Taasisi dhaifu ni kitisho kwa usalama wa nchi. Kwa hali ilivo, TANESCO ni hatari namba moja kwa usalama wa Tanzania, na serikali bado imelala fofofo!

Itikadi za kiliberali zinahitajika sana kwenye management ya uchumi... Nimependa ulivosema shida ya umeme ipo tangu unatafuta mchumba mpaka sasa unatafuta wajukuu, maana yake ni kwamba inaonesha, kwa miaka yote hiyoo serilali imekosa kuwa na plan za kuleta mageuzi kwenye hii sekta
 
Ndo madhara ya monopoly kwenye umeme kwa shirika ambalo ni dhaifu.. kwahiyo hiyo ineleta mashaka kwenye kuendesha SGR na Viwanda.... ndo maana nikamalizia kwa kusema kuna siku Tanesco itaangusha huu uchumi
 
Waruhusiwe wazalishaji binafsi kuuza umeme hapa nchini. Tanesco wabaki wanapiga siasa. Kama iliwezekana kwenye mawasiliano ya simu baada ya kuondoa ukiritimba wa TTCL, kwanini tuendelee na hawa wapiga porojo wa Tanesco?
Huko ndo kunatakiwa tuende... soko huria. Kuendelea kuipa nguvu Tanesco na kuwapa monopoly power hakuna sustainability yoyote. Tanesco hawana ufanisi.

Ukipita mtaani kuna manguzo kibao ya zege yamezagaa chini. Hiyo ndo inakupa taswira hili ni shirika la namna gani
 
Hahahaha msamehe mkuu
 
Kwamba kila mkoa kuwe na Generation source ya umeme? Hilo linawezekana?
KWa maana ya mikoa isiyokuwa na source ya umeme itatumia umeme wa mikoa ya jirani... lakini kikubwa ukishakuwa na private sekta efficiency lazima ipatikane tu.... kuna mambo tunaona hayawezekani ila ni kwasababu bado hayajafanyika
 
Nje ya mada ...hivi mkuu wewe Ndio Nantoomba Mushi ,unehariri jina au ni Ndugu yake!?
Hahahaaa ndo mimi mkuuu.... niliamua kubadilisha tu baada ya wakuu kunipiga vijembe kila uchwao...
 
Pamoja mkuu
 
Inaonekana una chuki sana na JPM ila sikushangai maana hii nchi Ina wajinga wengi sana

JPM alipeleka umeme vijijini

Kwa Sasa hakuna anayepeleka umeme vijijini Wala anayefikiria hilo Makamba amekaa pale miaka 2 Kuna siku ulimsikia kuhusu kupeleka umeme vijijini? Ndio kwanza alipandisha bei ya kuvuta umeme vijijini

Hongera zote ziende Kwa JPM Kwa kuanzisha ujenzi wa bwawa la Nyerere ndio tumaini pekee la watanzania lililobakia kuhusu kutatua changamoto ya umeme

Wewe hauna tofauti na wananchi wa Libya waliomsaliti Gaddafi Leo hi wameingia katika dimbwi la mateso na wataka humo milele
 
Hakika...
KWa maana ya mikoa isiyokuwa na source ya umeme itatumia umeme wa mikoa ya jirani... lakini kikubwa ukishakuwa na private sekta efficiency lazima ipatikane tu.... kuna mambo tunaona hayawezekani ila ni kwasababu bado hayajafanyika
Hakika ...Matatizo hayatatuliwi na akili ileile iliyoyatengeneza ...labda kuwa na nguvu kutoka nje!
 
Hongera kwa uchambuzi mzuri!

Kwenye pendekezo lako, wananchi mpo tayari kununua UNIT 1 ya umeme kwa Tsh2500 kwa sasa?
Asante pamoja....

Hapo kwenye bei, unajua bei inaakisi ufanisi wa kampuni, historia inaonesha soko huria huwa linasababisha bei kupungua... ukitaka kuthibitisha hilo angalia mitandao ya simu.

Kwa Tanesco ya sasa, kama ikiendelea hivi, itapelekea bei ya umeme kupanda maradufu kwasababu hawajiendeshi kwa ufanisi
 
Ndugu huna uelewa wowote kuhusu Mpango wa Mkapa Rural Electrification...Tatizo mnapenda Siasa za makelele ...Ndio maana JPM aliwadanganya mkadanganyika! Kifunze kutoka nje ya box ...utawaelewa Wanasiasa! Namchukia JPM Kwa sababu alikuwa muongo n aliwafanya watu wote Wapumbavu...Angalia ule usanii wa Mashirika ya Umma yaliyokuwa yanapata faida enzi zake ...Eti yanatoa na Gawionkwa Serikali ...Uongo wa kitoto Kabisa! Bila shaka wewe ni mojawapo ya wajinga ,sijui Wapumbavu walio shangilia Mwamba alivyokuwa anawashughukikia Barrick/ACCACIA😂😂Kupitia Kwa Prof.Ossoro Et al na Tapeli Mwandamizi Prof .Kabudi! Unajua kinachoendelea au bado unasubiri mgao wa Noah!
 
Mkuu unqishi wapi...utekelezaji ukianza zamai sana...huyu mñayemtukuza alianza kujinadi kuwa anapeleka umeme Vijijini,kumbe watu walianza zamani!
Mi naishi Bukokwa, chuki dhidi jpm haziwezi kubadili mambo,ujinga unaendelea Sasa jamaa asingevumilia.
 
Hahahaha pole sana mkuu kwa kukaa gizani... huwa inatia hasira unakuta umeme umekatika zaidi ya 10, siku yote inakuwa imeshaisha
Biashara zinazo tegemea umeme ni vilio vitupu...
Yaan watu wanakosa Pato lao sabb ya kukosekana umeme..
Hahahaa... ndo kilema changu hicho. Yaani nisipoweka graf naona kama sieleweki hivi...
Tupo pamoja mkuu...
 
Asante mkuu pamoja
Umeandika hoja jadidifu ambayo kila nukta imejaa uzalendo na mahaba kwa nchi yetu.

Kuna wakati nikishauri kuwa serikali itumie wataalam wake kufanya haya yafuatayo
  1. Irasimishe dawati la biashara na uchumi kuwa kurugenzi kamili pale TISS. Wanajua
  2. Serikali ianzishe makapuni kwa ubia na watanzania wazalendo. Tanesco iuze hisa zake
  3. TIC yaani kituo cha uwekezaji kiwe na dawati la kuatamiza wawekezaji wa kati ili kuwezesha Watanzania kukua into investment sector worldwide.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…