Taifa limekuwa la kamari. Kila kona kila mahali kamari. Watu wanaibiwa pesa zao

Kamari ni starehe, kama ilivyo ngono, ulevi.. napendekeza serkali iongeze kodi zaidi kwenye kamari!
 
Walio kuwa wanauza viroba walikuwa wakwepa kodi? Mbona vilipigwa ban??
Kutetea upumbavu kz sana
 
Asante sana kwa thread hii. Ni swala ambalo hata mimi limekuwa linanikera sana. Kamari hulewesha watu kudhani kuwa kuna siku watatusua, na kuishia kumalizia hela yote kwenye Kamari kila siku badala ya kufikiria shughuli nyingine za kujipatia maendeleo. Inabidi Serikali iweke utaratibu wa kudhibiti mchezo wa kamari kwenye jamii, yaani kuwe na sehemu maalumu za kuchezea kamari kama kwenye casinos, na kuwe na kampuni chache tu za kamari. Siyo huu utititli wa kamari ulionenea nchi nzima kila pembe.
 
Umeongea vema ila hapo kwa Magu,utapeli na kubet viliongezeka zaidi enzi zake.Tukashuhudia sms za Tuma ile pesa kwenye namba000000 jina abcde kila siku na huku line zote zikiwa zimesajiliwa kwa alama za vidole.Tujenge hoja bila kufanya reference kwa wasiohusika.
 
Kamari iliwahi kuzuiwa lini na mwaka gani?

wacha watu wabeti kwani wewe inakuuma nini?
 
Ni wale wale wanaotaka kutuaminisha Kwamba Awamu ya Mama sio nzuri
 
Zimesahiriwa zingin Wasafi Bet na Bet Power🤣🤣
 
Inasikitisha kamali inapewa kipaumbe sana na watu kufanya kama Kazi na starehe ,tunapoeleka pabaya zaidi kama hali hii itashamiri zaidi.
Ni mbinu ya ccm kuendelea kutawala.

Sasa utaona kama wataipiga marufuku ng'oo.

Watakataza mikusanyiko ya kuelimishana kuhusu elimu ya Uraia, katiba, siasa na uchumi lakini wanaruhusu mikusanyiko ya Fiesta, Mpira, Starehe, michezo, Kamari, hadi ya mashoga.
 
Matangazo ya kamari yalirudi kipindi cha jiwe hichohicho..
 
Mi hata sijawahi kujaribu.
 
"Nakumbuka hayati Magufuli alizuia hizi kamari baada ya kuombwa na viongozi wa dini, ikawa banned kufanyika hadharani namna hii. Hivi sasa yoote imerudi ."

Wafuasi wa huyu jamaa sijui nilini mtaacha kutudanganya
Mkuu sina mambo ya ufuasi..hii ni kweli kabisa.
 
Mbona hamsemi watu wanavyopoteza fedha na nguvu kukimbiza moto unaoitwa mwenge?
 
Watu tunatusua mamilioni kwa mia (100) tu, endelea kuwa na akili zilizodumaa hivyohivyo. KILA JAMBO AFANYALO BINADAMU CHINI YA JUA NI BAHATI NASIBU TU.
 
Ndo nimefungua vimachine vyangu kadhaa hebu subiri nirudishe pesa yangu halafu tuendelee na huu mjadala
 
Ukifika ofisini za KAMALI, Utashangaa jinsi Vijana walivyojazana huku wameshika vikaratasi mkononi..yaani [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24] ki ukweli sishangai kuona panya road kwa hali tuliyofikia.
 
Niligombana na mwanangu inauma sana alikuwa mbele kidogo coz alishawai kula kama million 20 na kitu ila alinunua kiwanja zilizobaki kauza jamaa amekuwa addicted kushinda ndani mpaka kakonda hajali mahusiano yeye ni betting tu still ana Imani atafika mbali ila kifupo kazi hana maisha magumu kauza baadhi ya assets karudi chumba kimoja roho yake ipo kweny kiwanja anaweza kukilipua mda wowote
 
Umeongea kwa uchungu wa mtu mwenye uzoefu ... Ni vyema sana kuokoa vijana thanks
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…