Taja mwiko, mila au desturi za kabila lenu au mahali ulipokulia

Kwetu mkishazaa hampaswi kusex mpaka mtoto apewe dawa gani sijui au mpaka msubiri aache kunyonya. La sivyo mtamharibu (kiswahili kubemenda). Hiyo ni mwiko nimetamani sana kufuatilia kwenye jamii nyingin3 bado sijapata jibu.
Hii tuliifanyia utafiti wakati tupo shule lakini hatukufanikiwa. Hamna relationship kati ya mtoto anayenyonya na sperm za baba.
Ila kihalisia mtoto kudhoofu kupo. Na ukifatilia kwa nini hutopata jibu.
 
Hii tuliifanyia utafiti wakati tupo shule lakini hatukufanikiwa. Hamna relationship kati ya mtoto anayenyonya na sperm za baba.
Ila kihalisia mtoto kudhoofu kupo. Na ukifatilia kwa nini hutopata jibu.
Kiislam, mwanamke akimaliza "nifas" (post-partum bleeding) anakoga, anajitoharisha anaanza kusali, kufunga na kuingiliana na mumewe., haina muda maalum, isipokuwa wengi huku kwetu huiita na kungoja siku "arubaini".
 
Hii tuliifanyia utafiti wakati tupo shule lakini hatukufanikiwa. Hamna relationship kati ya mtoto anayenyonya na sperm za baba.
Ila kihalisia mtoto kudhoofu kupo. Na ukifatilia kwa nini hutopata jibu.
Hii huwakuta jamii zingine kama waarabu,wazungu,wachina?
 
Duh naamini nitajifunza mengi kupita huu Uzi, japo fact zenu zngine znatisha kwakweli
 
Kwenye jamii yangu;

1.Mtoto harusiwi kupanda kwenye paa la nyumba ya wazazi wake.Ikitokea amependa Basi lazima hiyo nyumba ibomolewe ijengwe nyingine.

2.Bundi aktua kwenye mti uliopo kwenye boma Ni dalili mbaya hususan msiba.

3.Ni mwiko kuchanja kuni Usiku kwa kutumia shoka.

4.Ukizini na mke wa jamaa uliyetahiri naye siku Moja( kwetu tunaita bakoki) hutakiwi kwenda kumuona akiwa mgonjwa.Ukifanya hivyo lazima Atakufa.
 
Wakuria ukoo wa wakira.
1. Mwanamke haruhusiwi kupanda juu ya nyumba kuezeka. Hata kama mumewe alishafariki anatafuta wanaume wamuezekee.
2. Ni marufuku kukata au kuharibu mti wenye matunda ambao tayari umezaa matunda(una matunda kwa muda huo)
3. Kuwapiga wazazi laana yake sio ya dunia hii na haisafishiki hata kwa damu.
4. Ni marufuku mwanaume uliyeoa kulala upande wa ukutani. Hii Mara nyingi ni ikiwa kuna dharura basi usimvuke mkeo(familia) kwani huenda hutarudi salama.
5. Ukiwa umetengewa chakula na mkeo,Mara ghafla yowe,mwano au nduru kuashiria hatari kweny jamii basi innashauriwa uonje japo kidogo kutia suna.. Usiache chakula bila kukigusa....ni mkosi.
6. Mwanaume uliyeoa ni lazima uwe na silaha yoyote ndani sime au panga.
Kwa sasa ni hayo kutokea sirari border
 
Sidhani kama ni miiko kweli kwamba utapata mabalaa hapana.

Bali ni taratibu au malezi ya kumjengea mtu tabia nzuri tu naamini tukizifuata hizo basi ni wazi tutakuwa na jamii Bora sana.

Kuhusu Jogoo kuwika nje ya muda tuliouzoea ni dhahania tu, kwakuwa viumbe nao huwa wanaota ndoto kama ilivyo kwa binadamu.

Bundi ni Moja ya ndege wasiopendwa na jamii nyingi kwakuwa yeye mawindo yake huyafanya usiku kama ilivyo kwa baadhi ya viumbe,pia wanahusishwa zaidi na ushirikina, lakini ni ndege wa kawaida hata akilia karibu yako sidhani kama Kuna ishu yeyote.
 
Daah kuna watu involuntarily ndio udhaifu wao huo na inatokea arbitrarily
 
Kutoosha vyombo usiku ni nuksi, mkipika chakula wakati wa kula jioni msimalize chote mbakize Kwa ajili ya mizimu yenu yaani wafu ndugu zenu wa familia, pia mwiko kupita ukimuona mtu wa jinsia tofauti au mtu mzima akiwa anakojoa kwenye njia, usimvuke mtu miguu yake
 
1. Kwetu ni mwiko kufagia jioni jua linapozama.
2. Vile vile kupiga mswaki baada ya saa sita ni mwiko.
3. Masharti ni mengi mno.
Hii ya kutofagia usiku hata kwetu ipo mkuu. Hebu taja nyingine zaidi watu wajifunze.

Kwetu mtu akiwa amelala chini usimvuke. Ukimvuka inasemekana hakuwi (harefuki). Ili ku undo au ku reverse hilo tatizo la kutokuwa, unatakiwa kumvuka kwa mara ya pili kuelekea upande uliomvukia.
 
Desturi ya nyumbani kwetu ukisonga ugali ukimaliza mwiko lazima uuoshe. Marufuku kuacha mwiko mchafu. Hata sijui ina maana gani ila nimekua nayo mpaka leo nikimaliza kusonga ugali lazima nioshe mwiko kabla hata chakula hakijafika mezani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…