Hivyo ndivyo ilivyo kwa taifa lolote ambalo litatoa uhai wa kiongozi wake ambaye anakuwa madarakani ili kulinda na kutetea mali za umma na maslahi ya taifa lake.
Angalia laana iliyoikumba Congo Drc mpaka leo laana hiyo inawaandama. Baada ya kumuua Lumumba, Mobutu na genge lake waligeuka mafidadi na walafi wa kutafuna mali za umma. Taifa lao pamoja na utajiri wa mali asili lakini lina umaskini mkubwa. Vita vya wenyewe kwa wenyewe visivyokwisha na matatizo lukuki.
Hui ni mfano tu wa namna damu ya kiongozi wa taifa ambaye ni mzalendo anapouwawa na kisha laana kulikumba taifa.
Watanzania tujitafakari sana.
Nyankurungu2020;
Unaandika kwa sababu ya kuandika tu siyo? Unatazama mambo kwa darubini dhaifu sana...
Soma historia ya dunia tangu kuumbwa kwake na tawala mbalimbali utaelewa jinsi Mungu ambavyo huwa anashughulika na viongozi wakatili na watesaji wa wananchi wao...
Kabla, watu walikuwa wanaongozwa na Mungu moja kwa moja kupitia kwa wajumbe wake maalumu...
Baadaye binadamu waliukataa uongozi wa Mungu. Waliandamana, waka - protest na kumlazimisha Mungu awape viongozi na watawala wa kibinadamu...
Mungu akawaonya ubaya wa kuongozwa na binadamu. Lakini wao hawakuelewa. Mungu akawapa walichokitaka...
Mtawala wa kibinadamu wa kwanza duniani aliitwa MFALME SAUL...
Alikuwa mtawala mwenye kuburi, katili aliyetesa wanadamu wenzake....
Mungu hakumruhusu kuendelea kutesa na kuumiza watu wake. Aliruhusu kifo kimwondoe....
Kutoka hapo kukawa na mlolongo wa wafalme. Kuna waliotawala miezi mitatu, mwaka, miaka 2, 6, 10 nk..
Kanuni ya Mungu ni moja tu. Ukianza kuumiza na kuonea watu wake, ni lazima atakuondoa kwenye "kiti chake" kwa namna yoyote anayoona yeye inafaa...
Hakuna laana kwenye hili. Dhana ya "laana" iko ndani yako na unaisema wewe. Kila kiongozi wa taifa lolote huruhusiwa kutawala kwa muda fulani ili atimize kusudi fulani...
Magufuli wa Tanzania alikuja kutekeleza kusudi fulani. Amelitimiza. Ameondolewa. Hakuna laana kwa yeyote. Kama ni laana amekufa nayo yeye, ni ya kwake...