Taja mwiko, mila au desturi za kabila lenu au mahali ulipokulia

Huo ukanda wa ntimaru,nyamagongwi,kwiribha na kuelekea vilima vya maeta jirani na MTO tebesi kuna upuuzi mwingi sana.
 
Ni kw
Huo ukanda wa ntimaru,nyamagongwi,kwiribha na kuelekea vilima vya maeta jirani na MTO tebesi kuna upuuzi mwingi sana.
Ni kweli mahali pale pana UNYAMA mwingi sana. Lakini ule ndio mzuri kwa kuwa unachangamsha akili
 

Hiyo ya kumpiga mzazi huwa ni vizazi vinne viishe ndipo nayo hukoma!

Ni mwiko mgeni kula firigisi ugenini kwa mkurya
 
Hiyo ya kumpiga mzazi huwa ni vizazi vinne viishe ndipo nayo hukoma!

Ni mwiko mgeni kula firigisi ugenini kwa mkurya
Hii dhambi nimeishuhudia pale kijijini kwetu hiki ni kizazi cha 3 sasa bado hali hii inaendelea kujirudia. Wazazi wanapigwa hatari!
 
1. Mwiko wa Ugali ukivunjika wakati Ugali unasongwa. Mwanaume haruhusiwi kula huo Ugali (labda asongewe mwingine).

2. Ni marufuku kumuachia sahani Mkubwa wako mkiwa mnakula pamoja hata kama umeshiba kabla yake.

3. Hutakiwi kutaja neno Chumvi wakati wa usiku (Badala yake sema Dawa ya Mboga) [emoji23]

4. Mkiwa meza moja ni marufuku kuanza kula kabla ya wakubwa zako. Wataanza wao kushika kijiko na kula ndio utafuata wewe.

5. Kiganja cha mkono wa Kushoto kikikuwasha, ni dalili za kupokea hela hiyo siku. Cha mkono wa Kulia kikikuwasha, ni dalili za kutoa/kupoteza hela.

6. Ikitokea umejikwaa mlangoni wakati wa kutoka nje halafu kuna safari ulikua umepanga hiyo siku, unatakiwa uhairishe kwenda mara moja. Haitakua salama kwako.

7. Ndege akikunyea ni ishara ya Bahati nzuri.

8. Ukipaliwa ghafla wakati wa kula basi jua kuna mtu anakusema vibaya muda huo huo unaokula.

9. Jicho la kushoto likikucheza ni machale. Kwahiyo kama kuna magendo unafanya mahali/ au upo mahali ambapo hutakiwi kuwepo basi ondoka haraka sana utakamatwa!

10. Mtu mzima akianguka bafuni ni ishara mbaya sana. (Wanasema hana muda mrefu wa kuishi).

11. Ni marufuku kumpiga mtoto mdogo wa Kiume kwa nguo. Atakosa Mke [emoji23]
 
Kuku jike akiwika lazima achinjwe maana anatabiri mabaya. You can imagine demu anaejikuta tom boy atafanywa nini akiingia kijijini kwetu
 
Sahihi, nyingi ni mila za kijima tu
 
Asante kwa nyongeza mkuu. Pia:

1. Udongo ukikuingia mdomoni wakati unalima shambani ni ishara njema kuwa utakula nyama siku hiyo.

2. Mkishambuliwa na siafu wakati mkiwa mnapanga njama za kwenda kuiba, ahirisha huo mpango wenu kwani inaashiria hamtarudi salama.

Siku moja vijana walishambuliwa na siafu kabla ya kwenda kuiba. Walipoenda, mmoja wao aliuawa huko huko. Na alikuwa amechaguliwa kwenda sekondari. Hadithi yake iliishia hapo hapo.
 
Na Mimi huwa nakerwa sana na hiyo tabia. Tena, wakati mwingine, unakuta anayefanya hivyo ni mtu anayehesabiwa kama mmoja wa "waheshimiwa".

Hiyo ni sambamba na tabia ya kupenga kamasi kwa kubinya pua bila kuwa na leso. Nilikuwa nafikiri ni watu wasiosoma tu ndiyo wenye hiyo tabia. Nimeshangaa hivi majuzi kumshuhudia Engineer mmoja naye akipenga kamasi kwa staili hiyo.

Huwa nakereka sana.
 
Sikupingi ila nakuliza tu....hivi umesha wahi patwa na mafua makali kitambaa kimoja kikawa hakitoshi ..... tena uwe maeneo ya arusha au njombe kwnye baridi
 
Sikupingi ila nakuliza tu....hivi umesha wahi patwa na mafua makali kitambaa kimoja kikawa hakitoshi ..... tena uwe maeneo ya arusha au njombe kwnye baridi
Arusha ndiko nilikozaliwa na kukukulia. Na kuna nyakati ambazo ni kama misimu ya mafua huko, hasa nyakati za baridi. Lakini tokea nilipoanza kutumia leso, nafikiri ilikuwa darasa la kwanza au la pili, sikumbuki kama nilishawahi kukosa leso ya kupengea kamasi. Nilipokuwa sina hela ya kununulia ya dukani, nilikuwa nikijitengenezea kwa kutumia nguo zilizochakaa. Na wakati nilipokuwa na mafua, kikishachafuka, nilikuwa nikiifua na kuilazimisha kukauka haraka. Ilikuwa nikiishaifua, naikamua na kisha kuifungia kisogoni ili ikaushwe na joto la mwili. Kwa hiyo muda mfupi tu baada ya kufuliwa inakuwa tayari kwa matumizi.
 
Ukichepuka na Mke wa nduguyo, na ikatokea huyo nduguyo akafariki hata ipite miaka 30 wewe na huyo Shemejiyo hamtashiriki kwenye mazishi mpaka mkaonane na Wazee wa mila wawagange,mkikiuka mtazikwa watatu.
 
Kwetu vitu 7 ni mwiko. Mtu akikuomba au ukiamua kumpa au kumzawadia mtu vitu vinavyohesabika (mfano vipande vya nyama, viazi, mahindi ya kuchoma, machungwa, mapera, pipi, nk ilmradi tu vinahesabika), hakikisha ni chini au zaidi ya 7. Unatakiwa uwe makini.....hakikisha unavihesabu. Ukijichanhanya usihesabu, aliyezawadiwa akivihesabu na kukuta viko 7, unalo. Atavitupa vyote na lawama zitakurudia wewe uliyetoa. Kumpa mtu vitu saba, ni zaidi ya UCHAWI.....mtu huyo hatakuja kupokea kitu au zawadi yoyote kutoka kwako kwa kuwa inaonekana humtakii mema. Tangu utotoni tumekuwa tukikaririshwa kuwa vitu 7 sio vizuri na imepokewa hivyo hadi leo. Chezea miiko ya watu wewe!!πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Hii nafikiri ni ndani ya Morogoro kama nitakuwa sahihi...
Sambamba na yote hapo, pia...
1. Ni mwiko kuingia shamba lenye mahindi baada ya kunyolewa, mpaka siku ya pili.

2. Ni mwiko kuburuza kuni au kamba na kuingia nayo ndani.

3. Ni mwiko kusimama wakati wakubwa wamekaa, au kukaa wakati wakubwa wamesimama.

4. Ni mwiko kukalia kaburi.

5. Ni mwiko kuacha mchi kwenye kinu usiku.

6. Ni mwiko kuua chura, mbayuwayu na vunjachungu.

7. Ni mwiko kukaa au kusimama mlangoni.

8. Ni mwiko kutokea dirishani.

9. Ni mwiko kupima kimo cha MTU kwa kiganja, tumia kiwiko.

10. Tuna majina ya Mizimu ambayo ni mwiko kutamka kwa kujifurahisha au kujiapiza huku unajua unadanganya, YATAKUFIKA TU UTAJUTIA.

11. Ukiwa na njaa njiani, ingia shambani kwa MTU, kata muwa au chimba muhogo ule ila usitoke nao, hata kipande kimoja. Ikiwezekana panda pegu.

12. Usiache nguo usiku nje, ulizofua.

13. Usilipite kaburi la babu au chifu bila kukata jani lolote na kuliweka juu ya kaburi. Hasa kama ni wa ukoo wako.

14. Ni mwiko kutupa chakula, hakikisha unakimaliza au unatafuta MTU.

15. Usimruke mtoto.

16. Usiimbe wala kuongea chooni, au kupiga mluzi.

17. Ni mwiko kumpiga mtoto kwa fagio.

18. Ni mwiko kuchezea chakula, hata kama hutakitupa. Mfano kulirusharusha tonge kisha ule.

19. Ni mwiko kurusha chochote nje kutokea ndani.

20. Ni mwiko kutoka au kuingia ndani ya nyumba kwa kukimbia.

21.....
 
Hatakusumbua, atakusalimia na kukupa pole.

Muhimu ni wewe kuhakikisha umepooza njaa, sio akukute na mzigo ambao unaviashiria vya wizi. Miwa kumi, mihogo mashina 5, nk...

Na ikitokea amekusumbua kwa namna yoyote, unaruhusiwa kumshitaki kwenye mahakama za kimila, kuomba kusafishwa jina lako, maana atakuwa amekutendea kama mwizi.
 
Asante mkuu, umenikumbusha kitu:

1. Ni mwiko kuua ndege aliyeingia ndani au zizini au aliyejenga kwenye nyumba.

2. Ukinawa mikono kisha ukaipukuta kwa kwa kuitikisa, maji hayo hayapaswi kumfikia mtu aliye jirani nawe; ni vibaya. Ikitokea, ili ku reverse huo ubaya unapaswa kuipuliza mikono kwa pumzi yako (kama vile unapuliza moto).

3. Ukigombana, kumpiga au kupigana na mtu halafu mtu huyo akakimbilia nyumba ya jirani kujiokoa, hupaswi kumfuata huko. Ukikaidi ukamfuata huko wenyeji wa nyumba alimokimbilia watakupiga vikali sana kwa kukiuka mwiko huo. Mtu akiomba hifadhi ya namna hiyo, imeisha....ni sawa na kuomba hifadhi kwenye ubalozi (embassy).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…