Taifa Stars waenda Cape Verde bila Dreamliner

Wakati wanatoa taarifa ya kusafiri na hiyo ndege yetu pendwa walikuwa hawajui kama inaweza kutua kwenye huo uwanja?
Huo uwanja unatua ndege nyingi kubwa tu.

Mwakyembe ameogopa kusema kuwa hili dege la kibisa ni hasara tupu kulipeleka huko imebidi atunge story za kipuuzi.
 
Taratibu mkuu, uchochezi huu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mimi bado naona mauzauza tu. Ratiba ya mechi inajulikana. Waziri anatangazia Taifa na wapenzi wa soka kuwa kuna usafiri wa ndege ya serikali (dreamliner). Kila anayehtaji kwenda anatakiwa kuchangia "gharama kidogo tu" dola 1500 - 2000. Siku ya safari wameshajitokeza watu 262 wa kujaza Dreamliner, ghafla inagundulika uwanja wa ndege kumbe ni mdooooogo!! Unafaa kutua helkopta na ndege ndogondogo tu. Binafsi nachanganyikiwa sijui abiria zaidi ya 200 waliotoa nauli zao tutawaambia nini? Tingewaambia mapema watangulie na boti za Azam wangeshafika masikini!! Hata hivyo hakijaharibika kitu, kama uwanja ni Mdogo na tumeahindwa kuonesha "Fahari" yetu basi kesho ile meli yetu tuliyohifadhi jeshini kama silaha ya akiba (Mv Dar es salaam) ianze safari Mara moja. Hatuahiiiindwiii!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…