Tabia ya kuweka miziki yenye video za nusu uchi kwenye usafiri wa umma ikome

Tabia ya kuweka miziki yenye video za nusu uchi kwenye usafiri wa umma ikome

Doctor Ngariba

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2020
Posts
588
Reaction score
951
Shalooom!

Wakuu, nilisafiri kwa basi fulani kuelekea mkoani Mtwara ila nilijiskia vibaya sana kuona kila muziki unaochezeshwa kwenye luninga ya gari unaonesha watu walio nusu uchi. Mbaya zaidi nilikuwa na mtoto wa sister naye macho yake yalikuwa yanakodolea kila kinachoendelea. Moyoni nilijisemea "dah hivi huyu dogo hapa anajifunza nini'?

Anyway, madereva wa magari nawashauri mufikirie mnavyotuonesha abiria wenu maana kuna ukakasi fulani tunauona kupitia luninga zenu. Msilazimishe haya maungo ya wadada yaonekane ya kawaida mbele ya watoto na wakwe zetu.

Tambueni ya kwamba mnatuharibia maadili ya watoto wetu kwa kiasi kikubwa kutokana na tabia ya kuwaonesha vitu kama hivi mbele ya macho yetu. Naamini zipo video ambazo mkizionesha watu watafurahi na pia hamtowapa huzuni mbele ya watu wanaowaheshimu.

Najua wapo ambao watapinga na kuniona pengine "a primitive guy" ila watambue kuwa usipoziba ufa utajenga ukutaa.
 
Kubaliana tu uhalisia. Uko kwenye dunia ya utandawazi. Hivyo hakuna namna nyingine ya kuepuka hiyo hali. Labda uwe unatumia usafiri wamo binafsi.
 
Na kwa siku hizi za sikukuu na kufungua shule wazazi wanasafiri na watoto wako, mzazi inabidi ujifanye huoni. Wakitoa miziki wanaweka muvi za kukatana mtapanga, kupigana risasi yaani full kuharibu maadili.
 
Watoto ndio walengwa wasipoziona kwenye mabus wataziona sebuleni kwako kupitia housegirl baada ya Kazi macho ukutani wanachoangalia wewe huwezi jua wewe upo kazini.
 
Lengo la miziki hii ya kizazi kipya ni kuibomoa jamii na kuondoa utu wa mwanamke kwa kumfanya bidhaa au jalala la kutupia uchafu. Leo wapo uchi hata bila kuvua
 
Utaongea utachoka na wala hawafanyi chochote.

Nimeshawahi kuja na uzi kama huu.
 
BASATA limeruhusu nyimbo nyingi zinazoonyeshwa. Wenye mabasi wanaona zimehalalishwa.
 
Watoto ndio walengwa wasipoziona kwenye mabus wataziona sebuleni kwako kupitia housegirl baada ya Kazi macho ukutani wanachoangalia wewe huwezi jua wewe upo kazini.
Oa mwanamke mwenye misingi ya hofu na Mungu ifundishe familia yako juu ya kuwa na maadili sebule yako itapunguza/itaacha kuangalia uchafu na Muombe Mungu utafanikiwa kwa rehema zake.
 
Hii nchi imejaa wapumbavu mtoa Mada pole Sana .

Wao utandawazi Ni. Kuonesha uchi wao

Hawajui utandawazi ni ubunifu wa kuleta Mabadiliko chanya kwa Taifa na dunia kwa ujumla , Dada zetu wamejiuza miaka nenda Rudi katika utandawazi Basi waulize Ni kitu gani wame-gain Cha maana!
 
Ila watoto wameharibika mno siku hizi nikivionaga vitoto vya kike vinavyokata viuno huko mtaani utafikiri vikahaba nikionaga hivyo najua tu vimeona kwenye haya manyimbo ya hovyohovyo
 
Back
Top Bottom