Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hii tuliifanyia utafiti wakati tupo shule lakini hatukufanikiwa. Hamna relationship kati ya mtoto anayenyonya na sperm za baba.Kwetu mkishazaa hampaswi kusex mpaka mtoto apewe dawa gani sijui au mpaka msubiri aache kunyonya. La sivyo mtamharibu (kiswahili kubemenda). Hiyo ni mwiko nimetamani sana kufuatilia kwenye jamii nyingin3 bado sijapata jibu.
Maneno hayajawahi kuishiwa wa kuyasema.Zinaitwa PhD za ubwete
Kiislam, mwanamke akimaliza "nifas" (post-partum bleeding) anakoga, anajitoharisha anaanza kusali, kufunga na kuingiliana na mumewe., haina muda maalum, isipokuwa wengi huku kwetu huiita na kungoja siku "arubaini".Hii tuliifanyia utafiti wakati tupo shule lakini hatukufanikiwa. Hamna relationship kati ya mtoto anayenyonya na sperm za baba.
Ila kihalisia mtoto kudhoofu kupo. Na ukifatilia kwa nini hutopata jibu.
Hii huwakuta jamii zingine kama waarabu,wazungu,wachina?Hii tuliifanyia utafiti wakati tupo shule lakini hatukufanikiwa. Hamna relationship kati ya mtoto anayenyonya na sperm za baba.
Ila kihalisia mtoto kudhoofu kupo. Na ukifatilia kwa nini hutopata jibu.
Duh naamini nitajifunza mengi kupita huu Uzi, japo fact zenu zngine znatisha kwakweliMakabila yote hapa Afrika au nchi nyingine za Ulaya, Asia na Marekani, wanayo miiko, mila au desturi zilizozoeleka kiasi cha kurithiwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
Hapa Tanzania, kwa mfano, kuna mambo fulani ambayo ni mwiko kufanyika katika jamii na ikitokea mmoja wa wanajamii akaenda kinyume na mwiko huo anaweza kupata balaa au kuwasababishia wanajamii wengine balaa.
Baadhi ya mambo/matendo hayo ni kama ifuatavyo:
1. Jogoo akiwika usiku kabla ya mapambazuko huchukuliwa kuwa ni laana ama uchuro. Adhabu yake ni kuchinjwa na kufanywa kitoweo.
2. Bundi akilia usiku karibu na maskani ni balaa. Ili kuepukana na hiyo balaa, unatakiwa kuamka ukoke moto na kuchoma punje za mtama kwenye moto huo hadi punje hizo zilipuke.
3. Kwa kabila letu, hairuhusiwi mtu kutupa tula (Sodom apple) kumvuka msichana au mvulana ambaye bado yupo jandoni. Kufanya hivyo kunaweza kusababisha kifo au kuleta balaa kwa mhusika.
4. Ukiwa unapita porini na kukuta uyoga (edible mushroom) usiuache hapo ulipo. Hata kama huutaki au hujisikii kuula, ungo’e na kuuweka sehemu iliyoinuka ili mtu mwingine anayeuhitaji akipita auchukue akale. Kuuacha bila kuung’oa inaweza kukusababishia matatizo au mikosi.
5. Maisha ya kijijini ni ya kijamaa na watu huishi kwa kusaidiana. Kuna wakati unaweza kukosa unga ukaenda kuomba kwa jirani. Hata kama huyo jirani uliyemuendea naye hana unga wa kukugawiwa, chombo ulichoenda nacho hakirudi bure. Angalau akuwekee unga kisoda kimoja kwenye chombo hicho ili kisirudi tupu. Ni mwiko chombo hicho kurudi tupu.
6. Ukitembelewa na mgeni ambaye hajakutembelea baada ya muda mrefu hata kama huna chakula mmegee ukoko kutoka kwenye sufuria atafune au hata fundo la maji anywe. Ni mwiko mgeni huyo kuondoka kwako bila kula chochote.
Hii ni baadhi ya miiko ninayoweza kukumbuka kwa haraka haraka. Nitaongezea mingine wasaa mwingine. Je, wewe kwenye kabila lako au mahali ulipokulia, ni miiko gani umewahi kuishuhudia na mpaka inaheshimiwa? Tupia mmoja hapa tujifunze kitu.
Nawasilisha.
Huko nilipotokea ni marufuku mwanamke aliyeolewa kulala na chupi isipokuwa tu kipindi akiwa mwezini1. Kwetu ni mwiko kufagia jioni jua linapozama.
2. Vile vile kupiga mswaki baada ya saa sita ni mwiko.
3. Masharti ni mengi mno.
Duh! Aisee 🤔Kijijini kwetu kama ww mgeni ikifika saa mbili ucku huruhusiwi kutoka nje ukitoka imekula kwako.
Asanten San🙏
Daah kuna watu involuntarily ndio udhaifu wao huo na inatokea arbitrarily- kujichokonowa pua mbele za watu. Ni tabia ambayo kwetu haijwahi kukubalika kuanzia kwa watoto wadogo mpaka watu wazima. Kwetu Pwani.
Imefikia mpaka mimi siikubali kabisa na nashindwa kujizuwia mtu akijichokonowa mbele yangu, nampa wazi, nendachooni jichokonowe mpaka uchoke kisha nawa mikono yako kwa sabuni, usije kuwapa watu mkonoau kutushikia vitu na mauchafu yako.
Kinyaa.
Hii ya kutofagia usiku hata kwetu ipo mkuu. Hebu taja nyingine zaidi watu wajifunze.1. Kwetu ni mwiko kufagia jioni jua linapozama.
2. Vile vile kupiga mswaki baada ya saa sita ni mwiko.
3. Masharti ni mengi mno.