Tafakuri ya FaizaFoxy 7: Shule za kusomea ujinga. Tanzania na propaganda za Udini Shuleni

Tafakuri ya FaizaFoxy 7: Shule za kusomea ujinga. Tanzania na propaganda za Udini Shuleni

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]... Toa maelezo maada inahusu nini ?? Siwez kuangalia documentary ya dk 47 kama bado huja ni inspire...

Enewei... Kwa hyo unasema waarabu wanaonewa hawajafanya biashara ya utumwa... Ila wanawachafua...[emoji23][emoji23][emoji23]

Endelea kukaririshwa tu ewe mfuasi wa paulo. Hapo najua umeshaisikiliza hadi mwisho na kuielewa, ila unataka kuanzisha ligi,,,umeshaona ukweli kuwa waarabu walikuja Afrika kibiashara na sio kwa nia mbaya kama wazungu na baadhi ya waafrika.
 
Kasome histori ya Dunia wewe Acha kubebwa kirahisi.
Hata kibiblia HAO waarabu walifanya hiyo biashara ushahidi upo
Ha

Ushahidi gani huo,,au ndio unataka kutuletea mliyokaririshwa na kanisa?😁 bado mko usingizini, wazungu waliwateka akili 😁 nanyi mkatekeka kirahisi bila kufanya research.
 
Ushahidi gani huo,,au ndio unataka kutuletea mliyokaririshwa na kanisa?😁 bado mko usingizini, wazungu waliwateka akili 😁 nanyi mkatekeka kirahisi bila kufanya research.

Unaumwa kweli!
So hivyo HAO waliposema hayo Kwa video wamenifunzia misikitini au walifundishwa na masheikhe?

Tofautisha elimu ya kidini na elimu ya kidunia.
 
Usituhusishe na magaidi we bibi,.. Kawaida ya wajinga huwaona wenzao ndio wajinga,.. Waarabu ni wahuni tu, tuache.
 
Labda huwaelewi tu, hao waliokudanganya kuwa Yesu mzungu unasema sio wanafiki, hao waliokudanganya kuwa fanya dhambi tu Yesu kishakubebea dhambi zako unasema siyo wanafiki. Hakika mmejazwa ujinga na mnauendeleza.

Tumia kichwa chako kufikiri japo kiduchu kabla hujatapika humu, maana uliyoyaandika ni mata

Ndio maana na wewe unamtete kipenzi chako mzungu kwa kuwa ni mkiristoo?
Wapi nimemtetea mzungu? Ushaskia nasema mzungu hajahusika kwenye biashara ya utumwa?
 
Wapi nimemtetea mzungu? Ushaskia nasema mzungu hajahusika kwenye biashara ya utumwa?
Umeitazama video clip? Video clip haiongelei nani kafanya biashara ya utumwa na nani hajafanya. Simply inaonesha watu kusomeshwa ujinga kwa makusudi kabisa. Nakushauri kaitazame video clip kabla hujaleta porojo zako binafsi.
 
Waislam kwanini tunatumia nguvu nyingi kutetea waarabu, iwe waarabu walifanya huku kwetu hiyo biashara ama hawakufanya, haimaanishi waarabu hawajafanya biashara ya utumwa, UARABU sio UISLAM, sio kila mwarabu ni mtu safi, mtume Muhammad s.a.w alipelekwa kwa waarabu sababu waarabu walikuwa wamekithiri kwa ushenzi, wapo waliomkubali wakaacha ushenzi na wapo walioendelea na ushenzi wao, walimkata mjumbe wa Mwenyezi Mungu, sasa isiwe kila muarabu akaonekana ni mtu saint saana, ni washenzi ndio maana mitume kadhaa ilishushwa huko kwao, BILALI(r.a) alikuwa ni mtumwa.

Dini tusizifate kwa mihemko. Utumwa ulikuwepo duniani koote, si ulaya, si uarabuni hadi uchina huko.
 
Kwa uandishi wako humu jamvini wewe kikongwe unaona una-suffer depression, una stress sana wew mfia dini ya mfu mudi
"depression" yangu mimi wewe unae "suffer".Majanga hayo.

Huyo "mudi" wako mimi simfahamu, mimi nafata dini ya Mitume wote na Yesu akiwemo, Uislam.

Sasa rudi kwenye mada, umeitazama video iliyopo post namba 1? Maana hiyo ndiyo iliyobeba mada, au mada hapa kwa ufinyu wako unadhani ni mimi?
 
Hiyo video nimeitazama mwanzo mwisho.

Msimamo wa huyo Profesa na huyo mwandishi anayemhoji ni mmoja na unamaudhui ya kupinga kuwa Ati waarabu hawakuhusika kusafirisha Watumwa kutoka bara kwenda Pwani.

Alafu kuna wakati wanajichanganya tena Kwa kusema Kama walifanya basi ni kidogo😄😄😄

Sasa watupe hoja zao Waarabu waliopo Tabora, Kilosa Hilo Morogoro, kigoma na vizalia vyao walitokana na nini.
Maana miaka hiyo Maeneo hayo yalikuwa sio Mimi labda huko ujiji Kigoma.

Kusema Waarabu walihusika kwenye biashara za kuuza Watumwa wakiwanunua Kwa Waswahili huko barani kisha kuwasafirisha haimaanishi tuna chuki nao bali ndio Biashara kubwa ya kipindi Hilo

Mwambie huyo Profesa akasome tena kisa cha Waishimael waliokuwa wakinunua Watumwa wakiwauza Maeneo mbalimbali ikiwemo Misri, mhanga wa Jambo Hilo hata wewe unamjua anaitwa Yusuph, si unamjua?

Unawatetea Waarabu Kwa kisingizio cha udini🤣🤣 Bibi Acha hizo bhana.

Mbona Wakristo hawawatetei Wazungu kwenye mabaya Yao ya ukoloni na mambo mwingine?

Wewe ndio umesomea ujinga Kwa kuukataa ukweli.

Huyo Profesa anasema ati HAO Watumwa waende Uarabuni kufanya nini?😄 Ameacha kujadili Kama msomi na mtaalamu anajadili kishabiki Kama wahuni wa vijiweni.

Yeye anachojua kuwa Watumwa kazi zao ni ngumu tuu, za kwenda shambani na migodini au viwandani🤣🤣

Hajaelezea maelfu Kwa maelfu ya Watumwa waliokuwa wanaenda huko uarabuni kugeuzwa Watumwa wa kazi za ndani na kuhasiwa, huitwa matowashi,😄😄

Hii mpaka Leo wapo maelfu Kwa maelfu ya wanawake na mabinti hupelekwa huko uarabuni na kuna AGENCY mamia Kwa kazi hizo.
Lakini hakuna mambo Kama hayo barani Ulaya.🤣🤣

Anazungumzia Nchi za Carribbean, sijui Brazil, Mexico na Agentina kuwa na wingi wa Waafrika akiichukulia Kama utetezi wa hoja yake kuhusu biashara za UTUMWA zilifanywa zaidi na Wazungu.

Kwenye biashara anashindwa kuelewa kuwa kuna muuzaji na mnunuaji😄😄
Wauzaji wa Watumwa walikuwa ni Waarabu na kidogo Waswahili, wanunuzi walikuwa Wazungu Kwa jamii zao.
Sasa utasema Kati ya muuzaji na mnunuzi Nani anafanya biashara.

Hivi wewe ukienda Kwa Mmasak au Mgogo kununua NG'OMBE, Kati ya wewe na muuzaji Nani anafanya biashara ya NG'OMBE?😄😄

Profesa wako mwambie aache kujadili mambo Kihuni badala Yale ajadili kitaalamu.

Yeye kaamua kuchambua kimrengo wa Kusini, tangu wanaanza kusalimiana tayari ilishaonekana wangejadili kitu gani.

Mjadala Kama huo wangetafuta mtaalamu mwingine hapo hapo ili a- criticise sio watu wajadili katika mrengo mmoja alafu wewe unahitimisha kama mjinga.
Wacha uongo. Hakuna mahala profesa kainga kuwa biashara ya utumwa haikufanyika. Maudhui ni mapicha tu. Umeyaona hayo mapicha yaliyobeba maudhui? Aliyachora Profesa yale?


Utaupingaje Utumwa wakati hata kwenye Biblia upo? Na ardhi yetu hii imetajwa katika maandiko hata kabla ya Biblia na dola lililotaja kwenye maandiko yake kuwa lilifanya biashara na ukanda huu miaka elfu 20 iliyopita. Ushahidi upo wazi kabisa kwenye "hieroglyphics" za mafarao.

Katazame tena maudhui, umekuja na porojo ndefu iliyo nje kabisa ya mada. Usitake kujaza watu ujinga uliojazwa nao wewe.
 
Umeitazama video clip? Video clip haiongelei nani kafanya biashara ya utumwa na nani hajafanya. Simply inaonesha watu kusomeshwa ujinga kwa makusudi kabisa. Nakushauri kaitazame video clip kabla hujaleta porojo zako binafsi.
Ujinga Gani Huo wanasomeshwa?
 
Hawa wanazuoni wako na vitabu vyao nimeanza kuwafuatilia zaidi ya miaka saba iliyopita. Kama wewe ndiyo umeanza kuwasikia sasa endelea kujifunza ujinga wao.
Hiimada si mara moja binafsi kuiibua humu JF, miaka kadhaa iliyopita niliibua kwenye uzi wa maandiko tu. Leo nimeileta video.

Umeitazama video? Ni nini ulichokiona humo? Au wewe ni katika waliojazwa ujinga na unataka kuundeleza huo ujinga?
 
Back
Top Bottom