Tabu ninayopata kutoka kwenye familia yangu

Tabu ninayopata kutoka kwenye familia yangu -15

Boss ;aise Dr yuhu ni Dr samweli tulikuwa nae hapa kwa muda mrefu lakini akawa amepata kazi sehemu nyingine yenye mshahara mkubwa zaidi akawa ameondoka na aliondoka kwa uzuri tu ,Sasa hivi yupo likizo kwa muda wa mwezi mmoja ,Sasa itabidi upokezane nae kwenye shift zako

Asassin Eagle ; ok bosi nimekusikia lakini Mimi Niko hapa nimelidhika na nikipatacho kutoka hapa ,Niko hapa muda wote Sasa nikimpisha jamaa nitadistabu kipato changu tofauti na hapo naona Kuna haja ya kutafuta kazi sehemu ingine ,yaani kunipumzisha jamaa kwenye muda wa likizo wa jamaa sidhani kama ni sawa

Bosi ; basi chagua moja kama kuacha kazi au kumpisha jamaa afanye kazi kwa muda .


Asassin [emoji1659] ;sawa bosi Mimi naona Bora niache kazi ,nilifanya hivyo kwa sababu tayari Nina sehemu ya kujishikiza nikaona sehemu za ubabaishaji zitanipotezea muda


Basi Mimi nikaamua kuondoka zangu ,nikachukua Kila kilicho changu nikasepa , niliendelea kufanya kazi kinondoni wakati huo naendelea kutafuta kazi sehemu ingine

Baadae nikapata kazi mbezi ,nikafanya interview pale ikaonekana Mambo mengi nayamudu ikiwemo swala la uongozi ,bosi akaniambia ,bosi akaniambia nahitaji uwe msimamizi wangu ,watumishi wa hapa ni changamoto wanapenda sana kudokoa dokoa pesa hivyo inahitajika umakini mkubwa ,nikamwambia hakuna shida ila naomba kufanya kazi siku tano ila naomba jumamosi na jumapili nipumzike hapo nilikuwa nalenga kinondoni

Baada ya Mimi kuondoka bunju yule jamaa aliendelea kufanya kazi lakini hata wiki mbili hazikuisha ,akaitajika ofisin kwao kwa kazi ya dharula ,basi jamaa ikabidi arudi kazini kwake pale akawaacha hawana mtu




Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Endelea kutiririka ili tukupe ushauri bora
 
Hii mico ndio ile ya sinza ya watoto au?
 
Tabu ninayopata kutoka kwenye familia yangu -16
Kote huko nilikozunguka kufanya kazi Kuna changamoto niliyokuwa naipitia kutoka kwenye familia yangu,kwangu Mimi naziita tabu ,tukianzia kwa kina anko mpaka na kwa ndugu ambao nilikuwa siwafahamu

Kina mjomba walivyosikia tu Nina kibarua Kila mtu akaanza kuniorodhoshea shida zake ,mara mwingine anahitaji nimnunulie gali la biashara , mwingine anunuliwe mashine ,duh kwa mshahara gani ninaopata mpaka nifanye hayo Mambo ,shida ndogo ndogo ambazo zilikuwa ndani ya uwezo wangu nilikuwa nawasaidia tatizo ni kwamba hawaridhiki ,siku ukiwa hauna basi maneno na dua mbaya hutozimaliza

Sema ukweli hiyo hali ilikuwa inaniongezea stress sana kwa sababu unajikuta una solve shida za watu mpaka unakosa pesa ya kutumia

Hali hii ilipelekea mpaka nikawa nashindwa kuwatafuta kwenye simu kuwasalimia ,yaani unampigia mtu kumsalimia ndio kwanza anakuelezea shida zake

Nisiseme wengine Hata mama yangu pia alikuwa hanitamkii maneno mazuri ,kwakweli nilikuwa na mawazo sana

Misaada hii tunayochukua kwa watu ni madeni makubwa ,sema kwa sababu katika safari ya maisha Kuna changamoto nyingi huwezi jua ,ukikutana na watu wanaosaidia kwa lengo ukifanikiwa na yeye anufaike aise utajuta

Basi baada ya kupata kazi mbezi ikabid niende kuhamisha vitu vyangu mkuranga ,tayari nilishakuwa na vitu vingi kidogo ikiwemo godoro na vyombo

Basi nilihamisha vitu vyangu kutoka mkuranga mpaka sehemu moja mwananyamara kwa manjunju ,pale ilikuwa rahisi kufika makumbusho lakini karibu sana na kinondoni

Chumba nilipata kwa elfu 40 ,kigeto geto niliona sio mbaya

Yule mchumba wangu tulikuwa bado tunawasiliana na nilipanga mwisho wa mwezi niende kwao kujitambulisha kama sio kuoa kabisa

Basi niliendelea kupiga kazi kwakweli maisha yangu yalibadilika sana ,ilivyofika mwisho wa mwezi niliomba ruhusa ya wiki moja kote nilikokua nafanyia kazi ili niweze kwenda mwanza kwao na mchumba wangu



Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…