Taifa liache unafiki. Hivi uovu wa Gekul unafikia hata robo ya ule wa Makonda?

Anza kuandaa ya makonda mkuu utasikilizwa
 
Alipovamia kituo cha habari cha Clouds nayo ni minong'ono tu??
 
Ina ushahidi wa katibu wa mbunge kumzuia mwandishi wa habari asitoke ofisini kwa mbunge ambacho ni sawa na kitendo cha utekaji.
 
Tatizo ni kwamba hayo ya Makonda mnazusha tuu bila Ushahidi. Mmesha ombwa mara nyingi tu, pelekeni Ushahidi! Hamna

Dogo kapeleka ushahidi, Gekul ameliwa kichwa!

Mtabakia hivyo hivyo, kulalama, kutuhumu, kukashifu na mwisho wake mnarudi usingizini kuanza tena ndoto za Kashfa mpya.

Mjitathmini, propaganda yenu ni kalas! Nyie ndio muache Unafiki
 
Ushahidi wa uovu wa Makonda uko wazi, labda useme lini Kinga yake ya kutoshitakiwa itaisha.
Wewe mbona unaandika kwa jina la bandia na kwa kificho?!,jitokeze ili uwe shahidi kwenye hizo kesi.kila siku wewe ni mtu wa kusema watu,na kutuhumu watu bira hata kuwa na ushahidi.

Wewe kwenye hii nchi watu wazuri na waadirifu ni chadema tu,wengine woote ni mashetani. Wewe sina shaka,una matatizo kisaikolojia.
 
Bila Makonda kukamatwa na kufikishwa mahakamani, yote yanayofanyika kuhusu haki, ni unafiki mtupu.

Nchi hii ni kama kuna watu wamepewa vibali vya kufanya uovu wa kila aina, hata kuua, kuteka watu na kupora mali za watu kwa namna watakayo. Halafu wapo watu wakifanya uovu hata mdogo sana, kwa unafiki mkubwa, wanachukuliwa hatua ili ionekane watawala wanachukia uovu, wakati kiuhaliasia wanapalilia uovu.

Makonda kuna ushahidi wa kila aina, mpaka Serikali ya Marekani ikaweka wazi kuwa mtu huyu anadhulumu haki ya watu kusihi (anaua), mpaka ikampiga marufuku kukanyaga kwenye nchi yao, halafu wajinga, punguani na wanafiki wakubwa utawasikia, eti kama mna ushahidi, mmpeleke mahakamani!! Punguani wakubwa nyie. Tangu lini mwovu wa makosa ya jinai anapelekwa mahakamani na raia? Hiyo ni kazi ya polisi. Katiba yetu imetoa mamlaka hayo kwa DPP pekee yake. Wananchi wengine wote uwezo wao kwenye makosa ya jinai, unaishia kuwa mashahidi lakini siyo kufungua kesi.
 
Makonda aliyafanya enzi zile, kwa sasa amewekwa tu kwa sababu maalumu
 
Africa Kusini baada ya kuunda tume ya maridhiano Kila uovi uliwekwa wazi, na watu wakaomba msamaha, kisha wakafungua ukurasa mpya. Hapa unataka nitoe ushahidi kwa vyombo vilivyoshiriki kufanikisha ukatali wa Makonda! Ukitaka kuona ushahidi wa mchana kweupe, kuwe na taasisi huru hasa toka nje ya nchi kisha uje uchukue mrejesho.
 
Tiss si wanakinga ya kutokushitakiwa wanapo tekeleza majukumu yao au unajisaulisha na huyo gekule si alikuwa bungeni acha watafunane wenyewe.
 
Kuvamia Clouds Fm ni minong'ono ya mitandaoni?

Alienda mwenyewe kuvamia akiwa na askari wenye silaha.

Unajua kosa la uvamizi wa kutumia silaha kifungo chake ni miaka mingapi?

Ndiyo maana watu wakasema sahizi angekuwa anaozea jela.
 
Tiambie kama alikutoa marinda tukutafutie wakili
 
mihemko na ghadhabu inashusha uzito wa hoja yako
 
Hatuna rais bali mama mswahili wa kizanzibari na Uswahili mwingi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…