Tafsiri ya picha katika ulimwengu wa kiroho

Tafsiri ya picha katika ulimwengu wa kiroho

Hayo tu ni maoni ya kisaikolojia, watu wanafanya maendeleo, muda ukipata maisha yanabadilika, classmate wangu primary wameo au kuolewa, tulipiga picha ya pamoja. Haimaanishi wameoa Kama mimi coz tulipiga picha pamoja. Niliosoma nap chuo tulipiga picha ya pamoja. Ni wahasabu kampuni mbali mbali, haimaniishi ni wahasaibu coz ya picha. Please Mshana unateka watu wenye uwelewa mdogo. Anzisha dini utakuwa na wafuasi wengi sana.
Naelewa zaidi kuliko wewe lakini haimaanishi kuwa nakudharau. Kwakuwa umetumia muda akili na mb zako kupost kile unachokijua...asante kwa ushauri ila sina mpango wa kufanya hivyo, pesa sio kipaumbele kwangu.
 
Lakin zaid mim huwa najkuta nakaa upande ule ule siku zote
 
1473272978064.jpg
 
Habari mkuu mshana jr shukrani sana kwa mada yako. Siku ya kwanza nilipoona uzi wako huu, sikuamini kwa asilimia 100% kile ulichokuwa umeandika. Lakini ilipofika mwezi wa tisa, nilirudi nyumbani, na baada ya kuchukua albamu, niliangalia picha za utotoni (ndizo pekee nilizonazo). Nilipoangalia picha ya mahafali ya darasa la saba, mimi peke yangu katika picha, ndiye niliyekuwa nimevaa shati tofauti na wengine. Niliporudisha kumbukumbu, nikakumuka, tulikuwa tumepanga kununua kitenge flani, siku ya kununua kitenge hicho, wenzangu walikwenda bila kunishirikisha. Walirudi na kunionyesha kitenge walichonunua, na nilipojitahidi kutafuta, nilitafuta hadi nikachoka na wakanishauri nitafute angalau kinachokaribiana rangi. Kifupi, nina mfumo tofauti na hao wote wa uingizaji wa hela. Wao wote wameaajiriwa serikalini, kasoro mimi.
 
Kweli lugha ya picha ni jambo la ajabu sana..hii tabia ya kusoma picha ninayo tangu mdogo.napenda kushika album na kuwacheki watu na mikao yangu na kutafakari mbele na nyuma..

Asante mshana jr
 
Mkuu unaufahamu usio wa kawaida... akili ndogo mara nyingi huwa hazikuelewi na kuishia kudhani unazungumzia uchawi.

Picha chini inaonesha marais wote wa Kenya, Jomo Kenyatta, Daniel arap Moi, Mwai Kibaki na Uhuru Kenyatta

117881_01_n_20130322150940.jpg
Naanza kumwelewa elewa mshana jr
 
Mshana Jr,

Asante Mshana kwa elimu ya rohoni ambayo umekuwa ikiitoa kila mara ila kuongeza fikra za mwanadamu na kumpa nafasi ya kuushiriki uumbaji wa MUNGU.

Tunajua kwa msingi wa uumbaji vitu vyote vimeumbwa na MUNGU, na elimu yote imeachiliwa na MUNGU, lakini pia ameachilia picha na taswira ya vitu mbalimbali ambavyo binadamu kwa kutumia nguvu ya fikra anaweza kuvileta kwenye uhalisia na uwepo kwenye ulimwengu wa mwili. mf uwepo wa ndege, nuklia,elements, magari nk ni nguvu ya fikra za watu.

Lakini pia tunajua kuwa sio vitu vyote vinakuja na nguvu za MUNGU kwani shetani naye ananguvu za kuleta vitu vyake ilikuimarisha utajiri wake na fahari yake, wote wawili wakitumia nguvu ya fikra ya mwanadamu. Nakama ulivyogusia kwenye nguvu ya kumeditati ambayo ndiyo chakula kikuu cha fikra, napenda kimsingi kabisa unisaidie je hiyo meditation uliyoitaja inahusianaje na ile ya MUNGU kwenye agano la kale wakati Mungu ana mwambia Joshua kitabu hiki cha torati kisitoke kinywani mwako, utafakari maneno yake usiku na mchana?

Je, unahisi kila unacho mediated kwa njia zilizotajwa hapo juu na wachangiaji kinakuongoza kumfunua MUNGU?, na kuna njia ambayo mcha Mungu anaweza kuitumia ili kurahisisha meditation yake kwenye maneno ya MUNGU na asije akawa anatoa sadaka kwa adui?

Nakushukuru tena kwa mchango mkubwa wa kuweka elimu hizi wazi, nawasihi watu wasiogope, uwe wa dini yoyote ile, pata maarifa changanya na za kwako, weka kwenye vipimo vya upande wa kule unakoamini na vipimo vinakubaliana songa mbele. Kumbuka awazavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo, watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa: hivyo tafuta sana maarifa ili ufanikiwe, kwa maana watu walioupande wa shetani wa maarifa sanaa, lakini watu wanao mtafuta MUNGU wavivu sana kutafuta maarifa kwa dhana ya uoga tuu na kudanganywaa.
 
Back
Top Bottom