Tabia yangu ya kutojipendekeza, kusujudia maboss na kutokuwa mfitini inanisotesha mtaani

Tabia yangu ya kutojipendekeza, kusujudia maboss na kutokuwa mfitini inanisotesha mtaani

Angalia maneno ya BWANA kwenye Mithali 26:28,. 29:5;. Ezekieli 12:24; Danieli 11:32; 1Wathesalonike 2:5.
Screenshot_20200802-072737.jpg
 
Daa pole sana boss pambana ujiajiri,kuna mshikaji wangu alipiga chini u lab manager kwa sababu ya majungu

California love
 
Kama kawaida baada ya kumaliza chuo nikaingia mtaani kusota na maisha bahati nzuri nikapata intern kwenye moja ya taasisi za serikali zinazolipa vizuri.​

Changamoto ikawa kumbe kwenye taasisi hizi za serikali inatakiwa ufanye kazi kwa bidii bila kusahau kujipendekeza kwa boss.​
Kwa jinsi nilivyo tabia yangu ya kutopenda kujipendekeza wala kufitini wafanyakazi wenzagu mm nikawa natimiza Majukumu kama kawaida.​

Kumbe ilitakiwa niwe naenda hata kumuona boss personly angalau mara moja kwa wiki kumsalimia tu ambavyo wengine hufanya sasa mm nawaza nikamuone manager nimweleze nini Cha zaidi wakati meeting za Kila wiki tunakutana na kila mtu anawasilisha ripoti yake?.​

Basi bwana boss akaanza kulalamika ooh sina msaada kwenye office ikabidi nifuatilie kujua ninakwama wapi bassi wadau wakanitonya jipendekeze nenda hata mara moja peleka umbea wowote ule atakukubali tu.​

Asikwambie mtu hakuna kazi ngumu Kama kuwa mmbeya eneo la kazi Kama hauna tabia hiyo.​

Mm nikasema potelea mbali ilimradi natimiza Majukumu yangu na nipo qualified siwezi kujipendekeza kwenye ofsi hii nitapata kazi hata kwingine.​

Mkataba wa intern ukaisha boss Kama kawaida akaaniambia nitafute kazi sehemu nyingine.​

Mwamba nikaona siyo kesi nikaingia mtaani nikapata kazi kampuni nyingine ya kibongo aisee kule ndo ikawa balaa bila kuwa mbeya humalizi mwezi unatimuliwa boss anataka kila siku mpishane na wafanyakazi ili apate taarifa mara huyu kapeleka fulani mwizi kaiba mafuta, kifusi.​

Daah nikaona pia isiwe kesi nikaacha kazi.​
Sasa Nina mwaka nasota mtaani nimezunguka kinoma hamna kazi kila Kona patupu wadau wanashauri tafuta hata viongozi wa kisiasa ujipendekeze kazi siku hizi kujuana mm naona wananisumbua tu.​

Natafuta kazi nikiamini qualifications zangu zitanibeba lakini patupu nimeapply sehemu nyingi hata kuitwa hakuna.​

Nikatafuta mpaka sehemu za vibarua patupu. Sasa nawaza hii tabia ya kutojipendekeza nitaachaa vipi maana kubadili tabia ni ngumu kama kubadili ngozi.​
yani mkuu umenigusa kabisa, mbaya zaidi Mimi nilikua mchapakazi Sana wakati naajiriwa, kwaiyo niiawa natokea kupendwa na mabosi bila jitihada kubwa, lakini Sasa hivi vimbilimbili ambavyo havijui kazi vinajua kujipendekeza tu ndio shida inapoanzia, Mana unamkuta mtu kazini unapiga mzigo kivyako anaona Kama unachukua nafasi yake vile, Kama unamfunika flani.
Dah kazi zote nilizoajiriwa isipokua moja- tu niliondoka kwa fitna za wajumbe, kazi ya mwisho nilikua na gari Fulani ya pfisi natumia ila weekend napaki natumia tu katikati ya wiki, j3 moja- naingia job nikachkua ndinga nikaisogeza kidogo tu nikajua Ina shida nikatoa taarifa kwa Kila mtu na kuuliza kwamba Nani katumia weekend, sikupata ushirikina mzuri ila baadae nilimbaini huyo mjumbe, kiufupi gari ilibidi ikae gereji siku tatu, na ikaonekana Mimi ni mzembe pamoja na kajitetea kote kumbe wadau walishapeleka maneno kwamba gari siijali halafu natoka nayo weekend. Nikajikataa nikawaachia kazi yao, ndani ya mwaka mmoja hakuna hata mjumbe mmoja alibaki kwenye ile kampuni, walitolewa wote. Mwisho nikajigundua Sina nyota ya ajira tu
 
kujipendekeza na kujikomba ni vitu ambacho nimefeli kwa kweli, ila kuwa friendly ni kitu ambacho kiasili nipo hivyo hivyo nimejikuta nina marafiki wengi sababu ya kuwa muwazi, kitu kinachosababisha wengi wanifate na kuniomba ushauri au kunikosoa pale napoyumba.

ila chuki makazini huwa zina sababu nyingi kuna jamaa yangu ye kazi anapiga fresh tu ila maboss wanamchukia kinoma sababu jamaa havungi akiona pisi kali kiasi kwamba kuna muda anapita na usingizi wa maboss zake
 
Hata mimi nimeona, kuna tofauti ya kumheshimu boss na kujipendekeza kwa boss, huyu jamaa anazarau either kwa kujiona ana elimu kubwa au sawa na boss wake.

Katika maisha mtu unatakiwa kuwa na heshima na sikujipendekeza kwa msimamizi wako au mkuu wako haijalishi unamzidi elimu au anakuzidi.
 
They didn't tell you the truth. Utendaji kazi wako uko below average. Hakuna mtu mwenye akili timamu atakubali kumpoteza mfanyakazi jembe kisa hajipendekezi.
 
They didn't tell you the truth. Utendaji kazi wako uko below average. Hakuna mtu mwenye akili timamu atakubali kumpoteza mfanyakazi jembe kisa hajipendekezi.
hujawajua maboss wa kibongo, eneo la kazi anakuwa na nyoka wake wawili hadi watatu wa kumpa udaku na umbea, hata akiwa hayupo nakuhakikishia atajua deep down ya kila jambo(kiofisi na yasiyo ya kiofisi!) hapo ndipo utakaposhangaa huyu jamaa anapata wapi taarifa!
 
Usiogope na usijali. Kaa ukijua wema na uaminifu unalipa sana. Pia kumbuka giza na nuru haviishi sehemu moja lazima nuru italiangamiza giza.

Brother, utapata kazi nzuri sana ambayo hukuwahi kuiwaza kabisa maana ni aina ya kazi ambayo ndio ndoto ya watu wengi.

Mungu akusimamie katika kila jambo.
Huu ni ushauri bora kabisa. Fuata ushauri huu
 
Kitu pekee ntakua mdogo na mnyenyekevu kuliko maelezo ni pale nimekamatwa na mke wa mtu..vinginevyo kwenye mambo ya kazi hapana kabisa kuendekeza kujipendekeza.

Mtu umeacha kazi zako na kwa nia njema umeenda kusabahi tu, anashindwa hata kuthamini akatumia lugha ya staha kukufukuza badala ya kuwa muungwana?

Niliwahi kuacha kazi sehem kwa mambo haya haya.
Mkuu ukifika kazini fanya kilichokupeleka, habari za kusabahi ni nje huko baada ya muda wa kazi. Mambo ya kusabahi watu ofisini ndio kujipendekeza kwenyewe. Unashindwa kutulia sehemu yako ya kazi unazunguka kusalimia watu, kama sio kujipendekeza ni nini?
 
Back
Top Bottom