TACAIDS: Wafadhili wa dawa za kupambana na kuzuia magonjwa nyemelezi ya UKIMWI wamejitoa

TACAIDS: Wafadhili wa dawa za kupambana na kuzuia magonjwa nyemelezi ya UKIMWI wamejitoa

Status
Not open for further replies.
UKIMWI,mbona kama unachukuliwa simple? Jamii imesahau adha za wagonjwa wa UKIMWI? Sasa kama dawa zitaadimika hali itakuwa mbaya,wagonjwa wengi watakufa mapema
 
Hii ni nzuri ili watu waogope na kuacha zinaa wazi wazi .maana leo watu wanajisifu uzinifu wamesahau km kuna magonjwa ikiwemo ukimwi .

Ccm oyeeee ccm juu zaidi
 
Bora waende. Ni aibu kuendelea kupokea msaada wa ARVs pamoja na condoms. Magufuli na regime yake sasa wafill hili gap. Hakuna namna nyingine
unadhan wanafill gap kama unavyofill udongo kuziba shimo? hadi serkali ishushe matumizi waishi kawaida. kitu ambacho si rahis hivyo.
 
Watu wametumia na wameishi miaka 20+, ukiwa mwathirika acha kunywa dawa uzikwe siku chache zijazo au kunywa dawa uwe na uhakika wa 20+ years.
Uhakika wa kufa kwa Liver failure, kidney failure na heartfailure, ndio uhakika huo?
 
Pneumonia na TB
Anaekupa ARV anakupa kwa sababu zipi? Na anaekunyima dawa za magonjwa nyemelezi anakunyima kwa sababu zipi? Hivi ni kwamba nchi hii watu wamejaza funza vichwani mwao kiasi kushindwa kutafakari concept rahisi kama hii, watz mna mtindio wa ubongo au? Shida ni nini hadi upeo wa kifikiri unakuanmdogo koasi hiki??!!!
 
Hizo ARV mbona hawajaacha kutoa? Waache kutoa na hizo uone kama kuna mtu atakufa, maana hizo ARV ndio zinaua watu kwa sasa
Nimeamua kuchangia kwasababu ningepata vijana 10 kama ninyi mngekaa jela mpaka kifo! Hivi unajua ni nini strategy ya WHO na Dunia kwasasa kuhusu maambukizi? Na trend ikoje kwenye jamii? Hivi unahisi zikisitishwa wewe utasalimika (familia yako)


Ifike pahala tuache mizaha kwenye mambo ya msingi.....

Mungu ainusuru jamii yetu....

Good night [emoji35]
 

Summary​

Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (Tacaids) imesema wafadhili wa dawa za kupambana na kuzuia magonjwa nyemelezi ya Ukimwi wamejitoa.
janet josephpic

By Janeth Joseph

Moshi. Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (Tacaids) imesema wafadhili wa dawa za kupambana na kuzuia magonjwa nyemelezi ya Ukimwi wamejitoa.

Taarifa hiyo imetolewa jana na mkurugenzi mtendaji wa Tacaids, Leonard Maboko kwenye ufunguzi wa wiki ya Ukimwi duniani uliofanyika viwanja vya Shule ya Msingi Mandela vilivyopo Kata ya Pasua, Moshi mjini.

Hata hivyo, alisema mfuko ulioanzishwa na tume hiyo (AIDS Trust Fund) ulioanzishwa mwaka 2015 utasaidia kuziba pengo litakalokuwepo kwa miaka miwili.

“Wafadhili wameendelea kupungua nchini lakini huu mfuko wa ndani utasaidia kupunguza haya mapengo,” alisema Maboko.

Sasa hivi, alisema wafadhili wanatoa dawa za ARV lakini dawa za kupambana na kuzuia magonjwa nyemelezi wamejitoa.

Alisema mfuko huo utawasaidia Watanzania wanaohitaji dawa zilizokuwa zinatolewa na wafadhili waliojitoa.

Kwa upande wake, mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira alisema takwimu zinaonyesha maambukizo ya Ukimwi yamepungua mkoani humo kutoka asilimia 7.2 mwaka 2004 mpaka asilimia 2.6 mwaka 2018.

Aidha aliwataka wananchi kujitokeza kupima afya zao kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kujua hali za afya zao na kupunguza maambukizi mapya ya vVirusi vya Ukimwi.

Kilele cha siku ya Ukimwi duniani ni Desemba mosi.

By gazeti la Mwananchi online
Wafunge kabisa ofisi zao wasepe; siyo wasitishe huduma zao halafu waendelee kuitafuna nchi ya Tanzania
 
Nimeamua kuchangia kwasababu ningepata vijana 10 kama ninyi mngekaa jela mpaka kifo! Hivi unajua ni nini strategy ya WHO na Dunia kwasasa kuhusu maambukizi? Na trend ikoje kwenye jamii? Hivi unahisi zikisitishwa wewe utasalimika (familia yako)


Ifike pahala tuache mizaha kwenye mambo ya msingi.....

Mungu ainusuru jamii yetu....

Good night [emoji35]
Acha zako wewe... kijana yupo sahihi huyo,

#Waache kutoa na ARVs#
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom