Tabia ya wachaga kurudi kwao Kilimanjaro kila ifikapo mwisho wa mwaka ni jambo zuri na la kuigwa na makabila mengine

Tabia ya wachaga kurudi kwao Kilimanjaro kila ifikapo mwisho wa mwaka ni jambo zuri na la kuigwa na makabila mengine

Niwapongeze sana wachaga kwa utaratibu wao wa kukutana kila ufikapo mwisho wa mwaka,
Sababu zao kukutana ni kama ifutavyo

1. Kukutana na kuonana live ndugu jamaa na marafiki baada ya kupotezana kwa takribani mwaka mzima kwenye harakati za utafutaji.

2. Kusherehekea kumaliza mwaka salama kwa kula nyama na kunywa mbege kwa wingi

3. Kuwapiga taff wenzao ambao hali zao kimaisha hazijatengemaa

4. Kufanya mambo ya kimila nk.

Najua yapo mengi ila leo nimetaja baadhi, kama kuna mengine unaweza kuongezea.

Mimi si mchaga lakini nawaonea wivu sana wachaga kwa tabia hii ya ushirikiano, kwani umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, Hii ni tofauti kabisa na makabila mengine.

Natamani kuwajengea wanangu haka katabia ili wakikua waishi kwa Kupendana na kushirikiana.

NB: Kama wewe ni mchaga popote ulipo hongera sana.
Mbona sisi Wamwera hii ni desturi yetu toka enzi na enzi sema tu hatuji proud maana hatuoni sababu ya kufanya hivyo.
 
Mkuu,
Jamii iliyo na maendeleo lazima wakumbuke nyumbani kwao ila jamii za kimaskini nikurogana na ushirikina dats why Kuna jamii hazipendi kwenda ma kwao....

Chagga's ni Moja ya highly & mosted civilized tribes in Tanzania
Sisi tuna tunadamu ya kiyahudi kwetu ni canan ...ukiona mtu haendi kwao jua hata pakulala ni shida
 
Unajuwa nauli ya Dar Bukoba, Dar Mwanza, Dar Kigoma?
Miaka kumi umejificha tu Dar hata kwenda kwenu hutaki kisa nauli? Achaeni utani kwenye masuala sirias bwana! Ila kwenye mbunye hata ukiambiwa uifuate Katavi nauli itapatikana! 😀 😀 😀

Hata kama hamtakwenda kila mwaka lakini mnaweza kujiwekea interval hata ya miaka miwili miwili. LABDA KAMA UNAOGOPA KUROGWA HUKO KWENU MAANA HICHO NACHO NI KIPENGELE KWA MIKOA MINGINE.
 
Issue sio kurudi kwenu, issue ni unarudi kwenu kufanya nini, kuna nini, utakuwa na nani na unaendaje?

Kama hujui tu, fahamu haya;
1. Wachaga wanaorudi kwao December huko kwao wamejenga miji, tena miji ya uhakika. Hivyo for real wanakwenda kwao.

2. Sehemu kubwa huwa wanakwenda kutambika pia. (Ukishaona uchagani kuna kaburi nyumbani la mzee, kuna kuchinja na kufa na kupona ukoo umepambana kurejea December, ijue kwa 90% kuna tambile unless ni walokole).

3. Wachaga wanaorudi kwao December ujue wana ndugu wa karibu kama wazazi wapo huko na ndugu zao wengine wa karibu watakuja December. Ni ujamaa ideology.

4. Safari ya December kurudi uchagani ni safari ya gharama kubwa kifamilia, ni lazima mfukoni uwe vizuri au ujipange kwa muda mrefu na kujinyima vilivyo.

Mwisho kabisa, huu utamaduni hata uchagani umepungua sana, karibu 50% ya wachaga hawarudi tena makwao December ukilinganisha na miaka 20 iliyopita.
Ukiona hivyo ujue asilimia kubwa ya wazee wa kichaga walikuwa town au sehemu mbalimbali hapa Tz na kwingineko wameshaumaliza mwendo. Waliobaki ni watoto wao ambao hawakuzaliwa huko uchagani hivyo hawana connection ya moja kwa moja ha huko. Hiyo inaweza kuwa mojawapo ya sababu zenye mashiko za idadi ya wachaga wanaorudi kwao mwezi December kupungua!
 
Kionjo
 
Niwapongeze sana wachaga kwa utaratibu wao wa kukutana kila ufikapo mwisho wa mwaka,
Sababu zao kukutana ni kama ifutavyo

1. Kukutana na kuonana live ndugu jamaa na marafiki baada ya kupotezana kwa takribani mwaka mzima kwenye harakati za utafutaji.

2. Kusherehekea kumaliza mwaka salama kwa kula nyama na kunywa mbege kwa wingi

3. Kuwapiga taff wenzao ambao hali zao kimaisha hazijatengemaa

4. Kufanya mambo ya kimila nk.

Najua yapo mengi ila leo nimetaja baadhi, kama kuna mengine unaweza kuongezea.

Mimi si mchaga lakini nawaonea wivu sana wachaga kwa tabia hii ya ushirikiano, kwani umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, Hii ni tofauti kabisa na makabila mengine.

Natamani kuwajengea wanangu haka katabia ili wakikua waishi kwa Kupendana na kushirikiana.

NB: Kama wewe ni mchaga popote ulipo hongera sana.
Linachangia wizi, kila mchaga anashindana kuiba ili arudi kwao aoneshe ana hela, yaani hata kuroga kwa ajili ya vyeo serikalini wanaongoza ilia wapate vyeo waibe na ukiwazibia kuiba wanakuua kwa sababu wanataka hela za show off uchagani. Kwa ufupi mashindano yao yanaitia hasara serikali rip Mafuru
 
Back
Top Bottom