. Francis Girls, Mbeya

2. Cardosa Girls, Dar es Salaam

3. Tengeru Boys, Arusha

4. Precious Blood Girls, Arusha

5. Bethel Girls, Mafinga

6. Mawua Seminary, Moshi

7. Anuarite Girls, Moshi

8. St. Mary's Mazinde Juu, Tanga

9. Marian Boys, Morogoro

10. St. Aloysius Girls, Dar es Salaam

PONGEZI NA MAPENDEKEZO
Tunaipongeza jamii nzima ya shule za Kanisa, ikiwemo walimu, viongozi wa shule, wafanyakazi, na wanafunzi kwa kazi kubwa iliyofanikisha matokeo haya. Pia, shukrani kwa wazazi ambao wamewajibika katika malezi na elimu ya watoto wao.

Tunawashukuru maaskofu kwa kusimamia shule hizi, kuhakikisha zinazingatia maadili ya Kanisa, na kuimarisha huduma za kiroho kwa wanafunzi. Huduma hizo zimechangia mafanikio haya makubwa.

Hadi kufikia mwaka 2025, lengo ni kupunguza kabisa wanafunzi wanaopata daraja la sifuri na kuboresha zaidi kiwango cha ufaulu. Idara ya Elimu inahimiza waalimu na wakuu wa shule kuendelea kuweka juhudi kubwa zaidi ili kuhakikisha elimu inayotolewa inaleta mabadiliko chanya kwa jamii.

Tunaendelea kuwaombea baraka za Mungu katika kutekeleza jukumu la elimu na malezi ya wanafunzi wetu.


View: https://youtu.be/BDXmTW0SIZ8

Tujenge VETA nyingi zaidi na kujikita kwenye special education kuanzia primary hadi chuo. Kanisa halipaswi kuendelea kujikita kufanya mambo ambayo watu wengine wanaweza kuyafanya vizuri.
 
Shule zimejengwa na waumini kwa kukabwa koo ya michango halafu ada inayowekwa waumini hawawezi kumudu kulipia watoto wao kwa shule waliyojenga wao wenyewe.

The same na hospitali, waumini wanachangishwa kujenga hospitali lakini wakiugua hawawezi kutibiwa bure kwenye hospitali walizojenga wenyewe. Huu ni wizi kama wizi mwingine kwa mgongo wa dini.

Dini ni utapeli kama utapeli mwingine Mungu hayupo.
Kwa kweli umenena mkuu
 
Tumsifu Yesu Kristo. Taarifa hii inatolewa na Idara ya Elimu ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kuhusu matokeo ya mtihani wa kidato cha nne wa mwaka 2024 kwa shule za Kanisa Katoliki.

Lengo la kutolewa kwa taarifa hii ni kutoa tathmini ya ufaulu wa shule hizo ili kubaini maendeleo ya kitaaluma, maeneo yanayohitaji maboresho, na mwelekeo wa jumla wa elimu katika taasisi hizo.

Kwa mujibu wa takwimu, jumla ya watahiniwa wote nchini Tanzania walikuwa 516,695. Kati yao, wanafunzi wa shule za Kanisa Katoliki walikuwa 19,182, sawa na asilimia 3.6 ya watahiniwa wote.

Kwa upande wa ufaulu, wanafunzi waliopata daraja la kwanza hadi la tatu walifikia 18,745, sawa na asilimia 97.72 ya watahiniwa wa shule za Kanisa. Wanafunzi waliopata daraja la nne walikuwa 128 (asilimia 2.23), huku waliopata daraja la sifuri wakiwa watu 9 tu, sawa na asilimia 0.04.

Ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2023, ufaulu wa shule za Kanisa umeendelea kuimarika. Mwaka huu, kiwango cha ufaulu kimeongezeka kwa asilimia 1.66, tofauti na ongezeko la asilimia 0.15 mwaka uliotangulia.

TAKWIMU ZA UFAULU KWA KILA DARAJA

Daraja la Kwanza
: Wanafunzi 12,308 (64.16%)

Daraja la Pili: Wanafunzi 4,991 (26.01%)

Daraja la Tatu: Wanafunzi 1,146 (7.53%)

Daraja la Nne: Wanafunzi 128 (2.23%)

Daraja la Sifuri: Wanafunzi 9 (0.04%)

TAKWIMU ZA UFAULU KWA SHULE
Katika shule za Kanisa, jumla ya shule 65 zilipata ufaulu wa A, shule 160 ufaulu wa B, shule 47 ufaulu wa C, huku shule 2 zikipata ufaulu wa D. Hakuna shule hata moja iliyopata ufaulu wa E.

SHULE KUMI ZILIZOONGOZA KWA UFAULU

1. St. Francis Girls, Mbeya

2. Cardosa Girls, Dar es Salaam

3. Tengeru Boys, Arusha

4. Precious Blood Girls, Arusha

5. Bethel Girls, Mafinga

6. Mawua Seminary, Moshi

7. Anuarite Girls, Moshi

8. St. Mary's Mazinde Juu, Tanga

9. Marian Boys, Morogoro

10. St. Aloysius Girls, Dar es Salaam

PONGEZI NA MAPENDEKEZO
Tunaipongeza jamii nzima ya shule za Kanisa, ikiwemo walimu, viongozi wa shule, wafanyakazi, na wanafunzi kwa kazi kubwa iliyofanikisha matokeo haya. Pia, shukrani kwa wazazi ambao wamewajibika katika malezi na elimu ya watoto wao.

Tunawashukuru maaskofu kwa kusimamia shule hizi, kuhakikisha zinazingatia maadili ya Kanisa, na kuimarisha huduma za kiroho kwa wanafunzi. Huduma hizo zimechangia mafanikio haya makubwa.

Hadi kufikia mwaka 2025, lengo ni kupunguza kabisa wanafunzi wanaopata daraja la sifuri na kuboresha zaidi kiwango cha ufaulu. Idara ya Elimu inahimiza waalimu na wakuu wa shule kuendelea kuweka juhudi kubwa zaidi ili kuhakikisha elimu inayotolewa inaleta mabadiliko chanya kwa jamii.

Tunaendelea kuwaombea baraka za Mungu katika kutekeleza jukumu la elimu na malezi ya wanafunzi wetu.


View: https://youtu.be/BDXmTW0SIZ8

Wale wa upande wa Munyazi Mungu wana cha kujifunza hapa!
 
Tumsifu Yesu Kristo. Taarifa hii inatolewa na Idara ya Elimu ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kuhusu matokeo ya mtihani wa kidato cha nne wa mwaka 2024 kwa shule za Kanisa Katoliki.

Lengo la kutolewa kwa taarifa hii ni kutoa tathmini ya ufaulu wa shule hizo ili kubaini maendeleo ya kitaaluma, maeneo yanayohitaji maboresho, na mwelekeo wa jumla wa elimu katika taasisi hizo.

Kwa mujibu wa takwimu, jumla ya watahiniwa wote nchini Tanzania walikuwa 516,695. Kati yao, wanafunzi wa shule za Kanisa Katoliki walikuwa 19,182, sawa na asilimia 3.6 ya watahiniwa wote.

Kwa upande wa ufaulu, wanafunzi waliopata daraja la kwanza hadi la tatu walifikia 18,745, sawa na asilimia 97.72 ya watahiniwa wa shule za Kanisa. Wanafunzi waliopata daraja la nne walikuwa 128 (asilimia 2.23), huku waliopata daraja la sifuri wakiwa watu 9 tu, sawa na asilimia 0.04.

Ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2023, ufaulu wa shule za Kanisa umeendelea kuimarika. Mwaka huu, kiwango cha ufaulu kimeongezeka kwa asilimia 1.66, tofauti na ongezeko la asilimia 0.15 mwaka uliotangulia.

TAKWIMU ZA UFAULU KWA KILA DARAJA

Daraja la Kwanza
: Wanafunzi 12,308 (64.16%)

Daraja la Pili: Wanafunzi 4,991 (26.01%)

Daraja la Tatu: Wanafunzi 1,146 (7.53%)

Daraja la Nne: Wanafunzi 128 (2.23%)

Daraja la Sifuri: Wanafunzi 9 (0.04%)

TAKWIMU ZA UFAULU KWA SHULE
Katika shule za Kanisa, jumla ya shule 65 zilipata ufaulu wa A, shule 160 ufaulu wa B, shule 47 ufaulu wa C, huku shule 2 zikipata ufaulu wa D. Hakuna shule hata moja iliyopata ufaulu wa E.

SHULE KUMI ZILIZOONGOZA KWA UFAULU

1. St. Francis Girls, Mbeya

2. Cardosa Girls, Dar es Salaam

3. Tengeru Boys, Arusha

4. Precious Blood Girls, Arusha

5. Bethel Girls, Mafinga

6. Mawua Seminary, Moshi

7. Anuarite Girls, Moshi

8. St. Mary's Mazinde Juu, Tanga

9. Marian Boys, Morogoro

10. St. Aloysius Girls, Dar es Salaam

PONGEZI NA MAPENDEKEZO
Tunaipongeza jamii nzima ya shule za Kanisa, ikiwemo walimu, viongozi wa shule, wafanyakazi, na wanafunzi kwa kazi kubwa iliyofanikisha matokeo haya. Pia, shukrani kwa wazazi ambao wamewajibika katika malezi na elimu ya watoto wao.

Tunawashukuru maaskofu kwa kusimamia shule hizi, kuhakikisha zinazingatia maadili ya Kanisa, na kuimarisha huduma za kiroho kwa wanafunzi. Huduma hizo zimechangia mafanikio haya makubwa.

Hadi kufikia mwaka 2025, lengo ni kupunguza kabisa wanafunzi wanaopata daraja la sifuri na kuboresha zaidi kiwango cha ufaulu. Idara ya Elimu inahimiza waalimu na wakuu wa shule kuendelea kuweka juhudi kubwa zaidi ili kuhakikisha elimu inayotolewa inaleta mabadiliko chanya kwa jamii.

Tunaendelea kuwaombea baraka za Mungu katika kutekeleza jukumu la elimu na malezi ya wanafunzi wetu.


View: https://youtu.be/BDXmTW0SIZ8

Hawa wapuuzi wanatangaza biashara kwa upande moja na kuleta mgawanyiko kwa msingi wa dini
 
Toka lini Marian boys ikawa Morogoro na St.Aloysius ikawa Dsm?
Marian boys ipo Bagamoyo jimbo katoliki la Morogoro na st. Aloysius ipo kibaha jimbo Kuu katoliki Dar es salaam. kwa hiyo sista alikuwa anataja shule kutokana na majimbo katoliki zilipo hizo shule
 
Ngoja niwahii masifu ya asubuhii sasa!

Atukuzwe Baba mwana na Roho Mtakatifu kama mwanzo na sasa na siku zote milele Amina 🙏

Eh Mungu uliye nguvu yetu na makimbilio ya wanadamu

Kwa wema usikilize sala za watu wako wanaokulilia.... Amen
 
Shule zimejengwa na waumini kwa kukabwa koo ya michango halafu ada inayowekwa waumini hawawezi kumudu kulipia watoto wao kwa shule waliyojenga wao wenyewe.

The same na hospitali, waumini wanachangishwa kujenga hospitali lakini wakiugua hawawezi kutibiwa bure kwenye hospitali walizojenga wenyewe. Huu ni wizi kama wizi mwingine kwa mgongo wa dini.

Dini ni utapeli kama utapeli mwingine Mungu hayupo.
Ni wapi ulikabwa koo wakati wa ujenzi wa hizo shule? Nitajie na mfano hata wa shule moja tu uliyokabwa koo kwa michango wakati wa kujengwa kwake! Halafu unataka hizo shule zisitoze ada, halafu wale walimu mahiri watalipwa na nani mishahara mizuri ya kuwafanya wawe na ari ya kufundisha kwa bidii zaidi?

Kwenye dunia ya leo ya survival of the fittest, bado unawaza kupewa huduma za afya za bure kwenye hospitali za Kanisa! Na wale wahudumu nao watakuhudumia bure? Je, wewe hapo ulipo unafanya kazi bure pasipo na malipo?
 
Mbinu ya kibiashara.

B.T.W! hongereni Sana RC kwa kuchukua jukumu la NECTA na kulifanyia kazi ninyi kama ninyi kwa Shule zenu tu.
 
Back
Top Bottom