Kumekuwa na tuhuma nyingi kuwa Taasisi ya Kuzuia Rushwa ni Toothless bull dog na kwamba taifa linapoteza fedha nyingi kuiendesha wakati haina tija yeyote. Na haya yamesemwa mpaka na wabunge wenyewe.
Kuna tuhuma ambazo zimekuja kama swali bungeni leo kuhusu wabunge wa CCM kupewa rushwa ya milioni 10 katika kikao alichohudhuria PM na Kinana ili mswada wa habari na mpango wa maendeleo upite.
Ni tuhuma mbaya na chafu sana kupata kutokea tokea Uhuru kwa serikali kwa ujumla wake kutoa hongo kwa kundi moja la wabunge walio wengi.
Haijalishi kama ni milioni 10 au 5, zote ni rushwa na ninauhakika wapo wabunge wamepokea lakini nafsini mwao hawajapendezwa na jambo hilo na hapo ndio pakuanzia.
Kufuta aibu hii ya kitaifa TAKUKURU watangaze kufuatilia jambo hili na kuchukua hatua hata kama itabidi serikali yote iathirike.
Nchi zingine hata rais au mfalme kwenye rushwa anachunguzwa iweje hapa waogopwe?
Na kama Rais atazuia uchunguzi huo basi ni kuwa rushwa hiyo ina baraka zake, na jee kumbe naye pamoja na kauli zake zote ni mtoa rushwa?
TAKUKURU ikishindwa ivunjwe haina maana kuwepo