Uchaguzi 2020 Tafakuri: Je, ni kwanini CCM inatumia nguvu kubwa kumnadi Dkt. Magufuli?

Subira the princess

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2018
Posts
3,474
Reaction score
3,744
Wasalaam,

Nimetafakari na kushangaa kwa ni nini chama dola chama pendwa CCM kinatumia nguvu nyingi ikiwamo vitisho kumnadi magufuli ili hali Mh kaleta maendeleo kama flyover, mabarabara na hospitali?

Tumeshudia CCM ikiandaa tamasha kubwa na kulipa wasanii zaidi ya mia2 ili kuwatumia katika kampeni, na leo tumeshuhudia ikikusanya viongozi na kuwatuma kwa waumini wao wakapigie kampeni CCM.

Ikiwa CCM na serikali yake ilipiga marafuku vyama vya upinzani kwa miaka5, kuzuia Uhuru wa vyombo vya habari wasiwasi na kuogopa uchaguzi vinatoka wapi?

Binafsi nimeshangaa vingozai wa dini kuelekezwa nn wakanye kama vile viongozi wote wanafurahia utawala wa CCM.

Maendeleo yana vyama.
 
1 SAMWELI 18

6 Hata ikawa, walipokuwa wakienda, hapo Daudi aliporudi baada ya kumwua yule Mfilisti, wanawake wakatoka katika miji yote ya Israeli, kwa kuimba na kucheza, ili kumlaki mfalme Sauli; wakatoka na matari, na shangwe, na vinanda.

7 Nao wale wanawake wakaitikiana wakicheza, wakasema, Sauli amewaua elfu zake, Na Daudi makumi elfu yake.

8 Basi Sauli akaghadhibika sana, na maneno haya yakamchukiza; akasema, Wamempa Daudi makumi elfu, na mimi wamenipa elfu tu; kuna nini tena awezayo kupata, isipokuwa ni ufalme?

9 Sauli akamwonea Daudi wivu tangu siku ile.
 
Mara hii tu mumeshaanza kuona hayo manyunyu? Na bado.. Mwaka huu mutabaki Ufipa tu wenfine wote hawawataki.
 
Sababu ni hii
1. Hawana hoja

2. Hawana Mgombea mzuri

3. Wametumia miaka 5 kuendesha nchi kwa udhalimu mkubwa sana.

4. Wameharibu maisha ya Watanzania kiuchumi vibaya sana hadi vijana hawana ajira kabisa!!

5. Kwa jinsi Lissu anavyopendwa na kukubalika kiasi ambacho hawana hoja ya kukabiliana nae, sasa kazi kubwa ni kupambana nae kwa nguvu tu!!
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…