Taja mwiko, mila au desturi za kabila lenu au mahali ulipokulia

Taja mwiko, mila au desturi za kabila lenu au mahali ulipokulia

- kujichokonowa pua mbele za watu. Ni tabia ambayo kwetu haijwahi kukubalika kuanzia kwa watoto wadogo mpaka watu wazima. Kwetu Pwani.

Imefikia mpaka mimi siikubali kabisa na nashindwa kujizuwia mtu akijichokonowa mbele yangu, nampa wazi, nendachooni jichokonowe mpaka uchoke kisha nawa mikono yako kwa sabuni, usije kuwapa watu mkonoau kutushikia vitu na mauchafu yako.

Kinyaa.
Kabisa au sehemu hadhara'mgahawa au ymemaliza kula wengine bado wanaendelea ww unachojonoa meno ama unasukutua maji mdomoni..nakereka sana kuna wale hawakufunzwa kutafuna chakula wakiwa wamefumba mdomo unaweza dhani anafua kumbe anakula ni chwa chwa pwa chwa khaa
 
Kabisa au sehemu hadhara'mgahawa au ymemaliza kula wengine bado wanaendelea ww unachojonoa meno ama unasukutua maji mdomoni..nakereka sana kuna wale hawakufunzwa kutafuna chakula wakiwa wamefumba mdomo unaweza dhani anafua kumbe anakula ni chwa chwa pwa chwa khaa
Kuna wengi sana hawana mafundisho ya maadili kutokea utotoni, nashukuru sisi wa shule za zamani na madrasa tulifunzwa mambo mengi ya kutokukahirisha watu.

Nakumbuka madrasa Ustadh wetu alikuwa na somo kabisa kila siku ya Jumatano mwenyewe akiliita "Kir'h", kwa maana "karaha".

Mengi sana madogo madogo ya kila siku tulifundishwa. Kwenye maadili ya kula tulifundishwa:

1) Tusinawe mikono kabla ya watu wazima.
2) Tusikae kula na watu wazima mpaka tukaribishwe.
3) tusijipitishe watu wanapokula.
4) tukinawa, tusikumute mikono mbele za watu, ikibidi kuikung'uta uebde pembeni kabisa.
5) hakuna kujamba kwa sauti au bila sauti wakati wa kula.
6) Namna ya kukohoa ukiwashwa koo wakati wa kula.
Dah mambo ni mengi sana tulifundishwa, yanayosaidia sana kuwa na tabia "natural" ambazo hazikirihishi wengine.

Sifahamu madrasa na shule za siku hizi kama wana wakati huo.

Shule tulikuwa na somo kabisa linaitwa "domestic science" moja ya mada zake ilikuwa ni "ethics". Hili kwa tuliosoma zamani, tulifundishwa na Mwalim Muhindi, simsahau anaitwa madam Jasmin, alikuwa kijana mtanashati enzi hizo. Alitunfundisha mema mengi sana tena sana.

Nikiwaelekeza vitu wajukuu zangu sasa hivi nilivyofundishwa "primary School" enzi hizo, wananiona mtu wa ajabu.
 
Huko nilipotokea ni marufuku mwanamke aliyeolewa kulala na chupi isipokuwa tu kipindi akiwa mwezini
Hii tamu sana aisee....akigeuka tu, imo. Natamani nihamie katika kijiji hicho
 
Kuna wengi sana hawana mafundisho ya maadili kutokea utotoni, nashukuru sisi wa shule za zamanai na madrasa tulifunzwa mambo mengi ya kutokukahirisha watu.

Nakumbuka madrasa Usraadh wetu alikuwa na somo kabisa kila siku ya Jumatano mwenyewqe akiliita "Kir'h", kwa maana "karaha".

Mengi sana madogoi madogoi ya kila siku tulifyundishwa. Kwenye maadili ya kula tulifundishwa:

1) Tusinawe mikono kabla ya watu wazima.
2) Tusikae kula na watu wazima mpaka tukaribishwe.
3) tusijipitishe watu wanapokula.
4) tukinawa, tusikumute mikono mbele za watu, ikibidi kuikung'uta uebde pembeni kabisa.
5) hakuna kujamba kwa sauti au bila sauti wakati wa kula.
6) Namna ya kukohoa ukiwashwa koo wakati wa kula.
Dah mambo ni mengi sana tulifundishwa, yanayosaidia sana kuwa na tabia "natural" ambazo hazikirihishi wengine.

Sifahamu madrasa na shule za siku hizi kama wana wakati huo.

Shule tulikuwa na somo kabisa linaitwa "domestic science" moja ya mada zake ilikuwa ni "ethics". Hili kwa tuliosoma zamani, tulifundishwa na Mwalim Muhindi, simsahau anaitwa madam Jasmin, alikuwa kijana mtanashati enzi hizo. Alitunfundisha mema mengi sana tena sana.

Nikiwaelekeza vitu wajukuu zangu sasa hivi nilivyofundishwa "primary School" enzi hizo, wananiona mtu wa ajabu.
Nielekeze mimi bibi
 
Ni Marufuku/mwiko kukata "Masalee"(Kwa Kiswahili sijui jina lake....

Mwiko kujiangalia kwenye kioo usiku...( Ila tunajiangalia tu)
Masalee ni kitu gani mkuu? Hebu elezea.

Kwetu ni mwiko mtu mdogo kuanza kula nyama au kitoweo kabla ya mkubwa. Kwa kawaida kitoweo huchanganywa na mboga za majani. Sasa mnapokula ugali mnaanza kula mboga za majani halafu mnamalizia na kitoweo.

Aidha, mnapokula ugali, mnaanza kumega kuanzia kwenye shina sio kileleni. Ukianzia kileleni wakubwa watakupiga kofi hutakuja kusahau.
 
Makabila yote hapa Afrika au nchi nyingine za Ulaya, Asia na Marekani, wanayo miiko, mila au desturi zilizozoeleka kiasi cha kurithiwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine.

Hapa Tanzania, kwa mfano, kuna mambo fulani ambayo ni mwiko kufanyika katika jamii na ikitokea mmoja wa wanajamii akaenda kinyume na mwiko huo anaweza kupata balaa au kuwasababishia wanajamii wengine balaa.

Baadhi ya mambo/matendo hayo ni kama ifuatavyo:

1. Jogoo akiwika usiku kabla ya mapambazuko huchukuliwa kuwa ni laana ama uchuro. Adhabu yake ni kuchinjwa na kufanywa kitoweo.

2. Bundi akilia usiku karibu na maskani ni balaa. Ili kuepukana na hiyo balaa, unatakiwa kuamka ukoke moto na kuchoma punje za mtama kwenye moto huo hadi punje hizo zilipuke.

3. Kwa kabila letu, hairuhusiwi mtu kutupa tula (Sodom apple) kumvuka msichana au mvulana ambaye bado yupo jandoni. Kufanya hivyo kunaweza kusababisha kifo au kuleta balaa kwa mhusika.

4. Ukiwa unapita porini na kukuta uyoga (edible mushroom) usiuache hapo ulipo. Hata kama huutaki au hujisikii kuula, ungo’e na kuuweka sehemu iliyoinuka ili mtu mwingine anayeuhitaji akipita auchukue akale. Kuuacha bila kuung’oa inaweza kukusababishia matatizo au mikosi.

5. Maisha ya kijijini ni ya kijamaa na watu huishi kwa kusaidiana. Kuna wakati unaweza kukosa unga ukaenda kuomba kwa jirani. Hata kama huyo jirani uliyemuendea naye hana unga wa kukugawiwa, chombo ulichoenda nacho hakirudi bure. Angalau akuwekee unga kisoda kimoja kwenye chombo hicho ili kisirudi tupu. Ni mwiko chombo hicho kurudi tupu.

6. Ukitembelewa na mgeni ambaye hajakutembelea baada ya muda mrefu hata kama huna chakula mmegee ukoko kutoka kwenye sufuria atafune au hata fundo la maji anywe. Ni mwiko mgeni huyo kuondoka kwako bila kula chochote.

Hii ni baadhi ya miiko ninayoweza kukumbuka kwa haraka haraka. Nitaongezea mingine wasaa mwingine. Je, wewe kwenye kabila lako au mahali ulipokulia, ni miiko gani umewahi kuishuhudia na mpaka inaheshimiwa? Tupia mmoja hapa tujifunze kitu.

Nawasilisha.
- kujichokonowa pua mbele za watu. Ni tabia ambayo kwetu haijwahi kukubalika kuanzia kwa watoto wadogo mpaka watu wazima. Kwetu Pwani.

Imefikia mpaka mimi siikubali kabisa na nashindwa kujizuwia mtu akijichokonowa mbele yangu, nampa wazi, nendachooni jichokonowe mpaka uchoke kisha nawa mikono yako kwa sabuni, usije kuwapa watu mkonoau kutushikia vitu na mauchafu yako.

Kinyaa.
iyo ni tabia mbaya ila sio mwiko
 
Makabila yote hapa Afrika au nchi nyingine za Ulaya, Asia na Marekani, wanayo miiko, mila au desturi zilizozoeleka kiasi cha kurithiwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine.

Hapa Tanzania, kwa mfano, kuna mambo fulani ambayo ni mwiko kufanyika katika jamii na ikitokea mmoja wa wanajamii akaenda kinyume na mwiko huo anaweza kupata balaa au kuwasababishia wanajamii wengine balaa.

Baadhi ya mambo/matendo hayo ni kama ifuatavyo:

1. Jogoo akiwika usiku kabla ya mapambazuko huchukuliwa kuwa ni laana ama uchuro. Adhabu yake ni kuchinjwa na kufanywa kitoweo.

2. Bundi akilia usiku karibu na maskani ni balaa. Ili kuepukana na hiyo balaa, unatakiwa kuamka ukoke moto na kuchoma punje za mtama kwenye moto huo hadi punje hizo zilipuke.

3. Kwa kabila letu, hairuhusiwi mtu kutupa tula (Sodom apple) kumvuka msichana au mvulana ambaye bado yupo jandoni. Kufanya hivyo kunaweza kusababisha kifo au kuleta balaa kwa mhusika.

4. Ukiwa unapita porini na kukuta uyoga (edible mushroom) usiuache hapo ulipo. Hata kama huutaki au hujisikii kuula, ungo’e na kuuweka sehemu iliyoinuka ili mtu mwingine anayeuhitaji akipita auchukue akale. Kuuacha bila kuung’oa inaweza kukusababishia matatizo au mikosi.

5. Maisha ya kijijini ni ya kijamaa na watu huishi kwa kusaidiana. Kuna wakati unaweza kukosa unga ukaenda kuomba kwa jirani. Hata kama huyo jirani uliyemuendea naye hana unga wa kukugawiwa, chombo ulichoenda nacho hakirudi bure. Angalau akuwekee unga kisoda kimoja kwenye chombo hicho ili kisirudi tupu. Ni mwiko chombo hicho kurudi tupu.

6. Ukitembelewa na mgeni ambaye hajakutembelea baada ya muda mrefu hata kama huna chakula mmegee ukoko kutoka kwenye sufuria atafune au hata fundo la maji anywe. Ni mwiko mgeni huyo kuondoka kwako bila kula chochote.

Hii ni baadhi ya miiko ninayoweza kukumbuka kwa haraka haraka. Nitaongezea mingine wasaa mwingine. Je, wewe kwenye kabila lako au mahali ulipokulia, ni miiko gani umewahi kuishuhudia na mpaka inaheshimiwa? Tupia mmoja hapa tujifunze kitu.

Nawasilisha.
Kwetu kumuua CHATU ni bora uue mifugo yote. NI mwiko hata kumuona amekufa

Kwetu ukichoma nyumba ni lazima ufanyiwe mambo flani
 
Back
Top Bottom