Doctor Ngariba
JF-Expert Member
- Jan 28, 2020
- 588
- 951
Shalooom!
Wakuu, nilisafiri kwa basi fulani kuelekea mkoani Mtwara ila nilijiskia vibaya sana kuona kila muziki unaochezeshwa kwenye luninga ya gari unaonesha watu walio nusu uchi. Mbaya zaidi nilikuwa na mtoto wa sister naye macho yake yalikuwa yanakodolea kila kinachoendelea. Moyoni nilijisemea "dah hivi huyu dogo hapa anajifunza nini'?
Anyway, madereva wa magari nawashauri mufikirie mnavyotuonesha abiria wenu maana kuna ukakasi fulani tunauona kupitia luninga zenu. Msilazimishe haya maungo ya wadada yaonekane ya kawaida mbele ya watoto na wakwe zetu.
Tambueni ya kwamba mnatuharibia maadili ya watoto wetu kwa kiasi kikubwa kutokana na tabia ya kuwaonesha vitu kama hivi mbele ya macho yetu. Naamini zipo video ambazo mkizionesha watu watafurahi na pia hamtowapa huzuni mbele ya watu wanaowaheshimu.
Najua wapo ambao watapinga na kuniona pengine "a primitive guy" ila watambue kuwa usipoziba ufa utajenga ukutaa.
Wakuu, nilisafiri kwa basi fulani kuelekea mkoani Mtwara ila nilijiskia vibaya sana kuona kila muziki unaochezeshwa kwenye luninga ya gari unaonesha watu walio nusu uchi. Mbaya zaidi nilikuwa na mtoto wa sister naye macho yake yalikuwa yanakodolea kila kinachoendelea. Moyoni nilijisemea "dah hivi huyu dogo hapa anajifunza nini'?
Anyway, madereva wa magari nawashauri mufikirie mnavyotuonesha abiria wenu maana kuna ukakasi fulani tunauona kupitia luninga zenu. Msilazimishe haya maungo ya wadada yaonekane ya kawaida mbele ya watoto na wakwe zetu.
Tambueni ya kwamba mnatuharibia maadili ya watoto wetu kwa kiasi kikubwa kutokana na tabia ya kuwaonesha vitu kama hivi mbele ya macho yetu. Naamini zipo video ambazo mkizionesha watu watafurahi na pia hamtowapa huzuni mbele ya watu wanaowaheshimu.
Najua wapo ambao watapinga na kuniona pengine "a primitive guy" ila watambue kuwa usipoziba ufa utajenga ukutaa.