Tafakuri kuhusu matokeo ya kidato cha 4 mwaka huu

Tafakuri kuhusu matokeo ya kidato cha 4 mwaka huu

Kulikoni siku hizi kwenye elimu ya nchi hii.?
Ni kwamba sisi zamani tulikuwa na uwezo mdogo wa kiakili ama la?
Au zamani elimu ilikuwa ngumu?
Au watoto wa siku hizi wana akili na uwezo mkubwa kuliko sie?
Au elimu na ufundishaji umekuwa bora sana kiasi kwamba Div. 1.7 zinaweza kutolewa na darasa zima...? Mpaka siku hizi shule za kata ambazo zinakuwaga na ufaulu wa kawaida nao wanatoa 1.7 hata mbili...? Au mitihani ni rahisi zaidi kipindi hiki?

Hii inamaanisha nini..? Sio husda...ila ina inafikirisha mno Div. 1.7 siku hizi zimekuwa kama njugu...VIPI ELIMU NA UPIMAJI ULIKUWA UPI...WA KIPINDI KILE DIV. 1.7 INAWEZEKANA KUWA MOJA TU TANZANIA NZIMA...AU HIVI SASA..?
Kwa Sisi maveteran A ilikuwa inaanzia 81 sasa Kwa Gz inaanzia 75 unategemea nini
 
Ila kiuhalisia...kunapaswa uchunguzi ufanyie...this is not really...no matter what...
 
Hawana maana wale,walishajikatia tamaa,
Nimekaa mahali moja hivi kama wiki (chumbageni) saa tatu ndo wanatoka kufungua maduka sasa hapo ni maali pa kuishi watu kweli, niliswaki saa nne hiyo siku sitosahau
Ahahahha wee bana weee kuna watu wakikusikia hapa jua huu ugomvi utaubeba peke yako mkuu
 
Kulikoni siku hizi kwenye elimu ya nchi hii.?
Ni kwamba sisi zamani tulikuwa na uwezo mdogo wa kiakili ama la?
Au zamani elimu ilikuwa ngumu?
Au watoto wa siku hizi wana akili na uwezo mkubwa kuliko sie?
Au elimu na ufundishaji umekuwa bora sana kiasi kwamba Div. 1.7 zinaweza kutolewa na darasa zima...? Mpaka siku hizi shule za kata ambazo zinakuwaga na ufaulu wa kawaida nao wanatoa 1.7 hata mbili...? Au mitihani ni rahisi zaidi kipindi hiki?

Hii inamaanisha nini..? Sio husda...ila ina inafikirisha mno Div. 1.7 siku hizi zimekuwa kama njugu...VIPI ELIMU NA UPIMAJI ULIKUWA UPI...WA KIPINDI KILE DIV. 1.7 INAWEZEKANA KUWA MOJA TU TANZANIA NZIMA...AU HIVI SASA..?
Watu wanapambana.... Tembelea hizo shule ukajionee.
Elimu ni uwekezaji.. Hakuna Cha Bure.

LIKUD
😂😂
 
Goli limetanuliwa ili mwenye uwezo wa kawaida, (ambao wengi ni shule "zetu") wa kupiga shuti afunge, sasa wale wenye uwezo mkubwa wa kupiga mashuti wanafunga wote
 
Nashukuru Mungu Binti yangu kapiga three masomo yote kapata c kasoro math na physics kachana mkeka nimechukia lkn hamna namna
 
Tutazunguka koooote mara materials za kusomea zinapatikana, mara madogo wanasoma sana nk, ila uhalisia elimu sasa imechakachuliwa sana hasa kwakuwa nchi hii hata masuala nyeti ccm wamechagua kuyaendesha kisiasa.

Hao watoto wanafaulu sana ila vyuoni uwezo wao ni mdogo ajabu kiasi mtu unashangaa ukisikia wengi wao wana div 1!

Bahati mbaya vyuoni nako tangu mwaka juzi AI imeingia, yaani ndio imekuja kupigilia msumari wa mwisho kwenye jeneza. Ikitolewa assignment wachache sana wataumiza vichwa vyao, zaidi ya 90% wata copy swali kama lilivyo na kulitupia kwenye ChatGPT ambayo itatiririka majibu yote na reference za kubuni, wao ni ku copy na ku paste kisha mbio steshenari. Usipotafutwa mwarobaini wa kuidhibiti basi kuna hatari ya watu kuingia vyuoni na kutoka kama walivyoingia.
 
Back
Top Bottom