FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 100,246
- 123,145
Huo utakuwa ni upawa.iyo ni tabia mbaya ila sio mwiko
Hapo naona tafsiri ya llugha tu, mwiko kwako sijuwi unachukulia vipi, mimi nachukulia kila kisichofaa kinachokatazwa kukifanya ni mwiko.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huo utakuwa ni upawa.iyo ni tabia mbaya ila sio mwiko
Mbona mimi nilikuwa nakatia mbuzi masale manka?Ni Marufuku/mwiko kukata "Masalee"(Kwa Kiswahili sijui jina lake....
Mwiko kujiangalia kwenye kioo usiku...( Ila tunajiangalia tu)
Ni mwiko mwanaume kuimba wakati anakula inaweza kusababisha akaolea mbaliMakabila yote hapa Afrika au nchi nyingine za Ulaya, Asia na Marekani, wanayo miiko, mila au desturi zilizozoeleka kiasi cha kurithiwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
Hapa Tanzania, kwa mfano, kuna mambo fulani ambayo ni mwiko kufanyika katika jamii na ikitokea mmoja wa wanajamii akaenda kinyume na mwiko huo anaweza kupata balaa au kuwasababishia wanajamii wengine balaa.
Baadhi ya mambo/matendo hayo ni kama ifuatavyo:
1. Jogoo akiwika usiku kabla ya mapambazuko huchukuliwa kuwa ni laana ama uchuro. Adhabu yake ni kuchinjwa na kufanywa kitoweo.
2. Bundi akilia usiku karibu na maskani ni balaa. Ili kuepukana na hiyo balaa, unatakiwa kuamka ukoke moto na kuchoma punje za mtama kwenye moto huo hadi punje hizo zilipuke.
3. Kwa kabila letu, hairuhusiwi mtu kutupa tula (Sodom apple) kumvuka msichana au mvulana ambaye bado yupo jandoni. Kufanya hivyo kunaweza kusababisha kifo au kuleta balaa kwa mhusika.
4. Ukiwa unapita porini na kukuta uyoga (edible mushroom) usiuache hapo ulipo. Hata kama huutaki au hujisikii kuula, ungo’e na kuuweka sehemu iliyoinuka ili mtu mwingine anayeuhitaji akipita auchukue akale. Kuuacha bila kuung’oa inaweza kukusababishia matatizo au mikosi.
5. Maisha ya kijijini ni ya kijamaa na watu huishi kwa kusaidiana. Kuna wakati unaweza kukosa unga ukaenda kuomba kwa jirani. Hata kama huyo jirani uliyemuendea naye hana unga wa kukugawiwa, chombo ulichoenda nacho hakirudi bure. Angalau akuwekee unga kisoda kimoja kwenye chombo hicho ili kisirudi tupu. Ni mwiko chombo hicho kurudi tupu.
6. Ukitembelewa na mgeni ambaye hajakutembelea baada ya muda mrefu hata kama huna chakula mmegee ukoko kutoka kwenye sufuria atafune au hata fundo la maji anywe. Ni mwiko mgeni huyo kuondoka kwako bila kula chochote.
Hii ni baadhi ya miiko ninayoweza kukumbuka kwa haraka haraka. Nitaongezea mingine wasaa mwingine. Je, wewe kwenye kabila lako au mahali ulipokulia, ni miiko gani umewahi kuishuhudia na mpaka inaheshimiwa? Tupia mmoja hapa tujifunze kitu.
Nawasilisha.
MmakondeDesturi ya nyumbani kwetu ukisonga ugali ukimaliza mwiko lazima uuoshe. Marufuku kuacha mwiko mchafu. Hata sijui ina maana gani ila nimekua nayo mpaka leo nikimaliza kusonga ugali lazima nioshe mwiko kabla hata chakula hakijafika mezani.
Kweli?Mbona mimi nilikuwa nakatia mbuzi masale manka?
Ya mpakani kama ni mengi sana unakata (like pruning) unalisha mbuzi. Ya kaburini unakata pia kusafisha kaburi kama yamekuwa mengi. (Anyways ni kipindi nikiwa huko Uchaggani kabla sijaenda kwetu Umasaini).Kweli?
Yale ya Mpakani au yale mengine?
Kwetu ni mwiko hadi sasa hivi...Yanakatwa na wale Wazee..
Ooooh!!! Sawa...Ya mpakani kama ni mengi sana unakata (like prunning) unalisha mbuzi. Ya kaburini unakata pia kusafisha kaburi kama yamekuwa mengi. (Anyways ni kipindi nikiwa huko Uchaggani kabla sijaenda kwetu Umasaini).
Hapana.Mmakonde
Hii ni miiko kwa kabile letu piaKwenye kabila letu:
1. Ni mwiko mwanamke aliyejifungua kula nyama ya kuku. Inasemekana akila kuku maziwa yatakuwa hayatoki.
2. Ni marufuku mjamzito kula mayai. Ikiwa atakula mayai, atamzaa mtoto kipara (asiyekuwa na nywele).
Hiyo ya mwisho Ni noma sanaHiyo ya kumvuka mtu ipo na kwetu pia,
Kwetu huruhusiwi kulala kwenye kitanda shingoo ielekee kusini mwa kitanda bali ulale kaskazini mwa kitanda, mzungu wa nne kwetu ni marufuku.
Kwetu hurusiwi kushona nguo usiku.
Unapofiwa na mpendwa wako wote hamruhusiwi kuoga mpaka matanga yaishe kabisa.
Keiya nditooKwetu umasaini ni mwiko kumsalimia mtu mzima kwa mkono ni kichwa , kwetu hamruhusiwi kukaa karibu na watu wazima , sisi ni marufuku kuongea wakati mama anaongea , wakati wakula ni marufuku kuongea na kucheza cheza unatulia wakati wakula na mpaka watu wote wamalize kula ndio unaondoka . Nimarufuku kukiuka mila na desturi zetu
SidaiKeiya nditoo
Hahaha, kaiditi nanyorilai?Sidai
Dah hii ya matanga ilikuwepo kwetu enzi hizo na ni pamoja na kutonyoa au kuchana nywele mpaka mwezi(matanga) yaishe.Hiyo ya kumvuka mtu ipo na kwetu pia,
Kwetu huruhusiwi kulala kwenye kitanda shingoo ielekee kusini mwa kitanda bali ulale kaskazini mwa kitanda, mzungu wa nne kwetu ni marufuku.
Kwetu hurusiwi kushona nguo usiku.
Unapofiwa na mpendwa wako wote hamruhusiwi kuoga mpaka matanga yaishe kabisa.