TABORA: Mtu mmoja afariki baada ya kupokonywa hirizi zake

TABORA: Mtu mmoja afariki baada ya kupokonywa hirizi zake

Hivi hao Askari huwa hawajui hirizi huwa ni bima ya afya ya kiasili kabisa!! Wamesha mchomoa betri mtu wa watu😂😂
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Jamani..nacheka siyo kwamba yanafurahisha.

R.i.p
 
Mmmh polisi wetu hawa kweli tena kwa maelezo kuwa alikorofishana nao!! Hapo lazima kachezea kipigo kweli akawa hoi mpaka mauti sasa sababu iwe ipi ili wajinasue katika kumpekua wakagundua alikuwa na powerbank ya asili na kwa kuwa wengi wanaamini hayo ikabidi watokee huko.
Mtoa uzi anaye ripoti tukio hili ni Askari polisi. maelezo yake tu yanathibitisha.
 
Watanzania sio wajinga
Shida ya watu wenye mamlaka wanajua bado wanaishi na watu wenye akili ya 1950 ambao wengi hawajaenda shule. Sasa hivi Tanzania imebadilika sana mpaka ufikie hatua ya kumdanganya mtu inabidi ujipange sana.
Kwa hawa askari na wanajeshi wetu wa Afrika. Umchanie nguo au umtukane siyo rahisi kukuacha hai hata akikuacha lazima akuachie kilema.
POLISI + MWANAJESHI ADUI YAKE NAMBA MOJA NI MWANANCHI
 
Polisi wajue Watanzania sio wajinga kiasi hicho.

............Ifike mahali waache kupiga watuhumiwa hadi kuwasababishia vifo, hirizi haiwezi sababisha kifo hata siku moja.
 
Hakuna cha hirizi wala mavi ya kuku kapigwa na Polisi huyo wanamtafutia sababu.
kumchania sare afande...huyu atakuwa amekula kichapo heavy MPAKA akaona nyota.
Na Ni sawasawa, huwezi kuwadharau makamanda wetu namna hiyo...unawachania ngu????!!!!!
 
Inamaana alivyochana gwanda hakufanywa chochote? nahisi alipewa mkong'oto hawezi kuchana akaachwa tu! Hirizi is by the way ila watakuwa walimwonyesha cha mtema kuni.
ha ha ha ha ha ha mtema kuni alafu ni mtu wa huko huko tabora
 
neno kuporwa limetumika vibaya kwenye story, hakuna uwiano wa kisarufi. Polisi walichukua ndumba zake...hawakupora.
 
Michael Paschal mwenye umri wa miaka 33, mkazi wa Uhemeli Ndala, Nzega, mkoa wa Tabora, afariki baada ya kuporwa hirizi zake na polisi akifanyiwa upekuzi.

Kijana huyo ambaye ni bodaboda alifikishwa kituoni mara baada ya kumkaba na kumchania sare CPL Lucas aliyekuwa katika majukumu ya usalama barabarani.

Askari (Lucas) alipomsimamisha Michael akiwa anaendesha pikipiki yenye usajili MC.246 BXH kwa ukaguzi, Michael alifanya fujo kwa kumkaba polisi na kumchania sare zake.

Askari alifungua mashtaka ya kuzuiwa kufanya majukumu yake, kijana Michael alikamatwa na kufikishwa kituoni alipokuwa akifanyiwa upekuzi alikutwa na hirizi mbalimbali sehemu ya mwili wake.

Mtuhumiwa akaomba asitolewe hirizi zake kwani zikitolewa atakufa, kulingana na sheria za upekuzi kwa mtuhumiwa anayewekwa mahabusu walizitoa hirizi hizo.

Baada ya kuzitoa hirizi hali yake ikaanza kubadilika kwa kuishiwa nguvu na kuzilai alipelekwa zahanati ya Kashishi kwa matibabu ilipofika saa 3.00 usiku akafariki dunia. Mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora.
I DOUBT HUYU ALIKUWA NI JAMBAZI HATARI SANA.
 
Back
Top Bottom